_id
stringlengths
15
22
url
stringlengths
31
150
title
stringlengths
1
86
text
stringlengths
100
23.8k
20231101.sw_2488_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Jamhuri ya Madagaska (au Madagasikari) inaenea katika kisiwa cha Madagaska (pia: Bukini) kilichopo katika Bahari Hindi mashariki kwa pwani ya Afrika.
20231101.sw_2488_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Jina Madagaska lina maana ya "Kisiwa kikubwa" na linatokana na lugha ya wenyeji, Wamalagasi ambao waongea Kimalagasi.
20231101.sw_2488_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Upekee wa kisiwa unatokana na kwamba kilimeguka kutoka India miaka milioni 88 hivi iliyopita, halafu kilibaki bila watu hadi karne ya 5 hivi BK.
20231101.sw_2488_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Kisiwa hicho ni pia mazingira makubwa ya aina ya violezo ambayo ni asilimia 5 ya violezo vyote vya mimea na wanyama vya dunia nzima.
20231101.sw_2488_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Asilimia 90 ya viumbehai asili ni maalumu wa Madagaska, kama vile wanyama aina ya kima awali wanaoitwa lemuri, ndege ambao waambukiza ugonjwa na mti wa mbuyu.
20231101.sw_2488_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Baadaye tu walihamia watu kutoka bara la Afrika (mwaka 1000 hivi) na wengineo (Waarabu, Wahindi, Wazungu, Wachina n.k.).
20231101.sw_2488_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Watawala walikuwa watu kutoka familia ya Andrianampoinimerina, mwanzilishi wa taifa hilo, ambaye alikuwa ametokea katika kabila la Wamerina
20231101.sw_2488_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Kabila hilo lilikuwa kubwa na muhimu kuliko yote 18 ya kisiwa hicho. Makazi yake yalikuwa katika uwanda wa juu wa kati lakini lilienea sehemu kubwa ya Bukini.
20231101.sw_2488_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Wamerina walikuwa na makao makuu ya utawala wao Antananarivo; baada ya kugawiwa kwa ufalme wao mnamo 1710 kitovu cha malaka kati ya Wamerina ikahamia kwenye mlima wa Ambohimanga lakini tangu kuunganishwa kwa Wamerina mnamo 1794 mji mkuu ukulikuwa tena Atananarivo. Kutoka hapo waliweza kueneza mamlaka yao katika sehemu nyingine za kisiwa hicho.
20231101.sw_2488_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Makabila yote ya wenyeji yalizungumza lugha moja na yalikuwa na mila na desturi zinazofanana, hivyo yaliweza kujenga umoja wa kiutamaduni uliowafanya wawe jamii moja kimsingi.
20231101.sw_2488_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Watawala hao wa kifalme waliweza kutekeleza mambo mbalimbali kuendeleza Bukini katika vipindi vyao kabla ya kuja kwa wageni kutoka Uingereza na Ufaransa ambao kwa kiasi fulani ulidhoofisha mamlaka ya kifalme.
20231101.sw_2488_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Kisiwa hicho hatimaye kiligeuzwa kuwa koloni la Ufaransa. Hii ni kwa kuwa, ingawa sera ya kuisasisha ya Bukini kwa namna fulani iliimarisha uwezo wa nchi hiyo wa kutetea uhuru wake, lakini kwa ujumla sera hiyo ilidhoofisha ufalme huo kwa kuongeza utegemezi wake kwa mataifa ya kigeni.
20231101.sw_2488_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Mwaka 2018 idadi ya wakazi ilikadiriwa kuwa milioni 26.3. Wenyeji wengi wana mchanganyiko wa damu: DNA inaonyesha kuwa wakazi wa kwanza kutoka Indonesia wameichangia asilimia 50 hivi na Waafrika vilevile. Wanaoishi sehemu za ndani ni wa Kiindonesia zaidi, wakati wale wa pwani ni wa Kiafrika zaidi.
20231101.sw_2488_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Lugha ya taifa ni Kimalagasi. Lugha rasmi za Madagaska ni Kimalagasi na Kifaransa (angalia pia orodha ya lugha za Madagaska).
20231101.sw_2488_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Mwaka 1993 nchini Madagaska kulikuwa na dini za jadi (52% hivi), Ukristo (41%, Waprotestanti wakiwazidi kidogo Wakatoliki), Uislamu (7% hivi) n.k. Tangu hapo wafuasi wengi wa dini za jadi wameongokea Ukristo, hasa wa Kiprotestanti.
20231101.sw_2488_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madagaska
Madagaska
Pamoja na kutokea mazingira tofauti sana, Wamalagasi wamechanganyikana sana na kuwa na utamaduni na lugha aina moja, ya Kiindonesia zaidi.
