_id
stringlengths
15
22
url
stringlengths
31
150
title
stringlengths
1
86
text
stringlengths
100
23.8k
20231101.sw_1996_24
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Ingawa huyo akamfunga mapema akamuua, kazi ya Yohane ilikuwa imetimia kwa sababu aliweza kuwaandaa Waisraeli wengi (hasa watu wadogo na wakosefu) wampokee Yesu aliyebatizwa naye. Katika nafasi hiyo Yohane alimtambulisha kama Mwanakondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu.
20231101.sw_1996_25
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Ndipo Yesu naye alipoanza kuhubiri, lakini pia kutenda miujiza ya kila aina, akapata haraka wafuasi wengi. Kati yao akachagua Mitume wake 12 kama msingi mpya wa taifa la Mungu badala ya Israeli ya kale.
20231101.sw_1996_26
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Alifanya kazi hizo kuanzia Galilaya, akitangaza ujio wa ufalme wa Mungu, kwa maana ya kwamba ufalme uliotazamiwa na Wayahudi umewajia kwa njia yake.
20231101.sw_1996_27
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Ingawa hakupitia shule yoyote ya Biblia, Yesu alionekana anafundisha vizuri kuliko walimu wa sheria wa kawaida, kama mtu mwenye mamlaka juu ya Torati.
20231101.sw_1996_28
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Mafundisho yake yalilingana na yale ya Mafarisayo kuliko na yale ya Masadukayo, lakini alishindana pia na hao wa kwanza.
20231101.sw_1996_29
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Kijicho na upinzani vikazidi hasa Yerusalemu, walipoanza kufanya njama za kumuua. Ingawa Yesu alijua hayo, alijikaza kwenda katika huo mji mtakatifu autangazie habari njema na kufia huko.
20231101.sw_1996_30
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Baada ya kupokewa kwa shangwe kabla ya sherehe ya Pasaka ya mwaka 30 (au 33) akakamatwa na baraza la Israeli kwa tuhuma ya kufuru ya kujilinganisha na Mungu, halafu akakabidhiwa kwa liwali wa Kirumi aliyekuwa na mamlaka ya kutoa adhabu ya kifo.
20231101.sw_1996_31
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Baada ya kikao ambapo Wayahudi walitafuta kisingizio cha kisiasa, Ponsyo Pilato akalazimika kuagiza Yesu asulubiwe, na kisha kufa kwake kaburi lilindwe na askari.
20231101.sw_1996_32
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Hata hivyo siku ya tatu kaburi likaonekana tupu, na Yesu akaanza kuwatokea wanafunzi wake wa kike na wa kiume kwa muda wa siku arubaini, halafu akapaa mbinguni mbele ya macho yao.
20231101.sw_1996_33
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Kanisa linaheshimu kwa namna ya pekee, kama ushuhuda mkuu juu ya maisha na mafundisho ya Yesu na kama moyo wa Maandiko matakatifu yote, Injili nne zilizoandikwa na Marko, Mathayo, Mwinjili Luka na Yohane kati ya mwaka 65 na 100 hivi.
20231101.sw_1996_34
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Ni muhimu kujua maisha ya Yesu kwa sababu matendo na maneno yake, pamoja na kimya na sala yake, na hasa kifo na ufufuko wake, yote yanatufunulia Baba na matakwa yake kwetu. “Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote” (Lk 24:19).
20231101.sw_1996_35
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Baada ya kujua maisha ya Yesu tunapaswa kujilinganisha naye hadi aundwe na kuishi ndani mwetu akitushirikisha uhai, kifo na ufufuko wake. “Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu, na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu… Vitoto vyangu, ambao kwamba nawaonea utungu tena mpaka Kristo aumbike ndani yenu!” (Gal 2:20; 4:19).
20231101.sw_1996_36
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.
20231101.sw_1996_37
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako. Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika.
20231101.sw_1996_38
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma,
20231101.sw_1996_39
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Waumini wake wanaunda Kanisa la Kikristo ambalo linapatikana leo katika madhehebu mengi. Karibu wote wanamwamini kuwa Mungu aliyechukua umbile la mwanadamu au, kwa lugha nyingine, kuwa Mwana wa Mungu.
