_id
stringlengths 15
22
| url
stringlengths 31
150
| title
stringlengths 1
86
| text
stringlengths 100
23.8k
|
---|---|---|---|
20231101.sw_2012_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
"Chad". International Religious Freedom Report 2006. 15 September 2006. Bureau of Democracy, Human Rights, and Labor, U.S. Department of State.
|
20231101.sw_2012_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
"Chad " (PDF). Women of the World: Laws and Policies Affecting Their Reproductive Lives – Francophone Africa. Center for Reproductive Rights. 2000
|
20231101.sw_2012_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
"Chad – Community Based Integrated Ecosystem Management Project" (PDF). 24 September 2002. World Bank.
|
20231101.sw_2012_18
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
"Chad: Humanitarian Profile – 2006/2007" (PDF). 8 January 2007. Office for the Coordination of Humanitarian Affairs.
|
20231101.sw_2012_19
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
Chowdhury, Anwarul Karim & Sandagdorj Erdenbileg (2006); . New York: United Nations. ISBN 92-1-104540-1
|
20231101.sw_2012_20
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
East, Roger & Richard J. Thomas (2003); Profiles of People in Power: The World's Government Leaders. Routledge. ISBN 1-85743-126-X
|
20231101.sw_2012_21
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
Dinar, Ariel (1995); Restoring and Protecting the World's Lakes and Reservoirs. World Bank Publications. ISBN 0-8213-3321-6
|
20231101.sw_2012_22
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
Lange, Dierk (1988). "The Chad region as a crossroad" (PDF), in UNESCO General History of Africa – Africa from the Seventh to the Eleventh Century, vol. 3: 436–460. University of California Press. ISBN 978-0-520-03914-8
|
20231101.sw_2012_23
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
Macedo, Stephen (2006); Universal Jurisdiction: National Courts and the Prosecution of Serious Crimes Under International Law. University of Pennsylvania Press. ISBN 0-8122-1950-3
|
20231101.sw_2012_24
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
Ndang, Tabo Symphorien (2005); " " (PDF). 4th PEP Research Network General Meeting. Poverty and Economic Policy.
|
20231101.sw_2012_25
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
Pollack, Kenneth M. (2002); Arabs at War: Military Effectiveness, 1948–1991. Lincoln: University of Nebraska Press. ISBN 0-8032-3733-2
|
20231101.sw_2012_26
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
"Republic of Chad – Public Administration Country Profile " (PDF). United Nations, Department of Economic and Social Affairs. November 2004.
|
20231101.sw_2012_27
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
"Symposium on the evaluation of fishery resources in the development and management of inland fisheries". CIFA Technical Paper No. 2. FAO. 29 November – 1 December 1972.
|
20231101.sw_2012_28
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
"http://www.crisisgroup.org/~/media/Files/africa/central-africa/chad/French%20translations/Chad%20Back%20towards%20War%20French.pdf " (PDF). International Crisis Group. 1 June 2006.
|
20231101.sw_2012_29
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
World Bank (14 July 2006). World Bank, Govt. of Chad Sign Memorandum of Understanding on Poverty Reduction. Press release.
|
20231101.sw_2012_30
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
World Population Prospects: The 2006 Revision Population Database. 2006. United Nations Population Division.
|
20231101.sw_2012_31
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chad
|
Chad
|
Young, Neil (August 2002); An interview with Mahamet-Saleh Haroun, writer and director of Abouna ("Our Father").
|
20231101.sw_2016_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Athi
|
Athi
|
Athi ni jina la mto katika kaunti ya Kitui, Kenya, Afrika Mashariki. Sehemu za mto hujulikana pia kwa majina ya Galana na Sabaki, kwa hiyo mto wote huitwa pia Athi-Galana-Sabaki.
|
20231101.sw_2016_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Athi
|
Athi
|
Mto wa Athi umeupatia jina lake mji wa Athi River karibu na Nairobi pia kwa kampuni ya Athi River Mining.
|
20231101.sw_2016_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Athi
|
Athi
|
Athi inaanza karibu na Nairobi ikielekea Bahari Hindi. Inapita Mbuga ya Kitaifa ya Tsavo Mashariki pia tambarare ya juu ya Yatta ilipotafuta njia yake kuvukia eneo kubwa la mawe ya kivolkeno.
