_id
stringlengths 15
22
| url
stringlengths 31
150
| title
stringlengths 1
86
| text
stringlengths 100
23.8k
|
---|---|---|---|
20231101.sw_2119_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Duma
|
Duma
|
Kichwa chake ni kidogo zaidi ukilinganisha na wanyama wengine wa jamii yake kama chui. Duma anatofautiana na chui pia kwa sehemu ya mgongo na sehemu ya machoni: mgongo wa duma huwa kama alama ya "S", tofauti na mgongo wa chui. Macho ya duma yana weusi mkali ukilinganisha na chui.
|
20231101.sw_2119_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Duma
|
Duma
|
Manyoya yake yana rangi ya manjano inayoelekea kwenye rangi ya udongo iliyopambwa na madoa meusi. Rangi ya duma inashabihiana na mazingira yake ya mawindo hutegemea zaidi mbio na kuona ukilinganisha na wanyama wengine wawindaji ambao hutegemea kunusa na kuvizia katika mawindo yao. Ndiye mnyama anayeaminika kuwa na mwendo kasi zaidi kuliko wanyama wengine watembeao kwa miguu: hukimbia kilometa 113 kwa saa.
|
20231101.sw_2119_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Duma
|
Duma
|
Wanapokua, madume hutembea peke yao katika makundi ya duma watatu au wawili. Wanajamiana na majike wanapokuwa kwenye joto tu na si vinginevyo.
|
20231101.sw_2120_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hijra
|
Hijra
|
Hijra (هجرة) ni neno la Kiarabu linalomaanisha tendo la Mtume Muhammad la kutoka Makka na kuhamia Madina mwaka 622 BK. Mwaka huo umekuwa tarehe ya kuanzisha kalenda ya Kiislamu ambayo miaka yake huhesabu miaka baada ya hijra.
|
20231101.sw_2120_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hijra
|
Hijra
|
Maana asili ya neno lenyewe ni "kuachana" au "kutengana", kutokana na historia ya Muhammad limechukua pia maana ya "kukimbilia" au "kuhamia".
|
20231101.sw_2120_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hijra
|
Hijra
|
Muhammad alianza kuhubiri habari za Qurani na za Uislamu katika mji wa Makka alipozaliwa na kuishi. Lakini hakupata wafuasi wengi. Kinyume chake kabila lake yeye mwenyewe la Waquraishi walimchukia na kumtesa kwani viongozi waliogopa ataharibu biashara kubwa iliyoletwa na Kaaba iliyokuwa kama hekalu ya kidini mjini.
|
20231101.sw_2120_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hijra
|
Hijra
|
Hivyo Muhammad aliondoka Makka pamoja na babake mkubwa Abu Bakr; wafuasi wake kama 70 waliwahi kuondoka Makka siku zilizotangulia. Wote walipokelewa na watu wa Madina mji wa jirani.
|
20231101.sw_2120_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hijra
|
Hijra
|
Hapo Madina Muhammad akawa kiongozi aliyekubaliwa na watu wengi katika miaka iliyofuata aliunganisha Waarabu katika Uislamu mwishowe akarudi Makka ambako Waquraishi walipaswa kumkubali yeye na dini ya Usilamu.
|
20231101.sw_2120_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hijra
|
Hijra
|
Katika kumbukumbu ya Waislamu wa kwanza tendo la hijra lilikuwa jambo muhimu sana. Sura za Qurani zilipokusanywa kila moja imeandikwa kama imepatikana kabla au baada ya hijra. Kila sura inaonyesha chini ya kichwa chake maneno ama (imeteremka Makka) au (imeteremka Madina).
|
20231101.sw_2120_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hijra
|
Hijra
|
Pia hesabu ya miaka ilianzishwa wakati wa khalifa wa pili Umar ikihesabu kuanzia tarehe ile ya kuhamia kwake Muhammad Madina.
|
20231101.sw_2121_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Adolf Hitler (Braunau, Austria, 20 Aprili 1889; Berlin, Ujerumani, 30 Aprili 1945) alikuwa dikteta wa Ujerumani kuanzia mwaka 1933 hadi kifo chake.
|
20231101.sw_2121_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Alihutubia dharau na chuki ya kimbari dhidi ya watu wote wasio Wagermanik na hasa dhidi ya Wayahudi. Alisababisha Vita Kuu ya Pili ya Dunia na mateso ya watu milioni kadhaa. Akitangaza shabaha ya Ujerumani Mkubwa alisababisha kushindwa na kugawiwa kwa taifa lake pamoja na kupotewa na maeneo makubwa, hasa upande wa mashariki.
|
20231101.sw_2121_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Alizaliwa nchini Austria mwaka 1889. Wazazi wake walikuwa mtumishi wa forodha ya Austria Alois Hitler na mama yake Klara aliyekuwa mke wa tatu wa Alois.