20231101.sw_1996_40
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Kwa imani hiyo, Yesu ni Mungu na mtu kwa pamoja, ndiyo sababu ni mshenga pekee kati ya Mungu na watu. “Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, mwanadamu Kristo Yesu” (1Tim 2:5). “Katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili” (Kol 2:9). Hivyo ni Mungu kweli na mtu kweli.
20231101.sw_1996_41
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Umungu na utu wa Yesu vimeunganika katika nafsi moja visichanganyikane, kwa kuwa ndani yake hali hizo mbili zinatenda kila moja ya kwake. “Basi yule akida, aliyesimama hapo akimwelekea, alipoona ya kuwa alikata roho jinsi hii, akasema, ‘Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu’” (Mk 15:39).
20231101.sw_1996_42
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Mwana wa Mungu tangu atwae mwili ni mtu kamili mwenye akili na utashi wa kibinadamu. Katika umoja wa nafsi yake vipawa hivyo vinatenda kulingana na Umungu anaouchanga na Baba na Roho Mtakatifu milele. “Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake” (Yoh 14:10).
20231101.sw_1996_43
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Hapa duniani Yesu alizaliwa na Bikira Maria kama malaika alivyomuambia: “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo, hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu” (Lk 1:35).
20231101.sw_1996_44
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Katika dini ya Uislamu, Yesu anajulikana kama Nabii Isa. Waislamu wanaamini kuwa yeye alikuwa nabii wa Mungu ila hakuwa mwana wa Mungu wala Mungu.
20231101.sw_1996_45
https://sw.wikipedia.org/wiki/Yesu
Yesu
Maisha yake yamekuwa msingi wa sikukuu mbalimbali zinazosheherekewa katika nchi nyingi duniani, kama vile Noeli au Krismasi (kuzaliwa kwake), Epifania (kuonekana kwake na kubatizwa kwake), Majilio (kuandaliwa kwa ujio wake wa kwanza na kutarajia ujio wa pili), Kwaresima (mafungo na mateso yake), Ijumaa Kuu (kifo chake); muhimu kuliko zote ni Pasaka (kufufuka kwake).
20231101.sw_1997_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Azania
Azania
Azania (kwa Kigiriki: Ἀζανία) ni jina la kihistoria la sehemu mbalimbali za pwani ya Afrika ya Mashariki. Asili yake ni zamani za Waroma na Wagiriki wa kale kwa eneo lililokuwa la watu wa Lugha za Kikushi.
20231101.sw_1997_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Azania
Azania
Mara ya kwanza jina hili limepatikana katika mwandishi Mroma Plinio Mzee (Gaius Plinius Secundus) aliyeishi wakati wa karne ya 1 B.K.
20231101.sw_1997_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Azania
Azania
Kufuatana na maelezo yake, Azania ni sehemu zile zilizoanza katika eneo la Adulis (leo: Eritrea) na kuelekea kusini.
20231101.sw_1997_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Azania
Azania
Kitabu cha mwongozo kwa ajili ya mabaharia "Periplus ya Bahari ya Eritrea" (karne ya 2 BK) kinatoa maelezo zaidi zinazoonyesha ya kwamba jina la Azania labda lilimaanisha pwani ya Afrika ya Mashariki kutoka Eritrea hadi Tanzania ya leo.
20231101.sw_1997_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Azania
Azania
Mwandishi Cosmas Indicopleustes wa karne ya 6 B.K. aliandika Azania ni nchi chini ya utawala wa ufalme wa Aksum, basi hapo isingeenea sana kusini kwa pembe la Afrika.
20231101.sw_1997_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Azania
Azania
Katika karne zilizofuata umbo la "Azania" halikutumika tena. Inawezekana ya kwamba sababu yake ilikuwa Waarabu Waislamu walichukua nafasi ya Wagiriki na Waroma wakitawala biashara ya nje ya pwani ya Afrika ya Mashariki. Kuna uwezekano ya kuwa Waarabu walitumia umbo tofauti la neno kuwa "Zanj" kwa ajili ya eneo lilelile.
