_id
stringlengths 15
22
| url
stringlengths 31
150
| title
stringlengths 1
86
| text
stringlengths 100
23.8k
|
---|---|---|---|
20231101.sw_2109_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Akishika dini yake kwa msimamo mkali akawa anapinga Ukristo kwa kukamata, kutesa na hata kuua Wakristo, kama vile Stefano Mfiadini.
|
20231101.sw_2109_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Alifanya hivyo mpaka alipotokewa na Yesu Kristo mfufuka akiwa njiani kwenda Damaski, Syria (kwa umuhimu wake katika Historia ya Wokovu habari hii inasimuliwa mara tatu katika kitabu cha Matendo ya Mitume: 9:1-19; 21:12-18 na 22:5-16). Jibu lake kwa Yesu lilikuwa (Mdo 22:10): "Nifanye nini, Bwana?"
|
20231101.sw_2109_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
1 Wakati huo Saulo alikuwa akizidisha vitisho vikali vya kuwaua wafuasi wa Bwana. Alikwenda kwa Kuhani Mkuu,
|
20231101.sw_2109_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
2 akaomba apatiwe barua za utambulisho kwa masunagogi ya Kiyahudi kule Damasko, ili akikuta huko wanaume au wanawake wanaofuata Njia ya Bwana, awakamate na kuwaleta Yerusalemu.
|
20231101.sw_2109_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
3 Lakini alipokuwa njiani karibu kufika Damasko, ghafla mwanga kutoka angani ulimwangazia pande zote.
|
20231101.sw_2109_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
5 Naye Saulo akauliza, "Ni nani wewe Bwana?" Na ile sauti ikajibu, "Mimi ni Yesu ambaye wewe unamtesa.
|
20231101.sw_2109_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
7 Wale watu waliokuwa wanasafiri pamoja na Saulo walisimama pale, wakiwa hawana la kusema; walisikia ile sauti lakini hawakumwona mtu.
|
20231101.sw_2109_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
8 Saulo aliinuka, na alipofumbua macho yake hakuweza kuona chochote; hivyo wale watu wakamwongoza kwa kumshika mkono mpaka mjini Damasko.
|
20231101.sw_2109_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
10 Basi, huko Damasko kulikuwa na mfuasi mmoja aitwaye Anania. Bwana akamwambia katika maono, "Anania!" Anania akaitika, "Niko hapa, Bwana."
|
20231101.sw_2109_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
11 Naye Bwana akamwambia, "Jitayarishe uende kwenye barabara inayoitwa Barabara ya Moja kwa Moja, na katika nyumba ya Yuda umtake mtu mmoja kutoka Tarso aitwaye Saulo. Sasa anasali;
|
20231101.sw_2109_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
12 na katika maono ameona mtu aitwaye Anania akiingia ndani na kumwekea mikono ili apate kuona tena."
|
20231101.sw_2109_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
13 Lakini Anania akajibu, "Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kutoka kwa watu wengi; nimesikia juu ya mabaya aliyowatendea watu wako huko Yerusalemu.
|
20231101.sw_2109_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
14 Na amekuja hapa akiwa na mamlaka kutoka kwa makuhani wakuu kuwatia nguvuni wote wanaoomba kwa jina lako."
|
20231101.sw_2109_18
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
15 Lakini Bwana akamwambia, "Nenda tu, kwa maana nimemchagua awe chombo changu, alitangaze jina langu kwa mataifa na wafalme wao na kwa watu wa Israeli.
|
20231101.sw_2109_19
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
17 Basi, Anania akaenda, akaingia katika hiyo nyumba. Kisha akaweka mikono yake juu ya Saulo, akasema, "Ndugu Saulo, Bwana ambaye ndiye Yesu mwenyewe aliyekutokea ulipokuwa njiani kuja hapa, amenituma ili upate kuona tena na kujazwa Roho Mtakatifu."
|
20231101.sw_2109_20
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
18 Mara vitu kama magamba vikaanguka kutoka macho ya Saulo, akaweza kuona tena. Akasimama, akabatizwa.
|
20231101.sw_2109_21
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
19 Na baada ya kula chakula, nguvu zake zikamrudia. Saulo alikaa siku chache pamoja na wafuasi huko Damasko.
|
20231101.sw_2109_22
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
21 Watu wote waliomsikia walishangaa, wakasema, "Je, mtu huyu si yuleyule aliyewaua wale waliokuwa wanaomba kwa jina hili kule Yerusalemu? Tena alikuja hapa akiwa na madhumuni ya kuwatia nguvuni watu hao na kuwapeleka kwa makuhani!"
