_id
stringlengths
15
22
url
stringlengths
31
150
title
stringlengths
1
86
text
stringlengths
100
23.8k
20231101.sw_2109_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Akishika dini yake kwa msimamo mkali akawa anapinga Ukristo kwa kukamata, kutesa na hata kuua Wakristo, kama vile Stefano Mfiadini.
20231101.sw_2109_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Alifanya hivyo mpaka alipotokewa na Yesu Kristo mfufuka akiwa njiani kwenda Damaski, Syria (kwa umuhimu wake katika Historia ya Wokovu habari hii inasimuliwa mara tatu katika kitabu cha Matendo ya Mitume: 9:1-19; 21:12-18 na 22:5-16). Jibu lake kwa Yesu lilikuwa (Mdo 22:10): "Nifanye nini, Bwana?"
20231101.sw_2109_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
1 Wakati huo Saulo alikuwa akizidisha vitisho vikali vya kuwaua wafuasi wa Bwana. Alikwenda kwa Kuhani Mkuu,
20231101.sw_2109_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
2 akaomba apatiwe barua za utambulisho kwa masunagogi ya Kiyahudi kule Damasko, ili akikuta huko wanaume au wanawake wanaofuata Njia ya Bwana, awakamate na kuwaleta Yerusalemu.
20231101.sw_2109_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
3 Lakini alipokuwa njiani karibu kufika Damasko, ghafla mwanga kutoka angani ulimwangazia pande zote.
20231101.sw_2109_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
5 Naye Saulo akauliza, "Ni nani wewe Bwana?" Na ile sauti ikajibu, "Mimi ni Yesu ambaye wewe unamtesa.
20231101.sw_2109_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
7 Wale watu waliokuwa wanasafiri pamoja na Saulo walisimama pale, wakiwa hawana la kusema; walisikia ile sauti lakini hawakumwona mtu.
20231101.sw_2109_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
8 Saulo aliinuka, na alipofumbua macho yake hakuweza kuona chochote; hivyo wale watu wakamwongoza kwa kumshika mkono mpaka mjini Damasko.
20231101.sw_2109_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
10 Basi, huko Damasko kulikuwa na mfuasi mmoja aitwaye Anania. Bwana akamwambia katika maono, "Anania!" Anania akaitika, "Niko hapa, Bwana."
20231101.sw_2109_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
11 Naye Bwana akamwambia, "Jitayarishe uende kwenye barabara inayoitwa Barabara ya Moja kwa Moja, na katika nyumba ya Yuda umtake mtu mmoja kutoka Tarso aitwaye Saulo. Sasa anasali;
20231101.sw_2109_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
12 na katika maono ameona mtu aitwaye Anania akiingia ndani na kumwekea mikono ili apate kuona tena."
20231101.sw_2109_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
13 Lakini Anania akajibu, "Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kutoka kwa watu wengi; nimesikia juu ya mabaya aliyowatendea watu wako huko Yerusalemu.
20231101.sw_2109_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
14 Na amekuja hapa akiwa na mamlaka kutoka kwa makuhani wakuu kuwatia nguvuni wote wanaoomba kwa jina lako."
20231101.sw_2109_18
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
15 Lakini Bwana akamwambia, "Nenda tu, kwa maana nimemchagua awe chombo changu, alitangaze jina langu kwa mataifa na wafalme wao na kwa watu wa Israeli.
20231101.sw_2109_19
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
17 Basi, Anania akaenda, akaingia katika hiyo nyumba. Kisha akaweka mikono yake juu ya Saulo, akasema, "Ndugu Saulo, Bwana ambaye ndiye Yesu mwenyewe aliyekutokea ulipokuwa njiani kuja hapa, amenituma ili upate kuona tena na kujazwa Roho Mtakatifu."
20231101.sw_2109_20
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
18 Mara vitu kama magamba vikaanguka kutoka macho ya Saulo, akaweza kuona tena. Akasimama, akabatizwa.
20231101.sw_2109_21
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
19 Na baada ya kula chakula, nguvu zake zikamrudia. Saulo alikaa siku chache pamoja na wafuasi huko Damasko.
20231101.sw_2109_22
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
21 Watu wote waliomsikia walishangaa, wakasema, "Je, mtu huyu si yuleyule aliyewaua wale waliokuwa wanaomba kwa jina hili kule Yerusalemu? Tena alikuja hapa akiwa na madhumuni ya kuwatia nguvuni watu hao na kuwapeleka kwa makuhani!"