20231101.sw_1997_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Azania
Azania
Katika karne ya 20 jina la Azania limefufuka tena. Nchi huru za Tanganyika na Zanzibar ziliungana tarehe 26 Aprili 1964 kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Jina jipya lilitafutwa. Hapo jina lile la kihistoria "Azania" lilikumbukwa tena; kwa kuunganisha maneno ya Tanganyika, Zanzibar na Azania jina la nchi "Tanzania" limepatikana.
20231101.sw_1997_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Azania
Azania
Kwa namna tofauti jina la Azania lilitumika pia Afrika Kusini. Wakati wa siasa ya ubaguzi wa rangi sehemu ya wapinzani wa siasa hii hawakutaka kutumia jina rasmi la "South Africa / Zuid Afrika" tena. Walitafuta jina katika historia iliyotangulia kufika kwa Makaburu wakichukua jina la Azania. Ni hasa vyama vya PAC na Azanian People´s Organization waliotaka kubadilisha jina la Afrika Kusini kuwa Azania. Lakini chama kikubwa cha ANC haikukubali, hivyo mipango ilishindikana.
20231101.sw_2000_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jumuiya%20ya%20Madola
Jumuiya ya Madola
Jumuiya ya Madola (jina la Kiingereza ni Commonwealth of Nations) inaunganisha nchi mbalimbali hasa Uingereza na nchi zilizokuwa koloni zake.
20231101.sw_2000_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jumuiya%20ya%20Madola
Jumuiya ya Madola
Umoja huu umeanzishwa mw. 1926 kama "Jumuiya ya Kibritania" (British Commonwealth) na kupewa jina lake la sasa tangu 1949. Inafuatana na Dola la Kibritania au Dola la Kiingereza ambayo ilikuwa dola kubwa kabisa katika historia ya dunia lakini maeneo yake yalianza kuachana baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia kutokana na kudhoofishwa kwa Uingereza vitani na miendo ya kupigania uhuru katika nchi mbalimbali hasa Uhindi.
20231101.sw_2000_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jumuiya%20ya%20Madola
Jumuiya ya Madola
Leo zipatao asilimia 30 ya watu wote duniani (watu 1,800,000) huishi katika nchi wanachama za Jumuiya ya Madola. Nchi za jumuiya hii wenye wakazi wengi ni hasa Uhindi, Pakistan, Bangladesh na Nigeria. Kuna pia nchi ndogo sana kama Tuvalu yenye wakazi 11,000 pekee.
20231101.sw_2000_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jumuiya%20ya%20Madola
Jumuiya ya Madola
Nchi kadhaa zilisimamishwa uanachama au kuondoka kwa hiari zao. Mfano Tanganyika na Zanzibar ziliungana kwa hiyo hazipo tena lakini mpya ya Tanzania imekuwa nchi mwanachama. Vilevile Newfoundland iliondoka katika jumuiya baada ya kujiunga na Kanada kama jimbo.
20231101.sw_2000_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jumuiya%20ya%20Madola
Jumuiya ya Madola
Pakistan ilisimamishwa uanachama mara kadhaa kwa sababu serikali yake ilipinduliwa na wanajeshi walioanzisha serikali ya kijeshi. Imerudishwa tena.
20231101.sw_2000_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jumuiya%20ya%20Madola
Jumuiya ya Madola
Jamhuri ya Ueire iliamua mwaka 1949 kuacha viungo vyote na Uingereza ikajitangaza kuwa jamhuri isiyokubali athira ya nje kama hali ya malkia wa Uingereza kuwa mkuuw a dola hivyo ikaondoka katika jumuiya.
20231101.sw_2000_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jumuiya%20ya%20Madola
Jumuiya ya Madola
Afrika Kusini ilijiondoa 1961 kwa sababu ya upinzani wa jumuiya dhidi ya sheria za apartheid. Baada mwisho wa ubaguzi wa rangi nchi ilirudi katika jumuiya.
