_id
stringlengths 15
22
| url
stringlengths 31
150
| title
stringlengths 1
86
| text
stringlengths 100
23.8k
|
---|---|---|---|
20231101.sw_2797_77
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Ni kawaida kwenye maduka ya Kiunzikuu kuhusika na kanzidata kubwa na mafaili. Mafaili yenye ukubwa wa Gigabyte mpaka terabyte si yasiyo ya kawaida. Ikilinganishwa na tarakilishi binafsi (PC), kwa kawaida Viunzikuu zina mara mia kwa maelfu ya vitunza data vitumikavyo, na vinaweza kufikiwa kwa kasi. Familia nyingine za seva pia zinapunguza kazi za I/O na kutilia mkazo mchakato wa kazi.
|
20231101.sw_2797_78
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Mainframe return on investment (ROI), kama jukwaa lingine lolote la mchakato, ni tegemezi katika uwezo wake wa kupima, kuhimili kazi michanganyiko, upunguzaji gharama za leba, ufikishaji huduma usiopingika kwa matumizi muhimu ya kibiashara, na vipengele vingine kadhaa vya gharama vilivyopunguzwa hatari.
|
20231101.sw_2797_79
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Aina hizi za kompyuta zilidhihiri katika kipindi cha miaka ya 1960. Ni kompyuta zenye umbile dogo kuliko zile zilizotangulia kutajwa, na ni bora kwa kuunganishia kompyuta nyingine zinazotumika viwandani na ndani ya nchi.
|
20231101.sw_2797_80
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Matumizi ya kompyuta yanatofautiana kutokana na malengo na makusudio ya mtumiaji mwenyewe. Yamegawanyika katika sehemu kuu mbili.
|
20231101.sw_2797_81
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kuna kompyuta zilizoandaliwa kwa ajili ya matumizi yote ambayo mtumiaji anaweza kutumia kutegemea na malengo yake binafsi, kwa mfano mhasibu anaweza kutumia kompyuta kwa ajili ya kufanyia kazi zake za uhasibu (hesabu).
|
20231101.sw_2797_82
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
pia mwanasayansi, fundi, mwalimu na mwanafunzi, wote hao wanaweza kutumia kompyuta kwa malengo yao tofauti.
|
20231101.sw_2797_83
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kompyuta hizi zimeandaliwa kwa ajili ya malengo maalumu tu, kama zile kompyuta zilizoandaliwa kwa ajili ya kuchorea moyo na kupigia picha za X-ray, ambazo ni vigumu kwa mtu mwingine kuzitumia kwa ajili ya kufanyia kazi zake binafsi ambazo zinatofautiana na hizo za hospitalini.
|
20231101.sw_2797_84
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kutokana na kuendelea kwa elimu ya teknolojia imetusaidia sana kujifunza mambo mbalimbali kupitia kompyuta, ambapo unaweza kuitumia kwa ajili ya kuuliza maswali na kujibiwa kwa haraka tena kwa njia tofauti, kwa ajili ya kufanya majadiliano ya kielimu, pia unaweza kuandaa vipindi mbalimbali vya masomo na kufundishia elimu tofauti.
|
20231101.sw_2797_85
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Pia unaweza kuonyeshea filamu zenye mafundisho mazuri, kama kuonyesha filamu zenye elimu ya jiografia na sayansi ya mifugo na kilimo, kuonyesha sehemu muhimu za nchi, kuonyesha athari za nchi ambazo ndiyo sehemu kuu zinazoleta fedha za kigeni katika nchi, na kuonyesha picha za maendeleo katika sekta mbali mbali za nchi yetu, pia kuonyeshea mila na tamaduni za taifa na mataifa mengine mbalimbali duniani na kadhalika.
|
20231101.sw_2797_86
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kompyuta zimeandaliwa ndani yake programu mbalimbali zenye michezo tofauti, ambayo inaweza kutumika na watu kulingana na umri wao, na ambayo inajulikana kama moja ya kazi za kukuza kipaji na kuchangamsha akili, na ni sehemu mojawapo ya kuburudisha nafsi.
|
20231101.sw_2797_87
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kompyuta zinaweza kutumika kwa ajili ya kufanyia kazi za ufundi, kama kuchora ramani ya nyumba na mazingira ya nje ya nyumba, kutengenezea picha kwa kuibadilisha na kuiremba na kuifanya ionekane katika sura nyengine ambayo ni tofauti na ile ya asili.
