_id
stringlengths 15
22
| url
stringlengths 31
150
| title
stringlengths 1
86
| text
stringlengths 100
23.8k
|
---|---|---|---|
20231101.sw_2849_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Leonard%20Mbotela
|
Leonard Mbotela
|
Katika maisha yake ya kazi alikuwa pia mhusika wa huduma ya "Presidential Press Service" chini ya Rais Moi kwa miaka saba.
|
20231101.sw_2849_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Leonard%20Mbotela
|
Leonard Mbotela
|
Hata baada ya kustaafu ameendelea kusikika redioni akisoma habari na kipindi chake "Je Huu ni Ungwana?".
|
20231101.sw_2851_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
William Booth (10 Aprili 1829 β 20 Agosti 1912) ni Mkristo aliyeanzisha Jeshi la Wokovu na kuwa mkurugenzi wake wa kwanza (1878 β 1912).
|
20231101.sw_2851_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Booth alizaliwa katika kijiji cha Sneiton, wilaya ya Nottingham, nchi ya Uingereza. Alikuwa mmoja wa watoto wanne, lakini mwana wa kiume wa pekee, wa Samuel Booth na Mary Moss. Baba yake alikuwa tajiri, lakini wakati wa utoto wa William, familia ilianza kuwa maskini.
|
20231101.sw_2851_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Mwaka 1842 Samuel, ambaye wakati huo alikuwa amefilisika, hakuweza kulipa ada za shule kwa William aliyekuwa na umri wa miaka 13. Hivyo William alianza kuwa mwanagenzi wa mweka rahani. Kabla mwaka huo haujaisha, baba yake alifariki.
|
20231101.sw_2851_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Wakati wa uanagenzi wake William aliingia Ukristo. Alianza kusoma vitabu vingi, kujifundisha kuandika na kutoa hotuba, na kuwa mhubiri mlei wa Kanisa la Metodisti.
|
20231101.sw_2851_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Alipomaliza uanagenzi wake mwaka 1848, alijaribu kupata kazi nyingine kwa vile hakupenda kazi ya mweka rahani. Mwaka 1849 aliacha familia yake na kuhamia jiji la London ambapo alipata kazi katika duka la mweka rahani tena. Pia aliendelea na huduma ya mhubiri mlei lakini hakuridhika na nafasi alizozipata. Kwa hiyo aliacha kazi ya mhubiri mlei na kuanza huduma ya uinjilisti mitaani.
|
20231101.sw_2851_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Mwaka 1851 alijiunga na Kanisa la Wesley, na tarehe 10 Aprili 1852, sikukuu yake ya kuzaliwa ya 23, aliacha kazi ya mweka rahani na kuwa mhubiri kwenye makao makuu yao kule Clapham. Baada ya wiki tano tu, alimchumbia Catherine Mumford.
|
20231101.sw_2851_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Mwezi wa Novemba 1852, Booth alialikwa kuwa mchungaji wa kanisa kule Spalding, wilaya ya Lincolnshire.
|
20231101.sw_2851_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
William Booth na Catherine Mumford walifunga ndoa tarehe 16 Juni 1855 katika kanisa la Stockwell Green kule London. Walikuwa na watoto wanane wafuatao:
|
20231101.sw_2851_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Ingawa Booth alikuwa mwinjilisti hodari, hakufurahia uchungaji. Mkutano wa kila mwaka wa kanisa lake walipoendelea kumpa majukumu ya uchungaji na kumkatalia ombi lake la kufanya uinjilisti tu, alijiuzulu uchungaji wake mwaka 1861.
|
20231101.sw_2851_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Kwa vile madhehebu yake hayakumruhusu kufanya uinjilisti ndani ya makanisa baada ya kujiuzulu kwake, akawa mwinjilisti aliyejitegemea. Hata hivyo, teolojia yake haikubadilika. Aliendelea kuhubiri kwamba wasiookoka watateswa milele, kwamba kila mtu anahitaji kutubu, na kwamba Mungu anatuwezesha kuwa watakatifu, yaani tukiishi maisha ya upendo kwa Mungu na wenzetu. Hatimaye, hata watoto wa Booth walishirikisha katika huduma yake.