20231101.sw_2002_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mzunguko%20wa%20Bahari%20Nyekundu
Mzunguko wa Bahari Nyekundu
Mzunguko wa Bahari Nyekundu (kwa Kiingereza: Periplous of the Erythrean Sea) ni kitabu cha mwongozo kwa ajili ya mabaharia kilichoandikwa mnamo mwaka 70 BK.
20231101.sw_2002_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mzunguko%20wa%20Bahari%20Nyekundu
Mzunguko wa Bahari Nyekundu
"Periplous" ni neno la Kigiriki linalomaanisha tendo la kuzunguka bara kupitia bahari kwa merikebu; "Bahari ya Eritrea" ni jina la kale kwa ajili ya Bahari ya Shamu (hadi Bahari Hindi). Jina hilo lilitungwa na watu wa nchi za mashariki ya Bahari ya Kati na Misri waliotumia lugha ya Kigiriki miaka 2000 iliyopita.
20231101.sw_2002_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mzunguko%20wa%20Bahari%20Nyekundu
Mzunguko wa Bahari Nyekundu
Kitabu hicho kimeandikwa na mwenyeji wa Aleksandria / Misri uliokuwa mji mkubwa wakati ule na kitovu cha biashara ya kimataifa kati ya Dola la Roma, Afrika ya Mashariki na Bara Hindi.
20231101.sw_2002_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mzunguko%20wa%20Bahari%20Nyekundu
Mzunguko wa Bahari Nyekundu
Kitabu kinaeleza juu ya bandari kuanzia Misri hadi Afrika ya Mashariki kwa upande mmoja na hadi Bara Hindi kwa upande mwingine. Kinataja majina ya bandari, bidhaa zilizopelekwa huko na bidhaa zilizopatikana kila mahali. Pia kuna habari za kando juu ya watu, watawala na mila zao.
20231101.sw_2002_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mzunguko%20wa%20Bahari%20Nyekundu
Mzunguko wa Bahari Nyekundu
Maelezo ni mengi kuhusu pwani ya Eritrea na Somalia hadi Pembe ya Afrika; kuelekea kusini majina ya bandari ni machache; mwisho wa eneo lililojulikana ni mji wa Rhapta katika nchi za Azania, lakini hadi leo wataalamu hawajaelewana Rhapta na Azania zilikuwa wapi.
20231101.sw_2003_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Eritrea
Bahari ya Eritrea
Bahari ya Eritrea (kwa Kigiriki ερυθρά θάλασσα, erythrá thálassa) ni jina la kale la Bahari ya Shamu na Bahari Hindi. Neno "erythra" katika lugha ya Kigiriki inamaanisha rangi nyekundu ("thalassa" = bahari). Hivyo bahari ile iliitwa "Bahari Nyekundu" (linganisha Kiingereza "Red Sea"). Inasemekana ya kwamba jina hilo limetokana na aina ya mwani unaoonyesha rangi hiyo wakati mwingine.
20231101.sw_2003_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Eritrea
Bahari ya Eritrea
Inaonekana ya kwamba waandishi wa kale hawakutofautisha kati ya Bahari ya Shamu na Bahari Hindi. Merikebu za zamani zile zilisafiri muda wote karibu na pwani kwa sababu dira haikulikana bado nje ya Uchina. Hivyo haikuwa rahisi kuvuka bahari moja kwa moja na kupata picha kamili ya umbo la bahari.
20231101.sw_2003_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Eritrea
Bahari ya Eritrea
Nahodha wa merikebu hizo walitumia maandiko kama Periplus ya Bahari ya Eritrea wakipanga safari zao.
20231101.sw_2004_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Shamu
Bahari ya Shamu
Bahari ya Shamu (kwa Kiingereza Red Sea; kwa Kiarabu البحر الأحمر Baḥr al-Aḥmar, al-Baḥru l-’Aḥmar; kwa Kiebrania ים סוף Yam Suf; kwa Kitigrinya ቀይሕ ባሕሪ QeyH baHri) ni ghuba kubwa ya Bahari ya Hindi. Jina la kihistoria katika lugha ya Kigiriki lilikuwa Bahari ya Eritrea (ερυθρά θάλασσα, erythrá thálassa).
