_id
stringlengths 15
22
| url
stringlengths 31
150
| title
stringlengths 1
86
| text
stringlengths 100
23.8k
|
---|---|---|---|
20231101.sw_2920_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hans%20Fischer
|
Hans Fischer
|
Hans Fischer (27 Julai 1881 – 31 Machi 1945) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa alijihusisha na rangi, k.m. rangi za mimea (klorofili), za damu na za nyongo. Mwaka wa 1930 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2921_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Heinrich%20Otto%20Wieland
|
Heinrich Otto Wieland
|
Heinrich Otto Wieland (4 Juni 1877 – 5 Agosti 1957) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Ujerumani. Alihariri kumbukumbu za kikemia za Justus von Liebig. Pia alichunguza mifumo ya kikemia ya sumu za uyoga na asidi ya nyongo. Mwaka wa 1927 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2922_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Irving%20Langmuir
|
Irving Langmuir
|
Irving Langmuir (31 Januari 1881 – 18 Agosti 1957) alikuwa mwanafizikia na mwanakemia kutoka nchi ya Marekani. Alifanya utafiti kuhusu taa za gesi, neli za elektroni na vivuta hewa. Mwaka wa 1932 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2923_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jean%20Perrin
|
Jean Perrin
|
Jean Baptiste Perrin (30 Septemba 1870 – 17 Aprili 1942) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ufaransa. Hasa alichunguza mada za fizikia ya kiini na kemia ya kifizikia. Mwaka wa 1926 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2924_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Theodor%20Svedberg
|
Theodor Svedberg
|
Theodor Svedberg (30 Agosti 1884 – 26 Februari 1971) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Sweden. Baadhi ya uchunguzi mwingi aliunda aina ya mashinepewa. Pia alitafiti mada za fizikia ya kiini. Mwaka wa 1926 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2925_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Artturi%20Ilmari%20Virtanen
|
Artturi Ilmari Virtanen
|
Artturi Ilmari Virtanen (15 Januari 1895 – 11 Novemba 1973) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Finland. Baadhi ya utafiti mwingi alichunguza virusi vikaavyo kwenye udongo. Mwaka wa 1945 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2926_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gerhard%20Domagk
|
Gerhard Domagk
|
Gerhard Johannes Paul Domagk (30 Oktoba 1895 – 24 Aprili 1964) alikuwa daktari kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa alichunguza virusi visababishavyo magonjwa mbalimbali, na kuchapa kazi kwa ajili ya tiba ya kikemia kukomesha magonjwa kama kifua kikuu na kansa. Mwaka wa 1939 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.
|
20231101.sw_2927_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Richard%20Kuhn
|
Richard Kuhn
|
Richard Kuhn (3 Desemba 1900 – 1 Agosti 1967) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa alichunguza vitamini. Mwaka wa 1938 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2928_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
Patrice Lumumba (2 Julai 1925 – 17 Januari 1961) alikuwa mwanasiasa na kiongozi wa uhuru wa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
|
20231101.sw_2928_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
Mwaka wa 1958 alikuwa miongoni mwa waanzishaji wa Chama cha Taifa la Kongo (kwa Kifaransa: Mouvement National Congolais).
|
20231101.sw_2928_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
Mwaka wa 1960 alipata kuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kuongoza harakati za kugombea uhuru toka kwa utawala wa kikoloni wa Wabelgiji.
|
20231101.sw_2928_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
Baada ya miezi miwili tu ya kuwa Waziri Mkuu, Lumumba alipinduliwa na baadaye kutiwa ndani kabla ya kuuawa katika mazingira ya kutatanisha katika eneo la Katanga upande wa kusini wa Kongo.
|
20231101.sw_2928_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
Patrice Lumumba alizaliwa katika familia ya Watetela, wazazi wake walikuwa François Tolenga Otetshima, na Julienne Wamato Lomendja, ambao walikuwa wafugaji katika eneo la Katakokombe kwenye Mkoa wa Kasai.
|
20231101.sw_2928_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Élias Okit'Asombo alilobadilisha baadaye. na asombó ('cursed or bewitched people who will die quickly'). Alikuwa na kaka watatu ambao ni Charles Lokolonga, Émile Kalema, and Louis Onema Pene Lumumba.Alilelewa katika makuzi ya Kikatoliki, alisoma katika shule ya msingi ya Waprotestanti, halafu katika shule ambayo iliyomilikiwa na wamisionari wa Kanisa Katoliki, na baadaye alipata mafunzo katika chuo kimoja cha serikali, alijishindia kozi mbalimbali na kisha kuajiriwa, alipata kazi katika mji wa Stanleyville ambao kwa sasa unajulikana kwa jina la Kisangani ambapo alifanya kazi kama karani wa posta.