|
20231101.sw_2797_88
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kompyuta inaweza kutumika kwa ajili ya kufanyia mawasiliano kupitia mtandao wa (Internet) ambao leo hii ndiyo umeshika nafasi kubwa sana ya mawasiliano kuliko kitu chengine ulimwenguni, kama kuwasiliana kwa kutumiana ujumbe wa barua pepe (E-mail) ambayo ni rahisi na inafika haraka kuliko barua za kupitia posta, pia kwa kutumia barua pepe hakuna haja ya kufikiria sehemu aliko mtu America au bara hindi au sehemu nyingine duniani, kuwasiliana kwa maneno ya maandishi (chat), pia kuwasiliana kwa maneno ya sauti na kuonekana picha (video chat).
|
20231101.sw_2797_89
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kwa kutumia kompyuta unaweza kuendeshea kazi za usafirishaji katika vituo vikuu vya usafirishaji, kama usafiri wa ardhini (mabasi, metro na treni), usafiri wa majini (meli), na usafiri wa angani (ndege).
|
20231101.sw_2797_90
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kama kuendeshea mashine viwandani kwa ajili ya kuzalisha bidhaa mbali mbali, kama kutengenezea magari, kuzalishia umeme na kutengenezea bidhaa nyengine za kawaida kama nguo mazulia na kadhalika.
|
20231101.sw_2797_91
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kompyuta hizi zina utofauti kidogo na zile nyingine hasa kwa sababu huwazimebuniwa na kuundwa kufanya operesheni fulani kulingana na kiwanda na zina uwezo wa kufanya kazi kwa mazingira magumu kuliko kompyuta ya kawaida kama vile mazingira yenye joto, vumbi, kemikali, mvuke, au baridi zaidi.
|
20231101.sw_2797_92
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kama ilivyokuwa ada na kawaida hivi sasa kutumia kompyuta kwa ajili ya kuendeshea kazi za benki,kwa ajili kurahisisha kazi za mahesabu.
|
20231101.sw_2797_93
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kompyuta zimekuwa na matumizi makubwa na muhimu sana katika kufanyia uchunguzi na matibabu hospitalini, kama kuchunguza na kuelekeza dawa ya kutibu ugonjwa uliyoonekana, pia kupimia na kujaribia mimba na kutoa maelekezo kuhusiana na siku na tarehe ya kujifungua.
|
20231101.sw_2797_94
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Sehemu zinazoshikika (Hardware), ni aina zote za vifaa vya kompyuta, navyo vimegawanyika katika sehemu kuu tatu.
|
20231101.sw_2797_95
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kibodi inatumika kwa ajili ya kuingizia herufi, namba, alama na michoro, nayo imegawanyika katika sehemu kuu nne, nazo ni kama ifuatavyo: Funguo za kuandikia (Typewriter keys), funguo za kuhama (Movement keys), funguo za namba pamoja na michoro mingine (Numeric keys) na funguo za kazi Function keys).
|
20231101.sw_2797_96
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kibonyezo (cha) mahesabu ‘numeral key’ Inatumika kwa ajili ya kufunga na kufungulia namba na michoro.
|
20231101.sw_2797_97
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kibonyezo (cha) kuendelea ‘enter key’ Inatumika kwa ajili ya kutekeleza amri, au kuanzisha fungu la maneno kwenye ukurasa..
|
20231101.sw_2797_98
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kibonyezo (cha) mpangilio ‘tab key’ Inatumika kwa ajili ya kuwacha masafa maalumu tofauti na ya kawaida (Normal).
|
20231101.sw_2797_99
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kibonyezo (cha) kudhibiti ‘control key’ inatumika daima pamoja na ufunguo mwengine kwa ajili ya kutekeleza amri maalumu.
|
20231101.sw_2797_100
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kibonyezo (cha) kibadalishi ‘alt(ernate) key’ inatumika daima pamoja na ufunguo mwengine kwa ajili ya kutekeleza amri maalumu.
|
20231101.sw_2797_101
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kibonyezo (cha) kuhama ‘shift key’ inatumika daima pamoja na ufunguo mwengine kwa ajili ya kutekeleza amri maalumu.
|
20231101.sw_2797_102
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kuna vitufe viwili kwenye kila mausi, kitufe cha upande wa kushoto (Left click) kinatumika kufungulia windozi, programu na kuchagulia maandishi, maneno na picha, na kitufe cha upande wa kulia (Right click) kinatumika kufungulia orodha ya mapendekezo ya kazi.