|
20231101.sw_2109_23
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
22 Saulo alizidi kupata nguvu, na kwa jinsi alivyothibitisha wazi kwamba Yesu ndiye Kristo, Wayahudi wa huko Damasko walivurugika kabisa.
|
20231101.sw_2109_24
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
2 Waliposikia akiongea nao kwa Kiebrania wakazidi kukaa kimya zaidi kuliko hapo awali. Naye Paulo akaendelea kusema,
|
20231101.sw_2109_25
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
3 "Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia. Lakini nililelewa papa hapa mjini Yerusalemu chini ya mkufunzi Gamalieli. Nilifundishwa kufuata kwa uthabiti Sheria ya wazee wetu. Nilijitolea kwa moyo wote kwa Mungu kama ninyi wenyewe mlivyo hivi leo.
|
20231101.sw_2109_26
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
4 Niliwatesa hata kuwaua wale watu waliofuata Njia hii. Niliwatia nguvuni wanaume kwa wanawake na kuwafunga gerezani.
|
20231101.sw_2109_27
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
5 Kuhani Mkuu na baraza lote la wazee wanaweza kushuhudia jambo hilo. Kutoka kwao nilipokea barua walioandikiwa wale ndugu Wayahudi waliokuwa huko Damasko. Nilikwenda Damasko ili niwatie nguvuni watu hao na kuwaleta wamefungwa mpaka Yerusalemu ili waadhibiwe.
|
20231101.sw_2109_28
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
6 "Basi, nilipokuwa njiani karibu kufika Damasko, yapata saa sita mchana, mwangu mkubwa kutoka mbinguni ulitokea ghafla ukaniangazia pande zote.
|
20231101.sw_2109_29
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
8 Nami nikauliza: `Nani wewe, Bwana?` Naye akaniambia: `Mimi ni Yesu wa Nazareti ambaye wewe unamtesa.`
|
20231101.sw_2109_30
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
10 Basi, mimi nikauliza: `Nifanye nini Bwana?` Naye Bwana akaniambia: `Simama, nenda Damasko na huko utaambiwa yote ambayo umepangiwa kufanya.`
|
20231101.sw_2109_31
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
11 Kutokana na ule mwanga mkali sikuweza kuona na hivyo iliwabidi wale wenzangu kuniongoza kwa kunishika mkono mpaka nikafika Damasko.
|
20231101.sw_2109_32
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
12 "Huko kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Anania, mtu mcha Mungu, mwenye kuitii Sheria yetu na aliyeheshimika sana mbele ya Wayahudi waliokuwa wanaishi Damasko.
|
20231101.sw_2109_33
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
13 Yeye alikuja kuniona, akasimama karibu nami, akasema: `Ndugu Saulo! Ona tena.` Papo hapo nikaona tena, nikamwangalia.
|
20231101.sw_2109_34
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
14 Halafu Anania akasema: `Mungu wa babu zetu amekuchagua upate kujua matakwa yake na kumwona yule mtumishi wake mwadilifu na kumsikia yeye mwenyewe akiongea.
|
20231101.sw_2109_35
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
16 Sasa basi, ya nini kukawia zaidi? Simama ubatizwe na uondolewe dhambi zako kwa kuliungama jina lake.`
|
20231101.sw_2109_36
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
18 Nilimwona Bwana akiniambia: `Haraka! Ondoka Yerusalemu upesi kwa maana watu wa hapa binadamu hawataukubali ushuhuda wako juu yangu.`
|
20231101.sw_2109_37
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
19 Nami nikamjibu: `Bwana, wao wanajua wazi kwamba mimi ni yule aliyekuwa anapitapita katika masunagogi na kuwatia nguvuni na kuwapiga wale waliokuwa wanakuamini.
|
20231101.sw_2109_38
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
20 Na kwamba wakati shahidi wako Stefano alipouawa, mimi binafsi nilikuwako pale nikakubaliana na kitendo hicho na kuyalinda makoti ya wale waliokuwa wanamuua.`
|
20231101.sw_2109_39
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Baada ya kufanya utume katika mazingira ya Kiarabu, Tarsus na Antiokia alianza safari za kitume, akienda mbali zaidi na zaidi, akilenga kumhubiri Yesu mahali ambapo bado hajafahamika, hata Hispania.