|
20231101.sw_2928_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
Baadaye alihamia Léopoldville ambao kwa sasa unajulikana kwa jina la Kinshasa alipofanya kazi ya uuzaji wa bia kwa wasafiri. Mnamo mwaka 1951 alimuoa Pauline Opangu. Mwaka 1955 Lumumba alijiunga na Cercles des évolués ambazo zilikuwa klabu za Waafrika wenye elimu ya kibelgiji na kutazamwa kuwa "wameendelea" mjini Stanleyville na baadaye alijiunga na chama cha Liberal Party of Belgium, ambapo alifanya kazi ya uhariri na usambazaji wa kijarida cha Chama cha Kiliberali cha Ubeljiji. Baadaye alifanya ziara ya mafunzo ya wiki tatu nchini Ubeljiji, mwaka 1956 alikamatwa na kushitakiwa kwa kosa la ubadhirifu na kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kifungo cha nje na, kisha wakili wa Kibelgiji kuthibitisha kwamba Lumumba amesharejesha zile fedha, aliachiliwa huru mapema mwaka uleule.
|
20231101.sw_2928_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
Baada ya kuachiliwa kwake alisaidiwa na kuanzisha chama cha w:Mouvement national congolais (MNC). Mwaka 1958, alichaguliwa kuwa Rais wa chama hicho. Mnamo Desemba 1958 Lumumba na wenzake walikiwakilisha chama chao katika mkutano wa Baraza la watu wote wa Afrika mjini Accra, Ghana, katika mkutano huo wa Desemba wa muungano wa Afrika uliokuwa chini ya Rais wa Ghana Kwame Nkrumah, Lumumba ambaye alionekana kuongea lugha nyingi, zikiwemo za Kitetela, Kifaransa, Lingala, Kiswahili, na Kiluba, alijitambulisha kwa imani yake kwa bara la Afrika.
|
20231101.sw_2928_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
Mnamo mwezi wa Oktoba, mwaka 1959, Lumumba, kama kiongozi wa chama cha MNC, alikamatwa kwa kosa la kuchochea vurugu za kupinga serikali ya kikoloni katika mji wa Stanleyville ambapo watu takriban 30 waliuawa na yeye alihukumiwa kwenda jela kwa muda wa miezi sita. Mnamo tarehe 18 Januari 1960 ambayo ilikuwa siku ya majaribio na hapohapo katika siku ya kwanza ya mkutano wa kuzungumzia hatma ya nchi ya Kongo itakumbukwa kwamba, licha ya Lumumba kuwa jela katika kipindi hicho, chama chake cha MNC kilifanikiwa kuwashawishi wananchi kwenye uchaguzi uliofanyika mwezi Desemba na kushinda katika jamhuri ya Kongo. Kutokana na nguvu ya umma iliyokuwa ikifanywa na wananchi wa Kongo dhidi ya kuachiliwa kwa Lumumba kutoka kila kona, aliachiliwa na kuruhusiwa kuhudhuria katika mkutano wa Brussels. Mkutano huo ulifikia kilele tarehe 27 June 1960 kwa azimio la uhuru wa nchi ya Kongo na kupanga uchaguzi kwa mwaka huohuo wa 1960 (Uchaguzi Mkuu wa Kongo 11–25 Mei 1960.
|
20231101.sw_2928_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
Lumumba na chama chake cha MNC walipata ushindi uliowawezesha kuunda serikali kwa tangazo la tarehe 23 June 1960 na Patrice Lumumba anapata cheo cha uwaziri mkuu akiwa na umri wa miaka 34 na Joseph Kasa-Vubu akiwa ndie Rais wake wa kwanza. Kwa mujibu wa katiba ya Congo mnamo tarehe 24 June serikali ilipitisha kura ya kijasiri ambayo iliamuliwa na baraza la maseneta kwamba tarehe 24 iwe ni siku ya ya kuadhimisha uhuru wa Congo.
|
20231101.sw_2928_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
Maadhimisho ya uhuru wa Congo kwa mara ya kwanza yalifanyika mnamo tarehe 30 June 1960 ambapo maadhimisho hayo yalihudhuriwa pia na Mfalme Baudouin wa Ubelgiji pamoja na vyombo mbalimbali vya habari kutoka nchi za nje. Lumumba alitoa hotuba yake kama Waziri mkuu katika nchi huru japo yeye alikuwa ameenguliwa katika ratiba ya shughuli hiyo. Mfalme wa Ubeljiji alihutubia kwa kutukuza utawala wa kikoloni, huku akilingania fikra za mjomba wake ambaye alikuwa mfalme wa Ubelgiji akiitwa Leopold II wa Ubelgiji bila kutaja maangamizi ya Dola huru la Kongo. Mfalme aliendelea kutoa masharti, "aliwataka kutokufanya mabadiliko yoyote mpaka wao watakapoona kwamba wanaweza kufanya vyema, na kwamba wataendelea kutoa ushauri. " Lumumba aliufahamisha umma kwamba uhuru uliotolewa na Wabeljiji haukuja hivihivi:
|
20231101.sw_2928_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Patrice%20Lumumba
|
Patrice Lumumba
|
kwa uhuru huu wa Congo hata kama tunasherehekea leo na Wabeljiji, nchi rafiki ambayo tupo sawa kwa sawa, hakuna Mkongo hata mmoja ambaye atasahau kwamba vita waliyipigana hatimaye wakashinda wamaeshinda, kwa mapambano yaliyokuwa yakiendelea, mapambano ambayo watu tulijitoa ambayo kwayo watu walikuwa tayari kwa lolote hata kumwaga damu, kwa namna kwa hakika yalikuwa mapambano matukufu na yalikuwa na mwelekeo wa kukomesha utumwa ambao ulikuwa ukiendeshwa dhidi yetu kwa nguvu.