|
20231101.sw_2851_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Mwaka wa 1865, Booth pamoja na mke wake walianzisha Shirika la Uamshaji la Kikristo (ββChristian Revival Societyββ)) katika eneo la East End la London. Waliendesha mikutano kila jioni na siku nzima ya Jumapili wakitoa huduma za toba, wokovu na maadili ya kikristo kwa fukara, pamoja na walevi, wahalifu na malaya. Jina la shirika lilibadilishwa baadaye kuwa Misheni ya Kikristo (ββChristian Missionββ).
|
20231101.sw_2851_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Booth na wanashirika wake walitenda walichohubiri, yaani waliishi maisha ya kikristo wakijitolea mhanga katika huduma kwa wengine. Kwa mfano, waligawa chakula kwa maskini bila kujali wakidharauliwa kwa ajili ya huduma zao za kikristo.
|
20231101.sw_2851_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Mwaka wa 1878, jina la shirika lilibadilishwa tena kuwa Jeshi la Wokovu. Kama majeshi mengine, lilipata bendera yake na nyimbo zake ambazo hufuata sauti za watu wa kawaida zikiunganishwa na maneno ya kikristo. Booth na wanajeshi wengine huvaa sare za jeshi la Mungu kwenye mikutano. Booth alianza kuitwa Jenerali, na watumishi wengine walipewa vyeo vya afisa vilivyofaa.
|
20231101.sw_2851_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Ingawa walibanwa kifedha, Jeshi la Wokovu na huduma zake zilienea haraka na kuzalia matawi katika nchi nyingine, baadhi yao Marekani, Ufaransa, Uswisi, Sweden, Australia, Kanada, Uhindi, Afrika ya Kusini, New Zealand, Jamaika, na kadhalika.
|
20231101.sw_2851_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Wakati wa maisha yake, William Booth alianzisha huduma za Jeshi la Wokovu katika nchi 58 akisafiri sana na kuendesha mikutano. Booth alitoa jarida na kuandika vitabu kadhaa. Pia alitunga nyimbo nyingi. Kitabu chake maarufu kabisa ni In Darkest England and the Way Out kilichotolewa mwaka wa 1890.
|
20231101.sw_2851_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Booth
|
William Booth
|
Ili kumheshimu Booth, mshairi Vachel Lindsay aliandika shairi liitwalo General William Booth Enters Into Heaven, na Charles Ives aliyekuwa jirani wa Booth alitunga sauti kwa shairi hilo.
|
20231101.sw_2852_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne (Ireland, 590 hivi - Northumberland, Uingereza, 31 Agosti 651) ndiye aliyeanzisha kituo cha utawa na kuwa askofu wake wa kwanza kwenye kisiwa cha Lindisfarne. Kabla hajafika Northumbria alikuwa mtawa katika kwenye kisiwa cha Iona katika nchi ya Uskoti.
|
20231101.sw_2852_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana kama mtakatifu kwa kufufua Ukristo katika eneo la Northumbria hata akaitwa Mtume wa Northumbria.
|
20231101.sw_2852_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Wakati wa enzi ya Warumi, Ukristo ulikuwa umeenea mpaka Uingereza, lakini kwa sababu ya kushindwa kwa Warumi, Upagani ukaanza kurudi upande wa kaskazini wa Uingereza.
|
20231101.sw_2852_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Oswald, mfalme wa Northumbria, mwaka 616 alilazimishwa kwenda uhamishoni katika kisiwa cha Iona ambako akabadilika kuwa Mkristo na kubatizwa.
|
20231101.sw_2852_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Mwaka 634 Oswald alirudishiwa ufalme wa Northumbria akaamua kuwaingiza katika Ukristo wananchi wake ambao wengi wao walikuwa Wapagani. Ili kutekeleza lengo hilo aliwaomba watawa wa Iona wamtumie wamisionari, naye Aidani akafika mwaka 635.
|
20231101.sw_2852_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Aidani alichagua kisiwa cha Lindisfarne kiwe makao makuu ya dayosisi yake kwa vile kilikuwa karibu na ngome ya kifalme kule Bamburgh.
|
20231101.sw_2852_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Mwanzoni alikuwa mfalme Oswald mwenyewe aliyewatafsiria Aidan na watawa wake kwa vile walikuwa hawajajifunza lugha ya kale ya Kiingereza. Baada ya kifo cha Oswald mwaka 642, Aidan alisaidiwa na mfalme Oswine wa Deira, nao wakawa marafiki wa karibu sana.