20231101.sw_2490_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Itifaki
Itifaki
Itifaki (kutoka neno la Kiarabu; pia "protokali", kutoka Kiingereza "protocol") ni orodha au mpangilio wa visa unaotumika katika kuendesha sherehe, mkutano, mjadala na kadhalika kutokana na utaratibu uliowekwa. Mathalani katika shughuli za mikutano ni kiongozi gani anatakiwa kuingia kwanza, kisha nani afuatie na nani awe wa mwisho kuingia katika sehemu ya mkutano. Mwenyeji wa mkutano anatakiwa kukaa upande gani na mgeni mwalikwa anatakiwa kukaa upande gani. Kama ni shughuli ya kitaifa ni wimbo wa taifa gani unatakiwa uanze, ule wa Rais mwenyeji au wa Rais mgeni? Baada ya mkutano nani anatakiwa kutoka kwanza na nani awe wa mwisho. Mambo kama haya au utaratibu kama huu ndio huitwa itifaki. Ila mwanafunzi afahamu kwamba itifaki ikitumika katika isimujamii inaleta dhana tofauti na maelezo haya.
20231101.sw_2492_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Gaius Julius Caesar (tamka gayus yulius kaesar - 100 - 44 KK) alikuwa kiongozi wa kisiasa na wa kijeshi wa Roma ya Kale.
20231101.sw_2492_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Kama kiongozi wa kijeshi aliteka Gallia (leo: Ufaransa) na kuifanya jimbo la Kiroma. Kutokana na hiyo lugha ya Kifaransa ni karibu sana na Kilatini, lugha ya Roma ya Kale.
20231101.sw_2492_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Waroma wa Kale walimheshimu kushinda viongozi wote waliomfuata au kutangulia akatangazwa kuwa mungu. Jina lake lilipata kuwa neno kwa ajili ya cheo cha watawala wa Kiroma waliomfuata. Kutokana na badiliko hilo la jina "Caesar" kuwa cheo, lugha mbalimbali zilipokea cheo hicho kama vile Kijerumani ("Kaiser"), Kirusi ("Tsar") na Kiswahili ("Kaisari" - kutokana na neno la Kijerumani).
20231101.sw_2492_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Aliunda kalenda ambayo imekuwa msingi wa kalenda ya kimataifa leo (Kalenda ya Juliasi). Kwa heshima yake, mwezi wa saba unaitwa Julai.
20231101.sw_2492_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Katika historia ya Roma alifunga kipindi cha Jamhuri - kilichofuata ni Dola la Roma aliloliwekea misingi.
20231101.sw_2492_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Alizaliwa katika familia ya makabaila wenye nafasi katika Senatus ilivyoitwa bunge la Roma. Aliingia katika siasa, akachaguliwa kwa vyeo mbalimbali kwa vipindi vya kawaida wa miezi kadhaa hadi mwaka moja.
20231101.sw_2492_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Cheo chake muhimu cha kwanza kilikuwa mkuu wa koloni la Kiroma la Hispania. Alifaulu kushinda ghasia ya Wahispania wenyeji waliojaribu kuwafukuza Waroma kutoka nchini mwao. Caesar aliporudi Roma alitajirika na kujipatia sifa kama kiongozi wa kijeshi pia mwanasiasa aliyeokoa koloni muhimu la Hispania.
20231101.sw_2492_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Baadaye Caesar alijiunga na wanasiasa wawili wengine: Gnaeus Pompeius Magnus aliyekuwa mkuu wa wanajeshi na Marcus Licinius Crassus aliyekuwa tajiri kushinda Waroma wote. Wote watatu waliunda umoja ulioitwa "triumviratus", yaani umoja wa wanaume watatu, wakashika mamlaka katika dola. Caesar alichaguliwa kwa cheo kikuu yaani Konsul kwa mwaka 59 KK. Baada ya mwisho wa kipindi chake alijipatia cheo cha Prokonsul au gavana wa eneo la Gallia ya Kiroma (Italia ya Kaskazini na eneo dogo la Ufaransa ya Kusini).
20231101.sw_2492_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Alitumia nafasi hii kuanzisha vita dhidi ya makabila ya Gallia huru yaani eneo lote la Ufaransa, Uswisi na Ubelgiji ya leo. Katika miaka minane ya 58 - 51 KK alitwaa Gallia yote. Aliingia pia ndani ya Germania (Ujerumani) na kuvuka bahari aliposhambulia upande wa kusini wa Britannia. Aliandika kitabu cha "De bello gallico" (yaani Vita ya Gallia) akieleza mapigano yake. Kitabu hicho kina habari muhimu za kihistoria juu ya utamaduni wa makabila ya Gallia, Germania na Britannia aliyopigana nayo.