|
20231101.sw_2929_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/George%20Gershwin
|
George Gershwin
|
George Gershwin (26 Septemba 1898 – 11 Julai 1937) alikuwa mtungaji wa muziki na mpiga kinanda kutoka nchi ya Marekani. Alitunga nyimbo nyingi zilizoathiriwa na mitindo ya Jazz. Pia alitunga opera moja iitwayo Porgy na Bess. Aliaga dunia mapema baada ya kupatwa na kansa ya ubongo. Mwaka wa 1998 alituzwa tuzo maalumu ya Tuzo ya Pulitzer ya Muziki kwa kazi ya maisha yake, yaani baada ya kifo chake.
|
20231101.sw_2930_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Murdock
|
William Murdock
|
William Murdock (25 Agosti 1754 – 15 Novemba 1839) alikuwa mhandisi kutoka nchi ya Uingereza. Alivumbua na kubuni taa ya gesi.
|
20231101.sw_2933_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Florini
|
Florini
|
Florini ni dutu sahili na halojeni simetali. Namba atomia yake ni 9. Katika mazingira yetu kawaida iko katika hali ya gesi yenye rangi njanokijani. Alama yake ya kikemia ni F.
|
20231101.sw_2933_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Florini
|
Florini
|
Kwa kawaida hupatikana kama molekuli ya F2. Kati ya elementi zote mmenyuko wake wa oksidisho ni kali sana. Tabia hii inasababisha Florini kuwa sumu kali. Inamenyuka vikali na karibu elementi zote.
|
20231101.sw_2940_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tuzo%20ya%20Nobel%20ya%20Fizikia
|
Tuzo ya Nobel ya Fizikia
|
Tuzo ya Nobel ya Fizikia hutolewa kila mwaka kufuatana na wasia ya Alfred Nobel na kamati ya Taasisi ya Taaluma ya Sayansi ya Sweden.
|
20231101.sw_2940_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tuzo%20ya%20Nobel%20ya%20Fizikia
|
Tuzo ya Nobel ya Fizikia
|
2016 David James Thouless, Frederick Duncan Michael Haldane na John Michael Kosterlitz "for theoretical discoveries of topological phase transitions and topological phases of matter"
|
20231101.sw_2941_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tuzo%20ya%20Nobel%20ya%20Kemia
|
Tuzo ya Nobel ya Kemia
|
Tuzo ya Nobeli ya Kemia hutolewa kila mwaka kufuatana na wasia wa Alfred Nobel na Kamati ya Taasisi ya Taaluma ya Sayansi ya Sweden.
|
20231101.sw_2942_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tuzo%20ya%20Nobel%20ya%20Tiba
|
Tuzo ya Nobel ya Tiba
|
Tuzo ya Nobel ya Tiba au Fiziolojia hutolewa kila mwaka kufuatana na wasia ya Alfred Nobel na kamati ya Taasisi ya Taaluma ya Sayansi ya Sweden.
|
20231101.sw_2944_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tuzo%20ya%20Nobel%20ya%20Amani
|
Tuzo ya Nobel ya Amani
|
Tuzo ya Nobel ya Amani inatolewa na kamati ya Nobel ya Norway iliyochaguliwa na Bunge ya Norway kufuatana na wasia ya Alfred Nobel.
|
20231101.sw_2946_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lilongwe
|
Lilongwe
|
Lilongwe ni mji mkuu wa Malawi wenye wakazi 597,619 (sensa ya mwaka 2003). Yenyewe iko kusini magharibi mwa nchi, magharibi mwa Mto Malawi karibu na mpaka wa Malawi na Msumbiji na Zambia. Lilongwe mahali pake ni (-13.98333, 33.78333).
|
20231101.sw_2946_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lilongwe
|
Lilongwe
|
Mji huo ulianza kama kijiji kwa ufuo wa Mto Malawi na kuwa Kituo cha amri ya wakoloni Waingereza kwa mwanzo wa karne 1900. Yasemekana kwamba, Lilongwe ilisaidia sana kama kituo cha serikali ya wakoloni kwa sababu Lilongwe ilikuwa kwa ruti ya kusini na kaskazini ambayo iliwezesha utawala wa Rhodesia ya kaskazini inayojulikana sasa kama Zambia. Mji wa Lilongwe baadaye ukawa mji wa pili kwa ukubwa Malawi. Mwaka wa 1974, Mji mkuu wa nchi ulihamishwa kutoka Zomba (mji ambao sasa ni wa tatu kwa ukubwa nchini Malawi), hadi kwa mji namba mbili kwa ukubwa, Lilongwe.
