_id
stringlengths
15
22
url
stringlengths
31
150
title
stringlengths
1
86
text
stringlengths
100
23.8k
20231101.sw_3189_20
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Mwaka 1990 Apartheid ilikwisha na serikali ya National Party ilipaswa kuendesha uchaguzi huru kwa wananchi wote na kukabidhi madaraka kwa serikali ya ANC chini ya Nelson Mandela.
20231101.sw_3189_21
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Afrika Kusini ni shirikisho. Katiba mpya ya mwaka 1997 iliendeleza muundo huu uliundwa kama "Umoja wa Afrika Kusini" baada ya vita ya makaburu dhidi Uingereza.
20231101.sw_3189_22
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Afrika Kusini ya kale ilikuwa na majimbo manne: Rasi, Natal, Dola Huru la Mto Orange na Transvaal. Maeneno makubwa yaliyokaliwa na Waafrika yalibaki nje katika katiba ya Apartheid yakiitwa bantustans (au: homeland). Katiba mpya ilichora mipaka upya.
20231101.sw_3189_23
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Afrika Kusini ina mchanganyiko mkubwa wa watu. Waafrika asili ni asilimia 80.7, Machotara ni 8.8%, Wazungu ni 7.9%, Waasia ni 2.6%.
20231101.sw_3189_24
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Lugha mama zinazotunika zaidi ni: Kizulu (22.7%), Kixhosa (16%), Kiafrikaans (13.5) na Kiingereza (9.6%), lakini hiyo ya mwisho ndiyo inayotumika zaidi kati ya makabila mbalimbali na karibu nusu ya wananchi wanajua kuiongea.
20231101.sw_3189_25
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Wengi (78.8%) ni Wakristo wa madhehebu mengi sana, hasa ya Uprotestanti; Wakatoliki ni 6.8%. Dini nyingine ni: Dini za jadi (4.4%), Uislamu (1.6%), Uhindu (1%) na Uyahudi (0.1%). Asilimia 12.3 ya watu hawana dini yoyote.
20231101.sw_3189_26
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Afrika Kusini inaongoza duniani kwa wingi wa watu wenye VVU/UKIMWI: mwaka 2015 walikuwa milioni 7. Mwaka 2018 silimia 20.4 za watu wenye umri wa miaka 15-49 walikuwa na virusi hivyo. Mayatima kutokana na ugonjwa huo ni 1,200,000.
20231101.sw_3189_27
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Sehemu ya uchumi ina hali ya kimaendeleo kabisa ikiwa na viwanda na huduma zinazolingana na hali ya juu kabisa duniani; hali ya maisha ya wananchi waliomo katika sekta hii inalingana na nchi kama Australia au Ulaya magharibi.
20231101.sw_3189_28
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Kwa upande mwingine hali ya maisha ya sehemu kubwa ya wananchi ni umaskini kama katika sehemu nyingine za Afrika au Uhindi wa mashambani. Lakini kwa ujumla hali ya maisha iko juu kuliko nchi nyingi za Afrika.
20231101.sw_3189_29
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Sekta muhimu za uchumi ni migodi ya kuchimba dhahabu au almasi, viwanda na huduma kama benki au bima.
20231101.sw_3189_30
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Jeshi la Afrika Kusini ina silaha za kisasa kushinda nchi zote za majirani. Uchumi unawezesha nchi kutumia kiasi kikubwa kwa ajili ya jeshi kuliko nchi zote za Afrika kusini kwa Sahara.
20231101.sw_3189_31
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
A History of South Africa, Third Edition. Leonard Thompson. Yale University Press. 1 March 2001. 384 pages. ISBN 0-300-08776-4.
20231101.sw_3189_32
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Economic Analysis and Policy Formulation for Post-Apartheid South Africa: Mission Report, Aug. 1991. International Development Research Centre. IDRC Canada, 1991. vi, 46 p. Without ISBN
20231101.sw_3189_33
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Emerging Johannesburg: Perspectives on the Postapartheid City. Richard Tomlinson, et al. 1 January 2003. 336 pages. ISBN 0-415-93559-8.
