_id
stringlengths 15
22
| url
stringlengths 31
150
| title
stringlengths 1
86
| text
stringlengths 100
23.8k
|
---|---|---|---|
20231101.sw_3189_20
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Mwaka 1990 Apartheid ilikwisha na serikali ya National Party ilipaswa kuendesha uchaguzi huru kwa wananchi wote na kukabidhi madaraka kwa serikali ya ANC chini ya Nelson Mandela.
|
20231101.sw_3189_21
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Afrika Kusini ni shirikisho. Katiba mpya ya mwaka 1997 iliendeleza muundo huu uliundwa kama "Umoja wa Afrika Kusini" baada ya vita ya makaburu dhidi Uingereza.
|
20231101.sw_3189_22
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Afrika Kusini ya kale ilikuwa na majimbo manne: Rasi, Natal, Dola Huru la Mto Orange na Transvaal. Maeneno makubwa yaliyokaliwa na Waafrika yalibaki nje katika katiba ya Apartheid yakiitwa bantustans (au: homeland). Katiba mpya ilichora mipaka upya.
|
20231101.sw_3189_23
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Afrika Kusini ina mchanganyiko mkubwa wa watu. Waafrika asili ni asilimia 80.7, Machotara ni 8.8%, Wazungu ni 7.9%, Waasia ni 2.6%.
|
20231101.sw_3189_24
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Lugha mama zinazotunika zaidi ni: Kizulu (22.7%), Kixhosa (16%), Kiafrikaans (13.5) na Kiingereza (9.6%), lakini hiyo ya mwisho ndiyo inayotumika zaidi kati ya makabila mbalimbali na karibu nusu ya wananchi wanajua kuiongea.
|
20231101.sw_3189_25
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Wengi (78.8%) ni Wakristo wa madhehebu mengi sana, hasa ya Uprotestanti; Wakatoliki ni 6.8%. Dini nyingine ni: Dini za jadi (4.4%), Uislamu (1.6%), Uhindu (1%) na Uyahudi (0.1%). Asilimia 12.3 ya watu hawana dini yoyote.
|
20231101.sw_3189_26
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Afrika Kusini inaongoza duniani kwa wingi wa watu wenye VVU/UKIMWI: mwaka 2015 walikuwa milioni 7. Mwaka 2018 silimia 20.4 za watu wenye umri wa miaka 15-49 walikuwa na virusi hivyo. Mayatima kutokana na ugonjwa huo ni 1,200,000.
|
20231101.sw_3189_27
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Sehemu ya uchumi ina hali ya kimaendeleo kabisa ikiwa na viwanda na huduma zinazolingana na hali ya juu kabisa duniani; hali ya maisha ya wananchi waliomo katika sekta hii inalingana na nchi kama Australia au Ulaya magharibi.
|
20231101.sw_3189_28
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Kwa upande mwingine hali ya maisha ya sehemu kubwa ya wananchi ni umaskini kama katika sehemu nyingine za Afrika au Uhindi wa mashambani. Lakini kwa ujumla hali ya maisha iko juu kuliko nchi nyingi za Afrika.
|
20231101.sw_3189_29
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Sekta muhimu za uchumi ni migodi ya kuchimba dhahabu au almasi, viwanda na huduma kama benki au bima.
|
20231101.sw_3189_30
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Jeshi la Afrika Kusini ina silaha za kisasa kushinda nchi zote za majirani. Uchumi unawezesha nchi kutumia kiasi kikubwa kwa ajili ya jeshi kuliko nchi zote za Afrika kusini kwa Sahara.
|
20231101.sw_3189_31
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
A History of South Africa, Third Edition. Leonard Thompson. Yale University Press. 1 March 2001. 384 pages. ISBN 0-300-08776-4.
|
20231101.sw_3189_32
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Economic Analysis and Policy Formulation for Post-Apartheid South Africa: Mission Report, Aug. 1991. International Development Research Centre. IDRC Canada, 1991. vi, 46 p. Without ISBN
|
20231101.sw_3189_33
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Emerging Johannesburg: Perspectives on the Postapartheid City. Richard Tomlinson, et al. 1 January 2003. 336 pages. ISBN 0-415-93559-8.
