_id
stringlengths 15
22
| url
stringlengths 31
150
| title
stringlengths 1
86
| text
stringlengths 100
23.8k
|
---|---|---|---|
20231101.sw_2326_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Unguja%20Kaskazini
|
Mkoa wa Unguja Kaskazini
|
Upande wa magharibi utalii umeanza kuwa muhimu. Eneo la Ras Nungwi ni sehemu moja yenye mahoteli ya watalii wa nje.
|
20231101.sw_2327_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tikisa
|
Tikisa
|
Wana mkia mrefu ambao wanautikisa mara kwa mara. Ndege hao ni wadogo na wembamba na spishi kadhaa zina rangi nzuri.
|
20231101.sw_2328_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Unguja%20Kusini
|
Mkoa wa Unguja Kusini
|
Mkoa wa Unguja Kusini ni mmojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 72000 na uko kwenye kisiwa cha Unguja.
|
20231101.sw_2328_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Unguja%20Kusini
|
Mkoa wa Unguja Kusini
|
Mwaka 2012 walikuwa 115,588 katika wilaya mbili ikiwa Wilaya ya Kati ina wakazi 73,346 na Wilaya ya Kusini ina wakazi 39,242.
|
20231101.sw_2328_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Unguja%20Kusini
|
Mkoa wa Unguja Kusini
|
Wakazi wa eneo hili la kisiwa cha Unguja, mbali na kujishughulisha na uvuvi kwenye Bahari ya Hindi, ni maarufu pia kwa kilimo cha zao la karafuu, zao linalokifanya Kisiwa cha Zanzibar kujulikana zaidi kama kisiwa cha viungo.
|
20231101.sw_2336_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Joseph%20Hill
|
Joseph Hill
|
Joseph Hill (22 Januari 1949 – 19 Agosti 2006) alikuwa mtunzi na mwimbaji wa Reggae toka nchini Jamaika. Alianza muziki katika kundi lijulikanalo kama The Soul Defender lililokuwa na makazi yake kitongoji cha St Catherine. Baadaye akaanzisha kundi la Culture akiwa na Telford Nelson na Albert Walker. Mwaka 1977 walitoa wimbo uliovuma sana uitwao Two Sevens Clash ambao ulizungumzia herufi mbili za 7 katika mwaka 1977. Hadi sasa Joseph Hill na wenzake wametoa album 22. Falsafa ya nyimbo za Joseph Hill ni ya kimapinduzi na kiroho inayopinga utumwa na ukosefu wa maadili na ucha mungu. Joseph Hill ni muumini wa imani na utamaduni wa Kirastafari. Katika wimbo wake wa wa PAY DAY anauliza ni lini watu walioumizwa na utumwa watalipwa. Pia amepinga aina zote za ukoloni na kumzumgumzia Chistopher Columbas kama muongo kwa kusema kwamba amegundua visiwa vya Jamaika ambavyo vilikuwapo tayari na watu. Joseph Hill pia anaenzi kitabu Bibilia anachoamini kuwa ni kitakatifu na amekuwa akitumia mistari na manabii toka kwenye Biblia kwenye nyimbo zake, kwa mfano wimbo wake kuhusu nabii Eliya.
|
20231101.sw_2338_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kaskazini-Mashariki%20%28Kenya%29
|
Mkoa wa Kaskazini-Mashariki (Kenya)
|
Kaskazini-Mashariki ulikuwa mmoja kati ya mikoa 9 ya Kenya. Eneo lake lilikuwa km² 127 000 na wakazi 962,143 (sensa ya 1999).
|
20231101.sw_2338_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kaskazini-Mashariki%20%28Kenya%29
|
Mkoa wa Kaskazini-Mashariki (Kenya)
|
Wakati wa ukoloni eneo hilo liliitwa "Northern Frontier District" (Eneo la mpakani wa kaskazini) likitawaliwa pekee na sehemu kubwa ya Kenya.
|
20231101.sw_2338_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kaskazini-Mashariki%20%28Kenya%29
|
Mkoa wa Kaskazini-Mashariki (Kenya)
|
Wakazi walio wengi ni Wasomalia kwa lugha na utamaduni; kuwepo kwao ndani ya Kenya badala ya Somalia ni urithi wa mipaka ya kikoloni. Wengine ni Waborana, Warendille na Waturkana.
|
20231101.sw_2338_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kaskazini-Mashariki%20%28Kenya%29
|
Mkoa wa Kaskazini-Mashariki (Kenya)
|
Eneo hili ni kavu sana. Mbali na bonde la mto Tana na maeneo mengine madogo, mkoa haufai kwa kilimo. Wakazi walio wengi hujipatia riziki kutokana na ufugaji.