|
20231101.sw_2016_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Athi
|
Athi
|
Baada ya maporomoko ya maji ya Lugard inapokea mto Tsavo ikibadilika jina lake. Mto unaitwa kuanzia hapa kwa jina la Galana. Kabla ya kufika katika Bara Hindi karibu na Malindi upande wa kaskazini jina linabadilika tena kuwa Sabaki.
|
20231101.sw_2017_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Johann Ludwig Krapf (11 Januari 1810 – 26 Novemba 1881) alikuwa mmisionari wa kwanza wa Uprotestanti nchini Kenya katika karne ya 19 akatunga kamusi ya kwanza ya lugha ya Kiswahili.
|
20231101.sw_2017_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Krapf alizaliwa tarehe 11 Januari 1810 katika kijiji cha Derendingen karibu na Tübingen, eneo la Württemberg, Ujerumani wa Kusini-Magharibi katika familia ya wakulima wadogo Walutheri.
|
20231101.sw_2017_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Alisoma shule ya msingi kijijini kwake halafu shule ya sekondari Tübingen. Akiwa mwanafunzi alipenda sana masomo yote yaliyohusu jiografia na lugha. Pamoja na Kilatini na Kigiriki alisoma pia Kifaransa na Kiitalia.
|
20231101.sw_2017_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Alipokuwa na umri wa miaka 16 alitembelea mara ya kwanza nyumba ya Misioni ya Basel, Uswisi. 1827 – 1829 alijiunga na kozi ya kuandaa wamisionari huko Basel lakini hakupendezwa na maisha ya pamoja; akishikwa na wasiwasi kuhusu wito wake akarudi nyumbani na kuingia masomo ya teolojia katika Chuo Kikuu cha Tübingen.
|
20231101.sw_2017_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Krapf alimaliza masomo yake mwaka 1834. Vituo vya huduma kama mchungaji msaidizi na mwalimu vilifuata. Wakati ule alikutana na mmisionari aliyempa moyo kurudi Basel.
|
20231101.sw_2017_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Mwaka 1836 alikutana na mwakilishi wa Church Missionary Society (CMS) aliyemkaribisha kufanya kazi na CMS. Misioni ya Basel ilimpa ruhsa akapokea wito wa kwenda Ethiopia. Krapf alianza mara moja kujiandaa akisoma Ge’ez (lugha ya Kale ya Ethiopia) na Kiamhari (lugha ya kisasa ya Wakristo katika nyanda za juu Ethiopia).
|
20231101.sw_2017_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
1837-1842 Krapf alifanya kazi ya umisionari huko Ethiopia. Mpango wa misioni ya CMS ilikuwa kuwaamsha Wakristo Waorthodoksi kwa matumaini ya kwamba watakuwa wenyewe wamisionari bora kwa wenzao Wapagani au Waislamu.
|
20231101.sw_2017_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Lakini Krapf hakuelewa vema Ukristo wa kiorthodoksi wa Waamhari. Alishindwa kuelewa maana ya liturgia, mila na desturi nyingi. Hakuelewa hasa kwa nini Wakristo Waorthodoksi walisoma Biblia katika lugha ya kale ya Ge’ez hata wasipoelewa lugha hiyo badala ya kutumia tafsiri ya Kiamahari aliyokuwa amefanya.
|
20231101.sw_2017_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Hivyo Krapf alijisikia amevutwa zaidi na Wagalla – hili ni jina la zamani za watu wanaojulikana leo kama Waoromo au Borana. Wagalla kwa jumla walikuwa wakifuata dini zao za kiasili, athira za kiislamu zikianza kuonekana. Krapf alijifunza lugha yao alianza kutafsiri sehemu za Agano Jipya katika Kigalla (Kioromo).
|
20231101.sw_2017_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Mwaka 1842 Krapf alipaswa kuondoka Ethiopia pamoja na wamisionari wengine wa Kiprotestanti, akiwa na ndoto ya kurudi na kufanya kazi kati ya Wagalla. Alikaa muda kidogo Kairo (Misri) akafunga ndoa, bibiarusi alikuwa amemfuata kutoka Ujerumani.