|
20231101.sw_3189_34
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Making of Modern South Africa: Conquest, Segregation and Apartheid. Nigel Worden. 1 July 2000. 194 pages. ISBN 0-631-21661-8.
|
20231101.sw_3189_35
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
South Africa: A Narrative History. Frank Welsh. Kodansha America. 1 February 1999. 606 pages. ISBN 1-56836-258-7.
|
20231101.sw_3189_36
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
South Africa in Contemporary Times. Godfrey Mwakikagile. New Africa Press. February 2008. 260 pages. ISBN 978-0-9802587-3-8.
|
20231101.sw_3189_37
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
The Atlas of Changing South Africa. A. J. Christopher. 1 October 2000. 216 pages. ISBN 0-415-21178-6.
|
20231101.sw_3189_38
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
The Politics of the New South Africa. Heather Deegan. 28 December 2000. 256 pages. ISBN 0-582-38227-0.
|
20231101.sw_3189_39
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
|
Afrika Kusini
|
Twentieth-Century South Africa. William Beinart. Oxford University Press 2001, 414 pages, ISBN 0-19-289318-1
|
20231101.sw_3191_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
|
Eswatini
|
Eswatini (jina rasmi tangu mwaka 2018 ni Umbuso weSwatini; kifupi cha Kiswati: eSwatini; kwa Kiswahili pia: Uswazi; kwa Kiingereza: Eswatini) ni nchi ndogo ya Kusini mwa Afrika isiyo na pwani katika bahari yoyote.
|
20231101.sw_3191_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
|
Eswatini
|
Waswati walianzisha ufalme wao katikati ya karne ya 18 chini ya Ngwane III; mipaka ya sasa ilikubalika mwaka 1881.
|
20231101.sw_3191_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
|
Eswatini
|
Baada ya vita kati ya Waingereza na Makaburu, Swaziland ilukuwa nchi lindwa ya Uingereza tangu mwaka 1903 hadi 1967.
|
20231101.sw_3191_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
|
Eswatini
|
Chini ya mfalme Sobhuza II aliyetawala kwa muda mrefu sana (1921-1982), Swaziland ilipata uhuru tarehe 6 Septemba 1968.
|
20231101.sw_3191_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
|
Eswatini
|
Eswatini inatawaliwa tangu mwaka 1986 na mfalme Mswati III. Mfalme anapingwa mara nyingi kwa sababu anatumia pesa nyingi kwa ajili yake binafsi ilhali wananchi ni maskini sana. Kwa muda mwingi wa uhuru wa nchi katiba imesimamishwa, na mfalme ametawala peke yake.
|
20231101.sw_3191_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
|
Eswatini
|
Wakazi wengi ni wa kabila la Waswati na kuongea lugha ya Kiswati ambacho ni lugha rasmi pamoja na Kiingereza. Shuleni kinafundishwa pia Kireno.
|
20231101.sw_3191_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
|
Eswatini
|
Upande wa dini, 89.3% ni Wakristo wa madhehebu mbalimbali, hasa Waprotestanti, lakini pia Wakatoliki (5%). Wanaoendelea kufuata dini asilia za Kiafrika ni 0.5% na Waislamu ni 1%.
|
20231101.sw_3191_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
|
Eswatini
|
Eswatini ni kati ya nchi duniani zilizoathiriwa zaidi na Ukimwi; umri wa wastani unafikia miaka 22 pekee kwa sababu ya vifo vingi (64%) vinavyotokana na ugonjwa huo uliopata 26% ya watu wazima wote.
|
20231101.sw_3191_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
|
Eswatini
|
The Kingdom of Eswatini – a royal experience, official Eswatini tourism website (richly illustrated, english)
|
20231101.sw_3191_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
|
Eswatini
|
Eswatini National Trust Commission – Conserving Eswatini's Natural and Cultural Heritage, (very extensive descriptions of history, culture and nature, English)
|
20231101.sw_3192_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mto%20Vaal
|
Mto Vaal
|
Inaelekea kusini-magharibi hadi kuungana na mto Oranje karibu na mji wa Kimberley mkoani Northern Cape.