20231101.sw_2492_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Baada ya kufanikiwa Gallia na kujenga jeshi kubwa tena hodari, wanasiasa wengine huko Roma walianza kumwogopa wakajaribu kumzuia asirudi Italia. Mwenzake Crassus alikuwa amekufa tayari vitani mashariki mwa dola; mwenzake Pompeius aliomwogopa Caesar akajaribu kushawishi viongozi wengine kumsimamisha.
20231101.sw_2492_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Lakini mwaka 49 KK Caesar aliongoza wanajeshi lake warudi Italia. Pompeius na wapinzani wake walitoka Roma wakaenda Ugiriki iliyokuwa jimbo la Kiroma. Mwaka 48 KK Caesar akachaguliwa tena kuwa Konsul. Akamfuata Pompeius kwa jeshi lake akamshinda katika mapigano. Pompeius alikimbia kwenda Misri lakini mfalme Ptolemaio XIII alimwogopa Caesar akamwua Pompeius akampatia Caesar kichwa chake alipofika Misri. Caesar alikutana na dada yake Ptolemaio Kleopatra akampenda na kuzaliana naye mwana wake pekee. Akamsaidia Kleopatra kuwa malkia na mtawala wa Misri.
20231101.sw_2492_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Caesar alirudi Roma kutoka Misri akiwa mshindi dhidi ya wapinzani wote. Bunge la Senatus lilimpa cheo na madaraka ya dikteta kwa miaka 10. Baada ya ushindi mwingine dhidi ya wapinzani huko Hispania bunge lilibadilisha azimio hilo kumpa cheo cha dikteta wa maisha. Caesar alipokea azimio hili.
20231101.sw_2492_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Sasa sehemu ya wabunge waliogopa ya kwamba nia yake ilikuwa kuwa mfalme wa Roma - jambo lililokuwa marufuku katika jamhuri ya Roma. Kikundi cha wabunge -wote makabaila wa familia za kale- kiliunga mikono wakamwua Caesar bungeni tarehe 15 Machi 44 KK kwa kumdunga kisu mara 23. Caesar anasemekana alimtambua mpwa wake Brutus akamwuliza kwa maneno yake ya mwisho: "Hata wewe mwanangu?"
20231101.sw_2492_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Julius%20Caesar
Julius Caesar
Caesar hakuwa na watoto ila huyu mwana wa Kleopatra asiyekuwa Mroma. Kabla ya kifo chake alikuwa amempanga mtoto mpwa wake Oktaviano. Huyu Oktaviano -aliyejulikana baadaye kama Augusto na mtawala wa kwanza wa Dola la Roma- alilipiza kisasi chake katika kipindi cha vita ya wenyewe kwa wenyewe na kuua wapinzani wote wa Caesar.
20231101.sw_2494_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kurow
Kurow
Kurow ni mji mdogo kwenye bonde la Waitaki kwenye kisiwa cha kusini cha New Zealand katika wilaya ya Otago. Mazingira ya Kurow ina miradi mbalimbali ya kutengeneza umeme kwa nguvu ya maji. Kuna kilimo cha matunda hasa mizabibu.
20231101.sw_2494_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kurow
Kurow
Kuna mvutano kuhusu asili ya jina la mji kama imetokana na neno la Wamaori wazalendo au kutoka kwa mji wa Kurów.
20231101.sw_2495_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gallia
Gallia
Gallia ilikuwa jina la kilatini kwa ajili maeneo yaliyokaliwa na "Wagallia". Hili ilikuwa namna jinsi Waroma wa Kale walivyowaita majirani wao Wakelti.
20231101.sw_2495_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gallia
Gallia
Kijiografia eneo hili lilijumlisha Ufaransa, Uswisi, Ubelgiji na Italia ya Kaskazini ya leo. Wakelti au Wagallia walikalia pia Uingereza ya Kusini (=Britania) na Hispania (=Iberia) lakini maeneo haya hayakuhesabiwa kuwa sehemu ya "Gallia" na Waroma. Wakelti walikuwa pia kati ya wakazi wa kale wa Ujerumani kabla ya uvamizi huko wa Wagermanik wenyewe.
20231101.sw_2495_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gallia
Gallia
Karibu habari zote za kimaandishi kuhusu Gallia na Wagalli zimetokana na Waroma wa kale. Sehemu kubwa ya habari zinapatikana katika kitabu cha Caesar "Vita ya Gallia".
20231101.sw_2495_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gallia
Gallia
Kuna pia mabaki ya kiarkolojia hasa makaburi pamoja na vitu vya maisha ya kila siku vilivyoweka makaburini kwa imani ya kwamba vitawasaidia marehemu katika ahera. Arkiolojia ya makaburi inaonyesha ya kwamba Wakelti (Wagallia) walikuwa sehemu ya biashara ya kimataifa pia walikuwa na mafundi wenye uwezo wa kutengeneza vitambaa na nguo, pia na wahunzi na wafinyanzi.