|
20231101.sw_2946_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lilongwe
|
Lilongwe
|
Mji wenyewe una wilaya nyingi ambazo zajulikana kama eneo, mbila kati ya mji kuwa eneo iliopewa namba. Eneo zenyewe hazijapewa namba kulingana vile eneo zimepakana.
|
20231101.sw_2946_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lilongwe
|
Lilongwe
|
Kuna mabasi na motokaa za abiria zinazosafirisha watu kwa miji ya kale, katikati ya Mji wenyewe na pia Kiwanja cha denge. Mataksi yapatikana rahisi kutoka kwa na taksi kwa jia inayoitwa Presidential Way, kaskazini mwa maduka za soko zilizokati ya Mji.
|
20231101.sw_2946_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lilongwe
|
Lilongwe
|
Kuna chuo cha ukulima mjini Lilongwe. Wakati wa mvua hasa ni Oktoba na Aprili. Wakati wa ukame ni kuanzia Aprili hadi Oktoba. Kati ya muda huu wa ukame, Juni na Julai kuna baridi na Agosti kukizidi na upepo na vumbi.
|
20231101.sw_2946_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lilongwe
|
Lilongwe
|
Ukulima ni kama wa tumbako, miwa, mipamba, chai, mahindi, viazi, mikota, mihogo, mituta, na pia kwa wanyama ni kama ng'ombe, mbuzi. Mashamba ya ukulima ni kama 34% za nchi.
|
20231101.sw_2946_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lilongwe
|
Lilongwe
|
Vifaa vinavyonunuliwa kutoka nchi za kigeni ni vyakula, mafuta, vifaa vilivyoundwa, vifaa vya utumizi na vifaa vya usafirishaji.
|
20231101.sw_2946_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lilongwe
|
Lilongwe
|
Madini na mali ni kama simiti, madini ya yuranimu ambayo hayajachimbwa, makaa ya miamba, madini ya shabu au alumini.
|
20231101.sw_2946_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lilongwe
|
Lilongwe
|
Mambo ya mazingira; ukataji wa miti; mmomonyoko wa udongo; ujanaba wa maji, maji ya siwa (ya choo), takataka za viwanda; samaki kupunguka kwa kuaribu eneo za yai za samaki.
|
20231101.sw_2947_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hendrik%20Antoon%20Lorentz
|
Hendrik Antoon Lorentz
|
Hendrik Antoon Lorentz (18 Julai 1853 – 4 Februari 1928) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Uholanzi. Alitafiti nadharia ya elektroni. Pia alichunguza nadharia ya Albert Einstein (Relativity Theory) na ya kwanta. Mwaka wa 1902, pamoja na Pieter Zeeman alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2948_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Albert%20Abraham%20Michelson
|
Albert Abraham Michelson
|
Albert Abraham Michelson (19 Desemba 1852 – 9 Mei 1931) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Marekani. Tafiti zake ziliweka msingi kwa nadharia ya Albert Einstein (Relativity Theory). Pia aliboresha vipimo vya mwendo wa nuru. Mwaka wa 1907 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2949_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Guglielmo%20Marconi
|
Guglielmo Marconi
|
Guglielmo Marconi (25 Aprili 1874 – 20 Julai 1937) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Italia. Baada ya uchunguzi mwingi, alivumbua njia ya mawasiliano bila waya.
|
20231101.sw_2949_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Guglielmo%20Marconi
|
Guglielmo Marconi
|
Mwaka wa 1909, pamoja na Ferdinand Braun alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia. Marconi ametajwa mara nyingi kama mvumbuzi wa redio pamoja na Nikola Tesla na Alexander Popov.
|
20231101.sw_2950_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Heike%20Kamerlingh%20Onnes
|
Heike Kamerlingh Onnes
|
Heike Kamerlingh Onnes (21 Septemba 1853 – 21 Februari 1926) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Uholanzi. Alichunguza elementi katika hali ya baridi sana. Pia alifaulu kuoesha elementi ya heliamu. Mwaka wa 1913 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2951_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Max%20von%20Laue
|
Max von Laue
|
Max von Laue (9 Oktoba 1879 – 24 Aprili 1960) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ujerumani. Pamoja na utafiti mwingine alichunguza mionzi ya eksirei. Mwaka wa 1914 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia. Tangu mwaka wa 1950 alikuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Max Planck kwa kemia ya kifizikia kule Berlin.
|
20231101.sw_2955_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Uholanzi ni nchi ya Ulaya ya Magharibi. Imepakana na Ujerumani upande wa mashariki, Ubelgiji upande wa kusini na Bahari ya Kaskazini (North Sea) upande wa magharibi na kaskazini.