|
20231101.sw_2121_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Adolf alikuwa na ndugu watano lakini kati yao ni dada yake Paula pekee aliyeishi kufikia umri wa mtu mzima, wengine wote walikufa mapema. Alikuwa pia na ndugu wawili kutoka ndoa ya mke wa pili wa baba na hao waliitwa Alois mdogo na Angela waliokaa katika familia ya Alois mzee baada ya kifo cha mama.
|
20231101.sw_2121_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Kutokana na kuhamishwa kwa baba mara kwa mara Adolf alisoma kwenye shule za msingi tofauti kati ya 1895 hadi 1899. Kuanzia mwaka 1900 alisoma kwenye shule ya sekondari mjini Linz lakini hakufaulu, alipaswa kurudia madarasa mawili. Hakupenda somo la dini, lakini alivutiwa na historia na jiografia. Baba alimpiga mara nyingi katika kipindi kile akikasirika juu ya kutofaulu shuleni.
|
20231101.sw_2121_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Baada ya kifo cha baba Alois mwaka 1903 mamake alimhamisha kwenda shule nyingine mjini lakini alishindwa hapa pia, akarudi nyumbani kwa mama bila ya kumaliza masomo yake.
|
20231101.sw_2121_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Alipokaa Linz Adolf alifahamika na mafundisho ya kiongozi wa chama cha "Alldeutsch" na hapa alianza kusikia habari za chuki dhidi ya Wayahudi na dharau dhidi ya mataifa ya Waslavi ya Ulaya.
|
20231101.sw_2121_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Tangu 1906 Hitler alijisikia kuwa msanii alipeleleza nafasi za kusoma uchoraji. Mwaka 1907 aliomba kupokewa katika chuo cha sanaa mjini Vienna, lakini alishindwa. Akarudi nyumbani baada ya kusikia mamake alikuwa mgonjwa wa kansa. Aliangalia nyumba hadi kifo cha mama kwenye Desemba 1907. Mama alitibiwa na daktari Eduard Bloch aliyekuwa Myahudi; Adolf alimshukuru sana kwa juhudi zake na baadaye alimlinda Bloch dhidi ya mateso yaliyoandaliwa kwa Wayahudi katika miaka ya 1930 baada ya Hitler kuwa mtawala wa Ujerumani na tangu 1938 wa Austria pia.
|
20231101.sw_2121_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Tangu Januari 1908 alitumia urithi wa mama pamoja na pensheni ya mjane kwa kuhamia Vienna alipokaa hadi 1913. Alijaribu tena kupata nafasi kwenye chuo cha sanaa cha Vienna akashindwa tena. Mtu aliyeishi pamoja naye katika chumba kimoja alisema wakati ule Hitler alivutiwa zaidi na opera za Richard Wagner kuliko siasa.
|
20231101.sw_2121_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Tangu mwisho wa 1908 alihama mara kwa mara sehemu alipokaa akitafuta kupanga vyumba kwa bei nafuu zaidi; inaonekana matatizo ya pesa yaliongezeka. Miaka 1910-1911 alipaswa kuishi katika bweni la wanaume wasio na nyumba.
|
20231101.sw_2121_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Tangu 1910 Hitler alikuwa na mapato madogo kwa njia ya kunakili picha alizouza kupitia watu walioishi pamoja naye katika bweni. Wengine waliouza picha kwa niaba yake walikuwa Wayahudi lakini, tofauti na daktari wa mamake, hakuwapa usaidizi wowote baadaye: waliteswa kama Wayahudi wote baada ya kuvamiwa kwa Austria 1938.
|
20231101.sw_2121_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Hitler alisoma mengi wakati ule na hasa maandiko yaliyotangaza ubora wa mbari ya Kigermanik na chuki dhidi ya Wayahudi.
|
20231101.sw_2121_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Mwaka 1913 alihamia Munich katika jimbo la Bavaria, Ujerumani. Alikuwa amepokea hela kidogo kutoka urithi wa babake pia alitaka kujiondoa katika wajibu wa kufanya huduma ya lazima ya kijeshi katika Austria-Hungaria. Aliendelea kunakili picha na kuziuza kwenye maduka ya sanaa.
|
20231101.sw_2121_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Mnamo Februari 1914 alikamatwa na polisi ya Bavaria na kupelekwa Austria lakini huko iliamuliwa hafai kwa huduma ya kijeshi akarudi Munich. Wakati wa kukaa Munich alisoma maandiko ya Houston Stewart Chamberlain kuhusu ubaguzi wa kimbari.