|
20231101.sw_2017_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Wakati ule kwake nyumbani Tübingen Chuo Kikuu kilikuwa kimefuata taarifa zake na 1842 kikampa cheo cha udaktari (PhD) kwa ajili ya utafiti wake katika lugha na historia ya Ethiopia.
|
20231101.sw_2017_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Ethiopia ilikuwa imefunga milango yake, hivyo Krapf aliwaza njia nyingine. Alikuwa amesikia ya kuwa Wagalla waliwahi kufika hadi pwani za Afrika ya Mashariki. Hivyo akasafiri hadi Zanzibar kwa lengo la kuwafikia Wagalla kupitia eneo la Kenya ya leo. Sultani Seyyed Said alimpa ruhusa ya kuanzisha kituo cha misheni huko Mombasa.
|
20231101.sw_2017_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Mwaka 1844 Krapf alifika Mombasa akianza mara moja kujifunza Kiswahili pamoja na lugha ya wazalendo wa eneo la Mijikenda. Huko mke na mtoto waliugua malaria wakafa. Krapf alihamia Rabai iliyoko katika vilima juu ya Mombasa penye joto kidogo akaanzisha kituo cha Rabai Mpya.
|
20231101.sw_2017_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Mwaka 1846 mmisionari mwingine (Johannes Rebmann) alikuja kufanya kazi pamoja naye. Huko Rabai Mpya Krapf alitunga kamusi na sarufi ya kwanza ya Kiswahili.
|
20231101.sw_2017_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Krapf na Rebmann walikuwa Wazungu wa kwanza walioona milima yenye theluji Afrika. Rebmann aliona Kilimanjaro, Krapf aliona Mlima wa Kenya. Taarifa zao zilipofika Ulaya zilichekwa na wataalamu waliodai milima yenye theluji haiwezekani Afrika.
|
20231101.sw_2017_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Hadi kifo chake aliendelea kuboresha vitabu vyake kuhusu utamaduni na lugha za mataifa mbalimbali ya Afrika. Kwa jumla aliandika kamusi au kutafsiri sehemu za Biblia katika lugha zifuatazo: Ge’ez, Kiamhari, Kioromo, Kiswahili, Ki-mijikenda, Kikamba, Kimasai.
|
20231101.sw_2017_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Ludwig Krapf alitoa mchango mkubwa sana katika kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili kwani aliweza kutafsiri Injili ya Luka na ya Mathayo ,pia aliweza kuandika sarufi ya Kiswahili inayohusu jamii ya Wasambaa.
|
20231101.sw_2017_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Nyumba yake huko New Rabai imekuwa makumbusho chini ya Museums of Kenya. Jengo la Ubalozi wa Kijerumani huko Nairobi limepewa jina lake.
|
20231101.sw_2017_18
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Krapf alikuwa Mlutheri, lakini Kanisa Anglikana linamkumbuka kama mwanzilishi wa madhehebu yake nchini Kenya.
|
20231101.sw_2017_19
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Raupp, Werner: Gelebter Glaube. Metzingen/Württemberg 1993, 278 - 287: "Johann Ludwig Krapf - Bahnbrecher der ostafrikanischen Mission".
|
20231101.sw_2017_20
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Gütl, Clemens. 2001. Johann Ludwig Krapf - "Do' Missionar vo' Deradenga" zwischen pietistischem Ideal und afrikanischer Realität. Hamburg, 2001 (Beiträge zur Missionswissenschaft und interkulturellen Theologie, Bd. 17); ISBN 3-8258-5525-2.
|
20231101.sw_2017_21
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Gütl, Clemens: "Memoir on the East African Slave Trade" ya Johann Ludwig Krapf aliyoiandika mwaka wa 1853 bila kuichapisha rasmi. Imetolewa na Gütl pamoja na maelezo katika jarida. Vienna, 2002 (Beiträge zur Afrikanistik, 73).