|
20231101.sw_2852_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Aidani alikuwa huwatembelea watu kijiji hadi kijiji, na kuongea nao kwa adabu na kujaribu katika maongezi hayo wavutwe na Ukristo.
|
20231101.sw_2852_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Kufuatana na hadithi moja, mfalme alimpa Aidani farasi ili asihitaji kutembea kwa miguu lakini Aidan akatoa farasi kama zawadi kwa mtu maskini.
|
20231101.sw_2852_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Aidani aliweza kuongea na watu na hivyo alifaulu kuwasaidia wananchi wengi wa Northumbria wawe Wakristo. Pia katika kituo chake cha utawa aliwafundisha wavulana kumi na wawili, wenyeji wa Northumbria, ili kuhakikisha kwamba Kanisa la Uingereza liongozwe na Waingereza wenyewe.
|
20231101.sw_2852_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Aidani alifuata tawi la Kiselti la Ukristo, si mapokeo ya Kiroma. Hata hivyo tabia yake na bidii katika umisionari zilisababisha Papa Honorius I amheshimu.
|
20231101.sw_2852_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Kituo cha utawa cha Lindisfarne kiliendelea kukua na kuanzisha makanisa na vituo vingine. Pia kilikuwa kama hazina ya ujuzi wa kitaalamu.
|
20231101.sw_2852_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Attwater, Donald and Catherine Rachel John. The Penguin Dictionary of Saints. 3rd edition. New York: Penguin Books, 1993. ISBN 0-14-051312-4.
|
20231101.sw_2852_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Aidani%20wa%20Lindisfarne
|
Aidani wa Lindisfarne
|
Powicke, F. Maurice and E. B. Fryde Handbook of British Chronology 2nd. ed. London:Royal Historical Society 1961
|
20231101.sw_2856_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Alfred%20Nobel
|
Alfred Nobel
|
Alfred Nobel (21 Oktoba 1833 β 10 Desemba 1896) alikuwa mhandisi na mwenye viwanda wa nchi ya Sweden.
|
20231101.sw_2856_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Alfred%20Nobel
|
Alfred Nobel
|
Mwaka wa 1867 aligundua jinsi ya kutengeneza baruti kali. Pia aliboresha utoneshaji wa mafuta. Akafaulu kiuchumi akawa tajiri na wakati uleule mwenye wasiwasi kuhusu matumizi ya baruti aliyogundua kwa sababu aliona matumizi mabaya kwa ajili ya silaha. Hivyo katika hati yake ya wasia alianzisha Tuzo ya Nobel kwa ajili ya mafanikio ya kisayansi lakini pia kwa ajili ya amani duniani.
|
20231101.sw_2856_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Alfred%20Nobel
|
Alfred Nobel
|
Kuanzia ilipoanzishwa tuzo ya Nobel watu mbalimbali wametunukiwa tuzo hiyo kama vile Albert Einstein, Niels Bohr, Max Planck, Mama Teresa, Nelson Mandela n.k.
|
20231101.sw_2858_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Henri%20Dunant
|
Henri Dunant
|
Henri Dunant (8 Mei 1828 - 30 Oktoba 1910) alikuwa mwandishi na mfadhili wa nchi ya Uswisi. Mwaka wa 1859 alianzisha Chama cha Kimataifa cha Msalaba Mwekundu. Pia alisababisha Mapatano ya Geneva. Mwaka wa 1901, pamoja na Frederic Passy, alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel kwa Amani.
|
20231101.sw_2860_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Antoine%20Henri%20Becquerel
|
Antoine Henri Becquerel
|
Antoine Henri Becquerel (15 Desemba 1852 β 25 Agosti 1908) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ufaransa.