20231101.sw_2495_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gallia
Gallia
Mnamo mwaka 390 KK kabila fulani la Wagallia chini ya kiongozi Brennus lilivamia Italia na mji wa Roma lakini walishindwa kuteka boma la mji. Kwa muda mrefu Waroma walihofia majirani ya kaskazini.
20231101.sw_2495_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gallia
Gallia
Kuanzia mwaka 200 KK Waroma walikuwa waliendelea kisiasa, kiuchumi na kijeshi wakafaulu kuteka "Gallia Cisalpina" (Gallia upande wa kusini wa milima ya Alpi) ambayo leo hii ni Italia ya Kaskazini. Ikawa jimbo la Kiroma.
20231101.sw_2495_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gallia
Gallia
Kuanzia mwaka 125 KK Waroma walianza kuvamia sehemu za pwani la Gallia pamoja na bonde la mto wa Rhone. Ikawa jimbo la Gallia Narbonensis. Mji mkuu ulikuwa mji wa Narbo (leo: Narbonne).
20231101.sw_2495_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gallia
Gallia
Sehemu nyingine ya Gallia imebaki nchi huru ya makabila yaliyojitawala. Mwaka 58 KK mwanasiasa na jenerali Mroma Caesar akawa gavana wa Gallia Cisalpina pia Narbonensis. Alichukua nafasi ya vita kati ya makabila ya Wagallia katika eneo la Uswisi kuingilia ndani ya mambo ya Gallia huru. Katika vita ya miaka nane alishinda wapinzani wote. Mwaka 51 KK Gallia yote ikawa chini ya utawala wa Kiroma.
20231101.sw_2495_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gallia
Gallia
Katika karne zilizofuata Gallia imekuwa sehemu halisi ya Dola la Roma. Inaonekana Wagallia wenyewe walikubali utawala wa Kiroma hasa baada ya kupewa uraia wa Kiroma. Lugha ya Kilatini ilitumika kwa ajili ya habari za kiutawala ikapokelewa polepole na wenyeji. Kilatini hiki kilikuwa msingi wa lugha ya Kifaransa kilichotokea baadaye.
20231101.sw_2497_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
{| border="1" cellpadding="2" cellspacing="0" align="right" width="330px" style="margin-left:15px; border-collapse:collapse; border-color:#f2f2f4"
20231101.sw_2497_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Misri (kwa Kiarabu: مصر, Masr) ni nchi ya Afrika ya Kaskazini-Mashariki ikiwa na eneo la Rasi ya Sinai kwenye bara la Asia pia.
20231101.sw_2497_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Ni nchi yenye wakazi milioni 100 na mji mkuu Kairo ni kati ya miji mikubwa zaidi duniani (zaidi ya milioni 9).
20231101.sw_2497_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Jina la Misri kwa Kiswahili linalingana na jina rasmi la مصر Miṣr katika lugha ya Kiarabu. Ni jina la Kale jinsi inavyoonekana katika Biblia ya Kiebrania ambako inaitwa Mitzrayim (מִצְרַיִם, wingi wa Misri kumaanisha Misri ya Juu na Misri ya Chini). Maana ya jina hili ni "nchi".
20231101.sw_2497_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Katika enzi ya Misri ya Kale nchi iliitwa na wenyeji Km.t (Kemet) inayomaaniosha "nchi nyeusi" kwa kutaja ardhi "nyeusi" (=yenye rutuba) ya bonde la Naili, tofauti na ardhi nyekundu ya jangwa.
20231101.sw_2497_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Majina ya Kizungu ya "Egypt" (ing.), "Egypte" (far.), "Ägypten" (jer.) yanatokana na jina la Kigiriki Αίγυπτος (aigyptos). Hakuna hakika juu ya maana asilia ya neno. Wengine huamini neno limetokana na jina la hekalu muhimu mjini Memphis. Neno hili ni pia asili ya jina "Wakopti" na hii ni jinsi wenyeji wa Misri walivyojiita wakati wa utawala wa Dola la Roma
20231101.sw_2497_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Misri imepakana na Bahari ya Mediteranea, Israel, Eneo la mamlaka ya Palestina, ghuba ya Suez, ghuba ya Aqaba, Bahari ya Shamu, Sudan na Libya. Umbo la nchi hufanana na trapeza.
20231101.sw_2497_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Tabianchi ni yabisi sana na maeneo makubwa ni jangwa, pamoja na oasisi na maeneo ya savana ya miiba. Karibu wananchi wote huishi ndani ya kanda nyembamba ya bonde la mto Naili. Bonde hili linavuka nchi kuanzia mpakani na Sudani katika kusini kuelekea kaskazini hadi mdomo wa mto kwenye Bahari ya Mediteranea. Ardhi pande zote mbili za mto inamwagiliwa na kulimwa. Kwatika umbali mdogo kutoka mto jangwa inaanza.
