_id
stringlengths
15
22
url
stringlengths
31
150
title
stringlengths
1
86
text
stringlengths
100
23.8k
20231101.sw_2173_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Hatimaye alipaswa kukabidhi koloni lake binafsi mikononi mwa serikali ya Ubelgiji iliyomlipa fidia kwa mali aliyoacha.
20231101.sw_2173_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Kati ya mwaka 1908 hadi 1960 ilikuwa koloni la Ubelgiji kwa jina la Kongo ya Kibelgiji baada ya kuhamishiwa mikononi mwa serikali ya Ubelgiji.
20231101.sw_2173_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Katika miaka 1925 hadi 1946 maeneo ya Rwanda na Burundi yalitawaliwa kama sehemu za Kongo ya Kibelgiji.
20231101.sw_2173_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Wabelgiji walijitahidi kuboresha hali ya maisha ya wenyeji baada ya miaka mibaya ya Leopold II. Nia ilichelewa kuonekana hali halisi kwa sababu utaratibu wa kulazimisha Waafrika kufanyia kazi kampuni na shirika kubwa iliendelea hata bila idhini ya serikali mpya ukadai vifo vingi.
20231101.sw_2173_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Kwenye uwanja wa elimu, matibabu na mawasiliano jitihada za siasa mpya zilionekana zaidi. Kongo ilikuwa kati ya nchi chache ambako lugha za kienyeji zilifundishwa shuleni kwa sababu shule nyingi ziliendshwa na wamisionari.
20231101.sw_2173_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Kwa upande mwingine ubaguzi wa rangi uliwaruhusu Waafrika wachache sana kufikia ngazi za juu za elimu.
20231101.sw_2173_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Makampuni makubwa ya migodi kama vile "Société Générale" na "Union Minière du Haut Katanga" yalichimba madini hasa katika jimbo la Katanga. Makampuni haya yalikuwa na athira kubwa.
20231101.sw_2173_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Katanga ilikuwa maarufu kwa shaba iliyochimbwa huko. halafu pia kwa uranium iliyotumiwa kwa mabomu ya kwanza ya kinyuklia ya Marekani mwaka 1945.
20231101.sw_2173_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Baada ya unyama wa miaka ya Leopold II upinzani dhidi ya utawala wa kikoloni ulikuwa hafifu. Kuanzia miaka ya 1920 Wakongo wengi walionyesha upinzani huo katika mahudhurio katika madhehebu mapya ya wafuasi wa Simon Kimbangu yaliyopigwa marufuku na Wabelgiji kuanzia mwaka 1926.
20231101.sw_2173_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Wabelgiji ambao hawakujiandaa kwa madai hayo yalipaswa kukubali uchaguzi wa halmashauri za vijiji na miji mwaka 1957.
20231101.sw_2173_18
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Mwaka 1958 vyama vya kisiasa vilikubaliwa. Harakati mbili muhimu kati ya hivi zilikuwa Abako (Alliance de Bakongo) chini ya Joseph Kasavubu na MNC (Mouvement National Congolais) chini ya Patrice Lumumba.
20231101.sw_2173_19
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Wabelgiji walijaribu kuchelewesha harakati hizo lakini baada ya kutambua matatizo serikali ya Ubelgiji ilitangaza mnamo Januari 1960 kuwa uchaguzi utaendeshwa haraka na baada ya miezi sita Wabelgiji watakabidhi nchi kwa wenyeji.
20231101.sw_2173_20
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Chama cha Patrice Lumumba kilishinda kwa kura nyingi naye akawa kiongozi wa kwanza wa nchi huru kama waziri mkuu.
20231101.sw_2173_21
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Kati ya 27 Oktoba 1971 na 17 Mei 1997, chini ya utawala wa dikteta Mobutu, nchi ilijulikana kwa jina la "Zaire".
20231101.sw_2173_22
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Mwaka 2017 wakazi walikuwa 81,339,988: idadi hiyo ni ya 4 kati ya nchi zote za Afrika, baada ya Nigeria, Ethiopia na Misri.