|
20231101.sw_2339_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ali%20Farka%20Toure
|
Ali Farka Toure
|
Ali Farka Touré ni mmoja wa wanamuziki mahiri barani Afrika. Alizaliwa jijini Bamako nchini Mali mwaka 1939. Jina lake hasa ni Ali Ibrahim Touré. Muziki wa Ali Farka Touré ni mchanganyiko wa muziki wa asili wa Mali na muziki wa Amerika ya Kaskazini hasa blues.
|
20231101.sw_2339_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ali%20Farka%20Toure
|
Ali Farka Toure
|
Touré alizaliwa katika kijiji cha Kanau katika ukingo wa mto Niger, kaskazini magharibi mwa nchi ya Mali. Mama yake alikuwa na watoto kumi ambapo ndugu zake wote walifariki wakiwa wachanga. Jina la "Farka" ni jina la utani ambalo alipewa na wazazi wake likimaanisha mnyama punda kutokana na kuwa na msimamo mkali na kiburi.
|
20231101.sw_2339_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ali%20Farka%20Toure
|
Ali Farka Toure
|
Muziki wa Touré una nguvu kama za miujiza. Wapenzi wake dunia nzima wamelogwa na upigaji wake wa gitaa. Mara nyingi nyimbo zake amekuwa akiimba kwa lugha za Kisonghai, Kifula, na Kitamasheck. Albamu yake iitwayo Talking Timbukuta, ambayo aliitoa kwa kushirikiana na mwanamuziki Ry Cooder, iliuzwa na kumpatia umaarufu mkubwa hasa katika soko la muziki la nchi za Magharibi. Mwaka 2005 alitoa albamu ya In the Heart of the Moon akishirikiana na mwanamuziki Toumani Diabaté. Albamu hii ilimpatia tuzo ya Grammy.
|
20231101.sw_2339_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ali%20Farka%20Toure
|
Ali Farka Toure
|
Pamoja na muziki, Ali Farka Touré alikuwa akijihusisha na masuala ya kisiasa. Mwaka 2004 alichaguliwa kuwa meya wa mji wa Niafunké.
|
20231101.sw_2340_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rupia
|
Rupia
|
Neno "rupia" limetokana na lugha ya Kihindi cha kale "rūp" au "rūpā" linalomaanisha "fedha". Katika lugha ya Sanskrit "rupyakam" (रूप्यकम्) inamaanisha sarafu ya fedha. Hii ni asili ya "Rūpaya" iliyotumika katika India kama sarafu yenye gramu 11.66 za fedha tangu mwaka 1540. Rupia moja ilikuwa na Anna 16, Paisa 64 au Pai 192.
|
20231101.sw_2340_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rupia
|
Rupia
|
Kwenye eneo la India ya leo katika makoloni ya nchi zifuatazo: Denmark, Ufaransa na Ureno, pia katika madola mbalimbali ya Kihindi kabla ya ukoloni na kabla ya uhuru kama vile Hyderabad.
|
20231101.sw_2341_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20ya%20Mashariki%20ya%20Kiingereza
|
Afrika ya Mashariki ya Kiingereza
|
Afrika ya Mashariki ya Kiingereza (kwa Kiingereza British East Africa Protectorate) lilikuwa jina la eneo la Kenya lililowekwa chini ya utawala wa ulinzi wa Uingereza kuanzia mwaka 1895 hadi 1920 BK kama mtangulizi wa koloni la Kiingereza la Kenya.
|
20231101.sw_2341_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20ya%20Mashariki%20ya%20Kiingereza
|
Afrika ya Mashariki ya Kiingereza
|
Wakati wa mashindano ya kugawa Afrika kati ya madola ya Ulaya, Kampuni ya Kifalme ya Kiingereza kwa Afrika ya Mashariki ilianza shughuli zake katika eneo hili kwa kibali cha sultani wa Zanzibar kuanzia mwaka 1888.
|
20231101.sw_2341_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20ya%20Mashariki%20ya%20Kiingereza
|
Afrika ya Mashariki ya Kiingereza
|
Kampuni hiyo ilitakiwa kuwa na mamlaka juu ya eneo hili kwa kusudi la kufanya biashara, lakini uwezo wake haukutosha kutimiza shughuli, hasa maandalizi ya kujenga reli ya Uganda kati ya Mombasa na Kampala.