20231101.sw_2497_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Takriban kilomita 250 kabla ya mdomo Naili inagawanyika katika mikono mbalimbali na kuunda delta ya mto.
20231101.sw_2497_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Kanda hili bichi si zaidi ya asilimia 5 za eneo lote la nchi, ila 98% za wananchi wote huishi humo. Kwa hiyo Naili huitwa "Baba wa Misri", kwa maana bila mto huo pasingekuwepo taifa hili.
20231101.sw_2497_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Oasisi ya mto Naili: mto umechimba bonde kama mfereji katika mwamba asilia ya nchi. Ndani ya bonde hili jembamba lenye upana hadi kilomita 25 kuna kanda la ardhi yenye rutuba kuanzia Ziwa Nasser hadi Kairo.
20231101.sw_2497_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Delta ya Naili: upande wa kaskazini wa Kairo Naili inajigawa katika mikono miwili mikuu na kati ya mikono hiyo miwili kuna eneo la delta yenye km² 23,000 kwa umbo la pembetatu. Inajaa ardhi ya rutuba kutokana na matope ya Naili iliyopelekwa huko na mafuriko katika muda wa miaka elfu kadhaa. Eneo hili linalimwa kote na kumwagiliwa likiwa na mikono midogo ya kando ya Naili.
20231101.sw_2497_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Jangwa la Magharibi: ni eneo kubwa upande wa magharibi wa Naili lisilo na milima mikubwa. Kaskazini mwake kuna tambarare ya Lybia iliyo takriban mita 240 juu ya uwiano wa bahari. Kusini mwake linainama eneo la mbonyeo wa Qatara hadi mita 133 chini ya UB, halafu jangwa linapanda tena juu kuelekea kusini magharibi.
20231101.sw_2497_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Ndani ya eneo hili kubwa kuna beseni kadhaa pamoja na oasisi za Siwa, Bahariyya, Farafra, Dakhla na Charga. Kilomita 100 upande wa kusini-magharibi wa Kairo kuna oasisi kubwa ya Fayyum pamoja na ziwa la Warun lenye eneo la km² 230.
20231101.sw_2497_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Jangwa la Mashariki: ni eneo upande wa mashariki wa mto Naili. Huko kuna milima inayopanda juu ya mita 2,000 pamoja na wadi yaani bonde kali. Jangwa linatelemka hadi mfereji wa Bahari ya Shamu ambao ni sehemu ya Bonde la Ufa linaloanza Palestina na kuendelea hadi Ziwa Nyasa.
20231101.sw_2497_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Katika kipindi cha historia ya awali tangu takriban miaka 6000 KK wakazi wa Misri walikuwa na kilimo cha nafaka. Walikuwa na teknolojia ya Zama za Mawe. Wakati ule Jangwa la Sahara lilipanuka na kuwalazimisha watu kukaa karibu zaidi kwenye mto Nile na kwenye oasisi kama Faiyum.
20231101.sw_2497_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Katika mazingira ya jangwa bonde la Nile liliwavuta watu kutokana na rutuba kubwa ya ardhi iliyoongezwa kila mwaka upya kwa njia ya mafuriko yaliyotandaza matope kutoka nyanda za juu kwenye ardhi.
20231101.sw_2497_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Utafiti wa akiolojia umegundua ya kwamba wakazi hao wa bonde walianzisha tamaduni mbalimbali zilizokuwa tofauti kati yao lakini zilizowasiliana kibiashara. Mifano ya kwanza ya mwandiko wa hiroglifi imepatikana kwenye vyungu vilivyofinyangwa mnamo 3200 KK.
20231101.sw_2497_18
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Katika karne zilizofuata, mnamo 3000 KK yalitokea muungano wa sehemu mbalimbali wa Misri chini ya wafalme wenye nguvu wanaotajwa kwa cheo cha farao. Katika historia iliyotungwa na waandishi Wagiriki wa Kale ni kwa kawaida Farao Menes anayetajwa kuwa mtawala wa kwanza aliyeunganisha Misri ya Kaskazini na Misri ya Kusini kuwa milki moja. Lakini leo hii inajulikana kuna wafalme waliomtangulia waliokuwa tayari na milki kubwa. Hata hivyo Menes alianzisha utawala wa nasaba mbalimbali zilizofuatana, pamoja na vipindi vya kati ambako vita vya wenyewe kwa wenyewe na mafarakano katika nasaba ziliweza kugawa nchi tena kwa muda.