|
20231101.sw_2860_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Antoine%20Henri%20Becquerel
|
Antoine Henri Becquerel
|
Mwaka wa 1896 aligundua mionzi nururishi. Mwaka wa 1903, pamoja na Pierre Curie na Marie Curie alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2861_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Robert%20Koch
|
Robert Koch
|
Heinrich Hermann Robert Koch (11 Desemba 1843 β 27 Mei 1910) alikuwa daktari kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa alichunguza virusi visababishavyo magonjwa mbalimbali. Mwaka wa 1882 aligundua kirusi kinachosababisha kifua kikuu, na mwaka wa 1883 kirusi kinachosababisha kipindupindu. Mwaka wa 1905 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2862_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rudyard%20Kipling
|
Rudyard Kipling
|
Rudyard Kipling (30 Desemba 1865 β 18 Januari 1936) alikuwa mwandishi kutoka nchi ya Uingereza. Hasa aliandika riwaya fupi kwa ajili ya kutetea ukoloni. Mwaka wa 1907 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2863_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gabriel%20Lippmann
|
Gabriel Lippmann
|
Gabriel Lippmann (16 Agosti 1845 β 13 Julai 1921) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ufaransa. Hasa alichunguza taalamu ya kupiga picha kwa rangi. Mwaka wa 1908 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2864_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Albrecht%20Kossel
|
Albrecht Kossel
|
Ludwig Karl Martin Leonhard Albrecht Kossel (16 Septemba 1853 β 5 Julai 1927) alikuwa daktari kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa alichunguza protini. Mwaka wa 1910 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2865_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Maurice%20Maeterlinck
|
Maurice Maeterlinck
|
Maurice Polydore Marie Bernard Maeterlinck (29 Agosti 1862 β 5 Mei 1949) alikuwa mwandishi na mshairi kutoka nchi ya Ubelgiji. Mwaka wa 1911 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2866_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Alexis%20Carrel
|
Alexis Carrel
|
Alexis Carrel (28 Juni 1873 β 5 Novemba 1944) alikuwa daktari mpasuaji kutoka nchi ya Marekani. Hasa alichunguza mkusanyiko wa vyembe mwilini (tishu) na mbinu za kuuhamisha. Mwaka wa 1912 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2867_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Elihu%20Root
|
Elihu Root
|
Elihu Root (15 Februari 1845 β 7 Februari 1937) alikuwa mwanasiasa kutoka nchi ya Marekani. Alikuwa mwanachama wa Chama cha Jamhuri cha Marekani. Kutoka 1905 hadi 1909 alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani. Mwaka wa 1912 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani.
|
20231101.sw_2868_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rabindranath%20Tagore
|
Rabindranath Tagore
|
Rabindranath Tagore (7 Mei 1861 β 7 Agosti 1941) alikuwa mwandishi na mwanafalsafa kutoka nchi ya Uhindi. Tagore ni mwakilishi mkuu wa fasihi ya Kihindi ya kisasa. Pia alitafuta mawasiliano ya kitamaduni na Ulaya na Marekani ambako amesafari mara kadhaa. Mwaka wa 1913 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2869_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Romain%20Rolland
|
Romain Rolland
|
Romain Rolland (29 Januari 1866 β 30 Desemba 1944) alikuwa mwandishi kutoka nchi ya Ufaransa. Baadhi ya maandiko yake aliandika wasifu ya maisha ya Ludwig van Beethoven. Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia alifuata mawazo ya Gandhi na ya kikomunisti. Mwaka wa 1915 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2870_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Johannes%20Stark
|
Johannes Stark
|
Johannes Stark (15 Aprili 1874 β 21 Juni 1957) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa alichunguza maswali ya umeme. Mwaka wa 1905 aligundua athari ya Doppler katika mionzi maalumu. Mwaka wa 1919 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2871_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jules%20Bordet
|
Jules Bordet
|
Jules Bordet (13 Juni 1870 β 6 Aprili 1961) alikuwa daktari kutoka nchi ya Ubelgiji. Hasa alichunguza virusi visababishavyo magonjwa mbalimbali. Mwaka wa 1919 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2872_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Carl%20Spitteler
|
Carl Spitteler
|
Carl Friedrich Georg Spitteler (24 Aprili 1845 β 29 Desemba 1924) alikuwa mshairi kutoka nchi ya Uswisi. Hasa aliandika mashairi, riwaya fupi na insha. Mwaka wa 1919 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2873_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/August%20Krogh
|
August Krogh
|
August Krogh (15 Novemba 1874 β 13 Septemba 1949) alikuwa daktari na mwanafiziolojia kutoka nchi ya Denmark. Hasa alichunguza maswali ya uvutaji pumzi. Mwaka wa 1920 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2874_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Knut%20Hamsun
|
Knut Hamsun
|
Knut Hamsun (4 Agosti 1859 β 19 Februari 1952) alikuwa mwandishi kutoka nchi ya Norway. Hasa aliandika mashairi na riwaya. Mwaka wa 1920 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2875_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jacinto%20Benavente
|
Jacinto Benavente
|
Jacinto Benavente (12 Agosti 1866 β 14 Julai 1954) alikuwa mwandishi kutoka nchi ya Hispania. Hasa aliandika tamthiliya. Mwaka wa 1922 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2876_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Fridtjof%20Nansen
|
Fridtjof Nansen
|
Fridtjof Nansen (10 Oktoba 1861 β 13 Mei 1930) alikuwa mpelelezi wa maeneo ya ncha ya Kaskazini, mwanazuolojia na mwanasiasa kutoka nchi ya Norwei. Katika safari yake ya miaka 1888-89 alikuwa mpelelezi wa kwanza kuvuka kisiwa cha Greenland kutoka Mashariki kwenda Magharibi. Miaka ya 1893-96 alisafiri na meli yake iliyoitwa Fram ndani ya barafu ya Bahari ya Ncha ya Kaskazini. Miaka ya 1906-08 alikuwa balozi ya Norwei kule London, Uingereza. Mwaka wa 1922 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani.