|
20231101.sw_2955_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Uholanzi ni sehemu ya "Ufalme wa Nchi za Chini" (Kingdom of the Netherlands) pamoja na visiwa vya Aruba, Curaçao na Sint Maarten, mbali ya visiwa vingine vitatu vya Karibi vya Uholanzi.
|
20231101.sw_2955_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Jina la Uholanzi limetokana na “Holland”, eneo la magharibi la nchi hii. Watu wengi hutumia jina hilo, lakini wakazi wenyewe wanaiita nchi yao “Nederland” inayomaanisha "nchi ya chini". Kwa kweli, sehemu kubwa ya Uholanzi iko chini ya usawa wa bahari. Waholanzi wamejenga maboma kuzuia maji yasienee yakifurika.
|
20231101.sw_2955_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Akifika Uholanzi kwa uwanja wa ndege wa Schiphol, msafiri anastaajabu nchi ilivyo tambarare. Kwa kweli, kuna sehemu zenye vilima, lakini sehemu kubwa zaidi ya Uholanzi ni tambarare.
|
20231101.sw_2955_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Mahali pa juu kabisa nchini ni Kilima cha Vaals, upande wa kusini wa mkoa wa Limburg, kwa 322 m. Mahali pa chini kabisa ni karibu na Nieuwerkerk aan de IJssel, mkoa wa Zuid Holland, kwa -6.76 m (mita 6.76 chini ya usawa wa wastani wa bahari).
|
20231101.sw_2955_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Vipande vikubwa vya nchi vimepatikana kutoka ziwa au bahari. Ili kufanya hivyo boma linajengwa kuzunguka ziwa au sehemu ya bahari, kisha maji yanavutwa kwa bomba. Mahali kati ya boma huitwa “polder”. Mkoa mmoja mzima, Flevoland, umepatwa kwa maji ya “Zuiderzee” (Bahari ya Kusini). Kwa sababu hiyo watu husema: “Mungu aliumba dunia lakini Waholanzi waliumba Uholanzi.” Hata sasa sehemu muhimu ya Uholanzi ni maji: 18%.
|
20231101.sw_2955_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Maboma mengine makubwa yamejengwa upande wa kusini magharibi wa nchi ili ya kuzuia maji yasienee mikoa ya Zeeland na Zuid Holland. Mradi huu huitwa “Deltawerken” au Ujenzi wa Delta. “Oosterscheldekering” au boma la mto wa Oosterschelde ni jengo linaloshangaza. Urefu wake ni 9 km na katikati yake kuna malango makubwa 62 ambayo hujifunga wenyewe kila wakati ambapo maji ya bahari yakifura zaidi ya 3 m. Barabara kuu inapitia juu ya boma hili.
|
20231101.sw_2955_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Mito mikubwa kadhaa inaingia Uholanzi na kutiririka katika Bahari ya Kaskazini. Mto Rijn (Mto Rhine) unaingia kwa Tolkamer upande wa mashiriki, na karibu na Nijmegen Mto Waal unajitenga ambao unachukua 70% ya maji. Mto IJssel unajitenga karibu na Westervoort na kwenda upande wa kaskazini. Mto Maas (Mto Meuse) unaingia Uholanzi upande wa kusini wa Limburg, na karibu na Mook unageuka upande wa magharibi. Mto Schelde unaingia upande wa kusini wa Zeeland.
|
20231101.sw_2955_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Uholanzi umegawanyika katika mikoa 12. Kila mkoa unatawaliwa na gavana ambaye huitwa “Commissaris van de Koningin” isipokuwa yule wa Limburg ambaye huitwa “Gouverneur”. Mikoa na miji mikuu yao ni :
|
20231101.sw_2955_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Katika Uholanzi barabara daima zina msongamano wa magari. Hii ni kwa sababu watu wanakwenda kazini asubuhi hadi kurejea jioni, na wanaoishi Uholanzi ni wengi, na kufanya kazi nyingi sana.
|
20231101.sw_2955_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Kisha kutekwa na Julius Caesar katika karne ya 1 KK, kusini mwa nchi ikawa mpaka wa kaskazini wa Dola la Roma hadi lilipokoma (karne ya 5).
|
20231101.sw_2955_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Baadaye nchi ilivamiwa na makabila mbalimbali ya Wagermanik: Wasaksoni, Wabatavi, Wafrisi na Wafaranki.
|
20231101.sw_2955_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Katika karne ya 8 nchi ilikuwa sehemu ya dola la Karolo Mkuu, na katika karne ya 10 ya Dola Takatifu la Kiroma.
|
20231101.sw_2955_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Katika karne ya 16 nchi ilikuwa chini ya familia ya makaisari (Absburg), lakini ilipokea Matengezo ya Kiprotestanti kinyume cha matakwa ya kaisari Karolo V.