20231101.sw_2004_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Shamu
Bahari ya Shamu
Kaskazini kuna rasi ya Sinai pamoja ghuba ndogo za Aqaba na Suez; pia kwa sasa imeunganika na Mediteranea kwa njia ya Mfereji wa Suez. Kusini Bahari ya Shamu imeunganika na Bahari Hindi kwa njia ya mlango wa bahari wa Bab el Mandeb.
20231101.sw_2004_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Shamu
Bahari ya Shamu
Ghuba yote ina urefu wa takriban kilomita 2000; upana wake ni kati ya km 300 na 20 tu kwenye Bab el Mandeb. Eneo lake ni km² 450,000.
20231101.sw_2004_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Shamu
Bahari ya Shamu
Vilindi vyake vinaelekea hadi mita 2500 chini ya uwiano wa bahari. Vilindi hivyo ni sehemu ya Bonde la Ufa.
20231101.sw_2006_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ingawa inajitawala katika mambo ya ndani.
20231101.sw_2006_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Eneo lake ni sawa na funguvisiwa la Zanzibar lililopo mbele ya mwambao wa Afrika ya Mashariki karibu na Tanganyika (Tanzania bara).
20231101.sw_2006_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Linajumuisha visiwa vikubwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vidogo, lakini si kile cha Mafia kilichopo kusini zaidi.
20231101.sw_2006_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Historia inaonyesha kwamba kwa kiasi cha miaka 20,000 kumekuwepo makazi ya binadamu katika visiwa vya Zanzibar.
20231101.sw_2006_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Visiwa hivyo ni sehemu ya kumbukumbu ya kihistoria ya ulimwengu wakati Waajemi wafanyabiashara walivigundua na kuvifanya makao makuu kwa safari kati ya Mashariki ya Kati, India na Afrika.
20231101.sw_2006_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Katika kipindi cha karne ya 3 na ya 4, Wabantu walianza biashara na Waarabu waliofika Afrika ya Mashariki.
20231101.sw_2006_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Katika karne ya 7, Waarabu walifika Zanzibar kibiashara pamoja na kusambaza dini ya Uislamu; Waarabu ndio walioipa jina ZANZIBAR kutokana na maneno ya Kiajemi ZINJI BAR yaani sehemu ya Watu Weusi.
20231101.sw_2006_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Lugha ya Kiswahili ilianza kutumika kiasi cha karne ya 13 ikitokana na mchanganyiko wa lugha ya Kiarabu na lugha za Kiafrika.
20231101.sw_2006_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Katika karne ya 16 Wareno walifika Zanzibar lakini utawala wao ulifuatiwa na kutokuwepo utulivu, lakini biashara ya utumwa iliwaweka watu pamoja.
20231101.sw_2006_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Waarabu kutoka Oman walichukua utawala Zanzibar katika karne ya 17 na Zanzibar ilikuwa makao makuu ya utawala wa Waomani.
20231101.sw_2006_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Miaka 1820-1870 Zanzibar ilifaidi matunda mazuri ya kiuchumi na maendeleo yaliyosababishwa na utawala wa masultani na hivyo kupelekea kuenea kwa dini ya Kiislamu Zanzibar pamoja na kuwa na mwakilishi nchini Marekani.
20231101.sw_2006_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Katika karne ya 19 Zanzibar ilikuwa chini ya utawala wa Oman, mwaka 1830 Zanzibar ilikuwa inaongoza kwa kilimo cha karafuu, na hiyo kupelekea haja ya watumwa kuongezeka kutumika katika kilimo. Hatimaye watumwa walikuwa 90% za wakazi wote.
20231101.sw_2006_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Mwaka 1885 kamisheni kutoka Uingereza na Ujerumani iliamua kuigawa Zanzibar kutoka katika utawala wa Kisultani na ndio ulikuwa mwisho wa utawala wa kujitegemea kwa Zanzibar. Mnamo mwaka 1886 sultani alikubali maridhiano hayo.