|
20231101.sw_2121_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Kuhamia kwake Munich kulifuatwa na vita mwaka 1914. Mnamo Agosti 1914, wakati wa mwanzo wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia alijitolea kwa jeshi la Bavaria ambapo kutokana na bidii na ukakamavu wake alipanda cheo na kuwa praiveti. Mwisho wa vita mwaka 1918 alikuwa na cheo cha koplo. Hakupewa shughuli za kupigania maadui moja kwa moja bali sehemu kubwa ya vita alihudumia kama tarishi aliyebeba habari na barua kati ya maafisa wa ngazi ya juu na hivyo mbali kiasi na eneo la mapigano. Alijeruhiwa mwaka 1916 alipopigwa na kibanzi cha kombora na tena kwenye Oktoba 1918 alipoathiriwa na gesi ya sumu iliyosababisha kipindi cha upofu. Alikuwa hospitalini bado aliposikia habari za mapinduzi katika Ujerumani na azimio la kusimamisha vita tarehe 11 Novemba 1918.
|
20231101.sw_2121_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Mwezi Novemba 1918 Hitler alirudi Munich alipoendelea kuwa mwanajeshi hadi mwaka 1920. Munich iliona kipindi cha vuguvugu ya mapinduzi. Kwa muda alishiriki katika kamati zilizochaguliwa na wanajeshi na kuwawakilisha mbele ya serikali na maafisa. Munich iliona kipindi kifupi cha mapinduzi makali ambako viongozi wake walijaribu kuiga mfano wa Urusi. Kipindi hiki kilikwisha baada ya mashambulio ya sehemu za jeshi zilizofuata amri za serikali kuu ya Berlin.
|
20231101.sw_2121_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Sasa maafisa wa jeshi walioshika tena amri walipambana na mielekeo ya kikomunisti na kisoshalisti kati ya askari na wafanyakazi wa viwanda. Hapa Hitler aliteuliwa na wakuu wake kwa propaganda dhidi ya wanamapinduzi wasoshalisti. Alipelekwa kwa mafundisho ya kiitikadi akapewa mazoezi ya kuhutubia watu. Inaonekana ya kwamba ilikuwa katika kipindi hiki Hitler alipopokea mafundisho yaliyoimarisha itikadi ya chuki dhidi ya Wayahudi walioshtakiwa na wafuasi wa ufalme kuwa sababu ya kushindwa vitani pamoja na kuchochea mapinduzi.
|
20231101.sw_2121_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Hapa ilitokea ya kwamba kwenye Septemba 1919 alihudhuria mkutano wa chama kidogo na kichanga kilichojiita "Chama cha Wafanyakazi Wajerumani" (Deutsche Arbeiterpartei, DAP). Hitler alishiriki katika majadiliano akakaribishwa kujiunga na chama hicho. Aliomba kibali cha mkuu wake jeshini kwa hatua hii akawa mwanachama wa 55 wa chama hiki.
|
20231101.sw_2121_18
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Aliteuliwa kuwa katibu mwenezi wa DAP na chama kilianza kupokea zawadi kutoka matajiri waliomwona Hiler kama mhubiri mwenye kipaji kikubwa aliyepinga usoshalisti na ukomunisti. Mwezi Februari DAP ilibadilisha jina lake kuwa "Nationalsozialistische Deutsche Arbeiterpartei" (Chama cha Kizalendo - Kisoshialisti cha Wafanyakazi Wajerumani) kifupi NSDAP.
|
20231101.sw_2121_19
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Kwenye Aprili 1920 Hitler alitoka katika jeshi akipata riziki yake kwa njia ya kuhutubia mikutano alipolipwa. Sifa zake kama mhubiri zilijulikana kote Munich na alianza kuwasiliana pia na wanasiasa waliokuwa na mielekeo ya kufanana huko Berlin.
|
20231101.sw_2121_20
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Mwaka 1921 hatimaye aliweza kushinda viongozi wa awali katika chama na kuwa kiongozi mkuu wa NSDAP ambao hadi wakati ule bado ilikuwa moja ya vyama vingi vidogo vilivyotangaza siasa ya kizalendo dhidi ya ukomunisti na pia dhidi ya demokrasia.
|
20231101.sw_2121_21
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Hitler alivutiwa sana na mfano wa Benito Mussolini, kiongozi wa kifashisti wa Italia, aliyefaulu mwaka 1922 kupindua serikali ya Italia kwa maandamano makubwa ya wafuasi wake kuelekea Roma.
|
20231101.sw_2121_22
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Mwaka 1923 Hitler alijaribu kumwiga Mussolini kwa kupindua serikali ya jimbo la Bavaria - kama utangulizi wa kupindua serikali ya kitaifa huko Berlin - lakini alikamatwa na kuhukumiwa kwa uasi huo kifungo cha miaka mitano, ingawa alitumikia miezi tisa tu. Chama chake kilipigwa marufuku.
|
20231101.sw_2121_23
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Hitler akiwa kijana aliwahi kusoma vitabu vya Mwingereza Neville Chamberlain aliyedai kwamba kuna mbari mbalimbali za watu zenye tabia na thamani tofauti sana.
|
20231101.sw_2121_24
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Akiwa gerezani aliandika kitabu kilichoitwa "Mein Kampf" ("Mapambano Yangu") alimojaribu kueleza imani na siasa zake. Humo alieleza pia chuki dhidi ya Wayahudi na itikadi yake ya ubaguzi wa kimbari.