20231101.sw_2497_19
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Mafarao wa Misri ya Kale walifaulu mara kadhaa kupanua mamlaka yao hadi ndani ya Sudani ya leo, na pia kwa vipindi juu ya sehemu za Palestina na Syria ya leo. Mara kadhaa wavamizi kutoka nje walifaulu kushika utawala juu ya Misri kama vile Wahyksos kutoka Palestina / Kanaan, Wakushi kutoka Nubia au watu kutoka Lybia. Wavamizi hao walitumia pia cheo cha Farao wakijaribu kuendeleza tabia nyingi za milki za awali. Hatimaye wote walipinduliwa tena na viongozi wazalendo walioanzisha nasaba mpya.
20231101.sw_2497_20
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Mwaka 525 KK mfalme wa Uajemi aliteka Misri. Kwa kipindi kifupi Wamisri waliweza kuwaondoa tena na kuendelea chini ya watawala wazalendo.
20231101.sw_2497_21
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Uvamizi wa Aleksander Mkuu mwaka 332 KK ulianzisha kipindi cha Misri ya Kigiriki. Mji mpya wa Aleksandria ulikuwa mji mkuu mpya. Jemadari wa Wagiriki walitumia pia cheo cha Farao na kutawala kama nasaba ya Ptolemi, lakini tabaka ya watawala ilikuwa na utamaduni tofauti sana na wananchi wakulima wa kawaida.
20231101.sw_2497_22
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Wakati wafalme Wagiriki waliendelea kutawala milki mpya ilienea kutoka magharibi ya Mediteranea iliyokuwa Dola la Roma. Malkia wa mwisho wa Misri alikuwa Kleopatra. Baada ya kifo chake Misri ilikuwa jimbo la Dola la Roma.
20231101.sw_2497_23
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Utawala wa Kiroma uliendelea kwa karne 6. Katika muda huu Ukristo ulianza kuenea katika Misri. Nchi ilikuwa haraka kitovu muhimu cha imani mpya na Ukristo wa Kikopti uliendeleza liturgia na mapokeo ya pekee na kupeleka mfumo huu wa Ukristo hadi Sudani na Ethiopia.
20231101.sw_2497_24
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Lakini hali ilikuwa ngumu baada ya magavana wa Roma na baadaye wa Bizanti kujaribu kuwalazimisha Wakopti kufuata liturgia na mafundisho ya Kanisa rasmi yaani Kanisa la Kiorthodoksi.
20231101.sw_2497_25
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Kwenye mwaka 639 jeshi la Waarabu Waislamu lilivamia Misri na kuteka nchi yote katika muda wa miaka 3. Wenyeji wengi waliokuwa Wakristo Wakopti hawakuwapinga kwa sababu walipendelea Waislamu kuliko Wakristo Waorthodoksi waliowahi kuwakandamiza vikali katika miaka iliyotangulia. Kwa karne kadhaa idadi kubwa bado walikuwa Wakristo lakini kuanzia karne ya 12 idadi ya Waislamu ilikuwa kubwa zaidi kwa sababu Wakristo walipaswa kulipa kodi zaidi na vipindi kadhaa vya mateso vilitokea na yote ilisababisha kuhamia kwa wananchi kwenda dini mpya.
20231101.sw_2497_26
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Watawala wapya hawakutumia Aleksandria kuwa mji mkuu bali walianzisha mji mpya wa Fustat karibu na Babylon ya Misri, pale ambako mto Nile unajigawa na kuanzisha delta yake.
20231101.sw_2497_27
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Hadi mwaka 969 Misri ilitawaliwa na watawala Waislamu Wasunni waliokuwa kwa jina magavana na wawakilishi wa makhalifa huko Dameski au Baghdad, lakini zaidi watawala wa kujitegemea hali halisi. Mwaka 969 Wafatimi kutoka sehemu za Tunisia ya leo walivamia na kuteka nchi wakianzisha ukhalifa wao. Wafatimi walikuwa Waismaili, wakati ule mwelekeo wa kimapinduzi ya Shia. Walianzisha makao makuu yao nje ya Fustat na Babylon wakaiita "Al-Qahira", yaani mwenye ushindi, na hii ilikuwa chanzo cha Kairo ya leo.
20231101.sw_2497_28
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Wakati wa vita za misalaba Wafatimi walishindwa na askari wa Wasunni waliendelea kuunda nasaba ya masultani wa Mamluki wa Misri.
20231101.sw_2497_29
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Mnamo mwaka 1517 Waosmani walivamia na kuteka Misri. Hadi karne ya 19 Misri ikaendelea kama jimbo la Milki ya Osmani, kisheria hata hadi Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Hali halisi nchi ilikuwa na kipindi kifupi kama milki ya kujitegemea wakati wa karne ya 19, hadi kusimamiwa na Uingereza hasa kwa shabaha ya kutawala mfereji wa Suez na kushuka kwa ngazi ya nchi lindwa.
20231101.sw_2497_30
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Mwaka 1914 ilitangazwa kuwa nchi lindwa chini ya Uingereza; tangazo la uhuru la mwaka 1922 bado liliacha athira kubwa kwa Uingereza.