20231101.sw_2173_23
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Kifaransa ni lugha rasmi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Ilikuwa lugha ya utawala ya koloni ikaendelea kutumiwa kama lugha isiyoelekea upande wowote kati ya makabila, lugha na tamaduni za nchi hii.
20231101.sw_2173_24
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Kwa jumla kuna takriban lugha 242, hasa lugha za Kibantu, zinazozungumzwa nchini (angalia orodha ya lugha). Kati yake, lugha 4 zinatambuliwa kama lugha za kitaifa, nazo ni: Kikongo (Kituba), Kingala (Kongo), Kiluba (Tshiluba) na Kiswahili. Wakati wa ukoloni lugha hizo nne za kitaifa ziliwahi kutumiwa kieneo katika shule za msingi.
20231101.sw_2173_25
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Kingala kilikuwa lugha rasmi ya jeshi la kikoloni lililoitwa "Force Publique" chini ya utawala wa Ubelgiji likaendelea kuwa lugha ya jeshi la jamhuri baada ya uhuru.
20231101.sw_2173_26
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Wananchi wengi (zaidi ya 90%) wanajihesabu Wakristo wa madhehebu mbalimbali; kati yao asilimia 29.7 ni Wakatoliki. Waislamu ni asilimia 10-12. Wafuasi wa dini asilia za Kiafrika ni 3%.
20231101.sw_2173_27
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Edgerton, Robert, The Troubled Heart of Africa: A History of the Congo. St. Martin's Press, December 2002.
20231101.sw_2173_28
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Exenberger, Andreas/Hartmann, Simon. The Dark Side of Globalization. The Vicious Cycle of Exploitation from World Market Integration: Lesson from the Congo, Working Papers in Economics and Statistics 31, University Innsbruck 2007.
20231101.sw_2173_29
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Exenberger, Andreas/Hartmann, Simon. [http://vkc.library.uu.nl/vkc/seh/research/Lists/Events/Attachments/6/Paper.ExenbergerHartmann.pdf Doomed to Disaster? Long-term Trajectories of Exploitation in the Congo] , Paper to be presented at the Workshop "Colonial Extraction in the Netherlands Indies and Belgian Congo: Institutions, Institutional Change and Long Term Consequences", Utrecht 3–4 December 2010.
20231101.sw_2173_30
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Justenhoven, Heinz-Gerhard; Ehrhart, Hans Georg. Intervention im Kongo: eine kritische Analyse der Befriedungspolitik von UN und EU. Stuttgart: Kohlhammer, 2008. (In German) ISBN 978-3-17-020781-3.
20231101.sw_2173_31
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Larémont, Ricardo René, ed. 2005. Borders, nationalism and the African state. Boulder, Colorado and London: Lynne Rienner Publishers.
20231101.sw_2173_32
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Lemarchand, Reni and Hamilton, Lee; Burundi: Ethnic Conflict and Genocide. Woodrow Wilson Center Press, 1994.
20231101.sw_2173_33
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Melvern, Linda, Conspiracy to Murder: The Rwandan Genocide and the International Community. Verso, 2004.
20231101.sw_2173_34
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Miller, Eric: "The Inability of Peacekeeping to Address the Security Dilemma", 2010. ISBN 978-3-8383-4027-2.
20231101.sw_2173_35
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Mwakikagile, Godfrey, Nyerere and Africa: End of an Era, Third Edition, New Africa Press, 2006, "Chapter Six: Congo in The Sixties: The Bleeding Heart of Africa", pp. 147 – 205, ISBN 978-0-9802534-1-2; Mwakikagile, Godfrey, Africa and America in The Sixties: A Decade That Changed The Nation and The Destiny of A Continent, First Edition, New Africa Press, 2006, ISBN 978-0-9802534-2-9.
20231101.sw_2173_36
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Prunier, Gérard, Africa's World War: Congo, the Rwandan Genocide, and the Making of a Continental Catastrophe, 2011 (also published as From Genocide to Continental War: The Congolese Conflict and the Crisis of Contemporary Africa: The Congo Conflict and the Crisis of Contemporary Africa).