|
20231101.sw_2955_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Mwanae Filipo II wa Hispania alipomrithi hakukubali jambo hilo na kusababisha uasi ulioenea kote (1566-1581) hadi wilaya saba zilipounda jamhuri iliyotambuliwa na Hispania mwaka 1648 tu, katika amani ya Westfalia.
|
20231101.sw_2955_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Karne ya 17 ndipo nchi ilipofikia kilele cha ustawi wake, ikiwa na makoloni mengi huko India, Indonesia, Afrika na Amerika, pamoja na biashara kubwa ya kimataifa duniani kote.
|
20231101.sw_2955_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Baada ya mapinduzi ya Kifaransa (1789) nchi ilitekwa na Wafaransa hadi Amani ya Vienna (1814-1815) iliyopanua Uholanzi huru tena, lakini kwa mfumo wa ufalme.
|
20231101.sw_2955_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Uholanzi haukutaka kushiriki Vita vikuu vya kwanza vya dunia, lakini katika vita vikuu vya pili ulivamiwa na Ujerumani (1940-1945).
|
20231101.sw_2955_18
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Baadaye Uholanzi umejitahidi sana kushiriki katika mahusiano ya kimataifa na ni kati ya nchi waanzilishi wa Umoja wa Ulaya.
|
20231101.sw_2955_19
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Wakazi wengi wana asili ya makabila ya Kijerumani, lakini kuna wahamiaji wengi pia kutoka nchi nyingi. 22% za wakazi wana walau mzazi mmoja kutoka nchi za nje.
|
20231101.sw_2955_20
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uholanzi
|
Uholanzi
|
Upande wa dini, takwimu za serikali zinaonyesha kwamba mwaka 2015, 50.1% ya wakazi hawakuwa na dini yoyote, 43.8% walikuwa Wakristo (23.7% Wakatoliki, 21.1% Waprotestanti, hasa Wakalvini, 4.9% Waislamu, 1.1% Mabanyani, Wabuddha n.k.
|
20231101.sw_2957_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wole%20Soyinka
|
Wole Soyinka
|
Akinwande Oluwole (au "Wole" Soyinka) ni mwandishi Mnigeria na mshindi Mwafrika wa kwanza wa Tuzo ya Nobel ya fasihi (mwaka wa 1986). Wengi wanamwona ndiye mwandishi bora wa michezo ya kuigizwa Afrika.
|
20231101.sw_2957_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wole%20Soyinka
|
Wole Soyinka
|
Alizaliwa tarehe 13 Julai 1934 kwa wazazi Wayoruba huko Abeokuta, Nigeria. Alisoma shule ya msingi kwao Abeokuta halafu shule ya sekondari ya Ibadan. Alifuata masomo ya fasihi Chuo Kikuu huko Ibadan (1952-1954) na Leeds (Uingereza) 1954-1957.
|
20231101.sw_2957_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wole%20Soyinka
|
Wole Soyinka
|
Soyinka aligongana mara nyingi na serikali za kidikteta za nchi yake akipinga pia udikteta katika nchi mbalimbali kama vile utawala wa Mugabe huko Zimbabwe. Katika maandishi yake alilenga mara nyingi "buti linalokandamiza bila kujali rangi ya mguu ndani yake". Hasa wakati wa udikteta wa jenerali Sani Abacha (1993-1998) Soyinka alijikuta hatarini. Akaondoka Nigeria akaishi nje alipopata nafasi ya profesa ya fasihi kwenye Chuo Kikuu cha Emory (Atlanta - Marekani).
|
20231101.sw_2957_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wole%20Soyinka
|
Wole Soyinka
|
Baada ya mwisho wa utawala wa kijeshi mwaka 1999 Soyinka alikubali nafasi kwenye chuo kikuu cha Ife kwa masharti ya kwamba mwanajeshi mstaafu hatakuwa kamwe chansela wa chuo kikuu kile.
|
20231101.sw_2957_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wole%20Soyinka
|
Wole Soyinka
|
Wole Soyinka amemwoa mke wake Laide akazaa naye watoto wanne. Aliwahi kuwa na watoto wawili kabla ya kuoa.
|
20231101.sw_2963_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Charles%20%C3%89douard%20Guillaume
|
Charles Édouard Guillaume
|
Charles Édouard Guillaume (15 Februari 1861 – 13 Juni 1938) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Uswisi aliyeishi Ufaransa.
|
20231101.sw_2965_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Robert%20Millikan
|
Robert Millikan
|
Robert Andrews Millikan (22 Machi 1868 – 19 Desemba 1953) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Marekani. Baadhi ya uchunguzi mwingine alijishughulikia na vipimo vya umeme wa elementi. Mwaka wa 1923 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2968_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gustav%20Hertz
|
Gustav Hertz
|
Gustav Ludwig Hertz (22 Julai 1887 – 30 Oktoba 1975) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa alichunguza sifa za atomu. Pia alivumbua njia fulani ya kutenganisha isotopu. Mwaka wa 1925, pamoja na James Franck alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.