|
20231101.sw_3192_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mto%20Vaal
|
Mto Vaal
|
Jina la mto limetoka katika lugha ya Kiholanzi; walowezi wa kwanza Waholanzi walitaka kukumbuka mto Waal wa nyumbani kwao.
|
20231101.sw_3192_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mto%20Vaal
|
Mto Vaal
|
Katika historia ya Afrika Kusini mto Vaal ulikuwa mpaka kati ya koloni la Uingereza kusini kwa mto na jamhuri za Makaburu kaskazini kwa mto. Jina la kihistoria "Transvaal" limemaanisha "ng'ambo ya mto Vaal".
|
20231101.sw_3193_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
|
Cote d'Ivoire
|
Côte d'Ivoire (tamka: kot divwar; kwa Kifaransa jina lina maana ya Pwani ya pembe za ndovu; kwa Kiingereza: Ivory Coast; kwa Kiswahili pia: Kodivaa) ni nchi ya Afrika ya Magharibi.
|
20231101.sw_3193_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
|
Cote d'Ivoire
|
Imepakana na Liberia na Guinea upande wa magharibi, Mali na Burkina Faso kaskazini, Ghana mashariki na Ghuba ya Guinea ya Atlantiki upande wa kusini.
|
20231101.sw_3193_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
|
Cote d'Ivoire
|
Baada ya uhuru (7 Agosti 1960) iliwahi kuwa kati ya nchi tajiri zaidi za Afrika lakini tangu mwaka 2002 uchumi na hali ya maisha kwa jumla vimeharibika kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe (2002-2011).
|
20231101.sw_3193_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
|
Cote d'Ivoire
|
Wakazi walikadiriwa kuwa 23,919,000 mwaka 2014, lakini sensa ya mwaka huohuo ilihesabu idadi ndogo zaidi: 22,671,331.
|
20231101.sw_3193_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
|
Cote d'Ivoire
|
Kabila kubwa ni lile la Waakan (42.1%). Asilimia 24.2 ni wahamiaji, hasa kutoka nchi jirani (Liberia, Burkina Faso na Guinea). Asilimia 4 wana asili tofauti, hasa Ufaransa, Lebanoni, Vietnam na Hispania.
|
20231101.sw_3193_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
|
Cote d'Ivoire
|
Upande wa dini, Uislamu una 42.9%, Ukristo 33.9% (Kanisa Katoliki peke yake 17.2%), dini asilia za Kiafrika 3.6% na dini nyingine 0.5%. Wasio na dini ni 19.1%
|
20231101.sw_3194_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abidjan
|
Abidjan
|
Abidjan ndio mji mkubwa zaidi nchini Cote d'Ivoire pia ni bandari kuu ya nchi kwenye Ghuba ya Guinea ya bahari ya Atlantiki. Abidjan haiko baharini moja kwa moja lakini kwenye wangwa ya Ebrie inayotengwa na bahari kwa kanda nyembamba ya mchanga.
|
20231101.sw_3194_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abidjan
|
Abidjan
|
Ilikuwa pia mji mkuu rasmi tangu mwaka 1934 hadi 1983. Kwa sasa imetambulika rasmi kama mji mkuu kiuchumi na bado ofisi nyingi za serikali na balozi za nchi nyingine ziko Abidjan.
|
20231101.sw_3194_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abidjan
|
Abidjan
|
Abidjan ilikuwa kijiji tu hadi mwaka 1904. Wakati ule iliteuliwa kuwa mwanzo wa reli ya kuelekea bara. Reli ilianzishwa huko kwa sababu ng'ambo ya wangwa ilikuwepo bandari ndogo ya Port-Bouët. Tangu reli kujengwa Abidjan ilikua haraka. Mwaka 1934 ilitangazwa kuwa mji mkuu wa koloni la Ufaransa la Cote d'Ivoire.
|
20231101.sw_3194_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abidjan
|
Abidjan
|
Mwaka 1950 mfereji wa Vridi ulikata kanda la mchanga na kufungua wangwa kwa meli kutoka bahari; wangwa ikawa bandari kubwa yenye usalama mzuri kwa meli, na Abidjan ikawa mji wa bandari iliyosababisha kukua kwa uchumi na kuongezeka kwa watu.