20231101.sw_2109_23
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
22 Saulo alizidi kupata nguvu, na kwa jinsi alivyothibitisha wazi kwamba Yesu ndiye Kristo, Wayahudi wa huko Damasko walivurugika kabisa.
20231101.sw_2109_24
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
2 Waliposikia akiongea nao kwa Kiebrania wakazidi kukaa kimya zaidi kuliko hapo awali. Naye Paulo akaendelea kusema,
20231101.sw_2109_25
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
3 "Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia. Lakini nililelewa papa hapa mjini Yerusalemu chini ya mkufunzi Gamalieli. Nilifundishwa kufuata kwa uthabiti Sheria ya wazee wetu. Nilijitolea kwa moyo wote kwa Mungu kama ninyi wenyewe mlivyo hivi leo.
20231101.sw_2109_26
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
4 Niliwatesa hata kuwaua wale watu waliofuata Njia hii. Niliwatia nguvuni wanaume kwa wanawake na kuwafunga gerezani.
20231101.sw_2109_27
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
5 Kuhani Mkuu na baraza lote la wazee wanaweza kushuhudia jambo hilo. Kutoka kwao nilipokea barua walioandikiwa wale ndugu Wayahudi waliokuwa huko Damasko. Nilikwenda Damasko ili niwatie nguvuni watu hao na kuwaleta wamefungwa mpaka Yerusalemu ili waadhibiwe.
20231101.sw_2109_28
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
6 "Basi, nilipokuwa njiani karibu kufika Damasko, yapata saa sita mchana, mwangu mkubwa kutoka mbinguni ulitokea ghafla ukaniangazia pande zote.
20231101.sw_2109_29
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
8 Nami nikauliza: `Nani wewe, Bwana?` Naye akaniambia: `Mimi ni Yesu wa Nazareti ambaye wewe unamtesa.`
20231101.sw_2109_30
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
10 Basi, mimi nikauliza: `Nifanye nini Bwana?` Naye Bwana akaniambia: `Simama, nenda Damasko na huko utaambiwa yote ambayo umepangiwa kufanya.`
20231101.sw_2109_31
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
11 Kutokana na ule mwanga mkali sikuweza kuona na hivyo iliwabidi wale wenzangu kuniongoza kwa kunishika mkono mpaka nikafika Damasko.
20231101.sw_2109_32
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
12 "Huko kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Anania, mtu mcha Mungu, mwenye kuitii Sheria yetu na aliyeheshimika sana mbele ya Wayahudi waliokuwa wanaishi Damasko.
20231101.sw_2109_33
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
13 Yeye alikuja kuniona, akasimama karibu nami, akasema: `Ndugu Saulo! Ona tena.` Papo hapo nikaona tena, nikamwangalia.
20231101.sw_2109_34
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
14 Halafu Anania akasema: `Mungu wa babu zetu amekuchagua upate kujua matakwa yake na kumwona yule mtumishi wake mwadilifu na kumsikia yeye mwenyewe akiongea.
20231101.sw_2109_35
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
16 Sasa basi, ya nini kukawia zaidi? Simama ubatizwe na uondolewe dhambi zako kwa kuliungama jina lake.`
20231101.sw_2109_36
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
18 Nilimwona Bwana akiniambia: `Haraka! Ondoka Yerusalemu upesi kwa maana watu wa hapa binadamu hawataukubali ushuhuda wako juu yangu.`
20231101.sw_2109_37
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
19 Nami nikamjibu: `Bwana, wao wanajua wazi kwamba mimi ni yule aliyekuwa anapitapita katika masunagogi na kuwatia nguvuni na kuwapiga wale waliokuwa wanakuamini.
20231101.sw_2109_38
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
20 Na kwamba wakati shahidi wako Stefano alipouawa, mimi binafsi nilikuwako pale nikakubaliana na kitendo hicho na kuyalinda makoti ya wale waliokuwa wanamuua.`
20231101.sw_2109_39
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Baada ya kufanya utume katika mazingira ya Kiarabu, Tarsus na Antiokia alianza safari za kitume, akienda mbali zaidi na zaidi, akilenga kumhubiri Yesu mahali ambapo bado hajafahamika, hata Hispania.