|
20231101.sw_2797_103
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Printa inatumika kwa ajili ya kutolea vitu vya maandishi au picha kwenye kompyuta kwa njia ya karatasi (kuchapisha).
|
20231101.sw_2797_104
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Plota ni chombo kinachotumika kwa ajili ya kutolea vitu, ambacho kinafanana na printa katika ufanisi wake wa kazi, lakini umbile lake ni kubwa kuliko printa, na kinatumika kwa ajili ya kuchapishia picha na michoro ya kiufundi, pia kinaweza kutumika kwa ajili ya kuchapisha maandishi kama herufi namba na alama.
|
20231101.sw_2797_105
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kompyuta haiwezi kufanya kazi mpaka kipatikane kitu kinachoitwa software, ambacho kinawakilisha programu zinazoendesha kompyuta. Programu hizo zimegawanyika katika sehemu kuu mbili:
|
20231101.sw_2797_106
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
1. Programu za kuendeshea kompyuta (operating systems): programu hizo zinaitwa Windows, na kuna aina nyingi za Windows kulingana na toleo lake na ubora wake, kwani siku zinavyozidi kwenda mbele ndipo tunapozidi kupokea programu nyingine za Windows zenye ubora zaidi kuliko zile za awali.
|
20231101.sw_2797_107
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
2. Programu za kufanyia kazi (application systems), nazo ni: Microsoft Office na Graphics design; programu hizo daima zinafanya kazi ndani ya windows, ambazo zinatumika kwa ajili ya kazi mbalimbali za uandishi na hesabu, na kazi nyinginezo za kuunda na kutengeneza picha n.k.
|
20231101.sw_2797_108
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Vifaa hivi vipo ndani ya chombo kiitwacho C.P.U. (kifupi cha Central Processing Unit), ambacho ni kiini cha kompyuta na ndicho kinachofanya kazi ya kuviendesha vifaa vyote vya kompyuta na kutoa maelekezo yote.
|
20231101.sw_2797_109
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Ndani ya madhabodi (Motherboard) kinapatikana kifaa kinachoitwa Bios (kifupi cha Basic Input Output System), ambacho ndicho kinachofanya kazi ya kuviendesha vifaa vya kuingizia na kutolea vitu.
|
20231101.sw_2797_110
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Ni vigumu kufuta au kurekebisha vitu vilivyomo ndani ya kifaa hicho kwani vinazingatiwa ni vitu vya kusomea tu na si kwa kazi nyingine.
|
20231101.sw_2797_111
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Kazi za mahesabu ni kazi zote zinazofanywa na hesabu, kama vile kutoa, kujumlisha, kuzidisha na kugawanya.
|
20231101.sw_2797_112
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tarakilishi
|
Tarakilishi
|
Hakuna bei haswa ya tarakilishi. Bei huenda ikawa juu au chini kulingana na aina (model), uwezo wa kuhifadhi data, ukubwa wa diski, ukubwa wa RAM, spidi ya procesa na programu ambayo kompyuta yaweza kuzitumia.
|
20231101.sw_2800_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tripoli%20%28Libya%29
|
Tripoli (Libya)
|
Jina la Kiarabu ni طرابلس (tarāblus) au طرابلس الغربية (tarābulus al-gharbiyya - Tripoli ya Magharibi kwa sababu ya Tripoli ya mashariki huko Lebanon) lina asili ya lugha ya Kigiriki (Τρίπολη) likimaanisha "miji mitatu".
|
20231101.sw_2800_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tripoli%20%28Libya%29
|
Tripoli (Libya)
|
Tripoli ina wakazi 1,150,990 ambayo ni zaidi ya robo moja ya wakazi wote wa Libya na inaendelea kukua haraka.
|
20231101.sw_2800_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tripoli%20%28Libya%29
|
Tripoli (Libya)
|
Jiji hilo liko ufukoni mwa bahari ya Mediteranea likiwa na hali ya hewa ya wastani. Mwezi Agosti inafika halijoto ya sentigredi 28,1°, Januari sentigredi 12,1°. Miezi ya baridi kuna mvua, Juni hadi Agosti ni majira ya kiangazi.
|
20231101.sw_2800_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tripoli%20%28Libya%29
|
Tripoli (Libya)
|
Tripoli ni mji wa kale ambao bado historia yake imetunzwa ikionyesha mabaki ya historia yake ndefu tangu enzi za Wafinisia, Waroma, Waarabu, Wahispania, Waturuki na Waitalia.