20231101.sw_2006_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Mwaka 1890 Zanzibar ilikuwa chini ya uangalizi wa Waingereza rasmi, lakini uchaguzi wa mwanzo ulifanyika mwaka 1957, na miaka iliyofuata kukawepo fujo na machafuko kutoka kwa Waafrika wanaodai uhuru dhidi ya utawala wa Kiarabu.
20231101.sw_2006_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Mwezi Desemba mwaka 1963 Waingereza waliipa uhuru Zanzibar chini ya jumuiya ya madola, na tarehe 12 Januari 1964 Zanzibar ilifanya mapinduzi kujikomboa kutoka katika utawala wa sultani.
20231101.sw_2006_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Zanzibar ina bunge lake linaloitwa Baraza la Wawakilishi wa Zanzibar lenye wabunge 50 wanaochaguliwa kwa muda wa miaka mitano.
20231101.sw_2006_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Jamhuri ya watu wa Zanzibar ilianzishwa baada ya mapinduzi ya 1964 yaliyomaliza Usultani wa Zanzibar.
20231101.sw_2006_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Rais wa tatu aliyemfuata alikuwa Ali Hassan Mwinyi (1984-1995) aliyeendelea kuwa rais wa Tanzania tangu 1985.
20231101.sw_2006_18
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Rais Amani Abeid Karume ambaye ni mwana wa rais wa kwanza na alikuwa mgombea wa CCM alichaguliwa mara ya pili na wananchi wote tarehe 30 Oktoba 2005 katika kura iliyopingwa na chama cha upinzani CUF.
20231101.sw_2006_19
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Watu wa Zanzibar ni wa asili mbalimbali, hasa watu wa asili ya Afrika Bantu, yakiwemo makabila ya Wahamidu na Watumbatu; halafu Waasia, awali kutoka India na nchi za Kiarabu.
20231101.sw_2006_20
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Idadi ya wakazi wa Zanzibar ilikuwa 1,303,569 mwaka 2012, tarehe ya sensa ya mwisho, iliyoonyesha ongezeko la 3.1% kwa mwaka.
20231101.sw_2006_21
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Pemba ina jumla ya makazi sawa. Mji mkubwa ni Chake Chake, ukiwa na idadi ya 19,283, mengine ni Wete na Mkoani.
20231101.sw_2006_22
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Waliobaki ni hasa Wakristo. Wa kwanza walikuja wakati wa utawala wa Kireno, halafu wakati wa masultani kuwepo Zanzibar na wa ukoloni wa Uingereza.
20231101.sw_2006_23
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Kulikuwa na Wahindu pia lakini wengi wao walikimbia nchi au kuuawa wakati wa mapinduzi ya mwaka 1964.
20231101.sw_2006_24
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Kuna misikiti 51, ambayo waadhini wake hugongana wakati wa maombi, pamoja na mahekalu ya Uhindu sita na makanisa kadhaa, yakiwemo Kanisa Kuu Katoliki na Kanisa Kuu la Anglikana katika mji wa Zanzibar Stonetown.
20231101.sw_2006_25
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Hasa hilo la mwisho ni maarufu kwa sababu lilijengwa mahali pa soko la watumwa lililofungwa, altari ikiwa imejengwa juu ya nafasi ya mti wa kuwafunga watumwa walioadhibiwa kwa viboko, na batizio kuwa mahali walipotupwa watoto watumwa ambao hawakuuzwa pamoja na mama zao.
20231101.sw_2006_26
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Upande wa huduma ya afya, vifo vya watoto wachanga bado ni 83 kati ya wazaliwa 1000, na inakadiriwa kuwa utapiamlo huathiri mmoja katika watu watatu wa visiwa.
20231101.sw_2006_27
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Matarajio ya maisha wakati wa kuzaliwa ni miaka 48, wakati maambukizi ya VVU / UKIMWI ni madogo sana kwa Zanzibar kuliko Tanzania kwa ujumla (0.6% ya idadi ya watu dhidi ya wastani wa kitaifa wa 8%).