|
20231101.sw_2877_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Willem%20Einthoven
|
Willem Einthoven
|
Willem Einthoven (21 Mei 1860 β 29 Septemba 1927) alikuwa daktari na mwanafiziolojia kutoka nchi ya Uholanzi. Hasa alichunguza maswali ya umeme wa moyo na kuunda mbinu za kuupima. Mwaka wa 1924 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2878_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Johannes%20Fibiger
|
Johannes Fibiger
|
Johannes Fibiger (23 Aprili 1867 β 30 Januari 1928) alikuwa daktari na mwanapatholojia kutoka nchi ya Denmark. Hasa alichunguza ugonjwa wa kansa. Mwaka wa 1926 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2879_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Grazia%20Deledda
|
Grazia Deledda
|
Grazia Deledda (30 Septemba 1871 β 15 Agosti 1936) alikuwa mwandishi wa kike kutoka nchi ya Italia. Hasa aliandika riwaya ambazo wahusika wake wametoka kisiwa chake cha Sardinia. Mwaka wa 1926 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2880_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Henri%20Bergson
|
Henri Bergson
|
Henri Bergson (18 Oktoba 1859 β 4 Januari 1941) alikuwa mwanafalsafa na mwandishi kutoka nchi ya Ufaransa. Mwaka wa 1927 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2881_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Charles%20Nicolle
|
Charles Nicolle
|
Charles Jules Henri Nicolle (21 Septemba 1866 β 28 Februari 1936) alikuwa daktari kutoka nchi ya Ufaransa. Hasa alichunguza virusi visababishavyo magonjwa mbalimbali. Alikuwa wa kwanza kueleza jinsi ya kuenea kwa homa ya madoa madoa. Mwaka wa 1928 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2882_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sigrid%20Undset
|
Sigrid Undset
|
Sigrid Undset (20 Mei 1882 β 10 Juni 1949) alikuwa mwandishi wa kike kutoka nchi ya Norwei. Hasa aliandika riwaya ambazo ndani yake alijishughulikia na matatizo ya wanawake wa kisasa. Mwaka wa 1928 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2883_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Karl%20Landsteiner
|
Karl Landsteiner
|
Karl Landsteiner (14 Juni 1868 β 26 Juni 1943) alikuwa daktari kutoka nchi ya Austria. Baadhi ya utafiti mwingi alichunguza virusi visababishavyo magonjwa mbalimbali. Aligundua aina nne za damu ya mwanadamu. Mwaka wa 1930 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2884_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sinclair%20Lewis
|
Sinclair Lewis
|
Sinclair Lewis (7 Februari 1885 β 10 Januari 1951) alikuwa mwandishi kutoka nchi ya Marekani. Katika riwaya zake alikosoa jamii ya kimarekani. Mwaka wa 1926 alituzwa Tuzo ya Pulitzer ya Bunilizi lakini alikataa tuzo hiyo. Mwaka wa 1930 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2885_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/John%20Galsworthy
|
John Galsworthy
|
John Galsworthy (14 Agosti 1867 β 31 Januari 1933) alikuwa mwandishi kutoka nchi ya Uingereza. Aliandika hasa riwaya, tamthiliya na insha. Mwaka wa 1932 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2886_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Luigi%20Pirandello
|
Luigi Pirandello
|
Luigi Pirandello (28 Juni 1867 β 10 Desemba 1936) alikuwa mwandishi kutoka nchi ya Italia. Alijihusisha hasa na tamthiliya na nadharia yake. Mwaka wa 1934 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2887_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Arthur%20Henderson
|
Arthur Henderson
|
Arthur Henderson (20 Oktoba 1863 β 13 Septemba 1935) alikuwa mwanasiasa kutoka nchi ya Uingereza. Alikuwa kiongozi wa Chama cha Wafanyakazi (Labour Party) mara tatu: 1908-11, 1914-22, 1931-34. Pia alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza kuanzia 1929 hadi 1931. Mwaka wa 1934 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani.