|
20231101.sw_2109_40
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Ilikuwa kawaida yake kuanzisha makanisa katika miji mikubwa ili toka huko ujumbe ufike hadi vijijini.
|
20231101.sw_2109_41
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Muda wote wa utume wake Paulo alipambana na dhuluma kutoka kwa Wayahudi wenzake na matatizo mengine kutoka Wakristo wenye msimamo tofauti na wa kwake, hasa Wakristo wa Kiyahudi juu ya haja ya kufuata masharti ya Agano la Kale ili kupata wokovu.
|
20231101.sw_2109_42
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Hatimaye alikamatwa na wapinzani wake Wayahudi mjini Yerusalemu, lakini askari wakoloni walizuia asiuawe.
|
20231101.sw_2109_43
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Baada ya hapo alilazimika kukaa gerezani akisubiri hukumu ya Dola la Roma, kwanza Kaisaria Baharini miaka miwili, halafu akakata rufaa kwa Kaisari akapelekwa Roma, alipofika mwaka 61 akakaa miaka miwili tena kifungo cha nje katika nyumba ya kupanga.
|
20231101.sw_2109_44
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Kisha kufunguliwa (labda kwa sababu washtaki wake hawakuwasili) alisafiri tena ingawa hakuna hakika alielekea wapi.
|
20231101.sw_2109_45
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Aliuawa nje ya kuta za Roma kwa kukatwa kichwa wakati wa dhuluma za Nero kati ya mwaka 64 na 67 B.K.
|
20231101.sw_2109_46
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Juu ya kaburi lake lilijengwa kanisa kubwa ambalo liliteketea kwa moto katika karne ya 18 likajengwa upya na hadi leo linapokea hija za Wakristo wengi, hasa katika "Jubilei ya mtume Paulo" iliyotangazwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kwa mwaka 2008/2009.
|
20231101.sw_2109_47
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Kati ya barua nyingi alizoandika (kwa makanisa ya Thesalonike, Korintho, Galatia, Roma, Filipi, Kolosai, Efeso, kwa viongozi Wakristo kama Timotheo na Tito, tena kwa Filemoni), katika Agano Jipya zinatunzwa 13.
|
20231101.sw_2109_48
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Ukubwa na ubora wa mchango wa Paulo unaeleweka tukizingatia kwamba alifanya kazi na kuandika kabla ya vitabu vya Agano Jipya kupatikana. Ndiye aliyeanza kuliandika akipanua mawazo aliyoyapokea katika Kanisa kwa kuzingatia Agano la Kale na mafunuo na mang’amuzi yake mwenyewe.
|
20231101.sw_2109_49
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Hapo alifafanua vizuri ajabu maisha ya Kikristo kama neema ya kumshiriki Yesu kwa imani, sakramenti na juhudi za kushinda umimi hadi kugeuka sadaka hai, takatifu na ya kumpendeza Mungu.
|
20231101.sw_2109_50
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Wokovu huo, utakaokamilika katika ufufuko wa mwili, unapatikana katika Kanisa, ambalo Paulo alilitambulisha kama bibiarusi wa Kristo na mwili wake.
|
20231101.sw_2109_51
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Brown, Raymond E. An Introduction to the New Testament. Anchor Bible Series, 1997. ISBN 0-385-24767-2.
|
20231101.sw_2109_52
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Conzelmann, Hans, the Acts of the Apostles—a Commentary on the Acts of the Apostles (Augsburg Fortress 1987)
|
20231101.sw_2109_53
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Davies, W. D. "The Apostolic Age and the Life of Paul" in Matthew Black, ed. Peake's Commentary on the Bible. London: T. Nelson, 1962. ISBN 0-8407-5019-6
|
20231101.sw_2109_54
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Davies, W. D. Paul and Rabbinic Judaism: Some Rabbinic Elements in Pauline Theology. S.P.C.K., 3rd ed., 1970. ISBN 0-281-02449-9
|
20231101.sw_2109_55
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Dunn, James D.G., 1990, Jesus, Paul and the Law Louisville,KY: Westminster John Knox Press. ISBN 0-664-25095-5
|
20231101.sw_2109_56
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Holzbach, Mathis Christian, Die textpragmat. Bedeutung d. Kündereinsetzungen d. Simon Petrus u.d. Saulus Paulus im lukan. Doppelwerk, in: Jesus als Bote d. Heils. Stuttgart 2008, 166-172.
|
20231101.sw_2109_57
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Maccoby, Hyam. The Mythmaker: Paul and the Invention of Christianity. New York: Harper & Row, 1986. ISBN 0-06-015582-5.