20231101.sw_3189_34
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Making of Modern South Africa: Conquest, Segregation and Apartheid. Nigel Worden. 1 July 2000. 194 pages. ISBN 0-631-21661-8.
20231101.sw_3189_35
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
South Africa: A Narrative History. Frank Welsh. Kodansha America. 1 February 1999. 606 pages. ISBN 1-56836-258-7.
20231101.sw_3189_36
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
South Africa in Contemporary Times. Godfrey Mwakikagile. New Africa Press. February 2008. 260 pages. ISBN 978-0-9802587-3-8.
20231101.sw_3189_37
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
The Atlas of Changing South Africa. A. J. Christopher. 1 October 2000. 216 pages. ISBN 0-415-21178-6.
20231101.sw_3189_38
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
The Politics of the New South Africa. Heather Deegan. 28 December 2000. 256 pages. ISBN 0-582-38227-0.
20231101.sw_3189_39
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20Kusini
Afrika Kusini
Twentieth-Century South Africa. William Beinart. Oxford University Press 2001, 414 pages, ISBN 0-19-289318-1
20231101.sw_3191_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
Eswatini
Eswatini (jina rasmi tangu mwaka 2018 ni Umbuso weSwatini; kifupi cha Kiswati: eSwatini; kwa Kiswahili pia: Uswazi; kwa Kiingereza: Eswatini) ni nchi ndogo ya Kusini mwa Afrika isiyo na pwani katika bahari yoyote.
20231101.sw_3191_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
Eswatini
Waswati walianzisha ufalme wao katikati ya karne ya 18 chini ya Ngwane III; mipaka ya sasa ilikubalika mwaka 1881.
20231101.sw_3191_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
Eswatini
Baada ya vita kati ya Waingereza na Makaburu, Swaziland ilukuwa nchi lindwa ya Uingereza tangu mwaka 1903 hadi 1967.
20231101.sw_3191_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
Eswatini
Chini ya mfalme Sobhuza II aliyetawala kwa muda mrefu sana (1921-1982), Swaziland ilipata uhuru tarehe 6 Septemba 1968.
20231101.sw_3191_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
Eswatini
Eswatini inatawaliwa tangu mwaka 1986 na mfalme Mswati III. Mfalme anapingwa mara nyingi kwa sababu anatumia pesa nyingi kwa ajili yake binafsi ilhali wananchi ni maskini sana. Kwa muda mwingi wa uhuru wa nchi katiba imesimamishwa, na mfalme ametawala peke yake.
20231101.sw_3191_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
Eswatini
Wakazi wengi ni wa kabila la Waswati na kuongea lugha ya Kiswati ambacho ni lugha rasmi pamoja na Kiingereza. Shuleni kinafundishwa pia Kireno.
20231101.sw_3191_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
Eswatini
Upande wa dini, 89.3% ni Wakristo wa madhehebu mbalimbali, hasa Waprotestanti, lakini pia Wakatoliki (5%). Wanaoendelea kufuata dini asilia za Kiafrika ni 0.5% na Waislamu ni 1%.
20231101.sw_3191_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
Eswatini
Eswatini ni kati ya nchi duniani zilizoathiriwa zaidi na Ukimwi; umri wa wastani unafikia miaka 22 pekee kwa sababu ya vifo vingi (64%) vinavyotokana na ugonjwa huo uliopata 26% ya watu wazima wote.
20231101.sw_3191_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
Eswatini
The Kingdom of Eswatini – a royal experience, official Eswatini tourism website (richly illustrated, english)
20231101.sw_3191_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eswatini
Eswatini
Eswatini National Trust Commission – Conserving Eswatini's Natural and Cultural Heritage, (very extensive descriptions of history, culture and nature, English)
20231101.sw_3192_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mto%20Vaal
Mto Vaal
Inaelekea kusini-magharibi hadi kuungana na mto Oranje karibu na mji wa Kimberley mkoani Northern Cape.