|
20231101.sw_2017_22
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Raupp, Werner: Johann Ludwig Krapf. Missionar, Forschungsreisender und Sprachforscher. 1810–1881. In: Gerhard Taddey, Rainer Brüning (Hrsg.): Lebensbilder aus Baden-Württemberg, Band 22. Stuttgart 2007, (182) - 226.
|
20231101.sw_2017_23
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ludwig%20Krapf
|
Ludwig Krapf
|
Raupp, Werner: Johann Ludwig Krapf, "dr Missionar vo Deradinga". In: Hin und weg. Tübingen in aller Welt. Hrsg. von Karlheinz Wiegmann. Tübingen 2007 (Tübinger Kataloge, 77), (90) - 99.
|
20231101.sw_2018_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Komori (kwa Kiswahili pia: Visiwa vya Ngazija; kwa Kikomori: قمر, Komori, kwa Kifaransa: Comores) ni nchi huru kwenye funguvisiwa katika Bahari Hindi upande wa Mashariki wa Afrika. Iko katika Kanali ya Msumbiji kaskazini kwa Madagaska na mashariki kwa Msumbiji.
|
20231101.sw_2018_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Jina limetokana na lugha ya Kiarabu ambapo Juzur al-Qamar (جزر القمر) linamaanisha "visiwa vya mwezi".
|
20231101.sw_2018_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Komori ina visiwa vitatu vikubwa: Grande Comore (Ngazidja), Anjouan (Nzwani) na Moheli (Mwali). Kisiwa cha Mayotte ni sehemu ya funguvisiwa kijiografia lakini kisiasa ni sehemu ya Ufaransa kwa sababu wakati wa kupata uhuru watu wa Mayotte walitamka kwa kura nyingi (73%) ya kwamba wanataka kukaa na Ufaransa. Lakini Komori inadai ni sehemu ya eneo lake.
|
20231101.sw_2018_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Kitovu cha kisiwa kikubwa zaidi (Grande Comore) ni mlima wa volkano hai Karthala wenye mita 2,461 juu ya UB. Safari iliyopita Karthala ililipuka mwaka 1977 ikaharibu kijiji kimoja.
|
20231101.sw_2018_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Miji mikubwa ni (wakazi mwaka 2005): Moroni 42.872, Mutsamudu 23.594, Fomboni 14.966, Domoni 14.509 na Tsémbehou 11.552.
|
20231101.sw_2018_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Visiwa vya Komori vimekaliwa na watu mbalimbali kutoka Afrika na Asia Kusini katika historia ndefu. Wanaakiolojia walitambua mabaki ya makazi ya watu kutoka karne ya 6 kwenye kisiwa cha Nzwani lakini haijulikani kama watu walitangulia kufika mapema bila kuacha mabaki ya kutambulika.
|
20231101.sw_2018_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Kipindi cha kwanza huitwa kipindi cha Dembeni (karne ya 9 - 10) ambako Waswahili walianzisha kijiji kimoja katika kila kisiwa.
|
20231101.sw_2018_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Wakati wa karne ya 11 hadi ya 15 biashara iliongezeka na Madagaska pia na wafanyabiashara kutoka Uarabuni. Vijiji vidogo vikaongezeka na vijiji vya awali vikakua vikawa miji.
|
20231101.sw_2018_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Kumbukumbu ya wenyeji hutaja mara nyingi majina ya Waarabu kutoka Yemen na Saba' kama mababu wa koo asilia lakini hakuna uhakika kama kumbukumbu hizo zinalingana na historia halisi.
|
20231101.sw_2018_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Athira ya Kiarabu na ya Kiislamu ikaongezeka kutokana na biashara ya watumwa, dhahabu na pembe za ndovu kati ya Afrika ya Mashariki na nchi za Kiislamu.
|
20231101.sw_2018_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Waarabu na Waajemi walijenga vituo kwa ajili ya biashara yao pamoja na misikiti na kueneza dini ya Uislamu kwenye visiwa.
|
20231101.sw_2018_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Hata kama Komori si karibu sana na pwani, hata hivyo kutokana na mwendo wa upepo ni kituo muhimu cha jahazi kwenye safari kati ya Kilwa na Msumbiji iliyokuwa bandari kuu ya dhahabu ya Zimbabwe.