20231101.sw_2173_37
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Renton, David; Seddon, David; Zeilig, Leo. The Congo: Plunder and Resistance, 2007. ISBN 978-1-84277-485-4.
20231101.sw_2173_38
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Schulz, Manfred. Entwicklungsträger in der DR Kongo: Entwicklungen in Politik, Wirtschaft, Religion, Zivilgesellschaft und Kultur, Berlin: Lit, 2008, (in German) ISBN 978-3-8258-0425-1.
20231101.sw_2173_39
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Stearns, Jason: Dancing in the Glory of Monsters: the Collapse of the Congo and the Great War of Africa, Public Affairs, 2011.
20231101.sw_2173_40
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Osman, Mohamed Omer Guudle(November,2011) Africa: A rich Continent where poorest people live, The Case of DR Congo and the exploitation of the World Market
20231101.sw_2175_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Mkoa wa Mara ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 31000.. Umepakana na mikoa jirani ya Mwanza na Shinyanga upande wa kusini, Arusha upande wa kusini-mashariki, Kagera kwa njia ya Ziwa Nyanza (au Viktoria) na Kenya upande wa mashariki. Jina linatokana na lile la mto Mara.
20231101.sw_2175_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Idadi ya wakazi ilikuwa 2,372,015 wakati wa sensa ya mwaka 2022, kutoka 1,743,830 wa sensa ya mwaka 2012 , na 1,368,602 wa sensa ya 2002.
20231101.sw_2175_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Kuna wilaya zifuatazo katika mkoa wa Mara: Bunda, Serengeti, Tarime, Rorya, Butiama, Musoma mjini na Musoma vijijini.
20231101.sw_2175_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Makabila ya Mara ni mengi kuliko mikoa yote ya Tanzania, kama vile Waluo, Wajita, Waruri, Wazanaki, Wakuria, Wakabwa, Wakiroba, Wasimbiti, Wangoreme, Wakwaya, Waikoma, Wanata, Waisenye, Waikizu, Wasizaki, Wasukuma, Wataturu na makabila madogo kama Wanandi, Wakisii au Wamaragori.
20231101.sw_2175_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Kuna jumla ya makabila 30 yanayodai kujitegemea. Jamii zinazosahaulika huunganishwa katika kundi la Suba (Wategi, ambao pia huitwa Abhathegi maarufu kama Abhagirango, Waugu (Ugu), Warieri, Wakine, Wasweta na Waganjo, Wagire, Wakiseru, Wakamageta na Waturi). Baadhi ya jamii hizi zilimezwa na mila, lugha na desturi za Waluo zikaitwa Suba-Luo katika kipindi cha utawala wa DC Engram aliyekuwa wilaya ya Mara Kaskazini (North Mara).
20231101.sw_2175_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Baadhi ya jamii kwa upande wa Kenya iliyotawaliwa na Waingereza katika Wilaya za Kuria na South Nyanza huitwa Suna, Wagwasi, Ungoe, Kajulu na Kadem.
20231101.sw_2175_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Hata hivyo habari hizi bado zinafanyiwa utafiti kuangalia muingiliano wa lugha na tofauti za kilahaja kati ya jamii moja na nyingine hasa zilizopo Tanzania. Itakumbukwa jamii nyingi ziliingia upande ulioitwa South Nyanza kabla ya nchi za Afrika Mashariki kupata uhuru. Zipo tafiti nyingi siku hizi ambazo zinajaribu kubainisha makundi ya jamii hizo lakini muingiliano bado haujapata ufafanuzi makini.