|
20231101.sw_2121_25
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Katika itikadi hiyo mbari ya juu ni watu wa Ulaya ya Kaskazini aliowaita "Waaria", na wale ambao ni duni zaidi ni watu weusi. Vikundi vingine vimo katikati. Lakini watu wabaya kabisa katika itikadi hiyo ni Wayahudi ambao ni wajanja wakuu upande mmoja, lakini hawana uwezo wa kuunda kitu kwa upande mwingine. Hivyo wanajaribu kwa ujanja wao kutawala dunia kwa kuiba fikra na mafanikio ya Waaria.
|
20231101.sw_2121_26
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Baada ya kutoka gerezani alirudi katika siasa. Aliahidi za kwamba atafuata sheria, hivyo chama cha NSDAP kiliruhusiwa tena. Hitler alisafiri kote Ujerumani akiunda matawi ya chama. Ndani ya chama alianzisha vikosi viwili vilivyovaa sare vikifanya mazoezi kama wanamgambo na kuwa tayari kupigana na maadui wa kisiasa wakati wa maandamano.
|
20231101.sw_2121_27
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Kikundi cha SA ("Sturmabteilung" - "Kikosi cha kushambulia") kilikuwa na watu wengi sana kikavuta hasa wanaume wasio na kazi waliovaa sare ya kahawia. Kikosi cha pili kilikuwa na watu wachache kikaitwa "SS" ("Schutzstaffel" - "Kikosi cha ulinzi") waliovaa sare nyeusi na kuwa na wajibu hasa kumlinda Hitler.
|
20231101.sw_2121_28
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Chama chake hakikufaulu hadi 1929, wakati uchumi wa dunia pamoja na wa Ujerumani ulipoporomoka vibaya katika Mdodoro Mkuu. Mamilioni ya watu waliachishwa kazi na kuona njaa. Katika hali hiyo watu walianza kupigia kura vyama vyenye itikadi kali.
|
20231101.sw_2121_29
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Katika uchaguzi wa mwaka 1930 kura za NSDAP ziliongezeka kutoka 2.6% hadi 18.3%. Serikali za Ujerumani zilikuwa za vyama vingi na dhaifu.
|
20231101.sw_2121_30
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Mwaka 1932 chama cha NSDAP kilipata 33% za kura na kuwa chama chenye kura nyingi zaidi nchini na chama kikubwa katika bunge la Reichstag. Katika hali hiyo viongozi wa Dola la Ujerumani waliamua kumwingiza Hitler katika serikali mwaka 1933.
|
20231101.sw_2121_31
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Tarehe 30 Januari 1933 Hitler akawa Chansela wa Ujerumani. Mara moja alichukua nafasi kuwakandamiza wapinzani wake na baada ya mwaka mmoja hata wale waliomwingiza madarakani.
|
20231101.sw_2121_32
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Baada ya mwaka mmoja utawala wake ulisimama imara kabisa ilhali wapinzani wengi walikamatwa na kupelekwa katika makambi ya KZ.
|
20231101.sw_2121_33
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Hitler alifuata siasa ya kujenga uchumi na kurudisha watu kazini akibahatika kwamba uchumi wa dunia ukapaa tena.
|
20231101.sw_2121_34
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Hitler alifuta mapatano yote ya Ujerumani yaliyoweka mipaka kwa ukubwa wa jeshi lake kuwa watu 100,000 tu akajenga jeshi kubwa zaidi, akaanzisha utawala wa kidikteta wa "Dola la Tatu" akipiga marufuku vyama vya upinzani. Alitesa wapinzani wote na watu wa mbari alizochukia, hasa Wayahudi.
|
20231101.sw_2121_35
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Chuki dhidi ya Wajerumani waliokuwa Wayahudi aliionyesha kwa sheria mbalimbali zilizokuwa kali zaidi na zaidi. Idadi ya Wayahudi katika Ujerumani ilikuwa ndogo, takriban nusu milioni kati ya wakazi milioni 62. Kila Mjerumani akitaka kuajiriwa na serikali au kupata nafasi ya masomo alitakiwa kuorodhesha wazazi na mababu hadi kizazi cha pili. Kwa njia hiyo Hitler alipanga Wajerumani wote katika vikundi vya "Waaria" (ambao hawana Wayahudi katika familia), "Wayahudi" (watu wenye asili ya Kiyahudi, hata kama wameshakuwa Wakristo tangu vizazi kadhaa au hawakufuata dini), "Wayahudi nusu" kama mzazi mmoja alikuwa Myahudi, "Wayahudi robo" kama mmoja kati ya mababu na mabibi wanne alikuwa Myahudi. Wayahudi na Wayahudi nusu walifukuzwa katika ajira ya serikali na walikataliwa kufanya kazi mbalimbali.