|
20231101.sw_3194_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abidjan
|
Abidjan
|
Wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka 2002-2007, na hasa 2010-2011 hali ya usalama mjini ilipungua sana.
|
20231101.sw_3201_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
|
Sierra Leone
|
Nchi yenyewe ilianzishwa na Waingereza kwa kuunda mji wa Freetown ("Mji wa watu huru") mwaka 1787. Kusudi lake likuwa kuwarudisha Afrika watu waliowahi kuwa watumwa. Kiasili wale wakazi wa kwanza walikuwa watumwa weusi waliopewa uhuru kwa sababu walishikamana na Waingereza dhidi ya Wamarekani katika vita vya uhuru wa Marekani.
|
20231101.sw_3201_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
|
Sierra Leone
|
Tangu mwaka 1807 Uingereza ulikataza biashara ya watumwa (lakini utumwa wenyewe bado) na watumwa waliopatikana kwenye meli za biashara hiyo haramu walipelekwa Sierra Leone na kupewa uhuru.
|
20231101.sw_3201_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
|
Sierra Leone
|
Ikianzishwa na shirika la wapinzani wa utumwa Sierra Leone ikajwa koloni la kwanza la Uingereza katika Afrika ya Magharibi mwaka 1792. Kuanzia mwaka 1802 Freetown ilikuwa makao makuu ya Kiingereza kwa Afrika ya Magharibi.
|
20231101.sw_3201_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
|
Sierra Leone
|
Miaka 1994 - 2002 nchi ilikuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Tangu mwisho wake nchi inajengwa tena.
|
20231101.sw_3201_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
|
Sierra Leone
|
Wakazi asili wamegawanyika katika makabila 16, kila moja likiwa na lugha na utamaduni maalumu; kati yake makubwa zaidi ni Watemmne (35.5%) na Watembe (33.2%).
|
20231101.sw_3201_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
|
Sierra Leone
|
Lugha inayojulikana na asilimia 96 za wakazi ni Kikrio, aina ya Krioli ya Kiingereza iliyochanganya pia lugha mbalibali za Kiafrika. Lakini lugha rasmi ni Kiingereza.
|
20231101.sw_3201_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
|
Sierra Leone
|
Upande wa dini, Waislamu ni 78.5%, Wakristo ni 20.4% na wafuasi wa dini asilia za Kiafrika hawafikii 2%. Sierra Leone ni nchi isiyo na dini rasmi.
|
20231101.sw_3201_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
|
Sierra Leone
|
Acemoglu, Daron, Tristan Reed, and James A. Robinson. "Chiefs: Economic Development and Elite Control of Civil Society in Sierra Leone," Journal of Political Economy (2014) 122#2 pp. 319–368 in JSTOR
|
20231101.sw_3201_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
|
Sierra Leone
|
Imodale Caulker-Burnett, The Caulkers of Sierra Leone: The Story of a Ruling Family and Their Times (Xlibris, 2010)
|
20231101.sw_3201_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
|
Sierra Leone
|
Harris, David. Civil War and Democracy in West Africa: Conflict Resolution, Elections and Justice in Sierra Leone and Liberia, I.B. Tauris, 2012
|
20231101.sw_3202_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Freetown
|
Freetown
|
Freetown ni mji mkuu pamoja na badari kubwa na kitovu cha uchumi wa nchi Sierra Leone. Iko kwenye kando la Atlantiki kwenye rasi ya Freetown. Idadi ya wakazi ni 1,070,000.
|
20231101.sw_3202_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Freetown
|
Freetown
|
Mji uliundwa 1787 kwa ajili ya watumwa wenye asili ya Afrika waliowekwa huru. Hapo ni asili ya jina "Freetown" linalomaanisha "Mji wa watu huru".
|
20231101.sw_3202_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Freetown
|
Freetown
|
Hadi leo Makreoli ambao ni watoto wa watumwa waliopewa uhuru kama walowezi ni tabaka la pekee Freetown wakionekana kwa utamaduni na lugha ya pekee.
|
20231101.sw_3202_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Freetown
|
Freetown
|
Uchumi wa Freetown unategemea hasa bandari. Kuna pia viwanda vya sigara, vya kutengeneza petroli, vya chakula na za kusafisha almasi.
