_id
stringlengths
15
22
url
stringlengths
31
150
title
stringlengths
1
86
text
stringlengths
100
23.8k
20231101.sw_2229_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siku%20ya%20wapendanao
Siku ya wapendanao
Kulingana na tamaduni za kale, Askofu huyo alimponya mtoto kipofu wa mfungwa mwenzake. Ndipo mara nyingi matendo yake yanahusishwa na kitendo kikuu cha upendo: kuna baadhi ya historia zinasema kuwa askofu huyo alimtumia barua mtoto wa yule mfungwa mwenzake aliyemponya upofu, na barua hiyo ilikuwa ni katika hali ya kumuaga akiendea kutimiza kifungo chake na adhabu ya kunyongwa. Historia zinazidi kusema kuwa mwishoni mwa barua hiyo kulikuwa kumesainiwa kwa maneno yaliyosema "Valentinus wako".
20231101.sw_2229_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siku%20ya%20wapendanao
Siku ya wapendanao
Lakini pia baadhi ya tamaduni za watu zilizidi kusema kuwa askofu huyo aliwafungisha ndoa wanajeshi wawili ambao walikuwa wamekatazwa kufunga ndoa.
20231101.sw_2231_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Mkoa wa Kigoma uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
20231101.sw_2231_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu.
20231101.sw_2231_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750.
20231101.sw_2231_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Kuna maeneo mawili yenye sokwe: ndipo Hifadhi ya Taifa ya Gombe (alikofanya utafiti wake mwanabiolojia Jane Goddall) na Hifadhi ya Taifa ya Milima ya Mahale. Pia kuna Pori la Akiba la Moyowosi ambalo makao yake makuu yapo katika kijiji cha Kifura, Wilaya ya Kibondo.
20231101.sw_2231_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Kuna wilaya nane ambazo ni (idadi ya wakazi katika mabano): Kigoma Mjini (144,852), Kigoma Vijijini (490,816), Kibondo (414,764), Kasulu (628,677), Uvinza (383,640), Buhigwe (254,342) na Kakonko (167,555) . Jumla ya wakazi ni 2.127.930 (sensa ya mwaka 2012).
20231101.sw_2231_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Mji wa Ujiji ulioko karibu na Kigoma mjini ndio mji wa kale zaidi katika Tanzania ya Magharibi penye makumbusho ya David Livingstone.
20231101.sw_2231_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Kabila kubwa ni Waha, likifuatwa na Wamanyema, Wabembe na Watongwe. Kuna pia Wavinza, Wanyamwezi, Wasukuma, Wafipa na watu wenye asili ya Kongo, Rwanda na Burundi.
20231101.sw_2231_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Idadi au msongamano wa watu katika maeneo ya mkoa huu imetegemea sana shughuli zinazofanyika kama vile kilimo na uvuvi pamoja na kupatikana kwa nzi aina ya ndorobo: penye ndorobo wengi huwa na watu wachache.
20231101.sw_2231_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Mkoa wa Kigoma bado hauna maendeleo yanayolingana na mazingira yake. Hali ya barabara na mawasiliano mengine ni mbaya. Umbali hadi Dar es Salaam ni km 1316, hadi Mwanza 830, hadi Arusha 1204. Ipo barabara nzuri ya lami kuanzia wilaya ya Kaliua (mkoa wa Tabora) kupitia Uvinza, Malagarasi, Nguruka, Kaziramimba hadi Kigoma mjini, isipokuwa kipande cha kilomita 400 ni cha muramu ambayo nayo inapitika vizuri kama si kipindi cha mvua nyingi za uharibifu.
20231101.sw_2231_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Usafiri muhimu ni reli kutoka Kigoma kwenda Dar es Salaam kupitia Tabora na Dodoma. Isipokuwa reli hii imeshazeeka kutokana na kujengwa zamani za Afrika ya Mashariki ya Kijerumani kabla ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Treni (gari moshi) zake huchelewachelewa kwa kuchukua muda mrefu. Wakati wa mvua inatokea ya kwamba mawasiliano yanavurugika.
20231101.sw_2231_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Uwanja wa ndege wa Kigoma unashughulika na shirika la ndege la Tanzania lenye ndege nne zinazofanya safari kwa sasa nchi nzima na usafiri ni wa uhakika, pia yapo mashirika madogo yanyofanya shughuli zake kama auric air, nyingi zikiwa za kubeba watalii.Shukrani za kipekee zimwendee Rais wa nne(Mh Jakaya Mrisho Kikwete) wa Jamhuri ya Muungano aliepigana kiume kuufungua mkoa wa kigoma kwa njia ya mawasiliano ya barabara.