20231101.sw_2175_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Kimsingi Mkoa wa Mara una jamii hizo zipatazo 30 lakini lugha kuu ni saba tu na nyingine ni lahaja kutokana na makundi ya lugha hizi: Luo, Kuria, Sukuma, Suba, Shashi, Zanaki na Taturu. Yapo makundi ya Wanata, Waisenye na Wataturu, Wazanaki (kundi lake: Kabwa, Kirobha, Wasimbiti, Wairienyi, Waikizu, Wangoreme), Luo (Wakowak, Wakamoti), Wakuria (Nyebhasi, Nyamongo, Wanchari, Wasweta, Wakenye, Warenchoka, Watimbaru, Waregi, hadi 14/15), Sukuma, Nyantuzu na Shashi (Wajita, Wakwaya, Waruri, Wakerewe, Wakara). Jamii zote humezwa katika makundi saba ya lugha kuu lakini kila jamii inajitofautisha kwa lahaja yake.
20231101.sw_2175_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Ni jamii za Kibantu peke yake zinazoweza kuwasiliana na kuelewana kukiwa na tofauti kidogo katika matamshi ya maneno.
20231101.sw_2175_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Ukichunguza zaidi, wakazi wa asili wa Mkoa wa Mara ni makabila makuu mawili yenye uhusiano wa karibu sana, yaani Wakurya (na vikabila kadhaa: Wakurya ni jina ‘linalobeba’ mengi ya yale yanaoyoitwa 'makabila' mkoani Mara, ambayo tafsiri yake halisi ni 'vikabila') na Wajita (hawa nao wana vikabila kadhaa).
20231101.sw_2175_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Pia, Wakurya-Waghusii si 'Bantu halisi' bali ni mchanganyiko kati ya Wabantu na Waniloti. Katika makabila ya Kibantu, yaliyoathiri damu ya Wakurya ni pamoja na:
20231101.sw_2175_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Wachaga (kwa mfano, Wakerobha au Wakiroba, walichanganya damu sana na wahamiaji toka Machame na Marangu kwa Wachaga - na hadi leo Machame na Marangu ni majina ya vitongoji huko kwa Wakiroba Mkoa wa Mara!)
20231101.sw_2175_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Wakikuyu (kwa mfano, baadhi ya Wakurya wa North Mara wana asili ya Wakikuyu au 'Abhaghekoyo'). Pia Wakikuyu wanachanga majina mengi na Wakurya - kama Nyambura, Murughi, Mwita, n.k. na hata lugha zinafanana kwa kiasi kikubwa).
20231101.sw_2175_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Pia, kama makabila, Wakurya-Waghusii, Wakikuyu, na Wameru wa Kenya wana uhusiano wa karibu na asili moja. Makabila mengine yanayohusiana nao ni Wagisu (Uganda) na Waluya (Kenya). Kuna wakati ambapo makundi hayo yote yalikuwa kabila moja, lakini wakatengana kwa kuhamia sehemu za mbali, wakawa makabila tofauti tunayoyajua leo.
20231101.sw_2175_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Kwa hiyo, dhana ambayo imejengeka sana vichwani mwa watu kwamba Mara kuna makabila mengi, kwa kiasi kikubwa ni potofu. Ukiangalia kwa undani hata lugha na mila zilizopo, utaona kwamba hata hao kina yego/mbani (Wajita, Wakwaya, Wakara, Waruri, Wakerewe, n.k.) ni 'vikabila' tu vya kabila kubwa la Wajita.
20231101.sw_2175_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Ukiachia Wajaluo (au 'Jakowiny Luo'), mkoani Mara pia kuna Wataturu na Wanandi. Wanandi ni moja kati ya 'vikibila' vya Wakalenjin. Hata hivyo, idadi ya watu wa makabila haya ni ndogo ukilinganisha na ile ya 'Wakurya-Waghusii' na Wajita (ikiwa na maana ya kabila kubwa linalojumuisha pia Wajita, Wakwaya, na Waruri).
20231101.sw_2175_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Pia Mara, Wakurya hawaishi tu Tarime, bali huishi wilaya zote 6 za Mkoa wa Mara: Tarime, Rorya (hao ni Wakurya wa North Mara), Musoma Vijjini, Musoma Mjini, Bunda, na Serengati (hao ndio Wakurya wa South Mara). Abhaghusii (wanaoishi jimbo la Nyanza, Kenya) ni sehemu ya Wakurya wa 'North Mara'.