|
20231101.sw_2341_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20ya%20Mashariki%20ya%20Kiingereza
|
Afrika ya Mashariki ya Kiingereza
|
Baada ya kuazimia kujenga reli, Uingereza iliona haja ya kulinda eneo la reli hiyo: ndipo ikatangaza eneo lote kati ya Mombasa na Uganda kuwa chini ya ulinzi wake kuanzia tarehe 1 Julai 1895. Huo ndio mwanzo wa Afrika ya Mashariki ya Kiingereza ambaye baadaye iliitwa Kenya.
|
20231101.sw_2341_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20ya%20Mashariki%20ya%20Kiingereza
|
Afrika ya Mashariki ya Kiingereza
|
Eneo hilo baadaye lilipanuliwa zaidi hadi kukutana na maeneo yaliyokuwa chini ya utawala wa Italia (Somalia) na Ethiopia upande wa Kaskazini, utawala wa ushirikiano wa Misri na Uingereza (Sudan). Upande wa kusini mpaka ulifuata mapatano na Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.
|
20231101.sw_2341_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20ya%20Mashariki%20ya%20Kiingereza
|
Afrika ya Mashariki ya Kiingereza
|
Mpaka na eneo chini ya utawala wa ulinzi wa Uganda ulisahihishwa mwaka 1905; hadi wakati ule sehemu kubwa ya eneo la Kenya ya Magharibi ya leo ilihesabiwa kuwa upande wa Uganda.
|
20231101.sw_2343_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Siti binti Saad (alizaliwa Fumba, Zanzibari, 1880 akapewa jina la 'Mtumwa' kwa vile alizaliwa kipindi cha utumwa wa Kiarabu. Jina la Siti alipewa na kabaila mmoja wa Kiarabu) alikuwa mwimbaji wa Zanzibar.
|
20231101.sw_2343_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Baba yake bwana Saadi alikuwa ni Mnyamwezi kutoka Tabora na mama yake alikuwa Mzigua toka Tanga, lakini wote wawili walizaliwa Zanzibar. Hali ya maisha ya familia yao ilikuwa ni duni sana na walijishughulisha zaidi katika shughuli za kilimo na ufinyanzi kazi ambazo Siti alijifunza na kuzimudu vizuri pia.
|
20231101.sw_2343_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Kama Waswahili wasemavyo "kuzaliwa masikini si kufa masikini", Siti alibarikiwa kuwa na kipaji cha pekee cha uimbaji. Kipaji hiki kilimsaidia sana tangu siku za awali ya maisha yake kwani alitumia uimbaji wake kuuza vyungu vya mama yake alivyokuwa akimsaidia kuvitembeza. Siti alipoimba sauti yake iliweza kupaa na kusafiri kwa umbali wa maili nyingi na hii ndio ilikuwa ishara ya watu kujua kwamba vyungu vya kina Mtumwa vinapita leo. Alifananishwa kuwa na mapafu yenye nguvu kama ya simba kutokana na alivyoweza kupaza sauti yake mbali na bila kuachia pumzi.
|
20231101.sw_2343_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Kutokana na wakati huo elimu kwa watoto wa kike kutotiliwa mkazo, Siti hakuwahi kwenda shule wala kuhudhuria mafunzo ya Kurani. Hivyo mnamo mwaka 1911 aliona ni bora ahamie mjini ili kuboresha maisha yake zaidi. Ujio wake wa mjini ulikuwa wa neema kwani alikutana na bwana mmoja wa kundi la muziki wa Taarabu la "Nadi Ikhwani Safaa" aliyeitwa Muhsin Ali. Katika kipindi hicho, hilo ndilo lilikuwa kundi pekee la muziki wa taarabu lililoanzishwa na Sultani mpenda starehe na anasa bwana Seyyid Barghash Said. Kundi hili lilikuwa ni la wanaume peke yao, wanawake hawakuruhusiwa kujiunga na vikundi vya muziki kwa vile ilikuwa ikichukuliwa kama ni uhuni. Bwana Muhsin alikiona kipaji cha pekee cha Siti na hivyo akajitolea kumfundisha kuimba kwa kufuata vyombo vya muziki na lugha ya kiarabu. Baada ya hapo alikwenda kumtambulisha kwa wanamuziki wenzie wa "Nadi Ikhwani Safaa" ambao bila kusita wakaanza kufanya naye maonyesho mbalimbali katika jamii. Walipata mialiko mingi hasa kutoka kwa Sultani na matajiri wengine wa Kiarabu, pia katika harusi na sherehe zingine mbalimbali, inasemekana ulifika wakati ambapo sherehe ilishindwa kufana kama Siti binti Saadi hakuwepo kutumbuiza. Siti alikuwa ni moto wa kuotea mbali na jina lake lilivuma kwa haraka sana hadi nje ya mipaka ya nchi na bara la Afrika. Na punde Siti alianza kufananishwa na 'Umm Kulthum', mwimbaji mahiri wa kike aliyetamba wakati huo kutoka Misri.