20231101.sw_2109_40
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Ilikuwa kawaida yake kuanzisha makanisa katika miji mikubwa ili toka huko ujumbe ufike hadi vijijini.
20231101.sw_2109_41
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Muda wote wa utume wake Paulo alipambana na dhuluma kutoka kwa Wayahudi wenzake na matatizo mengine kutoka Wakristo wenye msimamo tofauti na wa kwake, hasa Wakristo wa Kiyahudi juu ya haja ya kufuata masharti ya Agano la Kale ili kupata wokovu.
20231101.sw_2109_42
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Hatimaye alikamatwa na wapinzani wake Wayahudi mjini Yerusalemu, lakini askari wakoloni walizuia asiuawe.
20231101.sw_2109_43
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Baada ya hapo alilazimika kukaa gerezani akisubiri hukumu ya Dola la Roma, kwanza Kaisaria Baharini miaka miwili, halafu akakata rufaa kwa Kaisari akapelekwa Roma, alipofika mwaka 61 akakaa miaka miwili tena kifungo cha nje katika nyumba ya kupanga.
20231101.sw_2109_44
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Kisha kufunguliwa (labda kwa sababu washtaki wake hawakuwasili) alisafiri tena ingawa hakuna hakika alielekea wapi.
20231101.sw_2109_45
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Aliuawa nje ya kuta za Roma kwa kukatwa kichwa wakati wa dhuluma za Nero kati ya mwaka 64 na 67 B.K.
20231101.sw_2109_46
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Juu ya kaburi lake lilijengwa kanisa kubwa ambalo liliteketea kwa moto katika karne ya 18 likajengwa upya na hadi leo linapokea hija za Wakristo wengi, hasa katika "Jubilei ya mtume Paulo" iliyotangazwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kwa mwaka 2008/2009.
20231101.sw_2109_47
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Kati ya barua nyingi alizoandika (kwa makanisa ya Thesalonike, Korintho, Galatia, Roma, Filipi, Kolosai, Efeso, kwa viongozi Wakristo kama Timotheo na Tito, tena kwa Filemoni), katika Agano Jipya zinatunzwa 13.
20231101.sw_2109_48
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Ukubwa na ubora wa mchango wa Paulo unaeleweka tukizingatia kwamba alifanya kazi na kuandika kabla ya vitabu vya Agano Jipya kupatikana. Ndiye aliyeanza kuliandika akipanua mawazo aliyoyapokea katika Kanisa kwa kuzingatia Agano la Kale na mafunuo na mang’amuzi yake mwenyewe.
20231101.sw_2109_49
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Hapo alifafanua vizuri ajabu maisha ya Kikristo kama neema ya kumshiriki Yesu kwa imani, sakramenti na juhudi za kushinda umimi hadi kugeuka sadaka hai, takatifu na ya kumpendeza Mungu.
20231101.sw_2109_50
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Wokovu huo, utakaokamilika katika ufufuko wa mwili, unapatikana katika Kanisa, ambalo Paulo alilitambulisha kama bibiarusi wa Kristo na mwili wake.
20231101.sw_2109_51
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Brown, Raymond E. An Introduction to the New Testament. Anchor Bible Series, 1997. ISBN 0-385-24767-2.
20231101.sw_2109_52
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Conzelmann, Hans, the Acts of the Apostles—a Commentary on the Acts of the Apostles (Augsburg Fortress 1987)
20231101.sw_2109_53
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Davies, W. D. "The Apostolic Age and the Life of Paul" in Matthew Black, ed. Peake's Commentary on the Bible. London: T. Nelson, 1962. ISBN 0-8407-5019-6
20231101.sw_2109_54
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Davies, W. D. Paul and Rabbinic Judaism: Some Rabbinic Elements in Pauline Theology. S.P.C.K., 3rd ed., 1970. ISBN 0-281-02449-9
20231101.sw_2109_55
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Dunn, James D.G., 1990, Jesus, Paul and the Law Louisville,KY: Westminster John Knox Press. ISBN 0-664-25095-5
20231101.sw_2109_56
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Holzbach, Mathis Christian, Die textpragmat. Bedeutung d. Kündereinsetzungen d. Simon Petrus u.d. Saulus Paulus im lukan. Doppelwerk, in: Jesus als Bote d. Heils. Stuttgart 2008, 166-172.