|
20231101.sw_2803_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Niger
|
Niger
|
Niger (pia Nijeri) ni nchi kubwa zaidi ya Afrika ya Magharibi kwa eneo, lakini 80% ni katika jangwa la Sahara.
|
20231101.sw_2803_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Niger
|
Niger
|
Imepakana na Algeria na Libya upande wa kaskazini, Mali na Burkina Faso upande wa magharibi, Chad upande wa mashariki na Nigeria pamoja na Benin upande wa kusini.
|
20231101.sw_2803_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Niger
|
Niger
|
Ni sehemu ya kanda la Sahel, yaani sehemu kubwa ya nchi ni yabisi, kaskazini mwake ni yabisi sana ikiwa jangwa la Sahara.
|
20231101.sw_2803_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Niger
|
Niger
|
Jaribio la mapinduzi lilifanyika usiku wa kuamkia Machi 31, 2021, siku chache kabla ya kuapishwa kwa Mohamed Bazoum, rais mteule.
|
20231101.sw_2803_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Niger
|
Niger
|
Mipaka ilichorwa wakati wa ukoloni wa Ufaransa, ikiunganisha watu wenye utamaduni tofautitofauti, kama vile Watuareg (9.3% za wakazi wote) wa Sahara, wahamaji Wafula (8.5%) na Wakanuri (4.7%) wa eneo la Sahel na wakulima wa kusini kama Wasonghai (21%) na Wahausa: hawa wa mwisho ni 55.4% .
|
20231101.sw_2803_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Niger
|
Niger
|
Tofauti hizo kubwa zilileta kipindi cha ugomvi kati ya makabila uliopoa tena baada ya mwaka 2000. Tatizo kubwa la nchi ni vipindi vya ukame na njaa vinavyorudiarudia mara kwa mara.
|
20231101.sw_2803_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Niger
|
Niger
|
Wakazi walikuwa zaidi ya milioni 17 katika sensa ya mwaka 2012. Kwa sasa ni 22.4 kutokana na ongezeko la haraka. Idadi kubwa wako kusini.
|
20231101.sw_2803_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Niger
|
Niger
|
Tangu wakati wa ukoloni, lugha rasmi ni Kifaransa. Lakini kuna lugha 10 za taifa kati ya lugha kuu za makabila asili. Muhimu zaidi ni Kihausa na Kizarma-Sonrai.
|
20231101.sw_2803_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Niger
|
Niger
|
Walio wengi kabisa (99.3%) ni wafuasi wa Uislamu; baadhi yao wanasemekana kuchanganya Uislamu na dini asilia za Kiafrika. Wakristo ni 0.3% tu. Hata hivyo Niger ni nchi isiyo na dini rasmi.
|
20231101.sw_2804_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mogadishu
|
Mogadishu
|
Mogadishu (kwa Kisomali Muqdisho; kwa Kiitalia Mogadiscio) ni mji mkuu wa Somalia. Iko ufukoni wa Bahari Hindi ikiwa na wakazi milioni 2.590 (2017).
|
20231101.sw_2804_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mogadishu
|
Mogadishu
|
Mogadishu imeundwa mnamo mwaka 900 BK ikawa mji wa kaskazini kabisa wa utamaduni wa Waswahili kwenye pwani ya Afrika ya Mashariki. Ilikuwa sehemu ya biashara ya kimataifa ya Waswahili jinsi inavyonekana kutokana na sarafu za kale za Uchina, Sri Lanka na Vietnam zilizokutwa na wanaakiolojia katika ardhi yake.
|
20231101.sw_2804_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mogadishu
|
Mogadishu
|
Msafiri Mwarabu Ibn Battuta alitembelea Mogadishu mnamo mwaka 1300 akaona matajiri akataja "watu wanene wengi".
|
20231101.sw_2804_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mogadishu
|
Mogadishu
|
Mji ulikuwa na vipindi vya kujitegemea na vipindi vya kutawaliwa na nchi za nje katika historia yake. Mnamo mwaka 1500 Wareno walikuwa mabwana wake. Tangu katikati ya karne ya 19 Mogadishu ilikuwa chini ya sultani wa Zanzibar.
|
20231101.sw_2804_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mogadishu
|
Mogadishu
|
Mwaka 1892 sultani alikodisha mji kwa Italia iliyoinunua kutoka kwake mwaka 1905 ukawa mji mkuu wa koloni la Somalia ya Kiitalia.
|
20231101.sw_2804_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mogadishu
|
Mogadishu
|
Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia mji ulivamiwa na Waingereza mwaka 1941 waliourudisha kwa Italia mwaka 1954.