20231101.sw_2175_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Kwa hiyo, wanahistoria wanatakiwa kuliweka hili sawa. Wazungu walichorekodi ni majina ya vikabila (au koo kubwa), kwani hata leo ukienda Mara, ukauliza swali lako kizembe, si ajabu usikute mtu atayekujibu kwamba anaitwa Mkurya: wote watakuambia, mimi Mzanaki, Mkiroba, Mtimbaru, n.k. Wengine watasema, mimi Mmjita, Mkwaya, Mruri, nk.
20231101.sw_2175_18
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Kwa wakereketwa wa historia, Wakiroba (kikabila cha Wakurya-Wakisii) na Wakwaya (kikabila cha Wajita) ndiyo makabila ya asili ya inayoitwa leo hii Musoma mjini. Makundi haya mawili, pamoja na kuwa makibali tofauti, yana uhusiano wa muda mrefu wa karibu sana. Hupendana sana, na hata vita walipigana kwa kushirikiana!
20231101.sw_2175_19
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Pia Wakurya na Wajita, uhusiano wao wa karibu, na hata kushabihiana kwa lugha zao (kwa makabila haya makubwa mawili ya Mkoa wa Mara, hakuna anayeweza akamsengenya mwenzie, na asijue anasema nini), si jambo lililoanza juzi. Mababu wanatuambia hawa watu wote wamehamia Mara, wakitokea maeneo ambayo kwa sasa yako katika nchi zinazojulikana kama Misri na Libya (hata Wajaluo nao, walikujua toka huko). Wakati wa msafara, waligawanyika makundi matatu:
20231101.sw_2175_20
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
• Moja likapita mashariki mwa Ziwa Victoria. Hili lilikuwa ndilo kundi kuu. Koo nyingi za Kikurya zilipita huko. Katika nyakati tofauti, zilitengana na Wagisu (Uganda), Waluya, Wameru, Wakikuyu (Kenya).
20231101.sw_2175_21
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
• Moja likapita magharibi mwa Ziwa Victoria. Koo nyingi za Wajita, pamoja na baadhi ya koo za Wakurya (kama Abhashanake) walipita huko.
20231101.sw_2175_22
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
• Moja likapita katikati ya Ziwa Victoria. Hili kundi lilikuwa dogo zaidi. Lilijumuisha zaidi koo chache za Kijita, kama vile Wakerewe.
20231101.sw_2175_23
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Hakuna historia ya vita kati ya Wakurya na Wajita, bali wameishi kwa kuelewana na kusaidiana. Hata hivyo, koo za Kikurya hupenda sana kupigana – na haya tunayaona hadi leo hii.
20231101.sw_2175_24
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Pia tukumbuke: Wabantu ni familia moja, na Waafrika ni ’kabila’ moja kubwa, na binadamu wote, bila kujali rangi zetu, tumetoka kwa Muumba mmoja na tuna asili moja – ni watoto wa Adamu na Eva (Waarabu humwita Hawa), kwa wale wanaoamini dini; au ni watoto wa Mwafrika kwa wale wanaoamini sayansi.
20231101.sw_2177_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Roma (pia Rumi) ni mji mkuu ("Roma Capitale") wa Jamhuri ya Italia. Pia ni mji mkuu wa mkoa wa Lazio.
20231101.sw_2177_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Roma iko katika sehemu ya magharibi ya kati ya Rasi ya Italia, katika makutano ya mito ya Tiber na Aniene karibu na Bahari ya Mediteranea.
20231101.sw_2177_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Roma ina wakazi 2,860,009 katika 1,285 km2 (496.1 sq mi), Roma ni komune yenye watu wengi zaidi nchini na ni jiji la tatu lenye watu wengi katika Umoja wa Ulaya kwa idadi ya watu ndani ya mipaka ya jiji.