20231101.sw_2109_57
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Maccoby, Hyam. The Mythmaker: Paul and the Invention of Christianity. New York: Harper & Row, 1986. ISBN 0-06-015582-5.
20231101.sw_2109_58
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Kim, Yung Suk. A Theological Introduction to Paul's Letters. Eugene, Oregon: Cascade Books, 2011. ISBN 978-1-60899-793-0
20231101.sw_2109_59
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
MacDonald, Dennis Ronald, 1983. The Legend and the Apostle: The Battle for Paul in Story and Canon Philadelphia: Westminster Press.
20231101.sw_2109_60
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Murphy-O'Connor, Jerome, Jesus and Paul: Parallel lives (Collegeville, Minn.: Liturgical Press, 2007) ISBN 0-8146-5173-9
20231101.sw_2109_61
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Murphy-O'Connor, Jerome, Paul the Letter-Writer: His World, His Options, His Skills (Collegeville, Minn.: Liturgical Press, 1995) ISBN 0-8146-5845-8
20231101.sw_2109_62
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Ogg, George. “Chronology of the New Testament.” Matthew Black, ed. ‘’Peake's Commentary on the Bible.’’ Nelson, 1962. ISBN 0-8407-5019-6
20231101.sw_2109_63
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Segal, Alan F. Paul, the Convert, (New Haven/London, Yale University Press, 1990) ISBN 0-300-04527-1.
20231101.sw_2109_64
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Segal, Alan F., "Paul, the Convert and Apostle" in Rebecca's Children: Judaism and Christianity in the Roman World (Harvard University Press 1986).
20231101.sw_2109_65
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Horrell, David G. "An Introduction to the Study of Paul." T&T Clark Approaches to Biblical Studies. 2nd edition. London: T&T Clark, 2006
20231101.sw_2109_66
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Bart D Ehrman. Peter, Paul and Mary Magdalene: The Followers of Jesus in History and Legend; 304 pages, Oxford University Press (Machi 2008)
20231101.sw_2109_67
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Bart D. Ehrman. The New Testament: A Historical Introduction to the Early Christian Writings; 608 pages, Oxford University Press (Julai 2011); ISBN 978-0-19-975753-4
20231101.sw_2109_68
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Hyam MacCoby. The Mythmaker: Paul and the Invention of Christianity; 238 pages, Barnes & Noble Books (1998); ISBN 978-0-7607-0787-6
20231101.sw_2109_69
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Hans Joachim Schoeps. Paul: The Theology of the Apostle in the Light of Jewish Religious History (Library of Theological Translations); 34 pages, Lutterworth Press (Julai 2002); ISBN 978-0-227-17013-7
20231101.sw_2109_70
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Pinchas Lapide, Peter Stuhlmacher. Paul: Rabbi and Apostle; 77 pages, Augsburg Publishing House; (Desemba 1984)
20231101.sw_2109_71
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
Mtakatifu Paulo
Pinchas Lapide, Leonard Swidler, Jurgen Moltmann. Jewish Monotheism and Christian Trinitarian Doctrine; 94 pages, Wipf & Stock Publishers (Mei 2002)
20231101.sw_2116_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Baada ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo (kifupi: BK) ni namna ya kutaja miaka ambayo imekuwa njia ya kuhesabu miaka inayotumika zaidi duniani.
20231101.sw_2116_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Kila mwaka huhesabiwa kuanzia ule uliodhaniwa kuwa mwaka wa kuzaliwa kwake Yesu Kristo. Miaka iliyotangulia kuzaliwa kwake Yesu huitwa Kabla ya Kuzaliwa kwake Yesu Kristo au kifupi: KK.
20231101.sw_2116_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Wakati ule mahesabu mbalimbali ya miaka yalikuwa kawaida. Mwaka uleule uliweza kuitwa kutokana na muda wa utawala wa Mfalme au Kaisari (kwa mfano: mwaka wa 5 wa Kaisari Iustiniano) na pia kuanzia tarehe ya kuundwa kwa mji wa Roma (kwa mfano: mwaka 1185 ab Urbe Condita = tangu kuanzishwa kwa mji).
20231101.sw_2116_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Mahesabu mengine yaliyokuwa kawaida wakati ule ni makadirio mbalimbali "tangu kuumbwa kwa dunia" na mengineyo.