20231101.sw_2231_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Takribani 85% ya wakazi wote hutegema kilimo, walio wengi kilimo cha kujitegemea tu, tena cha jembe la mkono.
20231101.sw_2231_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Sensa ya 2002 Kigoma Region Homepage for the 2002 Tanzania National Census*Serikali ya Tanzania Tanzanian Government Directory Database
20231101.sw_2234_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia ilikuwa vita iliyopigwa kuanzia mwaka 1914 hadi 1918. Mataifa wapiganaji yalikuwa Ujerumani, Austria-Hungaria, Bulgaria na Uturuki (ziliitwa "Mataifa ya Kati", ing. central powers) kwa upande mmoja dhidi ya Ufaransa, Urusi, Uingereza, Italia, Marekani na nchi mbalimbali zilizoshirikiana nazo (zilitwa "Mataifa ya Ushirikiano", ing. allied powers).
20231101.sw_2234_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Vita hii ilianza katika Ulaya ikapanuka haraka hadi Mashariki ya Kati. Kupitia koloni za Ujerumani ilipiganiwa pia Afrika na Asia ya Mashariki ikasababisha kifo cha takriban watu milioni tisa.
20231101.sw_2234_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Sababu yake ilikuwa mashindano makali kati ya mataifa ya Ulaya kuhusu kushika nafasi ya kipaumbele barani Ulaya na duniani kote.
20231101.sw_2234_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Matokeo yake yalikuwa mwisho wa kipaumbele cha Ulaya duniani na kupanda ngazi kwa Marekani, mapinduzi katika nchi mbalimbali, mwisho wa falme za Ujerumani, Austria na Urusi pamoja na mwanzo wa utawala wa kikomunisti katika Urusi, mwisho wa Dola la Austria-Hungaria na wa Milki ya Osmani pamoja na mwisho wa ukoloni wa Kijerumani duniani.
20231101.sw_2234_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Katika Ulaya nchi mpya zilijitokeza kama vile Chekoslovakia, Ufini, Latvia, Estonia, na Yugoslavia pamoja na nchi za zamani zilizotokea tena katika uwanja wa kimataifa ndizo Austria, Hungaria, Lithuania na Poland. Katika Mashariki ya Kati Uturuki ilianzishwa kama nchi mpya, ilhali kipindi kifupi cha ukoloni wa Uingereza na Ufaransa kilianza huko Syria, Iraq na Lebanoni.
20231101.sw_2234_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Shirikisho la Mataifa liliundwa kama chombo cha kwanza kilicholenga kuunganisha nchi zote za Dunia na kuzuia vita mpya. Koloni za awali za Ujerumani na majimbo ya Kiarabu ya Milki ya Osmani zilidhaminiwa kwa Uingereza na Ufaransa kwa niaba ya Shirikisho, hatua iliyoweka maeneo haya chini ya uangalizi wa kimataifa, tofauti na koloni za kawaida.
20231101.sw_2234_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Sehemu kubwa ya Ulaya iliwahi kuwa na kipindi kirefu cha amani tangu vita kati ya Ufaransa na Ujerumani mnamo 1870-1871. Mataifa ya Ulaya yalikuwa na mfumo wa mikataba na mapatano kati yao yaliyolenga kuhakikisha uwiano wa mataifa. Mataifa makubwa ya Ulaya yalikuwa Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Urusi na Italia pamoja na milki ya Austria-Hungaria.
20231101.sw_2234_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Hali ilikuwa tofauti katika Kusini-Mashariki mwa bara hilo. Hadi nusu ya pili ya karne ya 19 sehemu kubwa ya Balkani ilitawaliwa na Milki ya Osmani iliyokuwa milki ya Kiislamu ya kutawala Wakristo wengi. Milki hii iliendelea kudhoofika wakati wa karne ya 19. Nchi mbalimbali zilijitenga na kupata uhuru, kama vile Ugiriki, Serbia, Bulgaria na Romania. Nchi hizi mpya zilipigana kivita kati yao na Milki ya Osmani hadi mwaka 1912.
20231101.sw_2234_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Vita Kuu ilianza kutokana na ugomvi kati ya Austria-Hungaria na Serbia. Kutokana na muundo wa mikataba ya kusaidiana kati ya nchi za Ulaya mwanzo huo ulisababisha mfululizo wa hali ya vita kati ya mataifa, na mengine ya Balkani yaliyotafuta uhuru wao.