|
20231101.sw_2970_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Werner%20Heisenberg
|
Werner Heisenberg
|
Werner Karl Heisenberg (5 Desemba 1901 – 1 Februari 1976) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ujerumani. Alivumbua umekaniki wa kwanta na kutangaza Kanuni ya Heisenberg ya Utovu wa Hakika. Pia alifanya utafiti wa msingi kuhusu fizikia ya kiini. Mwaka wa 1932 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia. Mpaka mwaka wa 1970 alikuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Max Planck kwa Fizikia ya Nyota.
|
20231101.sw_2971_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kanuni%20ya%20Heisenberg%20ya%20Utovu%20wa%20Hakika
|
Kanuni ya Heisenberg ya Utovu wa Hakika
|
Kanuni ya Heisenberg ya Utovu wa Hakika (kwa kifupi: Kanuni ya Utovu wa Hakika) ni kanuni muhimu katika fizikia ya kwanta. Inasema kwamba haiwezekani kupima sifa mbili zinazotegemeana za kipande kimoja cha elementi kwa uhakika kabisa. Baadhi ya sifa hizo kuna mahali na mwendo. Maana yake, kwa mfano, haiwezekani kupima kabisa mahali na mwendo wa elektroni moja wakati huohuo.
|
20231101.sw_2975_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/San%20Marino
|
San Marino
|
San Marino (kwa Kiitalia maana yake ni "Mtakatifu Marino") ni kati ya nchi ndogo kabisa duniani. Eneo lake lote limo ndani ya mipaka ya Italia, kati ya wilaya za Rimini na Pesaro-Urbino, karibu na mwambao wa bahari ya Adria.
|
20231101.sw_2975_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/San%20Marino
|
San Marino
|
San Marino inatajwa kuwa jamhuri yenye umri mkubwa kuliko zote duniani. Ilianzishwa na Wakristo waliokimbia dhuluma ya Kaisari wa Roma Diokletiano wakitafuta kimbilio mlimani.
|
20231101.sw_2975_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/San%20Marino
|
San Marino
|
Tangu hapo imefaulu kudumisha uhuru wake. Ndiyo sababu tangu mwaka 2008 imeorodheshwa na UNESCO kati ya mahali pa Urithi wa Dunia.
|
20231101.sw_2975_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/San%20Marino
|
San Marino
|
San Marino ina wakazi 33,909 (2019) katika vijiji 9. Karibu wote (97.2%) ni waumini wa Kanisa Katoliki (jimbo la San Marino-Montefeltro) na wanaongea Kiitalia kwa lahaja ya Kiromagna.
|
20231101.sw_2975_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/San%20Marino
|
San Marino
|
San Marino imetunza utaratibu wa serikali inayofanana na muundo wa jamhuri ya Roma ya kale. Serikali inaongozwa na watawala wawili ("Capitani Reggenti") wanaochaguliwa kwa muda wa miezi sita tu kama zamani konsuli wa Kiroma.
|
20231101.sw_2975_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/San%20Marino
|
San Marino
|
Bunge linaitwa Halmashauri Kuu ("Consiglio Grande e Generale") likichaguliwa kila baada ya miaka mitano. Halmashauri inateua pia kamati ya watu 12 ("Consiglio dei XII") inayotekeleza kazi ya mahakama.
|
20231101.sw_2975_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/San%20Marino
|
San Marino
|
Wananchi wote hukutana mara mbili kwa mwaka kama mkutano mkubwa wa "Arengo" wakiamua juu ya matamko na mapendekezo kwa serikali.
|
20231101.sw_2976_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sully%20Prudhomme
|
Sully Prudhomme
|
Sully Prudhomme (16 Machi 1839 – 7 Septemba 1907) alikuwa mwandishi na mshairi kutoka nchi ya Ufaransa. Jina lake la kuzaliwa lilikuwa René-François-Armand Prudhomme. Mashairi yake yanaonyesha sifa za ujumi. Mwaka wa 1901 alikuwa mshindi wa kwanza wa Tuzo ya Nobel kwa Fasihi.
|
20231101.sw_2979_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Toni%20Morrison
|
Toni Morrison
|
Toni Morrison (18 Februari 1931 – 5 Agosti 2019) alikuwa mwandishi wa kike nchini Marekani na mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi ya mwaka 1993.
|
20231101.sw_2979_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Toni%20Morrison
|
Toni Morrison
|
Alizaliwa kwa jina la Chloe Anthony Wofford tarehe 18 Februari 1931 huko Lorain, Ohio - 2019 kama mtoto wa pili wa familia ya Waamerika weusi. Wazazi wake walikuwa wafanyakazi.