|
20231101.sw_2109_58
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Kim, Yung Suk. A Theological Introduction to Paul's Letters. Eugene, Oregon: Cascade Books, 2011. ISBN 978-1-60899-793-0
|
20231101.sw_2109_59
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
MacDonald, Dennis Ronald, 1983. The Legend and the Apostle: The Battle for Paul in Story and Canon Philadelphia: Westminster Press.
|
20231101.sw_2109_60
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Murphy-O'Connor, Jerome, Jesus and Paul: Parallel lives (Collegeville, Minn.: Liturgical Press, 2007) ISBN 0-8146-5173-9
|
20231101.sw_2109_61
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Murphy-O'Connor, Jerome, Paul the Letter-Writer: His World, His Options, His Skills (Collegeville, Minn.: Liturgical Press, 1995) ISBN 0-8146-5845-8
|
20231101.sw_2109_62
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Ogg, George. “Chronology of the New Testament.” Matthew Black, ed. ‘’Peake's Commentary on the Bible.’’ Nelson, 1962. ISBN 0-8407-5019-6
|
20231101.sw_2109_63
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Segal, Alan F. Paul, the Convert, (New Haven/London, Yale University Press, 1990) ISBN 0-300-04527-1.
|
20231101.sw_2109_64
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Segal, Alan F., "Paul, the Convert and Apostle" in Rebecca's Children: Judaism and Christianity in the Roman World (Harvard University Press 1986).
|
20231101.sw_2109_65
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Horrell, David G. "An Introduction to the Study of Paul." T&T Clark Approaches to Biblical Studies. 2nd edition. London: T&T Clark, 2006
|
20231101.sw_2109_66
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Bart D Ehrman. Peter, Paul and Mary Magdalene: The Followers of Jesus in History and Legend; 304 pages, Oxford University Press (Machi 2008)
|
20231101.sw_2109_67
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Bart D. Ehrman. The New Testament: A Historical Introduction to the Early Christian Writings; 608 pages, Oxford University Press (Julai 2011); ISBN 978-0-19-975753-4
|
20231101.sw_2109_68
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Hyam MacCoby. The Mythmaker: Paul and the Invention of Christianity; 238 pages, Barnes & Noble Books (1998); ISBN 978-0-7607-0787-6
|
20231101.sw_2109_69
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Hans Joachim Schoeps. Paul: The Theology of the Apostle in the Light of Jewish Religious History (Library of Theological Translations); 34 pages, Lutterworth Press (Julai 2002); ISBN 978-0-227-17013-7
|
20231101.sw_2109_70
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Pinchas Lapide, Peter Stuhlmacher. Paul: Rabbi and Apostle; 77 pages, Augsburg Publishing House; (Desemba 1984)
|
20231101.sw_2109_71
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtakatifu%20Paulo
|
Mtakatifu Paulo
|
Pinchas Lapide, Leonard Swidler, Jurgen Moltmann. Jewish Monotheism and Christian Trinitarian Doctrine; 94 pages, Wipf & Stock Publishers (Mei 2002)
|
20231101.sw_2116_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Baada ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo (kifupi: BK) ni namna ya kutaja miaka ambayo imekuwa njia ya kuhesabu miaka inayotumika zaidi duniani.
|
20231101.sw_2116_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Kila mwaka huhesabiwa kuanzia ule uliodhaniwa kuwa mwaka wa kuzaliwa kwake Yesu Kristo. Miaka iliyotangulia kuzaliwa kwake Yesu huitwa Kabla ya Kuzaliwa kwake Yesu Kristo au kifupi: KK.
|
20231101.sw_2116_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Wakati ule mahesabu mbalimbali ya miaka yalikuwa kawaida. Mwaka uleule uliweza kuitwa kutokana na muda wa utawala wa Mfalme au Kaisari (kwa mfano: mwaka wa 5 wa Kaisari Iustiniano) na pia kuanzia tarehe ya kuundwa kwa mji wa Roma (kwa mfano: mwaka 1185 ab Urbe Condita = tangu kuanzishwa kwa mji).
|
20231101.sw_2116_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Mahesabu mengine yaliyokuwa kawaida wakati ule ni makadirio mbalimbali "tangu kuumbwa kwa dunia" na mengineyo.