|
20231101.sw_2343_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Kama nilivyosema moto wa Siti ulikuwa si wa kuusogelea karibu, mwaka 1928 kampuni ya kurekodi muziki ya Columbia and His Master's voice yenye makazi yake Mumbai India ilisikia umaarufu wa Siti binti Saadi na hivyo ikamwalika yeye pamoja na kundi lake kwenda kurekodi kwa lugha ya Kiswahili ili kujaribu kama muziki wake utauzika. Kampuni ile haikuweza kuamini jinsi muziki ule ulivyouzika kwa kasi kubwa kwani wastani wa santuri 900 ziliweza kuuzika katika kipindi cha miaka miwili ya mwanzo, na hadi kufikia 1931 santuri 72,000 zilikuwa zimeuzwa. Kutokana na kusambaa kwa santuri hizi, umaarufu wa Siti ulizidi mara dufu na watu kutoka sehemu mbalimbali za dunia walizuru Zanzibari kumwona. Mambo yalizidi kuwa mazuri kwa Siti hadi ikafikia hatua kampuni ya kurekodi ya Columbia kuamua kujenga studio ya kurekodi muziki palepale Zanzibar maalumu kwa ajili ya Siti binti Saadi.
|
20231101.sw_2343_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Hatua hiyo ya hadi kujengewa studio iliwaumiza wengi wenye wivu, hivyo wakaanza kumtungia nyimbo za kumkejeli ili kumshusha na hasa walitumia kigezo kwamba hana uzuri wa sura, nyimbo nyingi ziliimbwa lakini huu ndio uliovuma sana:
|
20231101.sw_2343_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Kwa kujibu shambulio hilo kwa namna yake aliwafunga midomo wale wote waliokuwa wakimkejeli. Siti pia alikuwa ni mwanamke wa kwanza mwanaharakati katika kipindi chake kwa kuwatetea wanawake na wanyonge kwa ujumla, kwani katika kipindi chake watu matajiri walikuwa wakiwaonea masikini na walipofikishwa mbele ya haki waliweza kutoa hongo na kuachiwa huru halafu wewe uliyeshitaki ndiye unayefungwa.
|
20231101.sw_2343_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Utunzi wake wa wimbo wa Kijiti ulimpatia sifa kubwa kwani ulikuwa ukielezea kisa cha kweli kilichomkuta mwanamke mmoja mgeni kutoka bara, mwanamke huyu alipofika alikutana na Tajiri mmoja ambaye alijifanya amempenda, hivyo akamchukua na kulala naye halafu baadaye akamuua. Tajiri yule alishitakiwa na bahati nzuri walikuwepo mashahidi wawili walioshuhudia tukio lile, lakini kwa vile ni Tajiri alitoa pesa na kesi ikawageukia wale mashahidi na kufungwa.
|
20231101.sw_2343_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Siti aliendelea kumwambia katika nyimbo zake kwamba asijethubutu kwenda Dar es Salaam kwa maana watu wenye hasira wanamsubiri na wameapa kwa ajili yake.
|
20231101.sw_2343_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Siti aliendelea na shughuli yake ya muziki hadi uzeeni, muda mfupi kabla ya kifo chake alikutana na mwandishi maarufu na mwanamashairi Shaaban Robert ambaye alimhoji na kuweza kuandika wasifu wake katika kitabu alichokiita " Wasifu wa Siti binti Saadi." Wasifu huu unaonekana kuwa ndio bora zaidi uliowahi kuandikwa katika fasihi ya Tanzania. Kitabu hiki kinatumika kufundishia shule za sekondari za Tanzania.
|
20231101.sw_2343_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Tarehe 8 Julai 1950 Siti binti Saadi alifariki dunia na kuacha pengo kubwa katika fani ya Taarabu. Ingawa pengo hilo haliwezi kuzibika lakini kuna watu wengi walioweza kuibuka na umaarufu wa kuimba taarabu kupitia kwake, mfano hai ni Bi Kidude.
|
20231101.sw_2343_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
|
Siti Binti Saad
|
Hata baada ya kifo chake jina lake bado linatumika sana kama kielelezo cha ushujaa wake, Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania (TAMWA), kimetumia jina lake kulipa jina gazeti la chama chao "Sauti ya Siti". Hadi leo hii Siti hutumika kama kipimo cha kufundishia uimbaji wa Taarabu. Na anakumbukwa katika historia yake ya kuwa mwanamke wa kwanza Afrika mashariki kurekodi muziki katika santuri.