|
20231101.sw_2018_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Kufuatana na katiba ya uhuru ya mwaka 1975 Komori ilitangazwa kuwa jamhuri ya Kiislamu. Serikali zilipinduliwa mara kwa mara na wanajeshi au na mamluki.
|
20231101.sw_2018_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Katiba mpya ya mwaka 2001 imeondoa tabia ya kidini ya dola na iliunda utaratibu wa urais kuzunguka kati ya visiwa vitatu vikubwa.
|
20231101.sw_2018_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Katika uchaguzi ya mwaka 2002 rais Azali Assoumani alichaguliwa kutoka kisiwa cha Ngazidja (Komori Kuu). Katika uchaguzi wa 2006 rais amechaguliwa kati ya wagombea kutoka kisiwa cha Anjouan. Wananchi wa Anjouan walipiga kura ya kwanza. Wagombea watatu wenye kura nyingi wameteuliwa na kusimamishwa mbele ya wapiga kura wa visiwa vyote watakaomchagua rais wa jamhuri.
|
20231101.sw_2018_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Watu wa Komori ni mchanganyiko wa Waarabu, Wamadagaska, Waafrika wa bara ambao mababu walikuwa watumwa, Wahindi na Wazungu kadhaa.
|
20231101.sw_2018_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Wakazi wengi ni Waislamu (98%, hasa Wasunni), wakifuatwa na Wakristo (2%). Karibu nusu ya wananchi wote hawajui kusoma.
|
20231101.sw_2018_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Nje ya Kifaransa, Kiarabu na Kimalagasy Sanifu, kuna lugha tatu za asili ambazo huzungumzwa na Wakomori, yaani Kimwali, Kindzwani na Kingazidja ambazo ziko karibu na Kiswahili.
|
20231101.sw_2018_18
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Komori ni kati ya nchi maskini zaidi duniani. Kilimo, uvuvi, uwindaji na misitu ni misingi ya uchumi wote.
|
20231101.sw_2018_19
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Komori
|
Komori
|
Barabara na mawasiliano ya meli au ndege ni haba, idadi ya watu inakua haraka, elimu ni duni; haya yote yanasababisha kudumu kwa uchumi wa kijungujiko na uhaba wa ajira. 80% ya wafanyakazi wote wanashughulika kilimo.
|
20231101.sw_2021_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Jina lake halisi lilikuwa Johnstone Kamau wa Ngengi. Alipewa jina la utani ambalo ni Mkuki wa Moto (Burning Spear). Jina la Kenyatta lilitokana na mkanda aliopenda kuuvaa ambao ulitengenezwa kwa shanga. Wagĩkũyũ wanauita kenyaata.
|
20231101.sw_2021_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Baada ya kuhitimu aliajiriwa kama karani na msoma mita wa manispaa ya Nairobi, alioa mke wake wa kwanza ambaye ni Grace Wahu.
|
20231101.sw_2021_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Kabila lake lilikuwa ni Mgĩkũyũ. Azma yake ya kutaka kuikomboa ardhi ya Wagĩkũyũ ilimfanya aweze kuwaunganisha, naye akawa katibu wao mwaka 1928.
|
20231101.sw_2021_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Mwaka 1930 alizuru Marekani na Uingereza ambako aliishi miaka kumi na mitano na hata kuoa mwalimu wa Kiingereza ambaye aliitwa Edna Kenyatta.
|
20231101.sw_2021_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Alirudi Kenya mwaka 1946 na alichaguliwa kuwa rais wa chama cha siasa cha Kenya African Union (KANU). Alihamasisha kukomeshwa ubaguzi wa rangi; kuwa na mwamko kisiasa pamoja na mambo mengine yanayompa Mwafrika heshima na utu.
|
20231101.sw_2021_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Aliandika kitabu kiitwacho Facing Mount Kenya kilichohusu ukombozi na historia ya Wagĩkũyũ. Alikuwa pia mwanzilishi na mhariri wa gazeti la kwanza kwa lugha ya Gĩkũyũ ambalo liliitwa Mũigũithania.