|
20231101.sw_3204_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Imepakana na Mauritania upande wa kaskazini, Mali upande wa mashariki, Guinea na Guinea-Bisau kusini na Bahari Atlantiki upande wa magharibi.
|
20231101.sw_3204_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Uso wa nchi ni hasa tambarare zinazopanda juu polepole kuelekea kusini mashariki. Sehemu nyingine zinafikia mita 580 juu ya UB. Kusini kabisa iko kasoko kubwa la Velingara.
|
20231101.sw_3204_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Miji mikubwa ni Dakar (wakazi 2 476 400), Pikine (wakazi 874 062), Thiès (wakazi 252 320), Saint-Louis (wakazi 176 000), Kaolack (wakazi 172 305), Ziguinchor (wakazi 159,788), Tiebo (wakazi 100 289). Karibu nusu ya watu huishi mijini.
|
20231101.sw_3204_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Kwa wakati na kiasi tofauti eneo la Senegal lilikuwa sehemu ya Dola la Ghana, ya Dola la Mali na hatimaye ya Dola la Songhai
|
20231101.sw_3204_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Kuna wakazi milioni 13.5 na idadi kubwa ni wa chini ya umri wa miaka 20. Wameongezeka sana, mnamo mwaka 1985 idadi ilikuwa milioni 5 tu.
|
20231101.sw_3204_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Kikundi kikubwa nchini ni Wawolof (43%), wengine ni Wafula wakiwa pamoja na Watukulur (24%), halafu Waserer (14.7%), Wadiola (4%),Wamandinka (3%), Wasoninke.
|
20231101.sw_3204_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Kwa ujumla kuna lugha 37 nchini Senegal. Kiwolofu kinazidi kuenea, lakini mpaka sasa lugha rasmi ni Kifaransa. Shuleni kinatumika pia Kireno, hasa kusini.
|
20231101.sw_3204_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Senegal ni nchi isiyo na dini rasmi. Wakazi wengi sana (94%) ni Waislamu (hasa Wasunni); Wakristo (hasa Wakatoliki) ni takriban 5%.
|
20231101.sw_3204_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Babou, Cheikh Anta, Fighting the Greater Jihad: Amadu Bamba and the Founding of the Muridiyya of Senegal, 1853–1913, (Ohio University Press, 2007)
|
20231101.sw_3204_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Buggenhage, Beth A, Muslim Families in Global Senegal: Money Takes Care of Shame, (Indiana University Press, 2012)
|
20231101.sw_3204_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Bugul, Ken, The Abandoned Baobab: The Autobiography of a Senegalese Woman, (University of Virginia Press, 2008)
|
20231101.sw_3204_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Foley, Ellen E, Your Pocket is What Cures You: The Politics of Health in Senegal, (Rutgers University Press, 2010)
|
20231101.sw_3204_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Gellar, Sheldon, Democracy in Senegal: Tocquevillian Analytics in Africa, (Palgrave Macmillan, 2005)
|
20231101.sw_3204_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Glover, John, Sufism and Jihad in Modern Senegal: The Murid Order, (University of Rochester Press, 2007)
|
20231101.sw_3204_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
|
Senegal
|
Various, New Perspectives on Islam in Senegal: Conversion, Migration, Wealth, Power, and Femininity, (Palgrave Macmillan, 2009)
|
20231101.sw_3212_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Brazzaville
|
Brazzaville
|
Brazzaville ni mji mkuu wa Jamhuri ya Kongo. Una wakazi 2,308,000 (mwaka 2019) ambao ni sawa na 40% ya wananchi wote.
|
20231101.sw_3212_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Brazzaville
|
Brazzaville
|
Jina la Brazzaville limetokana na Mfaransa Pierre Savorgnan de Brazza aliyenunua hapa ardhi kutoka kwa chifu Makoko na kujenga kituo kilichokua na kuwa mji baadaye.
|
20231101.sw_3212_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Brazzaville
|
Brazzaville
|
Tangu mwaka 1898 Brazzaville ulikuwa mji mkuu wa Kongo ya Kifaransa ukawa na wakazi 5,000 mnamo 1900 walioongezeka kuwa lakhi moja mwaka 1950.