20231101.sw_2116_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Hesabu yake haijui mwaka "0"; tarehe ya kuzaliwa kwake Yesu huchukuliwa kama mwanzo wa mwaka. Kwa hiyo moja kwa moja inaingia katika mwaka "1" na mwaka kabla yake ni mwaka 1 kabla ya Kristo = KK.
20231101.sw_2116_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Hii ndiyo sababu ya kwamba dunia karibu yote ilikosa kusheherekea mwaka 2000 kuwa mwanzo wa milenia mpya. Mwaka 2000 ulikuwa mwaka wa mwisho wa karne iliyoanza mwaka 1901; karne na milenia mpya zilianza mwaka 2001.
20231101.sw_2116_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Hesabu ya Dionysio ilikosea miaka kadhaa. Ni kwa sababu wakati wake Dola la Roma lilikuwa limeshakwisha katika Italia, Kaisari alikaa Bizanti au Roma ya Mashariki. Kumbukumbu za Roma yenyewe hazikutunzwa tangu miaka mingi.
20231101.sw_2116_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Leo hii wataalamu wengi hukubaliana ya kwamba kasoro Ya Dionysio ni takriban miaka 4 - 8; yaani mwaka halisi wa kuzaliwa kwake Yesu ulikuwa kama miaka nne hadi nane kabla ya mwaka ambao tumezoea kuhesabu kama "1", kwa kuwa mwaka 4 K.K. ndipo alipokufa mfalme Herode Mkuu aliyejaribu kumuua akiwa mtoto mchanga.
20231101.sw_2116_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Wengi walijaribu kusahihisha kosa hilo lakini habari kamili kabisa haziwezi kupatikana, tena ni vigumu kubadilisha mahesabu yote, vitabu n.k.
20231101.sw_2116_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Mwanzoni hesabu ya Dionysio ilikuwa pendekezo la mtaalamu fulani tu, watu wakiendelea kutumia mahesabu yao mbalimbali.
20231101.sw_2116_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Miaka 60 baada ya Dionysio, Papa Bonifas IV, akiwa mkuu wa Kanisa Katoliki, alitumia tarehe zote mbili za "baada ya Kristo" na "tangu kuanzishwa kwa mji". Wataalamu walianza kutumia zaidi hesabu hiyo mpya.
20231101.sw_2116_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Mnamo mwaka 725 mtaalamu Beda Mheshimiwa alitunga kitabu "Kuhusu ugawaji wa wakati" (kwa Kilatini De Temporum Ratione) alikotumia mfumo ulioundwa na Dionysio akaendelea kuutumia pia katika kitabu kuhusu "Historia ya Kanisa". Kwa kuwa vitabu vya Beda vilikuja kutumiwa kote katika Ulaya ya Magharibi, vilichangia sana uenezi wa hesabu hiyo mpya.
20231101.sw_2116_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Wakati wa Karolo Mkuu, Mfalme (halafu Kaisari) aliyetawala Ufaransa pamoja na Ujerumani, Italia ya Kaskazini na maeneo ya Uholanzi na Ubelgiji, hesabu tangu Kristo ilikuwa rasmi kwa serikali.
20231101.sw_2116_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Kutokana na uenezaji wa uchumi, biashara na utawala wa Wazungu, hesabu "Baada ya Kristo" ilienea kote duniani.
20231101.sw_2116_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Siku hizi ni hesabu pekee katika nchi nyingi. Katika nchi mbalimbali inatumika sambamba na mahesabu mengine.
20231101.sw_2116_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Nchi mbalimbali za Kiislamu hutumia miaka tangu Hijra ya Muhammad (mwaka 622 BK), lakini mara nyingi pamoja na miaka ya hesabu ya Kikristo kwa ajili ya mambo ya biashara na mawasiliano ya kimataifa.
20231101.sw_2116_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Nchi ya Israeli inatumia kalenda rasmi tangu "kuumbwa kwa dunia", isipokuwa kando ya Kalenda ya BK kwa sababu zilizotajwa hapo juu kwa ajili ya nchi za Kiislamu.
20231101.sw_2116_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Dionysio hakutumia msamiati "baada ya Kristo" - alisema "Anno Domini" ("mwaka wa Bwana") akimaanisha Dominus = Bwana ndiye Yesu. Hivyo kifupi katika lugha ya Kilatini ni "AD" kilichoingia pia katika Kiingereza na lugha nyingine kadhaa.