|
20231101.sw_2116_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Hesabu yake haijui mwaka "0"; tarehe ya kuzaliwa kwake Yesu huchukuliwa kama mwanzo wa mwaka. Kwa hiyo moja kwa moja inaingia katika mwaka "1" na mwaka kabla yake ni mwaka 1 kabla ya Kristo = KK.
|
20231101.sw_2116_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Hii ndiyo sababu ya kwamba dunia karibu yote ilikosa kusheherekea mwaka 2000 kuwa mwanzo wa milenia mpya. Mwaka 2000 ulikuwa mwaka wa mwisho wa karne iliyoanza mwaka 1901; karne na milenia mpya zilianza mwaka 2001.
|
20231101.sw_2116_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Hesabu ya Dionysio ilikosea miaka kadhaa. Ni kwa sababu wakati wake Dola la Roma lilikuwa limeshakwisha katika Italia, Kaisari alikaa Bizanti au Roma ya Mashariki. Kumbukumbu za Roma yenyewe hazikutunzwa tangu miaka mingi.
|
20231101.sw_2116_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Leo hii wataalamu wengi hukubaliana ya kwamba kasoro Ya Dionysio ni takriban miaka 4 - 8; yaani mwaka halisi wa kuzaliwa kwake Yesu ulikuwa kama miaka nne hadi nane kabla ya mwaka ambao tumezoea kuhesabu kama "1", kwa kuwa mwaka 4 K.K. ndipo alipokufa mfalme Herode Mkuu aliyejaribu kumuua akiwa mtoto mchanga.
|
20231101.sw_2116_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Wengi walijaribu kusahihisha kosa hilo lakini habari kamili kabisa haziwezi kupatikana, tena ni vigumu kubadilisha mahesabu yote, vitabu n.k.
|
20231101.sw_2116_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Mwanzoni hesabu ya Dionysio ilikuwa pendekezo la mtaalamu fulani tu, watu wakiendelea kutumia mahesabu yao mbalimbali.
|
20231101.sw_2116_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Miaka 60 baada ya Dionysio, Papa Bonifas IV, akiwa mkuu wa Kanisa Katoliki, alitumia tarehe zote mbili za "baada ya Kristo" na "tangu kuanzishwa kwa mji". Wataalamu walianza kutumia zaidi hesabu hiyo mpya.
|
20231101.sw_2116_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Mnamo mwaka 725 mtaalamu Beda Mheshimiwa alitunga kitabu "Kuhusu ugawaji wa wakati" (kwa Kilatini De Temporum Ratione) alikotumia mfumo ulioundwa na Dionysio akaendelea kuutumia pia katika kitabu kuhusu "Historia ya Kanisa". Kwa kuwa vitabu vya Beda vilikuja kutumiwa kote katika Ulaya ya Magharibi, vilichangia sana uenezi wa hesabu hiyo mpya.
|
20231101.sw_2116_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Wakati wa Karolo Mkuu, Mfalme (halafu Kaisari) aliyetawala Ufaransa pamoja na Ujerumani, Italia ya Kaskazini na maeneo ya Uholanzi na Ubelgiji, hesabu tangu Kristo ilikuwa rasmi kwa serikali.
|
20231101.sw_2116_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Kutokana na uenezaji wa uchumi, biashara na utawala wa Wazungu, hesabu "Baada ya Kristo" ilienea kote duniani.
|
20231101.sw_2116_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Siku hizi ni hesabu pekee katika nchi nyingi. Katika nchi mbalimbali inatumika sambamba na mahesabu mengine.
|
20231101.sw_2116_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Nchi mbalimbali za Kiislamu hutumia miaka tangu Hijra ya Muhammad (mwaka 622 BK), lakini mara nyingi pamoja na miaka ya hesabu ya Kikristo kwa ajili ya mambo ya biashara na mawasiliano ya kimataifa.
|
20231101.sw_2116_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Nchi ya Israeli inatumia kalenda rasmi tangu "kuumbwa kwa dunia", isipokuwa kando ya Kalenda ya BK kwa sababu zilizotajwa hapo juu kwa ajili ya nchi za Kiislamu.
|
20231101.sw_2116_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Dionysio hakutumia msamiati "baada ya Kristo" - alisema "Anno Domini" ("mwaka wa Bwana") akimaanisha Dominus = Bwana ndiye Yesu. Hivyo kifupi katika lugha ya Kilatini ni "AD" kilichoingia pia katika Kiingereza na lugha nyingine kadhaa.