|
20231101.sw_2804_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mogadishu
|
Mogadishu
|
Mwaka 1990 dikteta Siad Barre alipinduliwa halafu Mogadishu pamoja na nchi yote iliingia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe. Wanajeshi wa Marekani walijaribu mwaka 1993 kurudisha hali ya usalama kwa niaba ya Umoja wa Mataifa lakini walikuta upinzani mkali kutoka kwa vikundi vya wanamgambo Wasomalia. Baada ya kupoteza askari Marekani iliondoka tena.
|
20231101.sw_2804_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mogadishu
|
Mogadishu
|
Hali ya vita imeendelea hadi mwaka 2012, na kwa muda mrefu nchi ikiwa haina serikali wala bunge na uharamia ulishamiri.
|
20231101.sw_2806_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kitenduli
|
Kitenduli
|
Vitenduli ni ndege wadogo wa jenasi Uraeginthus katika familia ya Estrildidae ambao wana rangi buluu. Kuna spishi mbili zingine kwa jenasi hii ambazo zinaitwa tunguhina na zina rangi kahawianyekundu, lakini wataalamu wengine wanaziweka katika jenasi Granatina. Vitenduli wanatokea Afrika chini ya Sahara tu. Hupenda kuwa karibu na makazi ya watu. Tago lao hutengenezwa na manyasi juu ya mti au ndani ya paa; limefunikika juu na mwingilio kando.
|
20231101.sw_2806_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kitenduli
|
Kitenduli
|
Uraeginthus angolensis, Kitenduli Mashavu-buluu (Southern au Blue-breasted Cordon-bleu au Blue Waxbill)
|
20231101.sw_2807_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tunguhina
|
Tunguhina
|
Tunguhina ni ndege wadogo wa jenasi Uraeginthus katika familia ya Estrildidae ambao wana rangi kahawianyekundu na viraka buluu au zambarau. Kuna spishi tatu zingine kwa jenasi hii ambazo zinaitwa vitenduli na zina rangi buluu. Wataalamu wengine wanaweka spishi mbili za tunguhina ndani ya jenasi Granatina. Spishi hizi zinatokea Afrika chini ya Sahara tu. Tunguhina ni ndege waoga, lakini kwa bustani ya hoteli na nyumba wanazoea watu. Tago lao hutengenezwa na manyasi ndani ya magugu; limefunikika juu na lina mwingilio kando.
|
20231101.sw_2810_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Morisi ni kisiwa karibu na Afrika, pia ni nchi inayoitwa rasmi Jamhuri ya Morisi (kwa Kiingereza: Republic of Mauritius, kwa Kifaransa: République de Maurice). Ni nchi ya visiwa katika Bahari Hindi takriban Km 900 mashariki kwa Madagaska na km 4000 kusini-magharibi kwa Bara Hindi.
|
20231101.sw_2810_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Eneo la jamhuri ni pamoja na kisiwa cha Morisi yenyewe, kisiwa cha Rodrigues, visiwa vidogo vya Cargados Carajos na Agalega.
|
20231101.sw_2810_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Kisiwa kikuu cha Mauritius ni km² 1,865 au 91% za ardhi yote ya jamhuri. Karibu wakazi wote (1,261,208) huishi huko.
|
20231101.sw_2810_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Kisiwa cha Rodrigues kipo km 560 mashariki kwa Morisi yenyewe. Eneo lake ni km² 109; kuna wakazi 41,000.
|
20231101.sw_2810_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Visiwa vya Cargados Carajos (vinaitwa pia Saint Brandon) ni visiwa 16 vidogo sana, vyenye eneo la km² 1.3 pekee. Viko km 300 kaskazini kwa Morisi. Kuna wakazi mia chache wavuvi.
|
20231101.sw_2810_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Agalega ni visiwa viwili, yaani Kisiwa cha Kaskazini na Kisiwa cha Kusini, takriban km 1,122 kaskazini kwa Morisi yenyewe. Visiwa hivyo vina eneo la km² 70. Kuna vijiji vya Vingt Cinq na La Fourche kwenye kisiwa cha kaskazini na kijiji cha Ste Rita kwenye kisiwa cha kusini. Wenyeji wanalima mazao ya mnazi pamoja na mboga kwa matumizi yao wenyewe.
|
20231101.sw_2810_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Baada ya Waarabu na Wareno kuvumbua Morisi, wakazi wa kwanza (1638) walikuwa Waholanzi, lakini hawakuacha dalili isipokuwa majina ya mahali kwa sababu waliondoka mwaka 1710 baada ya kushindwa kiuchumi.