20231101.sw_2006_28
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Uchumi wa Zanzibar unategemea kilimo na utalii. Mazao yanayouzwa nje ni hasa karafuu, basibasi, mdalasini na pilipili.
20231101.sw_2006_29
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Uchumi wa Zanzibar ni uchumi duni kabisa ambao mwananchi wa kawaida anaishi kwa kiasi cha chini ya dola moja kwa siku au hana uhakika wa kupata chochote.
20231101.sw_2006_30
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Wastani wa mapato ya kila mwaka ya US $ 250 na ukweli kwamba karibu nusu ya wakazi wanaishi chini ya mstari wa umaskini. Lakini kuna tofauti kubwa katika kiwango cha maisha kati ya wakazi wa Pemba na Unguja, tena kati ya wakazi wa mijini na vijijini.
20231101.sw_2006_31
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Hilo linatokana na viongozi kutoonesha mori katika kutatua matatizo au kuweka mbinu za kuleta maendeleo, badala yake ni kujadili siasa kwa muda mwingi.
20231101.sw_2006_32
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Watu%20wa%20Zanzibar
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
Zanzibar ni nchi yenye matumaini katika uchumi lakini, kutokana na migogoro ya kisiasa, imekuwa katika hali duni kabisa, na mabalozi wa Marekani na nchi nyingine walisisitiza mara nyingi umuhimu wa kuwepo ushirikiano katika siasa ili kuiwezesha Zanzibar kuinuka katika hali ya uchumi.
20231101.sw_2007_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Tsunami ni wimbi kubwa sana katika bahari linalosababishwa na tetemeko la ardhi, mlipuko wa volkano au matokeo mengine yanayoleta mshtuko wa ghafla chini ya maji. Mshtuko huo unasababisha kutokea kwa wimbi kali linaloanza kupaa juu likifika katika maji kame na kwenye ufuko wa bahari.
20231101.sw_2007_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Tsunami huweza kutokea na kusababisha vifo vya maelfu ya watu. Wakati mwingine inaweza kutokea bila kuleta madhara yoyote.
20231101.sw_2007_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Tsunami ya Krismasi 2004 ilikuwa mojawapo kati ya maafa makubwa yaliyotokea katika historia ya dunia yetu iliyoua malakhi ya watu huko Asia Kusini na kuleta madhara hadi pwani ya Afrika ya Mashariki.
20231101.sw_2007_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Tarehe 26 Desemba 2004 lilitokea tetemeko la ardhi chini ya Bahari Hindi karibu na pembe ya kaskazini ya Sumatra kwenye mstari ambako bamba la Uhindi linajisukuma chini ya bamba dogo la Burma. Siku ile km 1,200 za pembizo la bamba la Uhindi zilisogea mbele katika muda wa dakika chache kwa urefu wa takriban mita 15 chini ya bamba la Burma. Bamba la juu lilisukumwa na kupaa juu hadi mita 30. Mshtuko huo ulianzisha wimbi kubwa chini ya bahari lililotoka juu kwa umbo la tsunami iliyoua takriban watu 275,000.
20231101.sw_2007_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Katika maji marefu ya bahari wimbi halikuwa na hasara likaonekana kuwa na cm 30 pekee. Lakini ilifika mwambaoni kwenye maji kama likaanza kupaa juu kufikia hadi m 30.
20231101.sw_2007_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Kutoka kitovu cha tetemeko la ardhi mawimbi ya tsunami yalienea kotekote. Yalipiga vikali sana pwani za Indonesia, Sri Lanka, Thailand na India. Mawimbi yalifikia hadi pwani ya Afrika na kusababisha vifo Somalia, Kenya, Tanzania na Afrika Kusini.
20231101.sw_2007_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Baada ya kuokoa watu, jambo la msingi kwa afya ya umma ni kusafisha maji ya kunywa, chakula, makazi, na utunzaji wa majeraha.