|
20231101.sw_2979_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Toni%20Morrison
|
Toni Morrison
|
Alipenda kusoma vitabu tangu utoto. 1949 akajiunga na chuo kikuu cha Howard (chuo kwa Waamerika weusi katika mji mkuu Washington D.C.) akimaliza kwa digrii ya BA katika somo la Kiingereza. Wakati ule aliacha jina lake la Chloe akatumia "Toni" kama kifupi cha "Anthony". Mwaka 1955 alipata MA (shahada ya pili) kutoka chuo kikuu cha Cornell.
|
20231101.sw_2979_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Toni%20Morrison
|
Toni Morrison
|
Alianza kufundisha fasihi kwenye chuo kikuu cha Texas Kusini mjini Houston, tangu 1957 tena Howard. Aliolewa na Howard Morrison akazaa watoto wawili. Baada ya talaka mwaka 1964 alianza kazi ya uhariri wa vitabu kwa wachapishaji wa Random House. Alihariri vitabu vingi vya waandishi weusi.
|
20231101.sw_2979_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Toni%20Morrison
|
Toni Morrison
|
Mwaka 1970 alitoa kitabu chake cha kwanza "The Bluest Eye" (Jicho la buluu kabisa). Kitabu cha kwanza kilichofaulu kuuzwa vema kilikuwa "Song of Solomon" (Wimbo ya Suleimani) mwaka 1977. Mwaka wa 1988 alituzwa Tuzo ya Pulitzer ya Bunilizi kwa riwaya yake Beloved.
|
20231101.sw_2979_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Toni%20Morrison
|
Toni Morrison
|
Tangu 1989 amefundisha kama profesa katika chuo kikuu cha Princeton. 1993 alipokea Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2980_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Theodor%20Mommsen
|
Theodor Mommsen
|
Christian Matthias Theodor Mommsen (30 Novemba 1817 – 1 Novemba 1903) alikuwa mwanahistoria na mwandishi kutoka nchi ya Ujerumani. Anafahamika hasa kwa kitabu chake Historia ya Roma (kwa Kijerumani: Römische Geschichte). Mwaka wa 1902 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2981_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Henryk%20Sienkiewicz
|
Henryk Sienkiewicz
|
Henryk Adam Aleksander Pius Sienkiewicz (5 Mei 1846 – 15 Novemba 1916) alikuwa mwandishi kutoka nchi ya Poland.
|
20231101.sw_2981_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Henryk%20Sienkiewicz
|
Henryk Sienkiewicz
|
Riwaya zake zilikuwa hupendwa sana na watu wengi. Mwaka wa 1905 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2983_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Giosue%20Carducci
|
Giosue Carducci
|
Giosuè Carducci (27 Julai 1835 – 16 Februari 1907) alikuwa mwandishi na mshairi kutoka nchi ya Italia.
|
20231101.sw_2984_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rudolf%20Christoph%20Eucken
|
Rudolf Christoph Eucken
|
Rudolf Christoph Eucken (5 Januari 1846 – 14 Septemba 1926) alikuwa mwanafalsafa na mwandishi kutoka nchi ya Ujerumani. Alitafsiri vitabu vya Aristoteli na kuandika vitabu kuhusu maadili na dini. Mwaka wa 1908 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.
|
20231101.sw_2987_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Selma%20Lagerlof
|
Selma Lagerlof
|
Selma Lagerlöf (20 Novemba 1858 – 16 Machi 1940) alikuwa mwandishi wa kike kutoka nchi ya Sweden. Aliandika hasa riwaya. Mwaka wa 1909 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi akiwa mwanamke wa kwanza kupokea tuzo hiyo.
|
20231101.sw_2988_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Svante%20Arrhenius
|
Svante Arrhenius
|
Svante Arrhenius (19 Februari 1859 – 2 Oktoba 1927) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Sweden. Baadhi ya utafiti mwingine alichunguza uchanganuaji dutu kwa nguvu za umeme (elektrolisisi). Mwaka wa 1903 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2990_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William%20Ramsay
|
William Ramsay
|
William Ramsay (2 Oktoba 1852 – 23 Julai 1916) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Uingereza. Hasa alivumbua na kuchunguza elementi za gesi, yaani neoni, agoni, kriptoni na xenoni. Mwaka wa 1904 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2991_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Adolf%20von%20Baeyer
|
Adolf von Baeyer
|
Adolf von Baeyer (31 Oktoba 1835 – 20 Agosti 1917) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Ujerumani. Mwaka wa 1880 alifaulu kusanisi nili na kuendelea kuichunguza. Mwaka wa 1905 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.
|
20231101.sw_2993_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nili
|
Nili
|
Nili ni rangi ya buluu iliyoiva yaani kati ya buluu na zambarau. Katika lugha za magharibi huitwa "indigo" kwa sababu asili yake iko Uhindi.
|
20231101.sw_2993_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nili
|
Nili
|
Hutumika hasa kwa kutia rangi nguo. Inatoka kwa mimea fulani kiasili hasa kwenye mnili (Indigofera tinctoria). Siku hizi, rangi ya nili hutengenezwa mara nyingi kwa usanisi.
|
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.