|
20231101.sw_2121_36
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Sheria kuhusu "Aibu wa mbari" ilikataza ndoa kati ya "Waaria" na "Wayahudi"; "Wayahudi" waliondolewa uraia kamili.
|
20231101.sw_2121_37
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Tokeo moja la siasa hiyo lilikuwa kuondoka kwa Wayahudi wengi kidogo katika Ujerumani; baada ya mashambulizi makali na mauaji mwaka 1938 mwelekeo huo uliongezeka. Hasa wanasayansi na wasanii wengi walihamia nchi huru.
|
20231101.sw_2121_38
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Mwaka 1938 alifaulu kuteka Austria na maeneo ya Wajerumani katika Ucheki bila upingamizi wa kimataifa.
|
20231101.sw_2121_39
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Lakini aliposhambulia Poland tarehe 1 Septemba 1939 tendo hili lilikuwa mwanzo wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia kwa sababu Uingereza na Ufaransa walisimama imara kwa mikataba ya kusaidiana na Poland.
|
20231101.sw_2121_40
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Wakati wa vita Hitler alichukua mwenyewe uongozi mkuu wa jeshi. Mwanzoni alifaulu hata dhidi ya ushauri ya majenerali wake, hasa wakati wa vita dhidi ya Poland na Ufaransa. Lakini maazimio yake ya 1941 ya kushambulia Urusi na kutangaza hali ya vita dhidi ya Marekani yalikuwa mwanzo wa mwisho wake. Nguvu ya kiuchumi wa Ujerumani haikutosha kushindana na dunia yote.
|
20231101.sw_2121_41
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Wakati wa vita aliamuru uuaji wa Wayahudi wote wa Ulaya, na inakadiriwa alifaulu kuwaua takriban milioni sita (2/3 ya Wayahudi wote wa Ulaya) pamoja na watu vya mbari mbalimbali kama Wasinti (kati ya 200,000 na 1,500,000).
|
20231101.sw_2121_42
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Hasa alipoona ya kwamba vita dhidi ya Urusi haikufaulu haraka jinsi alivyotegemea aliamua kumaliza jambo lililosababisha chuki yake hasa. Azimio la "usuluhisho wa mwisho wa suala la Kiyahudi" lilichukuliwa mwisho wa mwaka 1941 na kutangazwa mbele ya viongozi wachache mnamo Januari 1942 katika Mkutano wa Wannsee.
|
20231101.sw_2121_43
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Baadaye siasa ya kuwatenda Wayahudi vibaya na kuwaua katika maeneo fulani ilibadilishwa kulenga Wayahudi wote katika nchi zote zilizokuwa chini ya athira ya Ujerumani au kutekwa na jeshi lake. Hadi mwisho wa vita Wayahudi walikusanywa kutoka kote Ulaya na kupelekwa kwa reli hadi makambi ya mauti.
|
20231101.sw_2121_44
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Maafisa wachache wa jeshi ya Ujerumani walipanga mara kadhaa kumwua Hitler. Tarehe 20 Julai 1944 kanali Stauffenberg alilipusha bomu katika ikulu ya Hitler pale Prussia ya Mashariki. Hitler alijeruhiwa lakini hakufa.
|
20231101.sw_2121_45
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Tangu Januari 1945 Hitler alihamia tena Berlin kutokana na uvamizi wa jeshi la Kirusi katika Ujerumani Mashariki. Hapa alikaa katika boma imara chini ya ardhi. Hakutoka mjini tena.
|
20231101.sw_2121_46
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Tarehe 20 Aprili alishehereka mara ya mwisho sikukuu yake na kupokea wageni wachache. Siku iliyofuata vikosi vya kwanza vya jeshi la Urusi vilianz kuingia katika maeneo ya Jiji la Berlin.
|
20231101.sw_2121_47
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Tarehe 25 Aprili 1945 Berlin yote ilizungukwa kama kisiwa na jeshi la Wasovyeti na tangu 28 Aprili waliingia katika kitovu cha Berlin. Hitler bado alikuwa na tumaini kwamba vikosi vya jeshi la Kijerumani kutoka magharibi vitafika Berlin lakini majaribio yote yalishindikana. Habari zilipokelewa Berlin ya kwamba makamu zake Hitler kama Himmler na Goering walijaribu kutafuta mapatano na Marekani au Uingereza. Hitler aliwatangaza ni wasaliti akaamuru kuwakamata lakini amri hizi hazikutekelezwa tena maana hawakuwa karibu naye.
|
20231101.sw_2121_48
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Katika hali hii Hitler alielewa ya kwamba hakuna njia ya kushinda na wataalamu hukubaliana ya kwamba hapo aliamua kujiua. Usiku wa 27 Aprili alimwoa mpenzi wake wa miaka mingi Eva Braun. Aliendelea kutunga wosia wake ambamo alimtaja mkuu wa jeshi la maji Karl Doenitz kuchukua madaraka yake kama mkuu wa dola na wa jeshi. Kwenye 29 Aprili jioni alipokea habari ya kwamba Benito Mussolini ameuawa huko Italia.