20231101.sw_2177_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Roma mara nyingi inajulikana kama Jiji la Milima Saba kutokana na eneo lake la kijiografia, na pia kama "Mji wa Milele". Roma kwa ujumla inachukuliwa kuwa "chimbuko la ustaarabu wa magharibi na Utamaduni wa Kikristo", na kitovu cha Kanisa Katoliki. Mji wa Vatikano (nchi ndogo zaidi duniani) ni nchi huru ndani ya mipaka ya jiji la Roma, mfano pekee uliopo wa nchi ndani ya jiji.
20231101.sw_2177_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Roma uko katikati ya Italia ikiwa mita 20 juu ya UB ndani ya tambarare ya bonde la mto Tiber linalopakana na milima ya Abruzzi, milima ya Sabini na milima ya Albani.
20231101.sw_2177_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Mwanzo wa Roma ulikuwa kwenye vilima saba vilivyo katikati ya mji wa leo vinavyoitwa: Palatino, Aventino, Campidoglio, Quirinale, Viminale, Esquilino na Celio.
20231101.sw_2177_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Hali ya hewa hutawaliwa na bahari iliyo karibu. Wastani wa halijoto kwa mwaka ni sentigredi 15,4. Mvua hunyesha wastani wa mm 758 kwa mwaka.
20231101.sw_2177_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Miezi yenye joto ni Juni hadi Agosti ikiwa na wastani wa sentigredi 21 hadi 23,8; ni miezi ya mvua kidogo.
20231101.sw_2177_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Historia ya mji inasemekana imeanza rasmi tarehe 21 Aprili 753 KK, lakini majengo ya kwanza ni ya karne ya 10 KK.
20231101.sw_2177_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Katika karne za KK ulikuwa mji mkuu wa ufalme wa Roma, halafu wa Jamhuri ya Roma, hatimaye wa Dola la Roma.
20231101.sw_2177_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Uenezi wa Ukristo kuanzia mwaka 30 na hasa ujio wa Mtume Petro na Mtume Paulo waliofia dini yao (64-68) huko viliathiri mji huo moja kwa moja.
20231101.sw_2177_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Kuanzia karne ya 7 BK ukawa mji mkuu wa Dola la Papa, halafu wa Ufalme wa Italia na sasa wa Jamhuri ya Italia. Huitwa mara nyingi "Mji wa Milele".
20231101.sw_2177_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Tangu kuondoka kwa makao makuu ya Kaisari na kupungua kwa nguvu ya Dola la Roma Magharibi idadi ya wakazi ilipungua hadi kuwa na takriban 100,000 mnamo mwaka 530.
20231101.sw_2177_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Katika karne zilizofuata Italia pamoja na Ulaya iliona vita na mashambulio ya makabila yasiyostaarabika. Mnamo mwaka 1000 Roma ilikuwa mji mdogo wenye wakazi 20,000 pekee walioishi ndani ya maghofu ya mji mkubwa wa kale.
20231101.sw_2177_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Tangu kuimarika kwa utawala wa mapapa mji ulianza kukua tena; mnamo mwaka 1900 ukawa na wakazi 400,000. Katika karne ya 20 mji ulipanuka sana hadi kufikia idadi ya wakazi wa zamani hata kuipita. Siku hizi asilimia 7.4 ni wageni.
20231101.sw_2177_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Roma ndiyo kitovu kimojawapo cha sekta ya viwanda na sekta ya huduma ya Italia. Utalii ni pia muhimu sana kiuchumi, kutokana na watalii 26,100,000 wanaoutembelea kila mwaka: 6.5% za Jumla ya Pato la Taifa zinapatikana ndani ya Roma ambazo ni kushinda miji mingine yote ya Italia.
20231101.sw_2177_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Roma ina makao makuu ya F.A.O. (Food and Agriculture Organisation - Shirika la Chakula na Kilimo) ya Umoja wa Mataifa pamoja na ofisi zote za serikali ya Italia.
20231101.sw_2177_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Info-Roma - Info-Rome ni tovuti kuhusu mambo ya kitalii katika mji wa Roma, hasa matukio ya aina mbalimbali, hoteli, maonyesho, nyumba za kumbukumbu na vyakula.