|
20231101.sw_2888_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/James%20Chadwick
|
James Chadwick
|
James Chadwick (20 Oktoba 1891 β 23 Julai 1974) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Uingereza. Aligundua na kuchunguza nutroni. Mwaka wa 1935 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2889_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hans%20Spemann
|
Hans Spemann
|
Hans Spemann (27 Juni 1869 β 12 Septemba 1941) alikuwa mwanazuolojia na mwanafiziolojia kutoka nchi ya Ujerumani. Kwa mfano alitafiti maendeleo ya miili ya aina ya chura. Mwaka wa 1935 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2890_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Carlos%20Saavedra%20Lamas
|
Carlos Saavedra Lamas
|
Carlos Saavedra Lamas (1 Novemba 1878 β 5 Mei 1959) alikuwa mwanasheria na mwanasiasa kutoka nchi ya Argentina. Alikuwa Waziri ya Mambo ya Nje kuanzia 1932 hadi 1938. Wakati ule alisaidia kukomesha Vita ya Chako. Mwaka wa 1936 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani.
|
20231101.sw_2891_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mikael%20Agricola
|
Mikael Agricola
|
Mikael Agricola (takriban 1509 β 9 Aprili 1557) alikuwa mwanateolojia katika nchi ya Ufini. Alikuwa mwanafunzi wa Martin Luther na Philipp Melanchthon na baadaye alileta mabadiliko ya kanisa kule Finland. Pia alianzisha fasihi katika lugha ya Kifini na kutafsiri Agano Jipya.
|
20231101.sw_2892_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Otto%20Stern
|
Otto Stern
|
Otto Stern (17 Februari 1888 β 17 Agosti 1969) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ujerumani. Wakati wa utawala wa Adolf Hitler alihamia Marekani. Hasa alichunguza usumaku wa atomu. Mwaka wa 1943 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2893_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Herbert%20Spencer%20Gasser
|
Herbert Spencer Gasser
|
Herbert Spencer Gasser (5 Julai 1888 β 11 Mei 1963) alikuwa mwanafiziolojia kutoka nchi ya Marekani. Hasa alichunguza na kugundua kazi za neva mwilini. Mwaka wa 1944, pamoja na Joseph Erlanger alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2894_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Joseph%20Erlanger
|
Joseph Erlanger
|
Joseph Erlanger (5 Januari 1874 β 5 Desemba 1965) alikuwa daktari na mwanafiziolojia kutoka nchi ya Marekani. Joseph alikuwa ni mtaalamu wa elimu ya neva. Mwaka wa 1944, pamoja na Herbert Spencer Gasser alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2895_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wolfgang%20Pauli
|
Wolfgang Pauli
|
Wolfgang Pauli (25 Aprili 1900 β 15 Desemba 1958) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Austria. Hasa alichunguza nadharia ya Albert Einstein (Relativity Theory) na nadharia ya kwanta. Mwaka wa 1925 alitangaza Kanuni ya Pauli. Mwaka wa 1945 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2896_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kanuni%20ya%20Pauli
|
Kanuni ya Pauli
|
Kanuni ya Pauli ilitangazwa mwaka wa 1925 na Wolfgang Pauli. Inahusu elektroni za atomu. Kila elektroni ina tarakimu nne za kwanta. Kanuni ya Pauli inadai kwamba tarakimu hizo nne haziwezekani kuwa sawa kwa elektroni mbili ndani ya atomu moja.