|
20231101.sw_2021_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Kutokana na kuhusishwa na harakati za vita vya msituni vya kundi la Mau Mau alihukumiwa miaka saba jela mwaka 1952. Huwezi kuzungumza historia ya Kenyatta bila ya kuitaja Maumau.
|
20231101.sw_2021_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Baadaye alioa mke wa tatu aliyeitwa Mama Ngina Kenyatta ambaye alikuja kuwa mke wa rais wa kwanza na ambaye ndiye mama yake Uhuru Kenyatta, rais wa sasa.
|
20231101.sw_2021_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Licha ya Waingereza kuwa na matumaini ya kuwapa wapinzani Waafrika mamlaka "ya wastani" zaidi, ilikuwa Kenya African National Union (KANU) ya Jomo Kenyatta, mfungwa wa zamani, ambayo iliunda serikali muda mfupi kabla ya Kenya kupata uhuru tarehe 12 Desemba 1963.
|
20231101.sw_2021_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Tarehe 1 Juni 1963 Kenya ilipata madaraka na Jomo Kenyatta alitawazwa kuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Kenya.
|
20231101.sw_2021_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Chama kidogo cha Kenya African Democratic Union (KADU), kilichowakilisha muungano wa makabila madogo ambayo yaliogopa utawala wa makabila makubwa, kilijitoa na kujivunja mwaka wa 1964 na wanachama wake wakajiunga na KANU.
|
20231101.sw_2021_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Chama kidogo cha upinzani, Kenya People's Union (KPU), kilianzishwa mwaka 1966, kiongozi wake akiwa Jaramogi Oginga Odinga aliyewahi kuwa makamu wa rais Kenyatta. KPU ilipigwa marufuku, na kiongozi kuwekwa kizuizini baada ya chachari za kisiasa zilizohusishwa na ziara za Kenyatta katika Mkoa wa Nyanza. Hakuna vyama vingine vya upinzani vilivyoanzishwa baada ya 1969, kupelekea Kenya kuwa mfumo wa chama kimoja chini ya KANU.
|
20231101.sw_2021_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jomo%20Kenyatta
|
Jomo Kenyatta
|
Kenyatta alifariki mjini Mombasa tarehe 18 Agosti 1978 na kuzikwa jijini Nairobi kwenye jengo la bunge.
|
20231101.sw_2022_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kwanza%20%28sarafu%29
|
Kwanza (sarafu)
|
Wakati wa uhuru Angola ilirithi pesa ya escudo kutoka Ureno. Mwaka 1977 Kwanza yenye Lwei 100 imeingizwa nchini kama pesa ya kwanza ya kitaifa. Kutokana na kushuka kwa thamani ya fedha mara kwa mara pesa ya Kwanza imebadilishwa mara nne tangu 1977:
|
20231101.sw_2023_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kwanzaa
|
Kwanzaa
|
Kwanzaa ni sikukuu inayosherehekewa kati ya Wamarekani Weusi nchini Marekani kwa muda wa siku saba toka tarehe 26 mwezi wa disemba hadi tarehe 1 mwezi wa Januari. Sikukuu hii ilianzishwa Kalifornia na Maulana Ron Karenga tarehe 26 Diesemba mwaka 1966.
|
20231101.sw_2023_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kwanzaa
|
Kwanzaa
|
Karenga alitunga neno jipya "Kwanzaa" kutokana na neno la Kiswahili "Kwanza" inayochukuliwa kumaanisha "matunda ya kwanza". Herufi "a" iliongezwa katika neno hilo ili kulifanya neno hilo kuwa na herufi saba, sawa na idadi ya siku za kusherehekea sikukuu hii.
|
20231101.sw_2023_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kwanzaa
|
Kwanzaa
|
Baadhi ya waamerika weusi huchukulia sikukuu hii kuwa na umuhimu sana kwao kama vile ilivyo Hanuka kwa Wayahudi au Krisimasi kwa Wakristo. Karenga aliagiza kutumia maneno kadhaa ya Kiswahili katika sikukuu hizi kwa kuonyesha uhusiano na utamaduni wa Afrika.