20231101.sw_2184_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
Mto Nile (pia: Naili; kwa Kiarabu: ‏ ,النيل‎ an-nīl) ni mto mkubwa upande wa mashariki ya bara la Afrika. Mara nyingi hutajwa kuwa pia ni mto mrefu kabisa duniani kushinda mto Amazonas. Kutoka Ziwa la Viktoria Nyanza hadi mdomo wake kwenye Bahari ya Mediteranea Nile inavuka nchi za Uganda, Sudan Kusini, Sudan na Misri kwa urefu wa km 6,650.
20231101.sw_2184_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
Beseni la Nile hukusanya maji ya eneo linalojumlisha 10% za eneo la Afrika yote au km² 3,349,000. Takriban watu milioni 250 hukalia beseni hilo.
20231101.sw_2184_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
"Nile" au "Naili" ni umbo la Kiingereza la jina la mto lililotokana na lile lililotumiwa na Wagiriki wa Kale: "Neilos" (Νεῖλος). Haijulikani Wagiriki walipata jina hilo kwa njia gani, lakini lilikuwa kawaida nje ya Misri.
20231101.sw_2184_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
Wamisri wa Kale waliita mto huu kwa jina Ḥ'pī au Iteru linalomaanisha "mto mkubwa". Wakopti walikuwa na jina la piaro lakini tangu utawala wa Kiroma jina la Kigiriki lilizidi kutumika, na Waarabu waliendelea na jina la Kigiriki pia, hivyo leo hii wananchi wanasema "an-nil".
20231101.sw_2184_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
Majina hayo ya "nyeupe" na "buluu" yana asili yake katika mji wa Khartoum ambako mito yote miwili inaunganika ilhali kila mmoja una rangi tofauti kutokana na udongo tofauti uliotia rangi yake kwenye maji hayo.
20231101.sw_2184_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
Vyanzo vya Nile ni mito yote inayopeleka maji kwenda Ziwa Viktoria Nyanza katika nchi za Tanzania, Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Uganda na Kenya. Chanzo cha mbali kabisa ni mto wa Luvironza huko Burundi unaoingia katika mto Kagera na kufika Ziwa Viktoria Nyanza.
20231101.sw_2184_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
Hakuna mapatano kabisa Nile inaanzia wapi. Kawaida ya waandishi Waingereza ni kuhesabu kuanzia Ziwa Viktoria; waandishi wa mataifa mengine huwa wanaweza wakaita tayari mto Kagera kwa jina "Nile ya Kagera".
20231101.sw_2184_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
ndani ya Sudan Kusini mto huitwa Bahr al-Jabal (mto wa mlimani) hadi kupokea tawimto la Bahr al-Ghazal
20231101.sw_2184_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
kwa sababu ya rangi wakati wa mvua yake kutokana na udongo katika maji jina linakuwa Bahr al-Abyad kuanzia Bahr al-Ghazal hadi Khartoum
20231101.sw_2184_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
kuanzia Khartoum jina pekee ni Bahr an-Nil (mto wa Nile) hadi mdomo wake wa delta kwenye Mediteranea.
20231101.sw_2184_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
Tangu milenia kadhaa maji ya Nile yamekuwa msingi wa maisha yote nchini Misri na pia kwa sehemu kubwa ya nchi ya Sudan.
20231101.sw_2184_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
Katika miaka ya 1920 Uingereza kama mtawala mkoloni wa Sudan na Misri ulikuwa na majadiliano juu ya ugawaji wa maji ya mto na kufikia mapatano juu ya matumizi ya maji ya mto Nile ya 1929.
20231101.sw_2184_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
Hadi leo Misri inadai ya kwamba mapatanao yale yanakataa ujenzi wa malambo na kuanzishwa kwa miradi ya umwagiliaji inayotumia maji ya Nile bila kibali cha serikali yake. Hapa Misri inadai ya kwamba nchi zote zilizokuwa makoloni ya Uingereza wakati ule zinafungwa na mapatano ya mwaka 1929 na hizi ni pamoja na Sudan, Uganda, Kenya, Tanzania, halafu pia Ethiopia iliyopatana na Uingereza wakati ule. Nchi nyingine hazikubali madai hayo, ila majadiliano juu ya mapatano mapya ya ushirikiano katika beseni la Nile yanaendelea.