|
20231101.sw_3212_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Brazzaville
|
Brazzaville
|
Mwaka 1940 Brazzaville ulikuwa kwa muda mfupi mji mkuu wa Ufaransa Huru yaani Ufaransa usio chini ya Ujerumani hadi kuhamia kwa serikali hiyo kwenda Algiers.
|
20231101.sw_3213_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Kinshasa (jina la awali kwa Kifaransa: Léopoldville, na kwa Kiholanzi: Leopoldstad) ni mji mkuu na mji mkubwa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, iliyojulikana kama Zaire miaka 1971-1997. Mji uko kwenye Mto Kongo .
|
20231101.sw_3213_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Zamani pahali pa vijiji vya uvuvi, Kinshasa sasa ni jiji lenye idadi ya wakazi 10,076,099 mwaka 2009. Mji wa Brazzaville (wenye wakazi milioni 1.5 mwaka 2007 pamoja na makazi yake), mji mkuu wa Jamhuri ya Kongo, hupatikana upande wa pili wa mto Kongo. Hivyo mrundiko wa Kinshasa-Brazzaville una wakazi karibu milioni 12.
|
20231101.sw_3213_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Kwa sababu mipaka ya kiutawala huzunguka eneo kubwa, zaidi ya 60% ya ardhi ya mji iko katika asili ya mashambani, na eneo la mji hutwaa sehemu ndogo magharibi mwa jimbo.
|
20231101.sw_3213_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Kinshasa imesawazishwa na Johannesburg kwa kuwa mji mkubwa wa pili katika Afrika kusini kwa Sahara na wa tatu kwa ukubwa katika bara zima baada ya Lagos na Cairo.
|
20231101.sw_3213_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Mara nyingi huchukuliwa kuwa mji wa pili mkubwa zaidi duniani kwa idadi ya wazungumzaji wa Kifaransa baada ya Paris. Kama idadi ya watu itaendelea kukua kama sasa, Kinshasa itakuwa na wakazi wengi kuliko Paris kabla ya mwaka 2020.
|
20231101.sw_3213_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Mji ulianzishwa na Henry Morton Stanley mwaka 1881 kama pahali pa biashara ukaitwa Léopoldville kwa heshima ya Mfalme Leopold II wa Ubelgiji, ambaye alidhibiti eneo zima la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kama mali yake binafsi.
|
20231101.sw_3213_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Pahali hapa palinawiri kama bandari ya kwanza juu ya mto Kongo juu ya Livingstone Falls, mfululizo wa maji kusini mwa Leopoldville. Awali, bidhaa zote zilizowasili kwa njia ya bahari zilibebwa na wapagazi kati ya Léopoldville na Matadi, bandari chini ya maji ya kasi na kutoka pwani.
|
20231101.sw_3213_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Kukamilika kwa bandari la reli la Matadi-Kinshasa mwaka 1898 kulitoa ufanisi zaidi katika njia ya kuzunguka maji ya kasi na pia kulisababisha maendeleo ya Léopoldville.
|
20231101.sw_3213_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Kufikia mwaka 1920, mji ulikuwa umeinuliwa kuwa mji mkuu wa Kongo ya Kibelgiji, kuondoa mji wa Boma katika mto Kongo.
|
20231101.sw_3213_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Mwaka 1965 Mobutu Sese Seko alipata kuwa rais wa Kongo katika mapinduzi yake ya pili akaanzisha sera ya kubadilisha majina ya watu na maeneo nchini kuwa ya Kiafrika. Mwaka wa 1966, Léopoldville ukabadilishIwa jina ukawa Kinshasa kufuatia jina la kijiji lililokuwa karibu na eneo hilo.
|
20231101.sw_3213_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Mji ulikua haraka chini ya Mobutu, ukivuta watu kutoka nchini kote ambao walikuja kutafuta bahati yao au kuepuka ugomvi wa kikabila mahali pengine. Hii ilileta mabadiliko mengi katika utungaji wa kabila na lugha za mji. Ingawa ipo katikka eneo la watu wa Bateke na Bahumbu, lingua franca katika Kinshasa leo ni Kilingala.