20231101.sw_2116_18
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
Baada ya Kristo
Hata miaka kabla ya Kristo kwa Kiingereza huitwa kwa kifupi cha Kilatini "a. Chr" (ante Christum natum = kabla ya kuzaliwa kwake Kristo). Wengine hutumia "BC" = "before Christ".
20231101.sw_2117_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Milenia
Milenia
Milenia (kutoka neno la Kiingereza millennium, ambalo mizizi yake ni katika Kilatini: mille, elfu, na annus, mwaka) ni kipindi cha miaka elfu moja.
20231101.sw_2117_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Milenia
Milenia
Kwa sasa tuko katika milenia ya pili BK iliyoanza tarehe 1 Januari 2001. Lakini watu wengi walisheherekea tarehe 1 Januari 2000 ingawa mwaka 2000 ilikuwa mwaka wa mwisho wa karne na milenia iliyotangulia.
20231101.sw_2118_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
Kaizari
Kaizari ni cheo cha mfalme mkuu. Neno la Kiswahili limetokana na lugha ya Kijerumani "Kaiser", lakini asili yake ni Kilatini "Caesar".
20231101.sw_2118_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
Kaizari
Asili ya cheo ni Julius Caesar aliyekuwa kiongozi wa Dola la Roma hadi kuuawa kwake na wapinzani mwaka 44 KK.
20231101.sw_2118_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
Kaizari
Cheo cha Kaizari kiliendelea kutumika katika eneo la Dola la Roma ya Mashariki (Bizanti) hadi mwaka 1453.
20231101.sw_2118_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
Kaizari
Katika Ulaya yenyewe mfalme wa Wafaranki Karolo Mkuu alipokea cheo cha "Caesar" au Kaizari. Baadaye wafalme Wajerumani waliomfuata Karolo Mkuu katika sehemu ya mashariki ya ufalme wake waliendelea kutumia cheo hiki cha Caesar au Kaizari.
20231101.sw_2118_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
Kaizari
Neno la Kaizari liliingia katika lugha ya Kiswahili wakati wa ukoloni wa Kijerumani huko Tanzania, kwa kuwa Austria na Ujerumani zilitawaliwa hadi mwisho wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia 1918 na wafalme wenye cheo cha "Kaizari".
20231101.sw_2118_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
Kaizari
Vilevile mfalme wa Urusi alikuwa na cheo kilekile kilichoitwa "Tsar" kwa Kirusi, ilhali neno hili limeundwa pia kutoka "Caesar".
20231101.sw_2118_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
Kaizari
Lugha za Kiingereza na Kifaransa zilitumia cheo tofauti cha macaesar wa Kiroma, ndicho "Imperator" (= mwenye amri, mwenye mamlaka, jemadari) kilichokuwa "Emperor" kwa Kiingereza au "Empereur" kwa Kifaransa.
20231101.sw_2118_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
Kaizari
Kaizari ni cheo cha mfalme aliye juu ya wafalme wengine. Kutokana na uzoefu huu hata Shah wa Uajemi, Tenno wa Japani, Huangdi wa China na Negus Negesti wa Ethiopia hutajwa kwa cheo cha "Kaizari".
20231101.sw_2118_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
Kaizari
Malkia Viktoria wa Uingereza alitumia cheo cha Kaizari ("empress") kama mtawala wa Uhindi tangu mwaka 1877.
20231101.sw_2118_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
Kaizari
Wakati wa ukoloni mtawala mkuu wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani alikuwa Kaizari Wilhelm II wa Ujerumani; kwenye sarafu ya rupia alionyeshwa pamoja cheo kwa lugha ya Kilatini "imperator".
20231101.sw_2118_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
Kaizari
Rais Jean-Bedel Bokassa alijitangaza kuwa Kaizari ("empereur") wa Afrika ya Kati mwaka 1977 akiiga mfano wa Napoleon Bonaparte aliyejiwekea taji la Kaizari ya Ufaransa mwaka 1804. Bokassa alipinduliwa mwaka 1979 na nchi kuwa jamhuri tena.
20231101.sw_2119_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Duma
Duma
Duma ni mnyama mbuai aliyemo katika jamii ya paka (Felinae) ambaye hupatikana Afrika na kidogo sehemu za Asia. Chakula chake ni wanyama jamii ya swala .