|
20231101.sw_2345_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Rwanda huitwa nchi ya vilima elfu (kwa Kinyarwanda: Igihugu cy'Imisozi Igihumbi; kwa Kifaransa: Pays de Mille Collines): ndivyo sehemu kubwa ya eneo lake inavyoonekana, hasa magharibi.
|
20231101.sw_2345_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Ni nyanda za juu na milima; sehemu kubwa ni mita 1500 juu ya UB. Milima kaskazini mwa nchi inapanda hadi mita 4507 juu ya UB. Kutokana na urefu huo hali ya hewa haina joto kali.
|
20231101.sw_2345_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Mpaka na Kongo ni hasa Ziwa Kivu ambalo ni mojawapo kati ya maziwa ya bonde la ufa la Afrika ya Mashariki.
|
20231101.sw_2345_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Huko kuna mazingira ya pekee duniani yenye sokwe wa milimani. Wako hatarini kuangamizwa kutokana na uwindaji na upanuzi wa mashamba unaopunguza mazingira wanamoishi.
|
20231101.sw_2345_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Miji mikubwa zaidi ndiyo: Kigali wakazi 745.261, Butare wakazi 89.800, Gitarama wakazi 87.613, Ruhengeri wakazi 86.685 na Gisenyi wakazi 83.623.(namba za Januari 2005)
|
20231101.sw_2345_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Gisenyi ni mji kwenye ncha ya kaskazini ya Ziwa la Kivu mpakani kwa Kongo ukiwa jirani na mji wa Goma. Kuna usafiri wa mashua kwenda Kibuye na Cyangugu.
|
20231101.sw_2345_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Kibuye ni mji mdogo ufukoni mwa Ziwa la Kivu. Una wavuvi wengi, kituo cha watalii na nyumba za kihistoria za wamisionari. Hadi mwaka 1994 Watutsi 250,000 waliishi katika wilaya ya Kibuye, lakini tangu uangamizaji wa Watutsi katika vita vya wenyewe kwa wenyewe wamebaki 8000 pekee.
|
20231101.sw_2345_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Wakazi wa Rwanda ni zaidi ya milioni 11. Banyarwanda milioni 2 wako Uganda na wengi zaidi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
|
20231101.sw_2345_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Kwa kawaida vikundi vitatu hutajwa kuwa wakazi wa Rwanda ndio Wahutu, Watutsi, Watwa. Lakini kuna tofauti kali kati ya mawazo kama vikundi hivyo ni makabila, mataifa ya pekee au matabaka ya kijamii. Hali halisi wanatumia lugha ileile ya Kinyarwanda na wanafuata utamaduni uleule.
|
20231101.sw_2345_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Wanahistoria wengi wanasema ya kuwa Watwa walikuwa wakazi wa kwanza wakiwa wawindaji, Wahutu ndio wakulima wa Kibantu waliopatikana kwa uenezi wa Wabantu katika Afrika ya Kati na mababu wa Watutsi waliingia kama wafugaji kutoka kaskazini.
|
20231101.sw_2345_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Watutsi walikuwa tabaka la kikabaila, pia mfalme alikuwa Mtutsi. Lakini wengine wanaamini ya kwamba vikundi vyote vitatu vilijitokeza nchini si kama tokeo la uhamiaji mbalimbali lakini zaidi kama matabaka yaliyotofautiana kikazi: wakulima, wavindaji na wafugaji waliokuwa pia askari wa mfalme.
|
20231101.sw_2345_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Wakati wa ukoloni Wabelgiji walihesabu mwaka 1931 wakazi wa nchi kama ifuatavyo: 84 % Wahutu, 15 % Watutsi na 1 % Watwa.
|
20231101.sw_2345_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Kabla ya uhuru vilitokea kwa mara ya kwanza vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya makabila mawili makubwa viliyosababisha kupungua kwa Watutsi kutokana na mauaji na zaidi kwa Watutsi kukimbilia nchi jirani. Mnamo 1990 asilimia ya Watutsi ilikadiriwa kuwa 9 - 10 %.
|
20231101.sw_2345_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka ya 1990 vilileta uangamizaji mkubwa wa Watutsi. Kati ya asilimia 75 hadi 90 za wakazi Watutsi waliuawa katika wiki chache za mwaka 1994. Baada ya mwisho wa vita Watutsi wengi ambao wenyewe au wazazi wao walikuwa wamekimbilia Uganda na Tanzania walirudi tena Rwanda.