|
20231101.sw_3213_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Mwaka 1974, Kinshasa ilikuwa na 'Rumble in the Jungle' mechi ya dondi kati ya Muhammad Ali na George Foreman, ambapo Ali alimshinda Foreman na kuchukua cheo cha bingwa duniani.
|
20231101.sw_3213_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Kinshasa iliteseka sana kutokana na uroho wa Mobutu, ufisadi wa hali ya juu, na vita vya wenyewe kwa wenyewe: ndivyo vilivyosababisha kuanguka kwake. Hata hivyo, bado ni eneo kubwa la kiutamaduni na kitaaluma katika Afrika ya Kati, na jumuiya inayonawiri wanamuziki na wasanii.
|
20231101.sw_3213_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Pia ni jiji kubwa lenye viwanda, usindikaji wengi wa bidhaa za asili kuletwa kutoka ndani. Mji hivi majuzi umekuwa ukifukuza maandamano ya askari waliokuwa wakipinga serikali kwa kutoweza kuwalipa.
|
20231101.sw_3213_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Kinshasa ina kumbukumbu ya tukio la kwanza la HIV-1, lililogunduliwa mwaka 1959 katika sampuli ya damu iliyohifadhiwa ya mwanadamu (angalia UKIMWI asili).
|
20231101.sw_3213_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Kinshasa ni mji (Ville kwa Kifaransa) na mkoa (province kwa Kifaransa), moja ya mikoa 11 ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Sasa hivi imesawazishwa na Paris ambayo ni mji na mmoja wa wilaya 100 Ufaransa.
|
20231101.sw_3213_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Mji-mkoa (Ville-province) wa Kinshasa umegawanywa katika wilaya 4 ambazo zimegawanya zaidi katika majimbo 24 (jamii)
|
20231101.sw_3213_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Kiini cha biashara na utawala cha Kinshasa ni jimbo ya La Gombe. Jimbo la Kinshasa lilitoa jina lake kwa mji mzima, lakini si kiini cha biashara wala utawala wa jiji.
|
20231101.sw_3213_18
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Kinshasa ni mji wa makazi tofauti sana, kuna maeneo ya fahari ya wakazi na biashara na vyuo vikuu vitatu pamoja na makazi duni.
|
20231101.sw_3213_19
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Iko kusini mwa mto Kongo, kando ya Brazzaville, mji mkuu wa Jamhuri ya Kongo. Hapa ndipo mahali pekee duniani ambapo miji mikuu imelainika kando ya mto, ikitazamana.
|
20231101.sw_3213_20
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Mto Kongo ni mto mrefu wa pili katika Afrika baada ya Nile, na ni mkubwa zaidi katika suala la kutoa maji. Kama njia ya maji, hutumiwa kusafiri kwa kiasi katika bonde la Kongo, na unaweza kusafiri kati ya mito ya Kinshasa na Kisangani, na matawi yake mengi yanaweza kusafiriwa. Mto ni chanzo muhimu cha umememaji, na kusini mwa Kinshasa unaweza kuzalisha nguvu za kutosheleza matumizi kwa bara zima.
|
20231101.sw_3213_21
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Chini ya hali ya hewa ya Koppen, Kinshasa ina hali ya hewa ya kitropiki ya Savanna. Huwa na msimu wa mvua ambao huanzia Oktoba kupitia Mei na kiangazi kifupi ambacho huanza Juni hadi Septemba. Kutokana na ukweli kuwa Kinshasa hupatikana kusini mwa ikweta, kiangazi chake huanza katika msimu wake wa "baridi", ambayo ni katika Juni. Hii ni tofauti na miji ya Afrika kaskazini zaidi ambapo hali ya hewa ya kiangazi kawaida huanza mwezi Januari. Msimu wa kiangazi wa Kinshasa una baridi kuliko msimu wake wa mvua, ingawa hali ya joto hubaki sawa mwaka mzima.
|
20231101.sw_3213_22
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
|
Kinshasa
|
Kinshasa ilipewa jina "Kin la Belle" (Kinshasa yenye urembo), lakini tangu kuanguka kwa huduma za umma na kuacha baadhi ya wakazi wake walibadili jina likawa "Kin la Poubelle" (Kinshasa takataka).
|
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.