20231101.sw_2234_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Tarehe 28 Juni 1914 katika mji wa Sarayevo, Bosnia, mwana wa Kaizari wa Austria aliyekuwa mfalme mteule aliuawa pamoja na mke wake na mgaidi Mserbia mwanachama wa kundi la "Mkono Mweusi" lililopinga utawala wa Austria-Hungaria katika Bosnia. Austria iliamuru Serbia ifuate masharti makali katika uchunguzi wa tendo lile. Serbia ilipokataa sehemu ya mwisho ya masharti, Austria ilitangaza hali ya vita dhidi ya Serbia tarehe 28 Julai 1914.
20231101.sw_2234_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Agosti ya 1914 iliona kupanuka kwa vita hiyo: Warusi walikuwa na mkataba wa usaidizi na Serbia wakatangaza hali ya vita dhidi ya Austria-Hungaria. Hapo wakaingia Wajerumani waliokuwa na mapatano ya usaidizi na Austria-Hungaria wakitangaza hali ya vita dhidi ya Urusi. Urusi kwa upande wake ulikuwa na mkataba wa kusaidiana na Ufaransa, kwa hivyo hali ya vita ikajitokeza pia kati ya Ufaransa na Ujerumani. Ujerumani ilishambulia Ufaransa kwa kuingia Ubelgiji na kupigana na jeshi la nchi hiyo. Mashambulio hayo yalisababisha Uingereza kujiunga na vita dhidi ya Ujerumani.
20231101.sw_2234_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Japan iliyokuwa na mkataba wa kusaidana na Uingereza tangu mwaka 1902 iliona nafasi ya kukamata koloni za Ujerumani katika Bahari Pasifiki ikaingia upande wa maadui wa Ujerumani.
20231101.sw_2234_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Kuanzia Oktoba 1914 Milki ya Osmani (Uturuki) ilijiunga na vita kufuatana na mkataba wake wa siri na Ujerumani.
20231101.sw_2234_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Mwaka 1915 Italia ilijiunga na Wafaransa na Waingereza kwa kushambulia Austria-Hungaria iliyotawala bado maeneo katika kaskazini ya rasi ya Italia, ingawa awali ilikuwa na mkataba na dola hilo.
20231101.sw_2234_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Vita ilipigwa kwa ukali miaka ya 1914-1918. Wajerumani waliingia ndani ya Ufaransa lakini walikwama kabla ya kufikia jiji kuu la Paris. Kwa muda mrefu mstari wa mapambano ulibaki palepale.
20231101.sw_2234_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Katika Mashariki Wajerumani na Waaustria walifaulu kurudisha mashambulio ya Kirusi na kuteka sehemu za Urusi.
20231101.sw_2234_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Katika Kusini mwa Ulaya Waustria walifaulu kwa shida kubwa kuteka Serbia na Montenegro pamoja na Albania. Mapigano dhidi ya Italia yalikwama kwenye milima ya Alpi.
20231101.sw_2234_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Waosmani walishindwa kwa ujumla katika mashambulio yao dhidi ya Warusi katika eneo la Kaukazi na dhidi ya Waingereza katika Misri. Lakini walifaulu kuzuia Waingereza wasifike Uturuki penyewe. Waingereza walipeleka jeshi katika Irak ya kusini wakafaulu kuwarudisha Waosmani hadi kaskazini ya nchi hii.
20231101.sw_2234_18
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Vita ilienea haraka baharini na katika koloni za Ujerumani zilizovamiwa na Waingereza, Wafaransa, Afrika Kusini na Japani. Koloni hizo zilikuwepo Afrika na kwenye visiwa vya Pasifiki pamoja na China. Ujerumani ilikuwa na vikosi vya kijeshi katika koloni za Afrika na pia huko Qingdao nchini China.
20231101.sw_2234_19
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Afrika ya Kusini-Magharibi ya Kijerumani ilivamiwa na Afrika Kusini na jeshi la ulinzi la Kijerumani likajisalimisha mnamo Julai 1915.
20231101.sw_2234_20
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Kamerun ilivamiwa na Ufaransa na Uingereza kutoka koloni zao za Nigeria na Afrika ya Kati ya Kifaransa. Wajerumani wakajisalimisha katika Februari 1916.