|
20231101.sw_2810_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Wafaransa walitawala visiwa kati ya 1715 hadi 1810. Walianzisha miji na mashamba ya miwa. Nje ya walowezi, Wafaransa walipeleka pia watumwa kutoka bara la Afrika. Mwaka 1767 walikuwepo Wafaransa 3,163 pamoja na watumwa Waafrika 15,000, pia Wahindi 587.
|
20231101.sw_2810_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Uingereza ulichukua utawala wa visiwa mwaka 1810 katika vita dhidi ya Napoleon. Tangu siku zile Kiingereza kilikuwa lugha rasmi ya serikali, lakini wakazi waliendelea kutumia lahaja za Kifaransa.
|
20231101.sw_2810_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Baada ya kuwapatia watumwa uhuru, Waingereza walileta Wahindi wengi, baadaye pia Wachina kama wafanyakazi kwenye mashamba ya sukari. Leo hii idadi kubwa ya wakazi ni wa asili ya Kihindi.
|
20231101.sw_2810_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Lakini 80% ya wananchi hutumia aina ya Kifaransa kama lugha ya kwanza (pamoja na krioli ya Kimorisyen. Asilimia 15 hutumia lugha za Kihindi kama vile Kibhojpuri, Kiurdu, Kitamil, na wengine Kichina na Kiingereza.
|
20231101.sw_2810_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Karibu nusu (48.5%) ya wakazi hufuata dini ya Uhindu, 32.7% Ukristo (hasa wa Kanisa Katoliki), 17.3% ni Waislamu (hasa Wasunni, lakini pia Washia), 0.4% Wabuddha.
|
20231101.sw_2810_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Morisi
|
Morisi
|
Nchi iliendelea kuwa na serikali zilizochaguliwa bila kupinduliwa: hali hii ya utulivu ilisaidia kukua kwa uchumi. Hali ya maisha ni ya juu kuliko nchi nyingi za Afrika.
|
20231101.sw_2811_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Antananarivo
|
Antananarivo
|
Antanànarìvo (matamushi [An/ta/na/ri/vo], Umma 1,403,449 (2001 sensa), ni Mji Mkuu wa Madagaska, kwa Mkoa wa Antananarivo.
|
20231101.sw_2811_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Antananarivo
|
Antananarivo
|
Pia mji huu wajulikana kwa jina la Kifaransa kama Tananarive ama kwa kifupi ni Tana. Antanànarivo iko kati ya kisiwa kulingana na usabaa wa kisiwa, lakini ni maili 90 kutoka pwani ya magharibi. Mji mwenyewe una kituo cha amri, kinachojengwa juu ya milima na mabonde marefu yenye miamba na nyembamba. Hii milima na mabonde imesambaa kusini na kaskazini kama 2-½ maili, ikigawa kaskazini kwa njiapanda, na kukwea mahali juu zaidi pakiwa 690 ft. juu ya viwanja dhihirifu za mchele upande wa magharibi, ambazo zenyewe zimo 4060 ft. juu ya usawa wa bahari. Mji huu ni mji mkubwa nchini Madagaska na ni kituo cha amri ya serikali, mawasiliano, na kituo cha uchumi. Mahali Mji huu uko ni 18°55' Kusini, 47°31' Magharibi (-18.916667, 47.516667) , Maili 135 Magharibi-kusini magharibi ya Tamatave, ni bandari ya kisiwa hiki, ambayo imeungwa kwa reli, na kwa maili 60 kwa pwani kuna jahazi za kusafirisha. Viwanda vyahusu utolezi wa kuunda sigara, na nguo.
|
20231101.sw_2811_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Antananarivo
|
Antananarivo
|
Antananarivo ilianza pengine mwaka wa 1625. Kwa muda mrefu machifu wa kijiji cha Hova pekee, waliweza kujipa Uhuru kutoka sehemu nyingine za Madagaska, na kwa hivyo Antananarivo kuwa mji wa maana, na baadaye kuwa mji asili kwa kuongezeka wa wakazi 80,000. Mwaka wa 1793 mji huu ulifanywa uwe mji mkuu wa Wafalme wa Merina. Kushindwa kwa Mfalme Radama (wa kwanza) iliifanya Antananarivo iwe mji mkuu wa Madagaska yote. Mwaka wa 1869 majengo yote kwa mji asili, yalikuwa ya mbao ama nyazi, na hata hivyo mji wenyewe ulikuwa na Jumba za kifalme kubwa, kubwa zaidi ikiwa 120 ft. kwenda juu. Hili jumba lilataji sehemu ya bonde la kati; na jumba hili kubwa zaidi, dari na minara yake imepaa juu, na kwahivyo kuonekana kutoka sehemu zote.