20231101.sw_2185_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Mediteranea
Bahari ya Mediteranea
Bahari ya Mediteranea (pia: Bahari ya Kati) ni bahari ya pembeni ya Atlantiki kati ya mabara ya Afrika, Ulaya na Asia ya Magharibi. Eneo lake ni takriban milioni 2,5 km². Kina chake kirefu ni 5,267 m. Ina kanda ya hali ya hewa ya pekee pamoja na mimea na wanyama.
20231101.sw_2185_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Mediteranea
Bahari ya Mediteranea
Neno "Mediteranea" limetokana na lugha ya Kilatini likiunganisha maneno ya "medium" (inamaanisha "kati ya, katikati") na "terra" (inamaanisha "bara"). Kwa hiyo neno lenyewe linamaanisha "Bahari katikati ya bara".
20231101.sw_2185_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Mediteranea
Bahari ya Mediteranea
Katika lugha ya Biblia Kiebrania iliitwa "Bahari ya Magharibi" au "Bahari Kuu"; Waroma wa Kale waliotwala nchi zote zinazopakana na Bahari ya Mediteranea waliita "mare nostrum" yaani "bahari yetu". Waarabu na Waturuki wanaiita "Bahari Nyeupe" (kwa Kituruki: Akdeniz; kwa Kiarabu: البحر الأبيض al-baHr-al-abyaD)
20231101.sw_2185_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Mediteranea
Bahari ya Mediteranea
Bahari ya Mediteranea ni bahari, si ziwa, kwa sababu imeunganishwa na Atlantiki kwa njia ya mlango wa bahari wa Gibraltar.
20231101.sw_2185_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Mediteranea
Bahari ya Mediteranea
Ina bahari za pembeni zake ambazo ni pamoja na Bahari Nyeusi, Bahari ya Aegean, Bahari ya Tyrrheni na mengine. Bahari Nyeusi inaunganishwa kwa njia ya mlangobahari wa Dardaneli, Bahari ya Marmara na mlangobahari wa Bosporus.
20231101.sw_2185_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Mediteranea
Bahari ya Mediteranea
Tangu mwaka 1869 kuna pia njia ya maji kati ya Mediteranea na Bahari ya Shamu ambayo ni Mfereji wa Suez.
20231101.sw_2185_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Mediteranea
Bahari ya Mediteranea
Kuna visiwa vingi sana hasa kati ya Ugiriki na Uturuki. Visiwa vikubwa ni Korsika, Sardinia, Sisilia, Kreta, Rhodos na Kibros.
20231101.sw_2185_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Mediteranea
Bahari ya Mediteranea
Hispania, Ufaransa, Monako, Italia, Malta (funguvisiwa), Slovenia, Kroatia, Bosnia - Herzegovina, Montenegro, Albania, Ugiriki, Uturuki
20231101.sw_2194_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jibuti
Jibuti
Jibuti (kwa Kifaransa: Djibouti, kwa Kiarabu: جيبوتي) ni nchi ndogo ya Afrika ya Mashariki kwenye Pembe la Afrika.
20231101.sw_2194_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jibuti
Jibuti
Imepakana na Eritrea, Ethiopia na Somalia upande wa bara. Kuna pwani ya Bahari ya Shamu na Ghuba ya Aden. Ng'ambo ya bahari iko nchi ya Yemen katika umbali wa km 20 pekee.
20231101.sw_2194_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jibuti
Jibuti
Hali ya nchi inalingana kwa karibu na ile ya mataifa mengine katika Mashariki mwa Afrika, Jibuti ilipo, ikipakana na Ghuba ya Aden na Bahari ya Shamu, katikati ya Eritrea, Ethiopia na Somalia.