20231101.sw_2234_21
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Afrika ya Mashariki ya Kijerumani ilikuwa mahali pa mapigano yaliyoendelea kwa miaka yote ya vita. Jeshi la Ulinzi la Kijerumani lililoitwa Schutztruppe chini ya uongozi wa Paul von Lettow-Vorbeck lilifaulu kutetea eneo la koloni dhidi ya mashambulio ya kwanza ya Waingereza kutoka Kenya hadi 1916. Kwenye Novemba 1914 jeshi la askari 8,000 kutoka Uhindi lilishindwa kwenye mapigano ya Tanga. Hadi mwanzo wa 1916 Waingereza walikusanya jeshi kubwa kutoka Afrika Kusini na Uhindi wakafaulu kutwaa sehemu kubwa ya koloni hadi Agosti 1916. Jeshi la Schutztruppe likaendelea kushika sehemu ya kusini ya koloni hadi 1917 ilipopaswa kuhamia eneo la Kireno katika Msumbiji. Waingereza na Wareno walishindwa kulishika kundi la Kijerumani. Mwaka 1918 Lettow-Vorbeck alirudi Tanganyika akaingia Rhodesia ya Kaskazini alipoambiwa na Waingereza mnamo Novemba 1918 ya kwamba vita ya Ulaya ilikwisha tayari.
20231101.sw_2234_22
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Wakati 1917 mataifa ya Ulaya yalionyesha dalili za uchovu. Katika hali hiyo mabadiliko mawili makubwa yalitokea: Marekani ilijiunga na vita dhidi ya Wajerumani na Urusi ilikuwa na mapinduzi yaliyolazimisha serikali mpya kutia sahihi mapatano ya kumaliza vita dhidi ya Ujerumani iliyoteka maeneo makubwa ya Urusi.
20231101.sw_2234_23
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Nguvu ya Marekani ilionekana haraka na bahati ya Ujerumani ilipungua sana. Austria-Hungaria ilidhoofishwa vilevile.
20231101.sw_2234_24
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Mwaka 1918 iliona mwisho wa vita. Jeshi la Kiosmani lilishindwa hadi serikali ya milki kuomba kusimamishwa kwa vita. Mataifa ya ushirikiano yalikaribia mipaka ya Ujerumani na hapo mgomo wa wanamaji ilifuatwa na migomo ya wafanyakazi katika viwanda vikubwa iliyosababisha mapinduzi yaliyoangusha serikali ya Kaisari Wilhelm II. Migomo ya wanajeshi ililazimisha Austria-Hungaria kuomba kusimamisha vita.
20231101.sw_2234_25
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Milki za Austria na Uturuki zilikwisha zikagawiwa na sehemu zao zilikuwa nchi mpya au nchi zilizoundwa upya.
20231101.sw_2234_26
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Mwaka 1919 mataifa washindi walikutana Paris (Ufaransa) wakikubaliana masharti ya kumaliza hali ya vita dhidi ya Mataifa ya Kati. Mikataba mbalimbali iliandaliwa kati ya washindi na kuwekwa mbele ya nchi zilizoshindwa.
20231101.sw_2234_27
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Mkataba wa Sèvres na Milki ya Osmani (Uturuki) (10 Agosti 1920; ukasahihishwa na mkataba wa Lausanne (24 Julai 1923).
20231101.sw_2234_28
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Mkutano wa Paris ulitoa masharti makali dhidi ya Ujerumani katika Mkataba wa Versailles. Ujerumani uliondolowa makoloni yote yaliyokabidhiwa kwa niaba ya Shirikisho la Mataifa kama maeneo ya kukabidhiwa kwa Uingereza, Ufaransa, Ubelgiji, Japani, Afrika Kusini na Australia.
20231101.sw_2234_29
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Mkutano wa Paris ulikuwa jaribio la kuunda utaratibu mpya duniani uliotakiwa kulindwa na Shirikisho la Mataifa. Lakini ukosefu wa nguvu kwa upande wa Shirikisho la Mataifa pamoja na kuanza na kupanuka kwa mwendo mpya wa Kifashisti iliyochukua utawala katika Italia na Ujerumani vilishinda nia hiyo.
20231101.sw_2234_30
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Wataalamu wasio wachache wanasema mwisho wa vita kuu ya kwanza ulipanda tayari mbegu za Vita Kuu ya Pili ya Dunia.
20231101.sw_2234_31
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Ni kwamba Wajerumani na wakazi wa nchi nyingine zilizoshindwa walijiona wamekosewa haki, lakini pia Waitalia walioshinda kwa gharama kubwa ya damu walijiona wamedanganywa kwa kutotimiziwa ahadi walizopewa ili wasaliti Ujerumani na Austria-Hungaria na kuingia vitani upande wa pili. Hivyo vyama vya mrengo wa kulia viliweza kupata nguvu na hatimaye kupanga kisasi.