|
20231101.sw_2116_18
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Baada%20ya%20Kristo
|
Baada ya Kristo
|
Hata miaka kabla ya Kristo kwa Kiingereza huitwa kwa kifupi cha Kilatini "a. Chr" (ante Christum natum = kabla ya kuzaliwa kwake Kristo). Wengine hutumia "BC" = "before Christ".
|
20231101.sw_2117_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Milenia
|
Milenia
|
Milenia (kutoka neno la Kiingereza millennium, ambalo mizizi yake ni katika Kilatini: mille, elfu, na annus, mwaka) ni kipindi cha miaka elfu moja.
|
20231101.sw_2117_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Milenia
|
Milenia
|
Kwa sasa tuko katika milenia ya pili BK iliyoanza tarehe 1 Januari 2001. Lakini watu wengi walisheherekea tarehe 1 Januari 2000 ingawa mwaka 2000 ilikuwa mwaka wa mwisho wa karne na milenia iliyotangulia.
|
20231101.sw_2118_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
|
Kaizari
|
Kaizari ni cheo cha mfalme mkuu. Neno la Kiswahili limetokana na lugha ya Kijerumani "Kaiser", lakini asili yake ni Kilatini "Caesar".
|
20231101.sw_2118_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
|
Kaizari
|
Asili ya cheo ni Julius Caesar aliyekuwa kiongozi wa Dola la Roma hadi kuuawa kwake na wapinzani mwaka 44 KK.
|
20231101.sw_2118_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
|
Kaizari
|
Cheo cha Kaizari kiliendelea kutumika katika eneo la Dola la Roma ya Mashariki (Bizanti) hadi mwaka 1453.
|
20231101.sw_2118_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
|
Kaizari
|
Katika Ulaya yenyewe mfalme wa Wafaranki Karolo Mkuu alipokea cheo cha "Caesar" au Kaizari. Baadaye wafalme Wajerumani waliomfuata Karolo Mkuu katika sehemu ya mashariki ya ufalme wake waliendelea kutumia cheo hiki cha Caesar au Kaizari.
|
20231101.sw_2118_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
|
Kaizari
|
Neno la Kaizari liliingia katika lugha ya Kiswahili wakati wa ukoloni wa Kijerumani huko Tanzania, kwa kuwa Austria na Ujerumani zilitawaliwa hadi mwisho wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia 1918 na wafalme wenye cheo cha "Kaizari".
|
20231101.sw_2118_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
|
Kaizari
|
Vilevile mfalme wa Urusi alikuwa na cheo kilekile kilichoitwa "Tsar" kwa Kirusi, ilhali neno hili limeundwa pia kutoka "Caesar".
|
20231101.sw_2118_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
|
Kaizari
|
Lugha za Kiingereza na Kifaransa zilitumia cheo tofauti cha macaesar wa Kiroma, ndicho "Imperator" (= mwenye amri, mwenye mamlaka, jemadari) kilichokuwa "Emperor" kwa Kiingereza au "Empereur" kwa Kifaransa.
|
20231101.sw_2118_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
|
Kaizari
|
Kaizari ni cheo cha mfalme aliye juu ya wafalme wengine. Kutokana na uzoefu huu hata Shah wa Uajemi, Tenno wa Japani, Huangdi wa China na Negus Negesti wa Ethiopia hutajwa kwa cheo cha "Kaizari".
|
20231101.sw_2118_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
|
Kaizari
|
Malkia Viktoria wa Uingereza alitumia cheo cha Kaizari ("empress") kama mtawala wa Uhindi tangu mwaka 1877.
|
20231101.sw_2118_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
|
Kaizari
|
Wakati wa ukoloni mtawala mkuu wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani alikuwa Kaizari Wilhelm II wa Ujerumani; kwenye sarafu ya rupia alionyeshwa pamoja cheo kwa lugha ya Kilatini "imperator".
|
20231101.sw_2118_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kaizari
|
Kaizari
|
Rais Jean-Bedel Bokassa alijitangaza kuwa Kaizari ("empereur") wa Afrika ya Kati mwaka 1977 akiiga mfano wa Napoleon Bonaparte aliyejiwekea taji la Kaizari ya Ufaransa mwaka 1804. Bokassa alipinduliwa mwaka 1979 na nchi kuwa jamhuri tena.
|
20231101.sw_2119_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Duma
|
Duma
|
Duma ni mnyama mbuai aliyemo katika jamii ya paka (Felinae) ambaye hupatikana Afrika na kidogo sehemu za Asia. Chakula chake ni wanyama jamii ya swala .
|
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.