20231101.sw_3192_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mto%20Vaal
Mto Vaal
Jina la mto limetoka katika lugha ya Kiholanzi; walowezi wa kwanza Waholanzi walitaka kukumbuka mto Waal wa nyumbani kwao.
20231101.sw_3192_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mto%20Vaal
Mto Vaal
Katika historia ya Afrika Kusini mto Vaal ulikuwa mpaka kati ya koloni la Uingereza kusini kwa mto na jamhuri za Makaburu kaskazini kwa mto. Jina la kihistoria "Transvaal" limemaanisha "ng'ambo ya mto Vaal".
20231101.sw_3193_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
Cote d'Ivoire
Côte d'Ivoire (tamka: kot divwar; kwa Kifaransa jina lina maana ya Pwani ya pembe za ndovu; kwa Kiingereza: Ivory Coast; kwa Kiswahili pia: Kodivaa) ni nchi ya Afrika ya Magharibi.
20231101.sw_3193_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
Cote d'Ivoire
Imepakana na Liberia na Guinea upande wa magharibi, Mali na Burkina Faso kaskazini, Ghana mashariki na Ghuba ya Guinea ya Atlantiki upande wa kusini.
20231101.sw_3193_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
Cote d'Ivoire
Baada ya uhuru (7 Agosti 1960) iliwahi kuwa kati ya nchi tajiri zaidi za Afrika lakini tangu mwaka 2002 uchumi na hali ya maisha kwa jumla vimeharibika kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe (2002-2011).
20231101.sw_3193_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
Cote d'Ivoire
Wakazi walikadiriwa kuwa 23,919,000 mwaka 2014, lakini sensa ya mwaka huohuo ilihesabu idadi ndogo zaidi: 22,671,331.
20231101.sw_3193_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
Cote d'Ivoire
Kabila kubwa ni lile la Waakan (42.1%). Asilimia 24.2 ni wahamiaji, hasa kutoka nchi jirani (Liberia, Burkina Faso na Guinea). Asilimia 4 wana asili tofauti, hasa Ufaransa, Lebanoni, Vietnam na Hispania.
20231101.sw_3193_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Cote%20d%27Ivoire
Cote d'Ivoire
Upande wa dini, Uislamu una 42.9%, Ukristo 33.9% (Kanisa Katoliki peke yake 17.2%), dini asilia za Kiafrika 3.6% na dini nyingine 0.5%. Wasio na dini ni 19.1%
20231101.sw_3194_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abidjan
Abidjan
Abidjan ndio mji mkubwa zaidi nchini Cote d'Ivoire pia ni bandari kuu ya nchi kwenye Ghuba ya Guinea ya bahari ya Atlantiki. Abidjan haiko baharini moja kwa moja lakini kwenye wangwa ya Ebrie inayotengwa na bahari kwa kanda nyembamba ya mchanga.
20231101.sw_3194_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abidjan
Abidjan
Ilikuwa pia mji mkuu rasmi tangu mwaka 1934 hadi 1983. Kwa sasa imetambulika rasmi kama mji mkuu kiuchumi na bado ofisi nyingi za serikali na balozi za nchi nyingine ziko Abidjan.
20231101.sw_3194_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abidjan
Abidjan
Abidjan ilikuwa kijiji tu hadi mwaka 1904. Wakati ule iliteuliwa kuwa mwanzo wa reli ya kuelekea bara. Reli ilianzishwa huko kwa sababu ng'ambo ya wangwa ilikuwepo bandari ndogo ya Port-Bouët. Tangu reli kujengwa Abidjan ilikua haraka. Mwaka 1934 ilitangazwa kuwa mji mkuu wa koloni la Ufaransa la Cote d'Ivoire.
20231101.sw_3194_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abidjan
Abidjan
Mwaka 1950 mfereji wa Vridi ulikata kanda la mchanga na kufungua wangwa kwa meli kutoka bahari; wangwa ikawa bandari kubwa yenye usalama mzuri kwa meli, na Abidjan ikawa mji wa bandari iliyosababisha kukua kwa uchumi na kuongezeka kwa watu.