|
20231101.sw_2811_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Antananarivo
|
Antananarivo
|
Kutoka uwanzo wa mawe na tofali, mji wote umejengwa na sasa kuna majengo ya aina nyingi na ya kuhifadhi, Jumba la Kifalme, Nyumba ambazo zilikuwa za Waziri mkuu na masharifu, makazi ya kifaransa, Kathidro ya Aglikan na Katoliki wa Kiromathe, Kanisa kadhaa za mawe na nyingine za matofali, Chuo, Shule, hospitali, Mahakama ya Sheria na Majengo ya Serikali, na nyumba nyingine za kuishi.
|
20231101.sw_2811_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Antananarivo
|
Antananarivo
|
Mji huu ulitekwa na Wafaransa mwaka wa 1895 na kuwekwa kwa koloni ya eneo ya Madagaska. Kutoka ukoloni wa ufaransa barabara njema zilitengenezwa kwa mji, ngazi pana za kupaa kwa eneo ya mabonde zimeunganisha sehemu zile ziko kwa ukwea zaidi na ziwezi kuundwa barabara za kawaida, na sehemu ya kati inayoitwa Andohalo, ni sehemu nzuri sana, ambayo inajia za kutembea na daraja za ukwea ambazo ni shamba za maua na miti. Hifadhi zimewekwa karibu na makazi ya watu, na upandaji wa miti na mashamba ya uhifadhi eneo nyingi za mji zaipatia mji urembo na utulifu. Maji ya patikana kwa chemchem chini ya milima lakini maji mengi yatoka kwa mto Ikopa, ambao mto huo wapitia kando ya Mji kusini na magharibi. Mji wenyewe umelindwa na Vigome viwili ambazo zilijengwa kwa mlima mashariki na kusini-magharibi. Pia kathidro ya Anglikani na katoliki ya kiroma, kuna Kanisa zaidi ya hamsini mjini na eneo za mji, na hata Miskiti za kiislamu. Antananarivo ni nyumbani kwa Chuo Kikuu cha Madagascar na Chuo cha Ambatobe (Collège Rural d'Ambatobe).
|
20231101.sw_2811_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Antananarivo
|
Antananarivo
|
Antanànarìvo ya maanisha "Mji wa Maelfu" (arivo=Elfu). Miaka ya ukoloni na hata miaka iliyofuatia Uhuru wa Madagaska, Antananarivo iliitwa 'Tananarive.
|
20231101.sw_2812_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Port%20Louis
|
Port Louis
|
Port Louis ni mji mkuu wa jamhuri ya Morisi. Ikiwa na wakazi 170,000 ni mji mkubwa wa taifa hili la visiwani katika Bahari Hindi.
|
20231101.sw_2812_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Port%20Louis
|
Port Louis
|
Kiwanja cha ndege cha kimataifacha Sir Seewoosagur Ramgoolam kipo 30 km kusini ya mji. Kutoka Port Louis kuna feri kwenda Saint Denis mji mkuu wa Réunion.
|
20231101.sw_2812_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Port%20Louis
|
Port Louis
|
Kuna viwanda vya nguo na vitambaa pia vya kemikali na madawa. Benki ziko nyingi. Kwa jumla Port Louis ni mji wa Afrika ambako wenyeji wana hali ya maisha iliyo juu kushinda miji mingine ya Afrika.
|
20231101.sw_2814_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Maskarena
|
Maskarena
|
Maskarena ni funguvisiwa katika Bahari Hindi takriban 900 km mashariki ya Madagaska. Kwa jumla ni visiwa vya dola la Morisi pamoja na kisiwa cha Kifaransa cha Réunion.
|
20231101.sw_2814_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Maskarena
|
Maskarena
|
Asili ya jina ni nahodha Mreno Pedro Mascarenhas aliyekuwa Mzungu wa kwanza wa kuzitembelea. Havikuwa na wakazi lakini Mascarenhas alitoa taarifa ya kwamba alikuta mabaki ya meli iliyowahi kuharibika kitambo.
|
20231101.sw_2814_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Maskarena
|
Maskarena
|
Kwa hiyo inaaminika ya kwamba mabaharia Waarabu labda pia Wahindi waliwahi kufika mara kwa visiwani bila kuanzisha makao ya kudumu. Lakini visiwa vilisaidia wasafiri baharini kupata chakula na maji na kupumzika kabla ya kuendelea na safari zao.