20231101.sw_2497_31
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Wakazi wengi (91%) ni Wamisri asili. Wengine ni Waazaba, Waturuki, Wagiriki, Wabeduini, Waberberi, Wanubi n.k. Wahamiaji kutoka Sudan na nchi nyingine ni milioni 5 hivi, wakati Wamisri wanaoishi ugenini ni milioni 2.7.
20231101.sw_2497_32
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Lugha rasmi ni Kiarabu Sanifu cha Kisasa, wakati wananchi wanatumia kwa kawaida aina mbalimbali za Kiarabu, hasa Kiarabu cha Kimisri (68%)
20231101.sw_2497_33
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
Uwiano wa wafuasi wa dini hizo haujulikani vizuri, lakini Waislamu (hasa Wasunni) ni kama 90%, Wakristo (hasa Wakopti wanaoendelea kufuata Ukristo uliokuwa unatawala kabla ya Waarabu kuteka nchi katika karne ya 7) ni walau 10%, wakati Wayahudi wamehama karibu wote.
20231101.sw_2497_34
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
History of Egypt, Chaldea, Syria, Babylonia, and Assyria in the Light of Recent Discovery by Leonard William King, at Project Gutenberg.
20231101.sw_2497_35
https://sw.wikipedia.org/wiki/Misri
Misri
By Nile and Tigris'' - a narrative of journeys in Egypt and Mesopotamia on behalf of the British museum between 1886 and 1913, by Sir E. A. Wallis Budge, 1920 (DjVu and layered PDF formats)
20231101.sw_2498_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Libya
Libya
Libya ni nchi ya Afrika ya Kaskazini kwenye Bahari ya Mediteraneo, inayopakana na Misri, Sudan, Niger, Chad, Algeria na Tunisia.
20231101.sw_2498_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Libya
Libya
Eneo kubwa la nchi (90%) ni sehemu ya jangwa la Sahara. Chini yake kuna akiba kubwa ya petroli, ambayo ndiyo utajiri wa nchi.
20231101.sw_2498_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Libya
Libya
Wakazi asili walikuwa Waberber. Baadaye wakaja Wafoinike upande wa magharibi na Wagiriki upande wa mashariki.
20231101.sw_2498_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Libya
Libya
Nchi ilitawaliwa na Waitalia tangu mwaka 1911 hadi 1941 ilipotekwa na Waingereza ambao, baada ya Vita vikuu vya pili kwisha, waliacha nchi mwaka 1951 mikononi mwa mfalme mwenyeji, Idris I, aliyekuwa amepinga ukoloni tangu mwaka 1920 (Vita vya Libya dhidi ya Italia).
20231101.sw_2498_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Libya
Libya
Kisha kumpindua mfalme huyo, Muammar al-Gaddafi alitawala kidikteta tangu mwaka 1969 hadi alipopinduliwa na kuuawa mwaka 2011 kwa mkono wa N.A.T.O.
20231101.sw_2498_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Libya
Libya
Baada ya hapo wananchi wanazidi kupigana katika vita vya wenyewe kwa wenyewe. Mwaka 2020 kulikuwa na makubaliano ya kusimamisha vita na kuunda serikali ya pamoja ili kuandaa uchaguzi mkuu.
20231101.sw_2498_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Libya
Libya
Wakazi wa Libya ni hasa mchanganyiko wa Waberberi, Waarabu na Waturuki (74%), mbali na Waberberi (25%) ambao ndio wakazi asilia, lakini wengi wao wameanza kutumia lugha ya Kiarabu pia. Kuna pia wahamiaji kutoka nchi za jirani, za kandokando ya Bahari ya Kati na kutoka Bara Hindi.
20231101.sw_2498_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Libya
Libya
Wakazi wameongezeka tangu mwaka 1970 kutoka milioni 2.5 hadi kuwa karibu milioni 7 mwaka 2022. Nusu ya wakazi wote ni vijana chini ya umri wa miaka 16. Sehemu kubwa kabisa (80%) huishi sehemu za pwani.
20231101.sw_2498_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Libya
Libya
Upande wa dini, unatawala Uislamu (97%). Wakristo ni zaidi ya 100,000, wakiwemo hasa Wakopti (60,000) na Wakatoliki (40,000).
20231101.sw_2499_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tripoli
Tripoli
Tripoli ni neno la asili ya Kigiriki (Τρίπολις - Trípolis au Τρίπολη - Trípoli) linalomaanisha "miji mitatu" au "mji mwenye sehemu tatu". Asili yake ni maungano ya miji mitatu ya jirani kuwa mji au dola moja. Katika lugha ya Kiarabu neno limekuwa "Trablus" au "Tarablus" (طرابلس).