|
20231101.sw_2345_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Kwa wastani kuna wakazi 300 kwa kilomita ya mraba ambayo ni msongamano mkubwa kabisa katika Afrika. Karibu nusu ya wakazi ni watoto hadi umri wa miaka 14.
|
20231101.sw_2345_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Lugha ya taifa, lugha rasmi na lugha ya mama kwa Wanyarwanda wote ni Kinyarwanda ambayo ni lugha ya Kibantu, mojawapo ya Niger-Kongo.
|
20231101.sw_2345_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Lugha rasmi tangu enzi za ukoloni ni Kifaransa. Tangu mwaka 1994 serikali mpya, iliyoongozwa na Watutsi walioishi miaka mingi Uganda, imetumia pia Kiingereza kama lugha rasmi ya tatu.
|
20231101.sw_2345_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Kadiri ya sensa ya mwaka 2012 wakazi wengi ni Wakristo, hasa Waprotestanti (49.5%) na Wakatoliki (43.7%). Waislamu ni 2%.
|
20231101.sw_2345_18
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Kwa sasa serikali inazidi kufungia maabadi. Miezi saba ya kwanza ya mwaka 2018, imefungia tayari makanisa 8,000.
|
20231101.sw_2345_19
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Mwanzo wa karne ya 20 ilikuwa sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani na sababu ya mzozo kati ya Ujerumani na Ubelgiji.
|
20231101.sw_2345_20
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Uhuru katika mwaka 1961 ulifika pamoja na vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya Wahutu na Watutsi. Uhusiano kati ya vikundi hivi viwili uliendelea kuwa vigumu.
|
20231101.sw_2345_21
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Kuuawa kwa rais Juvenal Habariyama mwaka 1994 kulisababisha mauaji ya watu karibu milioni moja (walau 600,000) kati ya Watutsi, Watwa pamoja na Wahutu wasio na msimamo mkali.
|
20231101.sw_2345_22
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Rwanda pamoja na Burundi zilijiunga na Kenya, Uganda na Tanzania kama wanashirika wa Jumuia ya Afrika Mashariki kwa maendeleo muhimu katika elimu, afya, uchumi na mambo mbalimbali. Mwaka 2017 bunge la Rwanda liliamua kufanya Kiswahili kuwa moja ya lugha rasmi nchini.
|
20231101.sw_2345_23
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
|
Rwanda
|
Vita vya Kongo vilivyokuwa na majeshi ya mataifa mbalimbali (Kivu Conflict) vilimalizika mwaka 2012.
|
20231101.sw_2347_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Malawi (wakati wa ukoloni iliitwa Unyasa au Nyasaland) ni nchi ya bara la Afrika iliyopo kusini-mashariki, ikipakana na Tanzania, Msumbiji na Zambia.
|
20231101.sw_2347_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Sehemu kubwa ya eneo lake ni ziwa linaloitwa na majirani "Ziwa Nyasa" au "Niassa", lakini "Ziwa Malawi" hapa nchini. Kati ya Malawi na Tanzania kuna mzozo kuhusu eneo la ziwa ambao unazidi kufanyiwa kazi.
|
20231101.sw_2347_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Katika karne ya 10 BK walifika Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi. Wengi walizidi kuelekea kusini, lakini wengine walihamia nchini.
|
20231101.sw_2347_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Hakuna habari za kimaandishi kabla ya kufika kwa Wazungu. Tangu karne ya 16 ufalme wa Wamaravi ulikuwepo upande wa kusini wa ziwa. Wamaravi walipanua utawala wao. Lakini katika karne ya 19 walishambuliwa sana na Wayao walioendesha biashara ya watumwa wakiwakamata katika eneo la ziwa na kuwapeleka hadi pwani ya Bahari Hindi kama vile Kilwa.
|
20231101.sw_2347_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Wamisionari walimfuata, hasa Wapresbiteri kutoka Uskoti, waliotafuta wafuasi wa Ukristo na kumpambana na wafanyabiashara ya utumwa.
|
20231101.sw_2347_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Mwaka 1891 serikali ya Uingereza iliweka nchi upande wa magharibi na kusini kwa ziwa chini ya ulinzi wake ikawa „Nyassaland Protectorate“, halafu tangu 1907 koloni la Unyasa.
|
20231101.sw_2347_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Waingereza waliogopa kushambuliwa kutoka Afrika ya Mashariki ya Kijerumani wakachukua hatua za kudai huduma za nyongeza kutoka kwa wananchi. Hii ilisababisha ghasia ya John Chilembwe dhidi ya wakoloni.