20231101.sw_3194_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abidjan
Abidjan
Wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka 2002-2007, na hasa 2010-2011 hali ya usalama mjini ilipungua sana.
20231101.sw_3201_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
Sierra Leone
Nchi yenyewe ilianzishwa na Waingereza kwa kuunda mji wa Freetown ("Mji wa watu huru") mwaka 1787. Kusudi lake likuwa kuwarudisha Afrika watu waliowahi kuwa watumwa. Kiasili wale wakazi wa kwanza walikuwa watumwa weusi waliopewa uhuru kwa sababu walishikamana na Waingereza dhidi ya Wamarekani katika vita vya uhuru wa Marekani.
20231101.sw_3201_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
Sierra Leone
Tangu mwaka 1807 Uingereza ulikataza biashara ya watumwa (lakini utumwa wenyewe bado) na watumwa waliopatikana kwenye meli za biashara hiyo haramu walipelekwa Sierra Leone na kupewa uhuru.
20231101.sw_3201_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
Sierra Leone
Ikianzishwa na shirika la wapinzani wa utumwa Sierra Leone ikajwa koloni la kwanza la Uingereza katika Afrika ya Magharibi mwaka 1792. Kuanzia mwaka 1802 Freetown ilikuwa makao makuu ya Kiingereza kwa Afrika ya Magharibi.
20231101.sw_3201_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
Sierra Leone
Miaka 1994 - 2002 nchi ilikuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Tangu mwisho wake nchi inajengwa tena.
20231101.sw_3201_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
Sierra Leone
Wakazi asili wamegawanyika katika makabila 16, kila moja likiwa na lugha na utamaduni maalumu; kati yake makubwa zaidi ni Watemmne (35.5%) na Watembe (33.2%).
20231101.sw_3201_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
Sierra Leone
Lugha inayojulikana na asilimia 96 za wakazi ni Kikrio, aina ya Krioli ya Kiingereza iliyochanganya pia lugha mbalibali za Kiafrika. Lakini lugha rasmi ni Kiingereza.
20231101.sw_3201_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
Sierra Leone
Upande wa dini, Waislamu ni 78.5%, Wakristo ni 20.4% na wafuasi wa dini asilia za Kiafrika hawafikii 2%. Sierra Leone ni nchi isiyo na dini rasmi.
20231101.sw_3201_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
Sierra Leone
Acemoglu, Daron, Tristan Reed, and James A. Robinson. "Chiefs: Economic Development and Elite Control of Civil Society in Sierra Leone," Journal of Political Economy (2014) 122#2 pp. 319–368 in JSTOR
20231101.sw_3201_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
Sierra Leone
Imodale Caulker-Burnett, The Caulkers of Sierra Leone: The Story of a Ruling Family and Their Times (Xlibris, 2010)
20231101.sw_3201_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sierra%20Leone
Sierra Leone
Harris, David. Civil War and Democracy in West Africa: Conflict Resolution, Elections and Justice in Sierra Leone and Liberia, I.B. Tauris, 2012
20231101.sw_3202_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Freetown
Freetown
Freetown ni mji mkuu pamoja na badari kubwa na kitovu cha uchumi wa nchi Sierra Leone. Iko kwenye kando la Atlantiki kwenye rasi ya Freetown. Idadi ya wakazi ni 1,070,000.
20231101.sw_3202_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Freetown
Freetown
Mji uliundwa 1787 kwa ajili ya watumwa wenye asili ya Afrika waliowekwa huru. Hapo ni asili ya jina "Freetown" linalomaanisha "Mji wa watu huru".
20231101.sw_3202_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Freetown
Freetown
Hadi leo Makreoli ambao ni watoto wa watumwa waliopewa uhuru kama walowezi ni tabaka la pekee Freetown wakionekana kwa utamaduni na lugha ya pekee.
20231101.sw_3202_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Freetown
Freetown
Uchumi wa Freetown unategemea hasa bandari. Kuna pia viwanda vya sigara, vya kutengeneza petroli, vya chakula na za kusafisha almasi.