|
20231101.sw_2121_49
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Tarehe 30 Aprili aligawa sumu kwa wote waliokuwa pamoja naye katika boma chini ya ardhi akawaruhusu kuondoka; aliagiza sumu ijaribishwe kwa mbwa wake mpendwa "Blondi". Mnamo saa 15.30 Eva Brau alijiua kwa kumeza sumu na Hitler alipigia risasi kichwani. Wasaidizi wa mwisho walibeba maiti hadi bustani ya ikulu na kuziweka katika shimo kutokana na mlipuko wa bomu; hapa wakazichoma kwa petroli.
|
20231101.sw_2121_50
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Warusi waliingia saa chache baada ya vifo hivi. Walikuta maiti tarehe 5 Mei bila kutambua ni Hitler na Eva Braun. Tarehe 10 Mei msaidizi wa daktari wa meno wa Hitler aliweza kutambua maiti kutokana na meno. Mabaki yalizikwa baadaye karibu na makao makuu ya jeshi la Kirusi katika Ujerumani ya Mashariki; yalihamishwa mara kadhaa kila wakati makao makuu yalipohamishwa. Mwishoni mabaki ya maiti yalichomwa na Warusi tarehe 5 Aprili 1970, majivu yalisagwa na yote kutupwa katika mto mdogo karibu na mji wa Magdeburg.
|
20231101.sw_2121_51
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20Hitler
|
Adolf Hitler
|
Taarifa hizi zilitunzwa kama siri kwa miaka mingi hadi mwisho wa Ukomunisti katika Urusi na hivi kulikuwa na uvumi wa kwamba Hitler hajafa na labda alikimbia hadi Amerika Kusini, jinsi idadi ya wasaidizi wake waliofaulu kutoroka.
|
20231101.sw_2122_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Miaka%20baada%20ya%20hijra
|
Miaka baada ya hijra
|
Hesabu hii ilianzishwa miaka 17 baada ya tukio lenyewe (638 BK) kufuatana na azimio la Khalifa Umar ibn al-Khattab.
|
20231101.sw_2122_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Miaka%20baada%20ya%20hijra
|
Miaka baada ya hijra
|
Waarabu waliwahi kuwa na kalenda iliyotumia mwendo wa mwezi lakini hawakuhesabu miaka. Kila mwaka ulitajwa kutokana na tukio fulani. Mwaka wa kuzaliwa kwake Mtume Muhammad hujulikana "Mwaka wa Tembo" kwa sababu mwaka ule Makka ilishambuliwa na jeshi la Waethiopia lililokuwa na tembo wa kijeshi.
|
20231101.sw_2122_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Miaka%20baada%20ya%20hijra
|
Miaka baada ya hijra
|
Hata baada ya Muhammad desturi hii iliendelea. Mwaka wa Hijra wenyewe uliitwa "Mwaka wa kukubaliwa kwa safari," mwaka uliofuata "Mwaka vita ilipoamriwa," n.k.
|
20231101.sw_2122_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Miaka%20baada%20ya%20hijra
|
Miaka baada ya hijra
|
Wakati wa Khalifa Umar ilionekana haja ya kuwa na hesabu inayoeleweka zaidi, hivyo hesabu ya Hijra ikachaguliwa.
|
20231101.sw_2122_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Miaka%20baada%20ya%20hijra
|
Miaka baada ya hijra
|
Waarabu Waislamu waliendelea kuhesabu miaka ya mwezi ya siku 29 au 30 kufuatana na kuonekana halisi kwa mwezi.
|
20231101.sw_2122_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Miaka%20baada%20ya%20hijra
|
Miaka baada ya hijra
|
Hivyo miaka ya Kiislamu ina jumla ya siku takriban 354. Mwaka huo wa Kiislamu una siku 11 pungufu kuliko siku zile 365 za mwaka wa jua katika kalenda ya Kikristo. Mwaka 2006 BK ni 1427 BH (baada ya Hijra).
|
20231101.sw_2122_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Miaka%20baada%20ya%20hijra
|
Miaka baada ya hijra
|
Uajemi hutumia hesabu ya miaka ya Hijra pamoja na mwaka wa jua. Hivyo mwanzo wa 2006 BK huko Uajemi ni mwaka 1384 BH (baada ya Hijra).
|
20231101.sw_2127_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu ni mtindo wa kuratibu wakati unaopatikana katika nchi mbalimbali za Kiislamu. Tofauti na kalenda ya kawaida inayofuata jua hii ni kalenda ya mwezi inayofuata kuandama kwa mwezi.
|
20231101.sw_2127_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Pia Waislamu wanaoishi katika mazingira yasiyo ya Kiislamu hutumia kalenda hii kwa ajili ya kupanga maisha yao ya kidini, hasa sikukuu na saumu.