|
20231101.sw_2897_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Paulo%20Diakono
|
Paulo Diakono
|
Paulo Diakono (takriban 720 - 13 Aprili 799) alikuwa mmonaki Mbenedikto, shemasi na mwanahistoria aliyetoka kabila la Walongobardi.
|
20231101.sw_2897_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Paulo%20Diakono
|
Paulo Diakono
|
Aliandika historia ya maaskofu wa mji wa Metz, historia ya Walangobardi, na wasifu wa Papa Gregori I.
|
20231101.sw_2897_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Paulo%20Diakono
|
Paulo Diakono
|
Carlo Cipolla, Note bibliografiche circa l'odierna condizione degli studi critici sul testo delle opere di Paolo Diacono (Venice, 1901)
|
20231101.sw_2897_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Paulo%20Diakono
|
Paulo Diakono
|
Paul the Deacon, Liber de episcopis Mettensibus, ed. and trans. Damien Kempf, Dallas Medieval Texts and Translations 19 (Paris/Louvain/Walpole, MA: Peeters, 2013).
|
20231101.sw_2898_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolphe%20Adam
|
Adolphe Adam
|
Adolphe Adam (24 Julai 1803 β 3 Mei 1856) alikuwa mtunzi wa nyimbo kutoka nchini Ufaransa. Adam alikuwa mtoto wa mtunzi na mpiga kinanda maarufu huko ufaransa, lakini baba yake hakupenda mtoto wake afuate kazi yake ya muziki.
|
20231101.sw_2898_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolphe%20Adam
|
Adolphe Adam
|
Adolphe alichaguliwa kama profesa katika Chuo cha Muziki cha Paris, Ufaransa. Na kupewa sifa na mwalimu wake wa zamani Daniel Auber na mwalimu wake Adrien Boieldieu kwa jitihada zake katika sanaa ya opera chuoni.
|
20231101.sw_2899_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Daniel%20Auber
|
Daniel Auber
|
Daniel Auber (29 Januari 1782 β 12 Mei 1871) alikuwa mtungaji wa muziki kutoka nchi ya Ufaransa. Alikuwa mwanafunzi wa Luigi Cherubini. Hasa alitunga muziki ya opera.
|
20231101.sw_2900_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bela%20Bartok
|
Bela Bartok
|
Bela Bartok (25 Machi 1881 β 26 Septemba 1945) alikuwa mtunzi wa muziki kutoka nchi ya Hungaria. Alichunguza na kukusanya nyimbo za jadi kutoka maeneo yapakanayo na mto Danube.
|
20231101.sw_2902_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Alexander%20Borodin
|
Alexander Borodin
|
Alexander Borodin (12 Novemba 1833 β 27 Februari 1887) alikuwa mtungaji wa muziki kutoka nchi ya Urusi. Baadhi ya muziki nyingi alitunga muziki ya simfoni.
|
20231101.sw_2903_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20wa%20Ockham
|
William wa Ockham
|
William wa Ockham (takriban 1285 β 9 Aprili 1349 au 1350) alikuwa mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo kutoka nchi ya Uingereza.
|
20231101.sw_2903_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20wa%20Ockham
|
William wa Ockham
|
Toleo bora la maandishi yake kuhusu falsafa na teolojia ni: William of Ockham: Opera philosophica et theologica, Gedeon GΓ‘l, et al., eds. 17 vols. St. Bonaventure, N. Y.: The Franciscan Institute, 1967β88.
|
20231101.sw_2903_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20wa%20Ockham
|
William wa Ockham
|
Karibu maandishi yake yote juu ya siasa yamo katika: William of Ockham, H. S. Offler, et al., eds. 4 vols., 1940β97, Manchester: Manchester University Press [vols. 1β3]; Oxford: Oxford University Press [vol. 4].
|
20231101.sw_2903_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20wa%20Ockham
|
William wa Ockham
|
Richard Utz and Terry Barakat, "Medieval Nominalism and the Literary Questions: Selected Studies." Perspicuitas
|
20231101.sw_2905_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Valentin%20Weigel
|
Valentin Weigel
|
Valentin Weigel (7 Agosti 1533 β 10 Juni 1588) alikuwa mwanateolojia wa Kiprotestanti kutoka nchi ya Ujerumani. Jina lake pia liliandikwa Weichel. Alitunga maandiko mengi yaliyoathiriwa na uchaji wa kutafakari sana habari za Mungu.