20231101.sw_3204_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Imepakana na Mauritania upande wa kaskazini, Mali upande wa mashariki, Guinea na Guinea-Bisau kusini na Bahari Atlantiki upande wa magharibi.
20231101.sw_3204_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Uso wa nchi ni hasa tambarare zinazopanda juu polepole kuelekea kusini mashariki. Sehemu nyingine zinafikia mita 580 juu ya UB. Kusini kabisa iko kasoko kubwa la Velingara.
20231101.sw_3204_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Miji mikubwa ni Dakar (wakazi 2 476 400), Pikine (wakazi 874 062), Thiès (wakazi 252 320), Saint-Louis (wakazi 176 000), Kaolack (wakazi 172 305), Ziguinchor (wakazi 159,788), Tiebo (wakazi 100 289). Karibu nusu ya watu huishi mijini.
20231101.sw_3204_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Kwa wakati na kiasi tofauti eneo la Senegal lilikuwa sehemu ya Dola la Ghana, ya Dola la Mali na hatimaye ya Dola la Songhai
20231101.sw_3204_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Kuna wakazi milioni 13.5 na idadi kubwa ni wa chini ya umri wa miaka 20. Wameongezeka sana, mnamo mwaka 1985 idadi ilikuwa milioni 5 tu.
20231101.sw_3204_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Kikundi kikubwa nchini ni Wawolof (43%), wengine ni Wafula wakiwa pamoja na Watukulur (24%), halafu Waserer (14.7%), Wadiola (4%),Wamandinka (3%), Wasoninke.
20231101.sw_3204_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Kwa ujumla kuna lugha 37 nchini Senegal. Kiwolofu kinazidi kuenea, lakini mpaka sasa lugha rasmi ni Kifaransa. Shuleni kinatumika pia Kireno, hasa kusini.
20231101.sw_3204_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Senegal ni nchi isiyo na dini rasmi. Wakazi wengi sana (94%) ni Waislamu (hasa Wasunni); Wakristo (hasa Wakatoliki) ni takriban 5%.
20231101.sw_3204_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Babou, Cheikh Anta, Fighting the Greater Jihad: Amadu Bamba and the Founding of the Muridiyya of Senegal, 1853–1913, (Ohio University Press, 2007)
20231101.sw_3204_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Buggenhage, Beth A, Muslim Families in Global Senegal: Money Takes Care of Shame, (Indiana University Press, 2012)
20231101.sw_3204_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Bugul, Ken, The Abandoned Baobab: The Autobiography of a Senegalese Woman, (University of Virginia Press, 2008)
20231101.sw_3204_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Foley, Ellen E, Your Pocket is What Cures You: The Politics of Health in Senegal, (Rutgers University Press, 2010)
20231101.sw_3204_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Gellar, Sheldon, Democracy in Senegal: Tocquevillian Analytics in Africa, (Palgrave Macmillan, 2005)
20231101.sw_3204_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Glover, John, Sufism and Jihad in Modern Senegal: The Murid Order, (University of Rochester Press, 2007)
20231101.sw_3204_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senegal
Senegal
Various, New Perspectives on Islam in Senegal: Conversion, Migration, Wealth, Power, and Femininity, (Palgrave Macmillan, 2009)
20231101.sw_3212_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Brazzaville
Brazzaville
Brazzaville ni mji mkuu wa Jamhuri ya Kongo. Una wakazi 2,308,000 (mwaka 2019) ambao ni sawa na 40% ya wananchi wote.
20231101.sw_3212_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Brazzaville
Brazzaville
Jina la Brazzaville limetokana na Mfaransa Pierre Savorgnan de Brazza aliyenunua hapa ardhi kutoka kwa chifu Makoko na kujenga kituo kilichokua na kuwa mji baadaye.
20231101.sw_3212_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Brazzaville
Brazzaville
Tangu mwaka 1898 Brazzaville ulikuwa mji mkuu wa Kongo ya Kifaransa ukawa na wakazi 5,000 mnamo 1900 walioongezeka kuwa lakhi moja mwaka 1950.