20231101.sw_2234_32
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Vita hii ilitwa "Vita ya Dunia" kwa sababu mapigano yalisambaa kote duniani. Sehemu kubwa ya mapigano yalitokea Ulaya na Asia ya Magharibi lakini pia katika makoloni ya Afrika, Asia na Pasifiki. Nchi za Amerika hazikuona mapigano kwenye nchi kavu lakini manowari za Ujerumani zilipigana na mataifa ya ushirikiano mbele ya pwani za Marekani na Amerika Kusini.
20231101.sw_2234_33
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Ilikuwa pia vita ya kwanza iliyopigwa kote duniani ilhali habari zake ziliweza kufika katika muda wa masaa au siku chache kwa mataifa yote kutokana na upatikanaji wa vyombo vya mawasiliano hasa simu za kimataifa na redio.
20231101.sw_2234_34
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Lakini kwa kweli haikuwa vita ya kwanza ya "Dunia" maana vita ya miaka saba (1756-1762) ilipigwa tayari kwenye mabara yote ya Dunia baina ya nchi zenye koloni, hasa Uingereza, Ufaransa na Hispania.
20231101.sw_2234_35
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Encyclopaedia Britannica (12th ed. 1922) comprises the 11th edition plus three new volumes 30-31-32 that cover events since 1911 with very thorough coverage of the war as well as every country and colony. partly online and list of article titles
20231101.sw_2234_36
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
{{citation|last=Grant|first=R.G.|title=Battle: A Visual Journey Through 5,000 Years of Combat|publisher=DK Publishing|year=2005|isbn=978-0-7566-5578-5}}
20231101.sw_2234_37
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
also published by Harper as "Ludendorff's Own Story, August 1914 – November 1918: The Great War from the Siege of Liège to the Signing of the Armistice as Viewed from the Grand Headquarters of the German Army" (original title Meine Kriegserinnerungen, 1914–1918)
20231101.sw_2234_38
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
The Heritage of the Great War/ First World War. Graphic color photos, pictures and music, Netherlands
20231101.sw_2234_39
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
World War I British press photograph collection – A sampling of images distributed by the British government during the war to diplomats overseas, from the UBC Library Digital Collections
20231101.sw_2235_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Réunion (kwa Kifaransa: La Réunion) ni kisiwa cha Afrika na mkoa wa ng'ambo wa Ufaransa (kwa Kifaransa: département d'outre-mer, au DOM) katika Bahari Hindi. Kisheria hali yake ni sawa na mikoa mingine ya Ufaransa hivyo ni pia sehemu ya Umoja wa Ulaya.
20231101.sw_2235_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Reunion iko km 800 upande wa mashariki wa Madagaska. Pamoja na visiwa vya Mauritius na Rodrigues inaunda funguvisiwa la Maskareni.
20231101.sw_2235_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Milima mikubwa ni ya kivolkeno. Upande wa mashariki wa kisiwa ndipo mlima wa "Piton de la Fournaise" wenye urefu wa mita 2611 uliolipuka zaidi ya mara 100 tangu kumbukumbu ya kimaandishi ilipoanzishwa mwaka 1640. Mlipuko wa mwisho hadi leo ulitokea tarehe 4 Oktoba 2005.
20231101.sw_2235_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Baharia Mreno Diego Dias alifika tarehe 9 Februari 1513 ambayo ni sikukuu ya Mt. Apolonia katika mapokeo ya Kanisa Katoliki na kukiita kisiwa kwa jina la mtakatifu huyu "Santa Apolonia", jinsi inavyoonekana katika ramani za kwanza.
20231101.sw_2235_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Baadaye Wareno walitumia jina la nahodha maarufu Pedro de Mascarenhas na kujumlisha visiwa vya Reunion, Mauritius na Rodrigues kwa jina la visiwa vya Maskareni. Visiwa hivyo vilikuwa na umuhimu fulani kama vituo vya kupumzika katika safari kati ya Ulaya na Bara Hindi, mabaharia wakitafuta maji ya kunywa, nafasi ya kutengeneza jahazi zao na kuongeza chakula. Lakini hapakuwa na makao ya kudumu kisiwani.
20231101.sw_2235_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Mwaka 1640 Wafaransa walivamia kisiwa na kukitangaza kuwa mali ya Ufaransa. Walikiita "Île Bourbon" kutokana na jina la familia ya wafalme wa Ufaransa.
20231101.sw_2235_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Ufalme ulipoondolewa wakati wa mapinduzi ya Ufaransa kisiwa kimepewa jina jipya la Reunion tarehe 17 Machi 1793.