|
20231101.sw_2906_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Alphonse%20Laveran
|
Alphonse Laveran
|
Charles Louis Alphonse Laveran (18 Juni 1845 β 18 Mei 1922) alikuwa daktari kutoka nchi ya Ufaransa. Hasa alichunguza virusi visababishavyo magonjwa mbalimbali. Aligundua kirusi kinachosababisha malaria. Mwaka wa 1907 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2907_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ernest%20Orlando%20Lawrence
|
Ernest Orlando Lawrence
|
Ernest Orlando Lawrence (8 Agosti 1901 β 27 Agosti 1958) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Marekani. Hasa alifanya utafiti wa fizikia ya kiini. Mwaka wa 1939 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia. Mwaka wa 1941 alifaulu kutenganisha isotopu za elementi ya urani.
|
20231101.sw_2909_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Fr%C3%A9d%C3%A9ric%20Mistral
|
FrΓ©dΓ©ric Mistral
|
FrΓ©dΓ©ric Mistral (8 Septemba 1830 β 25 Machi 1914) alikuwa mwandishi kutoka nchi ya Ufaransa. Hasa alijishughulikia na kufufua lugha ya Provence inayozungumzwa sehemu za Kusini za Ufaransa. Aliandika mashairi mengi katika lugha hiyo na kutolea kamusi. Mwaka wa 1904 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2911_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gabriela%20Mistral
|
Gabriela Mistral
|
Gabriela Mistral (6 Aprili 1889 β 10 Januari 1957) alikuwa mwandishi na mshairi wa kike kutoka nchi ya Chile. Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Lucila Godoy Alcayaga. Hasa aliuandikia upendo katika mashairi yake. Mwaka wa 1945 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2912_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Camillo%20Golgi
|
Camillo Golgi
|
Camillo Golgi (7 Julai 1844 β 21 Januari 1926) alikuwa daktari kutoka nchi ya Italia. Hasa alichunguza mfumo wa neva. Mwaka wa 1906, pamoja na Santiago Ramon y Cajal alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2913_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Philipp%20Lenard
|
Philipp Lenard
|
Philipp Eduard Anton Lenard (7 Juni 1862 β 20 Mei 1947) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ujerumani. Alitayarisha misingi ya nadharia za elektroni. Pia aliipinga nadharia ya Albert Einstein (Relativity Theory). Mwaka wa 1905 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2914_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Henri%20Moissan
|
Henri Moissan
|
Henri Moissan (28 Septemba 1852 β 20 Februari 1907) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Ufaransa. Baadhi ya utafiti mwingi alichunguza elementi ya florini. Mwaka wa 1906 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2915_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Alfred%20Werner
|
Alfred Werner
|
Alfred Werner (12 Desemba 1866 β 15 Novemba 1919) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Uswisi. Pamoja na utafiti mwingine alichunguza elementi ya naitrojeni. Mwaka wa 1913 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2916_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Frederick%20Soddy
|
Frederick Soddy
|
Frederick Soddy (2 Septemba 1877 β 22 Septemba 1956) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Uingereza. Hasa alichunguza unururifu. Aliunda istilahi mpya ya isotopu. Mwaka wa 1921 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2917_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Fritz%20Haber
|
Fritz Haber
|
Fritz Haber (9 Desemba 1868 β 29 Januari 1934) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Ujerumani. Pamoja na utafiti mwingine alichunguza maswali ya kemia ya umeme. Mwaka wa 1918 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2918_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Paul%20Ehrlich
|
Paul Ehrlich
|
Paul Ehrlich (14 Machi 1854 β 20 Agosti 1915) alikuwa daktari na mwanakemia kutoka nchi ya Ujerumani. Pamoja na Sahachiro Hata aligundua dawa ya kutibu kaswende. Mwaka wa 1908, pamoja na Ilya Mechnikov alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2919_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hermann%20Emil%20Fischer
|
Hermann Emil Fischer
|
Hermann Emil Fischer (9 Oktoba 1852 β 15 Julai 1919) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Ujerumani. Baadhi ya utafiti mwingine aligundua usanisi wa glukosi (aina ya sukari). Mwaka wa 1902 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.