|
20231101.sw_2023_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kwanzaa
|
Kwanzaa
|
Sherehe hii imejengwa juu ya maadili ya kitamaduni ya Kiafrika na huchukuliwa kuwa ni kama aina za sherehe za makabila mbalimbali Afrika wakati wa mavuno. Maadili haya ya Kiafrika yamegawanywa katika dhana iitwayo Nguzo Saba. Kwa siku saba, kila siku huwa na nguzo yake ya kukumbuka na kuenzi. Nguzo hizo ambazo zinafahamika kwa Kiswahili ni: Umoja, Kujichagulia, Ujima, Ujamaa, Nia, Kuumba, na Imani. Nguzo saba hizi hutumiwa kama moja ya njia ya kuimarisha umoja wa kifamilia miongoni mwa jamii za Wamarekani Weusi na pia njia ya kuwakumbusha historia na utamaduni wao.
|
20231101.sw_2023_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kwanzaa
|
Kwanzaa
|
Kati ya shughuli zinazofanywa wakati wa sikukuu hii ni kuwasha mishumaa saba (mshumaa mmoja kila siku) na kutoa tambiko la kuenzi mababu na mabibi waliotangulia. Mishumaa hii huwa ina rangi za kijani, nyekundu na nyeusi. Mshumaa mweusi huwekwa katikati na ndio huwa wa kwanza kuwashwa. Huwashwa siku ya kwanza. Rangi nyeusi huwakilisha watu weusi, rangi nyekundu hukumbusha mapambano na masahibu yaliyowakumba walitangulia, na rangi ya kijani humaanisha utajiri wa bara la Afrika na pia matumaini mema ya watu weusi.
|
20231101.sw_2024_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Visa%20vya%20Esopo
|
Visa vya Esopo
|
Visa vya Esopo vinatokana na masimulizi ya Esopo, ambaye inaaminika kuwa alikuwa ni mtumwa wa Kiafrika aliyeishi kati ya mwaka 620 na 560 Kabla ya Kristo katika Ugiriki wa Zamani. Visa vyake hutumiwa kutoa mafunzo na kuburudisha. Visa hivi hutumiwa kwa wingi katika vitabu vya watoto na vikaragosi.
|
20231101.sw_2024_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Visa%20vya%20Esopo
|
Visa vya Esopo
|
Historia ya Esopo haijulikani vyema. Inaaminiwa kuwa alikuwa ni mtumwa aliyeachiliwa huru na baadaye alikuja kuuliwa na Wadeliphi. Baadhi ya wanazuoni wanaamini kuwa hakuna mtu aliyewahi kuishi katika historia aliyeitwa Esopo.
|
20231101.sw_2026_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Guinea
|
Guinea
|
Guinea (pia: Gine, Gini) ni nchi katika Afrika ya Magharibi. Pengine inatajwa kama Guinea-Conakry ili kuitofautisha na nchi za Guinea-Bissau na Guinea ya Ikweta.
|
20231101.sw_2026_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Guinea
|
Guinea
|
Imepakana na Guinea-Bisau, Senegal na Mali upande wa kaskazini, Côte d'Ivoire, Liberia na Sierra Leone kusini halafu Bahari Atlantiki upande wa magharibi.
|
20231101.sw_2026_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Guinea
|
Guinea
|
Jina la "Guinea" liliwahi kutaja sehemu kubwa ya Afrika ya Magharibi kati ya jangwa la Sahara na Ghuba ya Guinea ya Atlantiki likimaanisha "nchi ya watu weusi" kwa lugha ya Kiberberi.
|
20231101.sw_2026_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Guinea
|
Guinea
|
Lugha rasmi ni Kifaransa, lakini wakazi wanatumia zaidi lugha asilia kadiri ya makabila, hasa Kipular, Kimaninka, Kisusu, Kikisi, Kikpelle na Kiloma,
|
20231101.sw_2026_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Guinea
|
Guinea
|
Upande wa dini, 85% ni Waislamu (hasa Wasuni), 8% ni Wakristo (hasa Wakatoliki) na 7% ni wafuasi wa dini asilia za Kiafrika.