|
20231101.sw_2127_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Kalenda hii ilianza kutumika rasmi kutokana na tukio la mtume Muhammad kuhama Makka kwenda Madina, tukio ambalo linajulikana kama Hijra.
|
20231101.sw_2127_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Mahali pengi Kalenda ya Kiislamu hutumika pamoja na kalenda zinazofuata mwendo wa jua, hasa kalenda ya Gregori ambayo ndiyo iliyoenea zaidi duniani.
|
20231101.sw_2127_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu imepokea kawaida ya mwaka wa Waarabu wa kale wenye miezi 12. Hesabu ya vipindi hivi 12 hufuata muonekano wa Mwezi angani, ambayo ni tofauti na "miezi" katika kalenda ya kimataifa ambayo hayana uhusiano na kuonekana kwa Mwezi kwenye anga.
|
20231101.sw_2127_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
"Mwezi" humaanisha kipindi kamili kati ya kuonekana kwa mwezi wa hilali mara ya kwanza hadi kurudia kwa kuonekana kwake. Kwa sababu muda huo ni siku 29.5, mwezi huhesabiwa kuwa na siku 29 au 30.
|
20231101.sw_2127_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Waislamu wanaofuata mfano wa Kisaudi hukubali kwamba mwezi mpya umeanza kama umeonekana kwa macho. Kwa sababu desturi hii imeleta matatizo ya kutokubaliana, pia ni rahisi kukadiria mwendo wa mwezi, nchi mbalimbali za Kiislamu hutumia makadirio ya kitaalamu kupanga tarehe za miezi.
|
20231101.sw_2127_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Idadi ya siku katika mwaka wa Kiislamu ni 354, kwa hiyo ni mfupi kuliko mwaka wa Jua wenye siku 3651/4. Kwa sababu hiyo sherehe zote za mwaka wa Kiislamu husogea polepole katika majira ya mwaka wa kalenda ya kiraia inayofuata Jua.
|
20231101.sw_2127_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Hesabu ya miaka katika kalenda ya Kiislamu hufuta utaratibu wa "miaka baada ya hijra" yaani tangu kuhamia kwake Mtume Muhammad kutoka Makka kwenda Madina. Hijra ilitokea mwaka 622 BK au katika mwaka 1 wa hesabu yenyewe.
|
20231101.sw_2127_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Njia inayofuata inasaidia kujua takriban tarehe gani ya Kiislamu inalingana na tarehe ipi katika kalenda ya kawaida:
|
20231101.sw_2127_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
K (Mwaka "baada ya Kristo" katika kalenda ya Kikristo), H (Mwaka "Baada ya Hijra" katika kalenda ya Kiislamu)
|
20231101.sw_2127_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Huko Uajemi (Iran) na Afghanistan kuna mfumo tofauti wa kupanga wakati. Huko wanatumia kalenda ya jua wakihesabu muda wa mwaka ni siku 365 jinsi ilivyo katika kalenda ya Gregori. Kila mwaka unaanza mnamo tarehe 20 Machi ambayo ni sikusare ya machipuo yaani usawa wa muda wa usiku na mchana kwenye nusutufe ya kaskazini ya Dunia.
|
20231101.sw_2127_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Ni kalenda ya Kiislamu kwa sababu inaanza kuhesabu miaka tangu hijra. Kalenda hii huitwa "Shamsi" (kutoka neno la Kiarabu / Kifarsi شمس shams = Jua). Kwa mfano, mwaka 1396 shamsi ya Iran inalingana na mwaka 1438 wa kalenda ya kawaida ya Kiislamu.
|
20231101.sw_2127_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Huko wanaita kalenda ya kidini "kalenda qamari" (yaani ya mwezi) na mara nyingi kuchapisha namba ya "mwaka qamari" kando ya "mwaka shamsi". Katika kupanga sikukuu za kidini hufuata kalenda qamari lakini sikukuu za serikali hufuata kalenda shamsi.
|
20231101.sw_2127_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Mwaka mpya katika kalenda hii inaanza kikamilifu wakati wa sikusare machipuo yaani tarehe 21 au 20 Machi ambayo ni maarufu kama sikuu ya Nowruz.
|
20231101.sw_2127_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
mwezi wa Rabi' ul-auwali wenye tarehe 12 Idd-ul-maulidi yaani sikukuu ya kuzaliwa kwake Mtume Muhammad (Maulidi-an-Nabii).
|
20231101.sw_2127_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Mwezi wa Muharram ni muhimu sana kati ya Washia wanaokumbuka mateso na kifo cha Imam Husain wakati wa mapigano ya Karbala.
|
20231101.sw_2127_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu hutumia juma au wiki ya siku saba jinsi ilivyo kawaida kwa Wayahudi na Wakristo. Siku muhimu zaidi ni Ijumaa ambako Waislamu hukusanyika kwa ajili ya sala ya pamoja.