20231101.sw_2235_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Wakati wa vita vya Napoleoni, Waingereza walivamia kisiwa mwaka 1810 lakini wakakirudisha kwa Wafaransa baada ya vita (1815).
20231101.sw_2235_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Kuanzia mwaka 1718 mazao ya biashara yalilimwa, kwanza kahawa baadaye pia vanilla na hasa sukari. Kwa kusudi hilo watumwa walipelekwa Reunion kutoka Afrika bara, Bara Hindi na Madagaska.
20231101.sw_2235_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Ufaransa ulitia sahihi maazimio ya Mkutano wa Vienna mwaka 1815 pamoja na kumaliza biashara ya watumwa lakini biashara hii iliendelea kwa siri na kupanuka hasa kwa wafungwa kutoka Afrika. Idadi ya watumwa iliendela kuongezeka hadi kuondolewa hali ya utumwa tarehe 20 Desemba 1848.
20231101.sw_2235_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Baada ya mwisho wa utumwa walowezi walitafuta wafanyakazi huko Bara Hindi wakachukua Wahindi wasiofika kama watu huru kwa miaka na haki kidogo.
20231101.sw_2235_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Mwaka 1946 Reunion ilipewa cheo cha Mkoa wa Ufaransa, na tangu 1997 imekuwa sehemu ya Umoja wa Ulaya.
20231101.sw_2235_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Wakazi wanaonyesha historia hii katika mchanganyiko wao wa aina za watu na tamaduni kutoka pande mbalimbali wa dunia.
20231101.sw_2235_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Sehemu kubwa ya wakazi ni wajukuu wa watumwa au wafanyakazi wasio huru wa zamani wakionyesha tabia za Wahindi, Waafrika na Wachina. Takriban robo ya wakazi ni wa asili ya Ulaya.
20231101.sw_2235_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Kuna lugha tatu tu ambazo huzungumzwa na wakazi wa Réunion, yaani Kifaransa (lugha rasmi), Kitamil na krioli inayotokana na Kifaransa. Pia kuna wahamiaji kutoka visiwa vya jirani ambao huzungumza lugha za Kichina na za Komori, kama vile Kimaore, Kimwali, Kindzwani na Kingazidja.
20231101.sw_2235_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Vikundi hivi havikai mbali: kuna mchanganyiko wa kila aina. Wakazi wengi hufuata Ukristo wa Kikatoliki, wengine Uislamu na Uhindu. Kuna pia Waprotestanti.
20231101.sw_2236_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Agostino wa Hippo (Thagaste, leo Souk Ahras nchini Algeria, 13 Novemba 354 – Hippo, leo Annaba, Algeria, 28 Agosti, 430) alikuwa mtawa, mwanateolojia, padri na hatimaye askofu mkuu wa Hippo.
20231101.sw_2236_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Kutokana na maisha, mafundisho na maandiko yake bora, tangu zamani anaheshimiwa kama mtakatifu na babu wa Kanisa.
20231101.sw_2236_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Katika sehemu za magharibi za Afrika ya Kaskazini wenyeji walikuwa Waberberi kama mama yake, lakini watu wa mjini, kama baba yake, na wenye mashamba makubwa walikuwa wa asili ya Ulaya wakitumia hasa lugha ya Kilatini. Kwa jumla sehemu hii ya Afrika ilikuwa karibu na utamaduni wa Ulaya ya Magharibi.
20231101.sw_2236_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Mama yake (Monika, anayeheshimiwa kama mtakatifu) alikuwa Mkristo, kumbe baba (Patrisi) alifuata dini ya jadi ya kuabudu miungu mingi kabla hajabatizwa mwishoni mwa maisha yake.
20231101.sw_2236_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Agostino alizaliwa tarehe 13 Novemba 354 mjini Thagaste katika mkoa wa Numidia. Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Aurelius Augustinus. Wakati ule Ukristo ulikuwa tayari dini iliyokubaliwa katika Dola la Roma; dhuluma dhidi ya Wakristo zilikuwa zimekwisha rasmi mwaka 313 kwa Hati ya Milano iliyotolewa na Konstantino Mkuu ili kuruhusu uhuru wa dini.
20231101.sw_2236_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Alikuwa na wadogo wawili, mmoja mwanamume, Naviji, na mwingine wa kike, ambaye hatujui jina lake, ila kwamba baada ya kufiwa mume wake akawa mmonaki na abesi.
20231101.sw_2236_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Monika alimuathiri sana Augustino na kumlea katika imani ya Kikristo. Mwanae aliweza kuandika kwamba alipokuwa ananyonya maziwa ya mama, alifyonza pia upendo kwa jina la Yesu. Akiwa mtoto alipokea chumvi kama ishara ya kuingia ukatekumeni akabaki daima anavutiwa na Yesu, hata alipozidi kusogea mbali na Kanisa lake.