20231101.sw_3212_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Brazzaville
Brazzaville
Mwaka 1940 Brazzaville ulikuwa kwa muda mfupi mji mkuu wa Ufaransa Huru yaani Ufaransa usio chini ya Ujerumani hadi kuhamia kwa serikali hiyo kwenda Algiers.
20231101.sw_3213_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Kinshasa (jina la awali kwa Kifaransa: Léopoldville, na kwa Kiholanzi: Leopoldstad) ni mji mkuu na mji mkubwa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, iliyojulikana kama Zaire miaka 1971-1997. Mji uko kwenye Mto Kongo .
20231101.sw_3213_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Zamani pahali pa vijiji vya uvuvi, Kinshasa sasa ni jiji lenye idadi ya wakazi 10,076,099 mwaka 2009. Mji wa Brazzaville (wenye wakazi milioni 1.5 mwaka 2007 pamoja na makazi yake), mji mkuu wa Jamhuri ya Kongo, hupatikana upande wa pili wa mto Kongo. Hivyo mrundiko wa Kinshasa-Brazzaville una wakazi karibu milioni 12.
20231101.sw_3213_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Kwa sababu mipaka ya kiutawala huzunguka eneo kubwa, zaidi ya 60% ya ardhi ya mji iko katika asili ya mashambani, na eneo la mji hutwaa sehemu ndogo magharibi mwa jimbo.
20231101.sw_3213_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Kinshasa imesawazishwa na Johannesburg kwa kuwa mji mkubwa wa pili katika Afrika kusini kwa Sahara na wa tatu kwa ukubwa katika bara zima baada ya Lagos na Cairo.
20231101.sw_3213_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Mara nyingi huchukuliwa kuwa mji wa pili mkubwa zaidi duniani kwa idadi ya wazungumzaji wa Kifaransa baada ya Paris. Kama idadi ya watu itaendelea kukua kama sasa, Kinshasa itakuwa na wakazi wengi kuliko Paris kabla ya mwaka 2020.
20231101.sw_3213_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Mji ulianzishwa na Henry Morton Stanley mwaka 1881 kama pahali pa biashara ukaitwa Léopoldville kwa heshima ya Mfalme Leopold II wa Ubelgiji, ambaye alidhibiti eneo zima la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kama mali yake binafsi.
20231101.sw_3213_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Pahali hapa palinawiri kama bandari ya kwanza juu ya mto Kongo juu ya Livingstone Falls, mfululizo wa maji kusini mwa Leopoldville. Awali, bidhaa zote zilizowasili kwa njia ya bahari zilibebwa na wapagazi kati ya Léopoldville na Matadi, bandari chini ya maji ya kasi na kutoka pwani.
20231101.sw_3213_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Kukamilika kwa bandari la reli la Matadi-Kinshasa mwaka 1898 kulitoa ufanisi zaidi katika njia ya kuzunguka maji ya kasi na pia kulisababisha maendeleo ya Léopoldville.
20231101.sw_3213_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Kufikia mwaka 1920, mji ulikuwa umeinuliwa kuwa mji mkuu wa Kongo ya Kibelgiji, kuondoa mji wa Boma katika mto Kongo.
20231101.sw_3213_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Mwaka 1965 Mobutu Sese Seko alipata kuwa rais wa Kongo katika mapinduzi yake ya pili akaanzisha sera ya kubadilisha majina ya watu na maeneo nchini kuwa ya Kiafrika. Mwaka wa 1966, Léopoldville ukabadilishIwa jina ukawa Kinshasa kufuatia jina la kijiji lililokuwa karibu na eneo hilo.
20231101.sw_3213_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Mji ulikua haraka chini ya Mobutu, ukivuta watu kutoka nchini kote ambao walikuja kutafuta bahati yao au kuepuka ugomvi wa kikabila mahali pengine. Hii ilileta mabadiliko mengi katika utungaji wa kabila na lugha za mji. Ingawa ipo katikka eneo la watu wa Bateke na Bahumbu, lingua franca katika Kinshasa leo ni Kilingala.