|
20231101.sw_2027_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abu%20Nuwas
|
Abu Nuwas
|
Abu Nuwas (kwa Kiarabu أبو نواس) alikuwa mshairi Mwarabu aliyeishi 760-815. Katika utamaduni wa Kiswahili ni jina la mhusika katika hadithi za “Hekaya za Abunuwasi”.
|
20231101.sw_2027_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abu%20Nuwas
|
Abu Nuwas
|
Mshairi Abu Nuwas alizaliwa Ahwaz (Irak). Mama yake alikuwa Mwajemi na baba alikuwa mwanajeshi Mwarabu ambaye hakupata kumjua. Jina lake halisi lilikuwa Hasan ibn Hani al-Hakami; 'Abu Nuwas' ni jina la kutania kutokana na nywele zake ndefu.
|
20231101.sw_2027_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abu%20Nuwas
|
Abu Nuwas
|
Akiwa kijana alipelekwa Basra (Iraq) akisaidia katika duka la moja al-Yashira. Huko Basra alihamia nyumba ya mshairi Walibah ibn al-Hubab aliyemfundisha elimu ya sarufi na pia elimu ya dini. Abu Nuwas aliendelea kujifunza mengi hata alikaa mwaka mmoja kati ya Waarabu Bedu jangwani ili aboreshe ujuzi wake wa lugha ya Kiarabu sanifu.
|
20231101.sw_2027_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abu%20Nuwas
|
Abu Nuwas
|
Akahamia Baghdad, mji mkuu wa Dola la Kiislamu lililotawala wakati ule maeneo makubwa kuanzia Afrika ya Mashariki hadi Afghanistan na Asia ya Kati. Alipendwa sana na watu wa mjini kwa sababu alianzisha aina mpya ya ushairi akiimba juu ya furaha za divai na mapenzi hasa na wavulana kuliko wasichana au wanawake.
|
20231101.sw_2027_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abu%20Nuwas
|
Abu Nuwas
|
Abu Nuwas akawa mshairi maarufu wa Kiarabu wa siku zile hadi ameitwa kutoa mashairi yake mbele ya Khalifa Harun ar-Rashid. Hata kama mashairi yake yalisababisha hasira ya wahubiri wa Kiislamu, Abu Nuwasi alilindwa na familia ya Barmaki waliokuwa mawaziri wa Khalifa. Wakati Abu Nuwas alipotupwa jela mara kadhaa waliweza kumwondoa gerezani tena.
|
20231101.sw_2027_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abu%20Nuwas
|
Abu Nuwas
|
Mwaka 798 Khalifa Harun ar-Rashid aliwaondoa Barmaki madarakani na kuwafunga jela; Abu Nuwasi alikimbilia Misri. Baada ya kifo cha Harun mwaka 809 alirudi Baghdad akikuta kuwa Khalifa mpya ni Muhammad ibn Harun al-Amin aliyewahi kuwa mwanafunzi wake. Miaka michache ya utawala wa al-Amin ilikuwa miaka ambako Abu Nuwasi alitunga mashairi mengi.
|
20231101.sw_2027_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abu%20Nuwas
|
Abu Nuwas
|
Baada ya al-Amin kupinduliwa na kaka yake al-Ma’amun aliyekuwa Mwislamu mkali, Abu Nuwas alianza kutunga mashairi yaliyolingana na mafundisho ya kidini. Lakini alishindwa kumbembeleza khalifa mpya.
|
20231101.sw_2027_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abu%20Nuwas
|
Abu Nuwas
|
Abu Nuwas anahesabiwa kati ya washairi wakuu wa lugha ya Kiarabu. Alikuwa na athira kubwa kwa washairi wa baadaye kama Omar Khayyám na Hafiz.
|
20231101.sw_2027_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abu%20Nuwas
|
Abu Nuwas
|
Waswahili wamejua zaidi umbo la jina kuwa "Abunuwasi" na wamecheka wakisoma "Riwaya za Abunuwasi". Lakini huyu Abunuwasi wa riwaya hana uhusiano na Abu Nuwas mshairi wa kihistoria zaidi ya kumpatia jina lake.
|
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.