|
20231101.sw_2127_18
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Kwa Kiarabu majina ya siku za juma hufuata hesabu ya Kiyahudi jinsi inavyoonekana katika Biblia. Jumapili inaitwa "siku ya kwanza", Jumatatu "siku ya pili" hadi "siku ya tano" = Alhamisi. Siku ya sita pekee imepewa jina jipya la Kiislamu kutokana na mkutano wa sala ya pamoja.
|
20231101.sw_2127_19
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Siku ya saba tena imebaki na jina lake la Kibiblia "Sabato" au siku ya saba. Hii ni kwa sababu utamaduni wa Kiarabu kabla ya Uislamu uliwahi kupokea athira nyingi kutoka kwa Wayahudi na Wakristo, pia walikuwepo Waarabu ambao upande wa dini walikuwa Wakristo na Wayahudi.
|
20231101.sw_2127_20
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kalenda%20ya%20Kiislamu
|
Kalenda ya Kiislamu
|
Majina ya siku katika lugha ya Kiswahili yanaonyesha ya kwamba lugha ilianza katika mazingira ya Kiislamu kabisa, bila athira za moja kwa moja kutoka Uyahudi au Ukristo. Majina ya siku yamepangwa kufuatana na Ijumaa ambayo ni siku muhimu hasa katika maisha ya Kiislamu. Maana ya Jumamosi, Jumapili n.k. ni "Siku ya kwanza, pili, tatu" baada ya Ijumaa. Alhamisi imebaki na jina la Kiarabu.
|
20231101.sw_2128_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Lindi
|
Mkoa wa Lindi
|
Umepakana na mikoa ya Pwani, Mtwara, Ruvuma na Morogoro. Upande wa mashariki hupakana na Bahari Hindi.
|
20231101.sw_2128_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Lindi
|
Mkoa wa Lindi
|
Mkoa huu umeanzishwa mwaka 1971 na una eneo la km² 67,000. Karibu robo ya eneo lake au km² 18,000 ni sehemu ya Hifadhi ya Taifa ya Nyerere.
|
20231101.sw_2128_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Lindi
|
Mkoa wa Lindi
|
Mkoa una wilaya sita za: Lindi Mjini, Mtama (hadi 2019 Lindi Vijijini), Kilwa, Nachingwea, Liwale na Ruangwa.
|
20231101.sw_2128_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Lindi
|
Mkoa wa Lindi
|
Makabila makubwa zaidi ni Wamwera, ambao wanapatikana hasa wilaya ya Nachingwea na Lindi vijijini katika kata za Rondo, halafu Wamachinga, Wamalaba ambao wako zaidi Lindi mjini, Wamatumbi na Wangindo huko Kilwa.
|
20231101.sw_2128_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Lindi
|
Mkoa wa Lindi
|
Wakazi kwa wilaya ni (idadi katika mabano): Kilwa (171,850), Lindi Mjini (41,549), Lindi Vijijini (215,764), Liwale (75,546), Nachingwea (162,081), Ruangwa (124,516),
|
20231101.sw_2128_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Lindi
|
Mkoa wa Lindi
|
Kuna barabara chache katika hali nzuri. Ndizo km 155 za barabara ya lami na km 3567 za barabara ya mavumbi, mara nyingi katika hali mbaya. Wakati wa mvua mara kwa mara njia ya kwenda Daressalaam imefungwa.
|
20231101.sw_2128_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Lindi
|
Mkoa wa Lindi
|
Kuna matumaini ya kuboreka kwa mawasiliano na jiji la Daresalaam tangu kumalizika kwa daraja la Rufiji.
|
20231101.sw_2128_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Lindi
|
Mkoa wa Lindi
|
Kwa sasa barabara ya kutoka Mingoyo mpaka Dar es Salaam imekamilika kwa kiwango cha lami, kimebaki kipande cha kilometa 60 tu kuanzia Muhoro, wilaya ya Kilwa, mpaka kukaribia daraja la Mkapa juu ya mto Rufiji ambacho kinamaliziwa kwa kiwango cha lami.
|
20231101.sw_2128_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Lindi
|
Mkoa wa Lindi
|
Kuna kiwanja cha ndege Lindi, Nachingwea na Kilwa Masoko. Lindi na Kilwa Masoko kuna pia bandari. Huduma za simu zimepata maendeleo kiasi tangu kuanzishwa kwa simu za mkononi.
|
20231101.sw_2128_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Lindi
|
Mkoa wa Lindi
|
Utalii haujafikia umuhimu sana kutokana na matatizo ya mawasiliano magumu, ingawa Lindi ina sehemu mbalimbali zenye uwezo wa kuwavuta watalii: Kilwa Kisiwani ndio mji wa kihistoria wa pwani ya Afrika ya Mashariki pamoja na magofu ya miji mingine ya Waswahili, Selous ni hifadhi kubwa kabisa katika Afrika, ufuko wa mchanga ni wa kuvutia sana, nafasi za zamia majini ni tele.
|
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.