20231101.sw_3213_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Mwaka 1974, Kinshasa ilikuwa na 'Rumble in the Jungle' mechi ya dondi kati ya Muhammad Ali na George Foreman, ambapo Ali alimshinda Foreman na kuchukua cheo cha bingwa duniani.
20231101.sw_3213_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Kinshasa iliteseka sana kutokana na uroho wa Mobutu, ufisadi wa hali ya juu, na vita vya wenyewe kwa wenyewe: ndivyo vilivyosababisha kuanguka kwake. Hata hivyo, bado ni eneo kubwa la kiutamaduni na kitaaluma katika Afrika ya Kati, na jumuiya inayonawiri wanamuziki na wasanii.
20231101.sw_3213_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Pia ni jiji kubwa lenye viwanda, usindikaji wengi wa bidhaa za asili kuletwa kutoka ndani. Mji hivi majuzi umekuwa ukifukuza maandamano ya askari waliokuwa wakipinga serikali kwa kutoweza kuwalipa.
20231101.sw_3213_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Kinshasa ina kumbukumbu ya tukio la kwanza la HIV-1, lililogunduliwa mwaka 1959 katika sampuli ya damu iliyohifadhiwa ya mwanadamu (angalia UKIMWI asili).
20231101.sw_3213_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Kinshasa ni mji (Ville kwa Kifaransa) na mkoa (province kwa Kifaransa), moja ya mikoa 11 ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Sasa hivi imesawazishwa na Paris ambayo ni mji na mmoja wa wilaya 100 Ufaransa.
20231101.sw_3213_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Mji-mkoa (Ville-province) wa Kinshasa umegawanywa katika wilaya 4 ambazo zimegawanya zaidi katika majimbo 24 (jamii)
20231101.sw_3213_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Kiini cha biashara na utawala cha Kinshasa ni jimbo ya La Gombe. Jimbo la Kinshasa lilitoa jina lake kwa mji mzima, lakini si kiini cha biashara wala utawala wa jiji.
20231101.sw_3213_18
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Kinshasa ni mji wa makazi tofauti sana, kuna maeneo ya fahari ya wakazi na biashara na vyuo vikuu vitatu pamoja na makazi duni.
20231101.sw_3213_19
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Iko kusini mwa mto Kongo, kando ya Brazzaville, mji mkuu wa Jamhuri ya Kongo. Hapa ndipo mahali pekee duniani ambapo miji mikuu imelainika kando ya mto, ikitazamana.
20231101.sw_3213_20
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Mto Kongo ni mto mrefu wa pili katika Afrika baada ya Nile, na ni mkubwa zaidi katika suala la kutoa maji. Kama njia ya maji, hutumiwa kusafiri kwa kiasi katika bonde la Kongo, na unaweza kusafiri kati ya mito ya Kinshasa na Kisangani, na matawi yake mengi yanaweza kusafiriwa. Mto ni chanzo muhimu cha umememaji, na kusini mwa Kinshasa unaweza kuzalisha nguvu za kutosheleza matumizi kwa bara zima.
20231101.sw_3213_21
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Chini ya hali ya hewa ya Koppen, Kinshasa ina hali ya hewa ya kitropiki ya Savanna. Huwa na msimu wa mvua ambao huanzia Oktoba kupitia Mei na kiangazi kifupi ambacho huanza Juni hadi Septemba. Kutokana na ukweli kuwa Kinshasa hupatikana kusini mwa ikweta, kiangazi chake huanza katika msimu wake wa "baridi", ambayo ni katika Juni. Hii ni tofauti na miji ya Afrika kaskazini zaidi ambapo hali ya hewa ya kiangazi kawaida huanza mwezi Januari. Msimu wa kiangazi wa Kinshasa una baridi kuliko msimu wake wa mvua, ingawa hali ya joto hubaki sawa mwaka mzima.
20231101.sw_3213_22
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinshasa
Kinshasa
Kinshasa ilipewa jina "Kin la Belle" (Kinshasa yenye urembo), lakini tangu kuanguka kwa huduma za umma na kuacha baadhi ya wakazi wake walibadili jina likawa "Kin la Poubelle" (Kinshasa takataka).