20231101.sw_2236_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Alipata elimu yake nzuri ya lugha na ya ufasaha wa kuhubiri huko Thagaste, Madaura na hata katika Chuo Kikuu cha Karthago (karibu na Tunis) ingawa hakuwa daima mwanafunzi mzuri, mbali ya kuwa na akili ya pekee. Alimudu kikamilifu Kilatini, lakini si sana Kigiriki.
20231101.sw_2236_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Akiwa huko Karthago, mwaka 373 alisoma kitabu cha maadili cha Sisero ambacho kilibadilisha hisia zake hivi kwamba “matumaini yote ya bure yakawa hayana maana kwangu, nikatamani hekima isiyokufa kwa ari isiyosemeka moyoni mwangu”.
20231101.sw_2236_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Lakini kwa kuamini ukweli haupatikani pasipo Yesu, ambaye hatajwi katika kitabu hicho, alianza kusoma Biblia, ila hakupenda tafsiri ya Kilatini wala yaliyomo, akiyaona tofauti na mtindo wa falsafa inayotafuta ukweli. Hivyo alisogea mbali na dini iliyoonekana kutotia maanani hoja za akili ambayo pamoja na imani ndizo “nguvu mbili zinazotuongoza kwenye ujuzi”. Ndivyo alivyoandika baadaye, akitoa pia kauli mbili za msingi kuhusu kulenga ukweli: “Usadiki ili uelewe”, halafu “uelewe ili usadiki”.
20231101.sw_2236_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Hapo, kusudi asiishi bila Mungu, alijitafutia dini ya kuridhisha hamu yake ya kujua ukweli na ya kuwa karibu na Yesu, akajiunga kwa karibu miaka 10 na Umani. Dini hiyo ilidai kufuata akili na kufafanua sababu ya mabaya kuwepo duniani kutokana na chanzo cha pili cha ulimwengu kilicho kinyume cha Mungu, ikikataa Agano la Kale ili kufuata Ukristo wa kiroho.
20231101.sw_2236_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Augustino alipenda pia maadili ya dini hiyo kwa sababu yalikuwa yanawadai sana baadhi ya waumini tu, yakiwaacha wengine wote wasijali zaidi. Hatimaye Wamani walikuwa wanasaidiana kupanda chati katika jamii. Lakini alipokutana na askofu wao Fausto, alikosa imani nao kwa kuona alivyoshindwa kujibu maswali yake.
20231101.sw_2236_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Baada ya kuhitimu masomo, alifundisha Kilatini huko Thagaste (374), halafu namna ya kuhubiri huko Kartago (375-383), akaendelea kufanya hivyo nchini Italia, kwanza Roma (384), halafu Milano (384-386), makao makuu ya Dola, alipopata kazi ya heshima sana.
20231101.sw_2236_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Wakati huo wote aliendelea kuishi bila ndoa na mwanamke aliyemzalia mtoto wa kiume mwenye akili sana, Adeodatus.
20231101.sw_2236_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Mahubiri bora ya Ambrosi aliyokwenda kuyasikiliza kwanza ili kuzidi kupata mbinu za kutoa hotuba, yalizidi kumgusa moyoni na kumfanya asadiki mamlaka ya Biblia nzima inavyosomwa rasmi na Kanisa. Aliona uzuri na udhati wa masimulizi ya Agano la Kale yakifafanuliwa kiroho kama mifano ya mambo ya Agano Jipya inayomuelekea Kristo, kiini cha yote. Katika barua za Mtume Paulo, Augustino alimtambua Kristo kama mwokozi, si mwalimu tu.
20231101.sw_2236_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Hasa aliguswa na maneno ya Rom 13:13-14 aliyoyasoma kwa kufungua tu kitabu kisha kumsikia mtoto wa jirani akiimba kwa kukariri, “Chukua usome, chukua usome”. Alitambua ameambiwa mwenyewe na Mungu maneno hayo yakimdai aachane na matendo ya mwili akamvae Kristo.
20231101.sw_2236_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Kisha kuongoka hivyo tarehe 15 Agosti 386, akiwa na umri wa miaka 32, aliacha kufundisha na hata kuishi na mama mtoto, akatawa kwa muda Cassiciaco karibu na ziwa la Como, akiwa na Monika, Adeodatus na marafiki wachache, akarudi Milano alipobatizwa na Ambrosi pamoja na mwanae na rafiki yake Alipio usiku wa Pasaka ya mwaka 387.