|
20231101.sw_2347_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia Waingereza waliunganisha Unyasa na Rhodesia (leo Zambia na Zimbabwe) kuwa Shirikisho la Afrika ya Kati mwaka 1953. Shirikisho hilo halikudumu hadi mwisho wa ukoloni kutokana mielekeo tofautitofauti katika sehemu tatu za shirikisho.
|
20231101.sw_2347_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Katika Unyasa daktari Hastings Kamuzu Banda alijitokeza kuwa mwanasiasa aliyependelewa na wananchi wengi, akawa waziri mkuu wakati wa Unyasa kupata madaraka ya kujitawala katika mambo ya ndani na baadaye rais wa kwanza wa taifa.
|
20231101.sw_2347_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Mwaka 1964 Unyasa (Nyassaland) ilikuwa nchi huru kabisa lakini bado sehemu ya Jumuiya ya Madola chini ya malkia wa Uingereza kwa miaka miwili ya kwanza.
|
20231101.sw_2347_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Mwaka 1966 Banda alitangaza kura ya katiba mpya iliyopokewa na wananchi. Nchi ilipata jina la Malawi na chama cha Malawi Congress Party kikawa chama pekee.
|
20231101.sw_2347_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Mabadiliko ya kimataifa baada ya kuporomoka kwa Ukomunisti na ukuta wa Berlin miaka 1989/1990 yalileta shinikizo kote Afrika dhidi ya serikali zilizofuata mtindo wa chama kimoja. Shinikizo hilo lilimkuta Banda mzee na mgonjwa ilhali watu wa familia yake wakitawala kupitia yeye. Hali ya uchumi ilikuwa duni, rushwa na magendo juu.
|
20231101.sw_2347_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Mwaka 1993 serikali yake ililazimishwa kukubali kura ya wananchi wote walioamua kumaliza mfumo wa chama kimoja na kuanzisha kipindi kipya.
|
20231101.sw_2347_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Uchaguzi huru wa mwaka 1994 ulimaliza utawala wa MCP ukamfanya Bakili Muluzi wa United Democratic Front (UDF) ndiye rais aliyechaguliwa mara ya pili 1999.
|
20231101.sw_2347_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Katika uchaguzi wa mwaka 2004 alishinda tena mgombea wa UDF, ndiye Bingu Mutharika aliyeapishwa kuwa rais wa Malawi tarehe 24 Mei 2004 huko Blantyre.
|
20231101.sw_2347_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Malawi ilikuwa na siasa ya chama kimoja chini ya rais wa kwanza Hastings Kamuzu Banda tangu kupata uhuru mwaka 1964 na masahihisho ya katiba 1966.
|
20231101.sw_2347_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Kutokana na katiba ya 1995 rais wa taifa anayechaguliwa na wananchi ndiye mkuu wa dola pia mkuu wa serikali. Makamu wa rais anachaguliwa pamoja naye lakini rais ana haki ya kumteua makamu wa pili asiyetoka katika chama chake.
|
20231101.sw_2347_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Mahakama zinafuata mtindo wa Uingereza. Majaji huteuliwa kwa muda wa maisha; wanatakiwa kuwa huru na kutoathiriwa na siasa.
|
20231101.sw_2347_18
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Utawala hutekelezwa katika mikoa mitatu ya nchi zinazogawiwa katika wilaya 28. Wakuu wa mikoa na wilaya huteuliwa na serikali kuu.
|
20231101.sw_2347_19
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Serikali za mitaa zimeundwa na wilaya 28 katika maeneo matatu (Kaskazini, Kati na Kusini) yanayotawaliwa na Watawala wa Maeneo na Wakuu wa Wilaya ambao wanachaguliwa na serikali kuu.
|
20231101.sw_2347_20
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Uchaguzi wa kwanza wa Serikali za mitaa katika historia ya mfumo wa vyama vingi ulifanyika mnamo 21 Novemba 2000. UDF ilishinda asilimia 70 ya viti hivi katika uchaguzi huu.
|
20231101.sw_2347_21
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Wakazi wengi ni wa makabila ya Wabantu na wanatumia lugha za Kibantu, hasa Kichewa (zaidi ya 57%), lakini lugha rasmi ni Kiingereza.
|
20231101.sw_2347_22
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Upande wa dini, kadiri ya sensa ya mwaka 2018, wakazi wengi ni Wakristo (77.5%, kati yao Wakatoliki 17.2%), wakifuatwa na Waislamu (13.8%).