20231101.sw_2007_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Upotezaji wa makazi huwaacha watu katika hali ya kutangamana na wadudu, joto na hatari zingine za kimazingira.
20231101.sw_2007_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Vingi vya vifo vinavyohusiana na tsunami husababishwa na kuzama, lakini majeraha ya kisaikolojia ni tatizo la msingi pia. Majeraha kama vile kuvunjika mikono au miguu na majeraha ya kichwa husababishwa na athari za kimwili za watu wanaosukumwa na maji kwenye vifusi kama vile nyumba, miti na vitu vingine visivyosonga. Maji yanapopungua, uvutaji na uondoaji wa vifusi kwenye maeneo yaliyo na watu wengi unaweza kusababisha majeraha zaidi na kudhoofisha majengo na huduma.
20231101.sw_2007_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Mikasa ya kiasili haisababishi ongezeko la magonjwa ya kuambukiza katika mkurupuko. Hata hivyo, maji na vyakula vilivyochafuliwa na aidha ukosefu wa makazi na huduma ya afya vinaweza kuwa na madhara ya baadaye ya kukithiri kwa maradhi yaliyo kwenye sehemu iliyoathiriwa.
20231101.sw_2007_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
ugeuzaji wa vifaa vya matibabu kutoka sehemu zisizoathiriwa ili kukidhi mahitaji ya sehemu zilizoathiriwa;
20231101.sw_2007_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Ili kuzuia magonjwa yanayotokana na chakula, nawa mikono yako kwa maji safi na sabuni kabla na baada ya kula au kutayarisha chakula na baada ya kutumia choo au bafu. Iwapo huna maji safi, tumia visafisha mikono visivyo na maji hadi maji safi yatakapopatikana.
20231101.sw_2007_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Usile chakula chochote ambacho hakijahifadhiwa kwenye vyombo visivyoingiza maji (vyombo vya mikebe au vya plastiki vilivyofungwa) na kile ambacho huenda kimetangamana na maji yasiyotibiwa, kama vile maji ya bahari, mafuriko, mto au dimbwi. Tupa chakula chochote kilicho katika mikebe isiyofungwa au inayoingiza maji ambacho kimetangamana na maji yasiyotibiwa.
20231101.sw_2007_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Vyakula vya mikebe ambavyo havijaharibika vinaweza kuokolewa. Ondoa vitambulisho kwenye mikebe, safisha sehemu ya nje ya mikebe hiyo kwa maji ya sabuni, na uue viini kikamilifu kwenye mikebe hiyo kwa mchanganyiko wa kikombe 1 (aunsi 8; takribani lita 0.25) cha klorini (asilimia 5.25) katika galoni 5 (takribani lita 19) za maji safi yaliyotibiwa. Tumia kalamu kuandika yaliyomo na tarehe ya kuharibika kwenye mikebe hiyo.
20231101.sw_2007_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Iwapo mikebe ya chakula iliyofunguliwa ina vifuniko vyenye hesi, meno, vilivyokunjwa (vifuniko vya chupa za soda), vilivyopinda, au vya kubingirika, au ikiwa imetengenezwa nyumbani, itupe ikiwa imetangamana na maji ambayo hayajatibiwa. Haiwezi kutiwa kiua viini.
20231101.sw_2007_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Ikiwa hunyonyeshi, katika kulisha watoto wachanga tumia chakula cha mtoto kilichotengenezwa na kuhifadhiwa mikebeni kisichohitaji kuongezwa maji.
20231101.sw_2007_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Ikiwa barafu kavu itapatikana, inaweza kutumiwa kudumisha ubaridi wa chakula — pauni 25 (takribani kilogramu 11.5) za barafu kavu zitadumisha friza ya futi 10 (lita 283) chini ya kiwango cha kuganda kwa siku 3 hadi 4.
20231101.sw_2007_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tsunami
Tsunami
Kuwa makini unaposhughulikia barafu kavu, kwa sababu hugandisha kila inachogusa. Vaa glavu kavu na nzito ili kuepuka majeraha. Barafu kavu inapoyeyuka hubadilika kutoka hali ngumu na kuwa gesi.