|
20231101.sw_2816_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Shomoro
|
Shomoro
|
Shomoro ni ndege wadogo wa jenasi Passer katika familia ya Passeridae ambao wana rangi ya nyeusi, nyeupe, majivu na kahawia. Ndege hawa huitwa korobindo pia, lakini jina hili litumike afadhali kwa kuita ndege wa jenasi Petronia. Shomoro wenye kichwa kijivu huitwa jurawa. Ndege hawa wana domo fupi na nene lifaalo kula mbegu, lakini hula wadudu wadogo pia hasa wanapokuwa vifaranga. Kwa asili shomoro wanatokea Ulaya, Afrika na Asia, lakini watu wamewaletea Australia na Marekani.
|
20231101.sw_2818_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Imepakana na nchi zifuatazo: Mali upande wa kaskazini, Niger upande wa mashariki, Benin, Togo, Ghana na Côte d'Ivoire upande wa kusini.
|
20231101.sw_2818_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Nchi ilianzishwa na Wafaransa kwa njia ya kugawa koloni la Cote d'Ivoire mwaka 1919. Jina la koloni jipya lilikuwa Volta ya Juu (kwa Kifaransa: Haute Volta). Jina limetokana na mto Volta unaoanzia hapa.
|
20231101.sw_2818_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Kiongozi wa nchi Thomas Sankara alibadilisha jina la nchi tarehe 4 Agosti 1984 kuwa Burkina Faso, yaani nchi ya watu waadilifu (kwa lugha ya Kimossi).
|
20231101.sw_2818_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Mlima wa juu ni Ténakourou (katika kusini) wenye m. 749. Sehemu ya chini ni bonde la mto Pendjari mpakani kwa Benin.
|
20231101.sw_2818_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Nchi imegawiwa kwa mikoa 13 (inaitwa region). Ndani ya mikoa kuna wilaya 45 (provinces) na tarafa 301 (departement). Kila mkoa husimamiwa na mkuu anayeitwa gouverneur.
|
20231101.sw_2818_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Burkina Faso ina chanzo cha matawimto ya mto Volta ambayo ni Mouhoun (pia Volta Nyeusi), Nakambé (pia Volta Nyeupe) na Nazinon (pia Volta Nyekundu). Mouhoun ni mto pekee wenye maji mwaka mzima.
|
20231101.sw_2818_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Sehemu za kaskazini na mashariki za nchi ambazo ni takriban robo ya eneo lake lote ni beseni yala mto Niger. Matawimto ya Niger (Béli, Gorouol, Goudébo na Dargol) yana maji kwa muda wa miezi 4-6 kila mwaka.
|
20231101.sw_2818_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Kuna kanda tatu ya hali ya hewa, kuanzia Sahel katika kaskazini hadi Sudan-Guinea katika kusini kwenye mvua zaidi.
|
20231101.sw_2818_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Katika maeneo yabisi ya kaskazini serikali mbalimbali zimejitahidi kupanda miti, jumla ya milioni 23 katika miaka 1996-2000.
|
20231101.sw_2818_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Miji mingine muhimu ni Bobo-Dioulasso (wakazi 366,383), Koudougou (wakazi 89,374), Ouahigouya (wakazi 62,325) na Banfora (wakazi 61,762). (takwimu za Januari 2006)
|
20231101.sw_2818_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Kabila kubwa nchini ni la Wamossi (karibu nusu ya wananchi wote) wakikaa karibu na Wagadugu. La pili ni la Wabobo hasa katika eneo la Bobo-Dioulasso. Kanda la Sahel katika kaskazini wako Wafula.
|
20231101.sw_2818_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Lugha ya Kifaransa ndiyo lugha rasmi. Lugha kuu za mawasiliano ni Kimossi na Kidiula. Kwa ujumla kuna lugha 68 nchini Burkina.
|
20231101.sw_2818_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Upande wa dini, wakazi Waislamu ni 60.5%, Wakristo ni 23.2% (Wakatoliki 19% na Waprotestanti 4.2%) na wafuasi wa dini asilia za Kiafrika ni 15.3%.
|
20231101.sw_2818_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Burkina%20Faso
|
Burkina Faso
|
Engberg-Perderson, Lars, Endangering Development: Politics, Projects, and Environment in Burkina Faso (Praeger Publishers, 2003).
|
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.