|
20231101.sw_2347_23
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
|
Malawi
|
Global Lives Project video recording of 24 hours of daily life of Edith Kaphuka in Ngwale Village, Malawi
|
20231101.sw_2351_0
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Msumbiji iko ufukoni mwa Bahari Hindi ikipakana na Tanzania, Malawi, Zambia, Zimbabwe, Afrika Kusini na Eswatini.
|
20231101.sw_2351_1
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Jina la nchi limetokana na Kisiwa cha Msumbiji (kwa Kireno: Ilha de Moçambique) kilichokuwa boma na makao makuu ya Ureno kwenye pwani ya Afrika ya Mashariki.
|
20231101.sw_2351_2
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Tambarare ya pwani ni sehemu kubwa ya kusini mwa nchi, lakini kwenda kaskazini upana wake unapungua.
|
20231101.sw_2351_3
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Milima mirefu zaidi inajulikana kama Inyanga yenye mita 2500 juu ya UB: iko katika jimbo la Tete inayopakana na Zimbabwe, Zambia na Malawi.
|
20231101.sw_2351_4
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Mito iko mingi, mkubwa zaidi ukiwa ndio Zambezi, halafu Ruvuma mpakani kwa Tanzania, Save na Limpopo.
|
20231101.sw_2351_5
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Umbo la eneo la nchi ni refu sana: ni kilomita 2000 kutoka mpaka wa Tanzania upande wa kaskazini hadi Maputo iliyoko karibu na Uswazi na Afrika Kusini.
|
20231101.sw_2351_6
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Katika karne za kwanza BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi ambao walimeza wakazi wa kwanza inavyothibitishwa na DNA.
|
20231101.sw_2351_7
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Haijulikani ni lini ya kwamba wafanyabiashara Waarabu walianza kufika ufukoni na kujenga vituo na miji yao. Lakini utamaduni wa Waswahili ulifika hadi sehemu za mwambao wa Msumbiji. Hadi leo aina ya Kiswahili inazungumzwa kwenye visiwa vya Kirimba.
|
20231101.sw_2351_8
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Mto wa Zambezi ilitumika kama njia ya mawasiliano na biashara kati ya Ufalme wa Mwene Mtapa (Zimbabwe) na wafanyabiashara wa pwani.
|
20231101.sw_2351_9
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Taarifa za kimaandishi zinaanza na kufika kwa Wareno. Mwaka 1498 Vasco da Gama alifika akiwa njiani kuelekea Bara Hindi.
|
20231101.sw_2351_10
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Baadaye Msumbiji ikawa koloni la Wareno hadi mwaka 1975 vita vya ukombozi vya miaka 1964-1974 vilipomalizika kwa ushindi.
|
20231101.sw_2351_11
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Nchini Msumbiji kuna makabila mengi sana, kama vile Wamakua, Wanyungwe, Wayao, Wamakonde na Watsonga.
|
20231101.sw_2351_12
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Kila kabila lina lugha yake, lakini lugha rasmi ni Kireno, ambacho kinaweza kuzungumzwa na 50.3% za wakazi, ingawa ni lugha ya nyumbani kwa 16.6% tu.
|
20231101.sw_2351_13
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Upande wa dini, sensa ya mwaka 2017 ilikuta 59.2% ni Wakristo (hasa Waprotestanti na Wakatoliki, ambao ni 28.4%) na 18.9% ni Waislamu. 7.3% wanafuata dini asilia za Kiafrika au nyingine. Kumbe 13.9% hawana dini yoyote, kufuatana na kampeni ya Ukomunisti ya miaka 1979-1982.
|
20231101.sw_2351_14
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Abrahamsson, Hans Mozambique: The Troubled Transition, from Socialist Construction to Free Market Capitalism London: Zed Books, 1995
|
20231101.sw_2351_15
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Gengenbach, Heidi. Binding Memories: Women as Makers and Tellers of History in Magude, Mozambique. Columbia University Press, 2004. Entire Text Online
|
20231101.sw_2351_16
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Mwakikagile, Godfrey, Africa and America in The Sixties: A Decade That Changed The Nation and The Destiny of A Continent, First Edition, New Africa Press, 2006, ISBN 978-0-9802534-2-9
|
20231101.sw_2351_17
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
|
Msumbiji
|
Mwakikagile, Godfrey, Nyerere and Africa: End of an Era, Third Edition, New Africa Press, 2006, "Chapter Seven: "The Struggle for Mozambique: The Founding of FRELIMO in Tanzania," pp. 206–225, ISBN 978-0-9802534-1-2
|
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.