20231101.sw_2501_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mahore
Mahore
Mahore (Kifaransa: Grande-Terre) ni kisiwa kikubwa cha eneo la ng’ambo la Ufaransa la Mayotte. Kisiwa cha pili ni Pamanzi (Kifaransa: Petite-Terre).
20231101.sw_2501_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mahore
Mahore
Mahore ina urefu wa 39 km na upana wa 22 km. Milima yake ni Mont Benara (660 m), Mont Choungui (594 m), Mont Mtsapere (572 m) et Mont Combani (477).
20231101.sw_2509_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Maulid
Maulid
Maulid (pia: maulidi, kwa kirefu: Maulid an-Nabii) ni sikukuu ya dini ya Uislamu ya kuadhimisha kuzaliwa kwake Mtume Muhammad takriban mwaka 570 BK.
20231101.sw_2509_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Maulid
Maulid
Neno lenyewe ni la asili ya Kiarabu kutokana na مولد النبي , maulid an-nabi, au ميلاد النبي , milaad an-nabi). Sikukuu inafuata kalenda ya Kiislamu. Waislamu wa dhehebu la Sunni husheherekea tarehe 12 Rabi'-ul-Awwal kwa mujibu ya kalenda ya Kiislamu ya Alhijria na Waislamu wa dhehebu la Shia husheherekea tarehe 17 Rabi'-ul-Awwal.
20231101.sw_2509_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Maulid
Maulid
Wataalamu wa historia wengine wanasema ya kwamba sherehe ya Maulid imeanzishwa mnamo karne ya 12 BK. Kuna Waislamu kadhaa wanaokataa sherehe hiyo kwa sababu hakuna sunna wala hadith ya Muhammad mwenyewe kuhusu kusheherekea maulid yake. Lakini kwa ujumla ni sikukuu inayopendwa sana na Waislamu wengi duniani. Misri maulid ni kati ya sikukuu za Kiislamu zinazokumbukwa sana na Waislamu. Katika Afrika ya Mashariki sherehe ya maulid huko Lamu imejulikana hasa ikivuta wageni kutoka pande zote za Afrika ya Mashariki hadi Uarabuni.
20231101.sw_2509_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Maulid
Maulid
Maulid kama vile sikukuu zote za Kiislamu inafuata kalenda ya Kiislamu ambayo ni kalenda ya mwezi. Kwa sababu hiyo tarehe yake hubadilikabadilika katika kalenda ya Gregori iliyoenea kimataifa.
20231101.sw_2509_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Maulid
Maulid
Zifuatazo ni tarehe za maulid kwa ajili ya miaka 2006 - 2021. Tarehe ya kwanza ni ile ya Wasunni (12 Rabi'-ul-Awwal) na tarehe ya pili katika mabano ni ile ya Washia (17. Rabi'-ul-Awwal). Tarehe hizo zinaweza kuwa tofauti na tarehe halisi kwa sababu kuna tofauti kati ya nchi na vikundi vya Waislamu jinsi gani kukubali kuhusu mwanzo wa miezi.
20231101.sw_2511_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mayotte
Mayotte
Mayotte ni eneo la ng’ambo la Ufaransa (kwa Kifaransa: Départment de Mayotte). Linaundwa na visiwa vya Mahore na Pamanzi pamoja na vingine vidogo. Eneo hili kijiografia ni hasa muungo wa funguvisiwa la Komoro lakini si kisiasa.
20231101.sw_2511_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mayotte
Mayotte
Mayotte iko katika kaskazini ya Mfereji wa Msumbiji kwenye Bahari Hindi, kati ya Madagaska upande wa mashariki-kusini na Msumbiji bara upande wa magharibi. Iko kilometa 295 magharibi kwa Madagaska na km 67 kusini mashariki mwa Anjouan.
20231101.sw_2511_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mayotte
Mayotte
Mayotte inaonekana kuwa imekaliwa na watu kutoka karne ya 7, wakitokea Madagaska, wengine wenye asili ya Asia na wengine wenye asili ya Afrika.
20231101.sw_2511_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mayotte
Mayotte
Kati ya karne ya 8 na karne ya 11 wakazi walisilimu, na kuna msikiti mkongwe (katika Tsingoni) wa karne ya 14, pamoja na mirhab ya matumbawe (1532). Visiwa vyote vya Komoro vinafuata utamaduni wa Kiswahili vikiwa pamoja na Mayotte.
20231101.sw_2511_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mayotte
Mayotte
Mwaka wa 1841, wakati idadi ya watu ilipungua kwa wakazi chini ya 3000, sultani wa mwisho Andriansoly (kutoka Madagaska) aliuza kisiwa kwa Ufaransa kwa kubadilishana ya ulinzi wa nchi hiyo, hivyo Mayotte ikawa koloni la Kifaransa.