20231101.sw_2236_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Baada ya kubatizwa na kunuia akaishi kitawa Thagaste, alirudi Afrika; njiani, huko Ostia, bandari ya Roma, alifiwa mamaye. Ndoto yake ilikuwa kujitosa katika maisha ya sala na masomo pamoja na marafiki wake. Lakini hiyo ilidumu miaka mitatu tu.
20231101.sw_2236_18
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Mwaka 391 bila kutarajia alipewa daraja ya upadri huko Hippo, alipoanzisha monasteri, akigawa muda wake kati ya sala, masomo na mahubiri, halafu mwaka 395 akachaguliwa kuwa askofu msaidizi wa mji huo na mwaka 397 akawa askofu wa jimbo hilo.
20231101.sw_2236_19
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Ilimbidi akubali matakwa ya Mungu kwake, kwamba ajitoe kwa wengine na kuwashirikisha ujuzi wake ili kuishi kweli kwa ajili ya Kristo. “Kuhubiri mfululizo, kujadili, kusisitiza, kujenga, kuwa tayari kwa yeyote ni jukumu kubwa sana, ni mzigo mzito, ni juhudi ya ajabu”. Ilikuwa kama wongofu wake wa pili.
20231101.sw_2236_20
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Hapo alitegemeza maskini na mayatima, alisimamia malezi ya wakleri, akiwadai waishi pamoja, akaeneza monasteri za kiume na za kike. Alifanya adhimisho la ekaristi kuwa kiini cha maisha ya jumuia zake.
20231101.sw_2236_21
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Mahubiri yake mengi yanaonyesha alivyojua kujadiliana na umati akitumia maneno rahisi na ya kawaida na hata ucheshi katika kulinganisha Neno la Mungu na mazingira yao.
20231101.sw_2236_22
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Kwa tabia yake karimu na pendevu, hisia zake, uvumilivu na utayari wa kusamehe alifanya hata maadui kadhaa kuwa marafiki.
20231101.sw_2236_23
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Maisha yake ya Kiroho yaliyoongoza uandishi wa kanuni yake kwa watawa yamefuatwa na mashirika mengi ya kiume na ya kike hadi leo.
20231101.sw_2236_24
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Kwa miaka 35 mpaka kifo chake, mbali na kutimiza majukumu yake mengi, aliendelea kueleza na kutetea imani sahihi ya Kikristo kwa mahubiri, maandishi na vitabu vingi sana (hata vya mitindo mipya) dhidi ya aina zote za uzushi za wakati ule: Wamani, Wadonati, Wapelaji na Waario. Hivyo tangu alipokuwa hai, hakuongoza Kanisa la Afrika Kaskazini tu, bali alitegemeza imani kila mahali.
20231101.sw_2236_25
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Kwa njia hiyo amekuwa mwalimu muhimu sana katika Ukristo, hasa wa Magharibi (yaani Kanisa Katoliki na katika Uprotestanti uliotokea katika Kanisa hilo. Kwa mfano Martin Luther alimtaja kuwa baba yake wa kiroho pamoja na Mtume Paulo). Augustino alijilisha tunu za Kikristo na kutokeza utajiri wake wa dhati, akibuni mawazo na mifumo ya kulisha vizazi vijavyo. Hata nakala za vitabu vyake ni nyingi sana, zikithibitisha vilivyopendwa na kuenea.
20231101.sw_2236_26
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Hivyo aliathiri sana ustaarabu wa Magharibi unaozidi kuenea leo duniani kote. Mawazo yote yaliyomtangulia yanakutana katika maandishi yake na kuwa chemchemi ya mafundisho kwa nyakati zilizofuata.
20231101.sw_2236_27
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Tarehe 26 Septemba 426 alikusanya waamini ili kuwatambulisha padri Eraklio aliyemchagua kama mwandamizi wake naye aweze kutumia miaka yake ya mwisho katika kusoma kwa dhati zaidi Maandiko matakatifu. Watu walimkubalia kwa shangwe.
20231101.sw_2236_28
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Miaka minne iliyofuata Augustino alifanya kazi kubwa kwa kumaliza vitabu mbalimbali na kuanza kuandika vingine. Kati ya vile vya wakati huo kuna “Retractationes” (yaani “Kupitia Upya” vile vilivyotangulia), ambamo tunaona unyofu wake kwa kuwa tayari kurekebisha baadhi ya mafundisho aliyowahi kuyatoa. Hivyo mpaka mwisho alionyesha alivyolenga ukweli kuliko yote.